Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Wana JF si kawaida yangu kuandika sanasana na imenilazimu leo... Tangu zamani niliamini kuwa CHADEMA kinaweza kuwa chama cha 'Demokrasia' na daima kitaruhusu 'Demokrasia' kuchukua mkondo wake lakini tunapoelekea inaelekea sivyo.

Naam, nazungumzia kikao kilichofanyika leo na 'wazee' wa CHADEMA kuanza 'kumshinikiza' Zitto Kabwe kuondoa jina katika kinyang'anyiro cha Uenyekiti.

Ndiyo, nilikuwa sioni sababu ya Zitto kugombea mwanzoni lakini kwakuwa alishaweka jina nilitarajia atapewa nafasi kuweza kudhihirisha kuwa demokrasia imeweza kuchukua mkondo wake ndani ya CHADEMA.

Nasisitiza, napinga kwa sana njia hii inayotumika kuhakikisha Freeman anabaki mgombea pekee, inawezekana kwa maslahi ya chama chenu mmefanya hivyo kukinusuru chama (kama mnavyodhania) lakini binafsi (si msimamo wa JF) naamini ndio mnakizika chama... Bado mna muda, mwacheni Zitto agombee na akishindwa ashindwe kidemokrasia...

Kama ni kuondoa basi wote wawili (Zitto na Freeman) waondoe majina na ifikiriwe namna mpya.

Katika hili, mmechemsha!
Watanzania ni wagumu kweli kweli kuelewa. Chinga amelalama weeee lakini hamkumuelewa.

Yaani mambo yapo hivi, CHADEMA kinakuwa chama cha kidemokrasia pale tu ambapo uongozi wa juu unabaki Moshi. Katika hili hakuna majadiliano.

Ikiwa kama ni Ndesamburo ndie aliyegombea, baraza la wazee usingelisikia na wote wangeenda katika uchaguzi na kihalali kabisa aliyeshinda ndiye angekuwa mwenyekiti.

Sasa kitachofuata ni kiini macho, yaani wote watajitoa halafu Ndesamburo ndiye atagombea. Kaa uonelakini usije ukaniita mimi mganga au mchawi.
 
Jamani hivi Mzee Mwanakijiji upo? sijaona mchango wako ktk hili sakata la zitto
Ngoma nzito kwake hii!!!! Uliona wapi ugomvi wa Kingunge na Nyerere eti David wakati achangie.

Hii ni mtihani mkubwa wa kwanza toka CHADEMA iundwe. Kimsingi, Chinga alishatabiri kuwa Chama hiki si cha kudumu kwa vile ni cha Moshi. Kama hayo ni kweli au si kweli dakika 90 +4 (za nyongeza) zitatoa jibu.
 
Wakuu, nimeamua kuchukua summary kwa ajili ya reference ya ambao wameanzia mjadala katikati...

Wasiwasi wangu ni kama watu mmemsoma kwa karibu Ansbert Ngurumo!

Asante Robot kwa Summar yako, nimemsoma Ngurumo kwa Umakini sana but I better reserve my comments coz nahisi kuna Mambo Mengi sana ni Mageni, Naogopa kuchaingia kwa Hisia.
 
Watanzania ni wagumu kweli kweli kuelewa. Chinga amelalama weeee lakini hamkumuelewa.

Yaani mambo yapo hivi, CHADEMA kinakuwa chama cha kidemokrasia pale tu ambapo uongozi wa juu unabaki Moshi. Katika hili hakuna majadiliano.

Ikiwa kama ni Ndesamburo ndie aliyegombea, baraza la wazee usingelisikia na wote wangeenda katika uchaguzi na kihalali kabisa aliyeshinda ndiye angekuwa mwenyekiti.

Sasa kitachofuata ni kiini macho, yaani wote watajitoa halafu Ndesamburo ndiye atagombea. Kaa uonelakini usije ukaniita mimi mganga au mchawi.

Hivi chinga yu wapi naona kimya
 
Watanzania ni wagumu kweli kweli kuelewa. Chinga amelalama weeee lakini hamkumuelewa.

Yaani mambo yapo hivi, CHADEMA kinakuwa chama cha kidemokrasia pale tu ambapo uongozi wa juu unabaki Moshi. Katika hili hakuna majadiliano.

Ikiwa kama ni Ndesamburo ndie aliyegombea, baraza la wazee usingelisikia na wote wangeenda katika uchaguzi na kihalali kabisa aliyeshinda ndiye angekuwa mwenyekiti.

Sasa kitachofuata ni kiini macho, yaani wote watajitoa halafu Ndesamburo ndiye atagombea. Kaa uonelakini usije ukaniita mimi mganga au mchawi.

Una Uhakika Ndesa Hajawahi kugombea Nafasi ya Uenyekiti CHADEMA?
 
Una Uhakika Ndesa Hajawahi kugombea Nafasi ya Uenyekiti CHADEMA?

Nilivyo elewa mimi nadhani Zawadi anamaana kwamba laiti zitto angekuwa ni kutoka moshi then kusingekuwa na ugomvi kwa sababu wote wanatoka sehemu moja hivyo bado chama kiko moshi.
 
Lidhwani, JK na Salma wote wako ndani ya CCM na wote viongozi .

