Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Wakati namsubiri Zitto aje kujibu barua yangu ya wazi, ngoja niendelee na dhahania:

Inawezekana Zitto alijua fika lililotokea litatokea wakati anajaza na kurudisha fomu.

- Kama alijua inawezekana basi alichukua fomu ili kulifanya lililotokea litokee
- Kama hakujua inawezekana basi hakuujua uzito wa Wazee na Mwenyekiti
- Na kama alifanya akijua basi inawezekana alifanya hivyo kufikisha ujumbe
- Na kama alifanya bila kujua basi inawezekana hakijui vyema chama chake

Swali la kujiuliza ni: Je, Viongozi na Wazee wa Chama wanajua walitendalo?

Pengine kuna umuhimu pia wa kuwasamehe wale wote wasiojua walitendalo!
 
Jembe Ulaya,na wanachadema wenzako,kwa hakika sasa mmefikia mahali pabaya,chadema kama vyama vyote vya upinzani tanzania sio maarufu bila ya kuweposome figures amazo wananchi wanazikubali,,,kama mnafanya character assassination ya kumuuwa zitto ,kitila etc soon mtakosa mvuto wa kisiasa na mtakuwa chama dhaifu....chadema kigoma ilidhoofishwa sana na mbowe as ugomvi wake na kabouru ulipelekea hata alipoenda kigoma asipande kumnadi kwenye mkutano wa hadhara.matokeo yake jama akarudi ccm.zitto kajitoa sasa mnadai kuwa anatoa rushwa....chadema mnahitaji mabadiliko walau mpunguze ata idadi ya madereva wachaga makao makuu yenu.
 
Zitto hongera sana wanajamii na watanzania wapenda demokrasia tupo pamoja wameyakoroga na watayanywa.
 
hahahah! jamni nafikiri yule ndugu yetu hajafikia umri. Unakumbuka usemi wa Baba wa Taifa alivyomsikolifai mheshimiwa mwenye nchi ile 95, watu tumeshupaaa nae sasa angalia inavyoendelea. Kuna watu wanaona mbali jamani tuwape chances zao.

Nafikiri Mtei yuko sahihi, ZItto awe mpole
 
Jembe Ulaya,na wanachadema wenzako,kwa hakika sasa mmefikia mahali pabaya,chadema kama vyama vyote vya upinzani tanzania sio maarufu bila ya kuweposome figures amazo wananchi wanazikubali,,,kama mnafanya character assassination ya kumuuwa zitto ,kitila etc soon mtakosa mvuto wa kisiasa na mtakuwa chama dhaifu....chadema kigoma ilidhoofishwa sana na mbowe as ugomvi wake na kabouru ulipelekea hata alipoenda kigoma asipande kumnadi kwenye mkutano wa hadhara.matokeo yake jama akarudi ccm.


mbowe "hakumnadi" kaburu kwasababu kaburu aliamua kusafiri katikati ya kampeni kwenda afrika kusini wakati anajua ratiba ya mbowe kulitembelea jimbo lake. Alimwombea kura lakini presence ya kaburu haikuwepo kwenye jukwaa, kosa la nani? na hio ndio sababu kaburu ahamie ccm???

zitto kajitoa sasa mnadai kuwa anatoa rushwa

Wajumbe wa mkutano wamedai kuna rushwa imetolewa na kambi ya Kafulila nyumbani kwa Zito. Wewe unashauri vipi? Watangaze matokeo bila kufanyia uchunguzi tuhuma?


....chadema mnahitaji mabadiliko walau mpunguze ata idadi ya madereva wachaga makao makuu yenu.

Kwanza tungeanza na serikali kupunguza madereva ambao ni wachaga halafu ndio tuje chadema. tatizo la tanzania wewe hulioni unaliona ni tatizo la chadema tu?
 
Last edited:
Omary ni nini kimekusukuma na ukaamua kuanzisha "Thread" ya uchochezi kama hii ilhali kilichotokea BAVICHA jana kule Mbezi kinafahamika na wajumbe na wanachama wote ambao walikuwepo pale. Naona hii ni direct attack kwa Mbowe na Baraza la Wazee.

Naamini wewe ni Muumini wa Zitto na hili halijaanza leo. Lakini ukiwa kama MwanaChadema (Kama ni Mwanachama) ulikuwa na jukumu la kuhamasisha Mshikamano na Umoja katika Chama badala ya kwa makusudi kabisa katika hii habari yako kuzidi kutengeneza mgawanyiko katika Chama kwa kuwaelezea watu kama Wafuasi wa Mbowe na Wafuasi wa Zitto.

Na mbona matokeo ya Baraza la Wazee yalikuwa yameshatangazwa na sehemu pekee ambayo ilikuwa na walakini ni BAVICHA. Ama hizo taarifa nazo hukupewa? Kaka jaribu kuweka personal interest pembeni unapojaribu kumtumikia Boss wako kwa maslahi ya Wanachadema na Taifa kwa Ujumla.
 
Tatizo ni ukaskazini, na ninashangaa watanzania walio wengi hawaliangalii hili,lazima apatikane Mwenyekiti asiye na chembe ya ukabila, au anatoka kabila ambalo kubebana si jadi yao, MAMBO NI MENGI YA AJABU YANAONEKANA, kwa sababu tunataka chadema iwe ndo tumaini, hata tulioko nje tupigeni kelele kieleweke.
 
    • I thank Invisible for his update. It makes the point that Zitto was not forced to abandon his move. Advising him to remove himself from the contest was not undemocratic.
    • Chadema has been bruised in this saga. So has Zitto. Both can emerge with minor injuries, but they have given ammunition to many detractors.
    • Tribalists and their CCM manipulators are using this difficulty to claim that Chadema is a tribal party. That is not true. It was founded by a most distinguished Tanzanian (Edwin Mtei) who, through no fault of his, happens to be Mchaga. I hate to see well educated groups of Tanzanians, like the ones we have here, being so tribal in their outlook.
    • It is not a sin for the son in law of a leader to be a leader. Freeman Mbowe was elected Chadema leader. He was not simply given the chairmanship by Mzee Mtei. In fact, Mzee Mtei was succeeded by Bob Makani, and after Makani, Chadema elected Freeman. What is so sinister about that? Freeman’s association with the founder of Chadema may have helped him, but that there is nothing undemocratic about that.
    • Those who would like to see CCM continue to misrule Tanzania some more will do all they can to exploit this episode. They have already began to try to dismantle the support that those who aim for change give to Chadema her at JF. Their argument that what transpired in Chadema was undemocratic has run out of steam, so they have now reverted to naked tribalism.
    • Change must come to Tanzania. As Obama puts it, we cannot continue to do the same things over and over again and expect a different result. We cannot afford to re-elect CCM. We must build up the opposition, and it seems to me, Chadema is the focal point of that.
We uchagga umekujaa mpaka umekuwa lijinga.
 
Omary ni nini kimekusukuma na ukaamua kuanzisha "Thread" ya uchochezi kama hii ilhali kilichotokea BAVICHA jana kule Mbezi kinafahamika na wajumbe na wanachama wote ambao walikuwepo pale. Naona hii ni direct attack kwa Mbowe na Baraza la Wazee.

Naamini wewe ni Muumini wa Zitto na hili halijaanza leo. Lakini ukiwa kama MwanaChadema (Kama ni Mwanachama) ulikuwa na jukumu la kuhamasisha Mshikamano na Umoja katika Chama badala