Mleta habari umesema Ndesa alipata kura 49 na hakuwa na mpinzani , sasa kama hakutokea mtu kupingana naye je ? Ukiona mzee anapita means anakubalika ambao ndiyo ukweli .Kwamba wapare hawakusimama sasa hii ni shida kubwa ya ukabila naona unakubana sana kaka .Sisi twende tukalazimishe makabila kuingia Siasa nakuoma kugombea ?

wanaogopa kugombea kwani chama kina wenyewe wazee wa Chama.tumejifunza kwa Zitto Kabwe.JK kapigiwa kura hakupitishwa na wazee kama Mbowe.hivi kuna faida gani Chadema kufanya uchaguzi wakati wazee wamekwishachagua.
 
Demokrasia si photocopy wadau, kumbukeni katika nchi maskini kama tanzania mchakato wa demokrasia ya kweli unajumlisha vitu vingi, hatuwezi tu kuamua mambo eti kwa vile demokrasia inaruhusu mtu yeyote mwenye sifa husika agombee nafasi husika...tanzania haijafikia demokrasia ya kiwango hicho, ndio maana kwa maendeleo ya kweli na dhati anahitajika dikteta ama kikundi cha watu wenye dira sahihi...ili kukuza demokrasia, kwa hatua tuliyopo, alichofanya zitto ni sahihi kabisa, kaonyesha anaweza, lakini pia kaonyesha ana usikivu na busara....kwa kifupi, kajiwekea imani kubwa sana ya baadae....chadema inatakiwa ikuze demokrasia nchini, hivyo inahitaji utulivu wa kweli, mbowe na zitto nadhani wamelielewa hilo...chadema msituangushe baada ya hili tukio, tunawategemea kwa sababu tu mnazo busara na mnajua kusoma nyakati....
 
Mkuu usiseme hivyo ni mkono wa CCM/mafisadi wamemrubuni zitto na nadhani zitto hafai tena kuwa hata mbunge, kaisha vimba kichwa lakini la DOWANS analo tu mpaka mwisho wake.

Ni kweli mkuu, hilo la Richmond/Dowans ni lake tu.

Tukumbuke kuwa alijaribu kupora madaraka yasiyo ya Kamati yake ili kufanikisha mpango huo kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umma. Alipoulizwa amtaje mmiliki wa Dowans akasema hamfahamu, na eti si muhimu kumfahamu. Je alipopigia debe ununuzi huo alitaka nani alipwe? Kuanzia hapo ndio watu wakaona kuwa Zitto ana maslahi binafsi hapo kwenye dili hilo la mafisadi.

Je tutakosea tukihisi hao ndio waliomtuma ili akivuruge Chadema kwa kuwa kinakuja juu?

Amefulia.
 
Najifariji kuwa aliload credit kwenye simu yake akataka afanye teleconference na Slaa, Mbowe na Makani ila kwa bahati mbaya hawakupatikana na kwa sababu alishacheck in while his friends wanamforce ikabidi ajaze form akirudi atawasikiliza. Then haya yametokea.

Sitaki niamini kuwa alifanya hivyo maana wengi tutaumia
Selous,

Nilikuwa nakuona una mawazo ya maana; yaani hii pumba hapo juu ni ya kwako kweli?

Kweli watu wakipenda hugeuka kuwa chongo na viziwi.

Zitto aligombea kwa hiari yake hata kama alishawishiwa na wanachama. Kwa Tanzania kila anayegombea anasema hivyo hivyo.

Hiyo yako hapo juu ni spinning!
 
Ndugu Sikonge Tamko lako hili tuu "Naona na sisi Wanyamwezi tuwe na chama chetu........." Linanipa mashaka juu ya ufahamua wako wa mambo na hasa Siasa

Mimi naamini kigezo cha nanikuchanguli au kutochanguliwa kisiwe baba na mtoto au mtu na rafiki Kiwe utendaji kama utandaji wa mtu(watu) ni mzuri then wachaguli na ndo walivyofanya wajumbe
 
Ukitaka kuona UNAFIKI wa wana JF ni kusoma thread hii yote kisha nenda ile thread ya Malecela na wale wanaotaka kumpinga JK au hata ile ya Mwakyembe vs Mwakalinga.

Mimi nabaki kucheka hasa na leo nimenunua na power yangu toka Malawi ili nione watu wanavyojikanyaga hapa kwenye thread hii.

Watanzania wote wako sawa tu, akili zetu mbovu mbovu, maamuzi yetu yana walakini, na tuna wivu wa kike according to Mkapa.

Leo Zitto kumpinga Mbowe tayari imeshazua balaa. CCM nafikiri wanacheka tu.


CHADEMA mmejifunga goli la kisigino au mmejitwanga kisigino wenyewe kwa bastola.
 
kura za Ndesa hazikutosha ukizingatia wajumbe kutoka mikoa yote ndo wanapiga kura.Hata Zitto angekuwa kaoa mchaga angeingizwa ulingoni na angeshinda.

Angeingizwa na Nani?
Wewe ni Mtabiri au unahisi?
 
Wazee wa Chadema wasiozidi watano walipohojiwa na vyombo vya habari mbali mbali walisema kuwa Zitto ana haki ya kugombea pia anatimiza demokrasia kama Chadema inavyosimama.

wazee hawa jana wamemzuia Zitto kugombea uenyekiti.kamati kuu na mkutano mkuu wa Chadema una maana gani wakati wazee wa Chadema wameshafanya maamuzi yao? bnaona kazi za kamati kuu na mkutano mkuu wameshazifanya hawa wazee wa Chadema,okoeni pesa hakuna haja ya kuwa na mkutano mkuu.
 
hao walomshauri atoke wangemuacha agombee.huo ndo ukweli wenyewe ukizingatia chadema ni sakosi

hisia zako tu, na kinachokusumbua ni INFERIORITY COMPLEX kwa wachagga, siyo peke yako ni watu wengi sana
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom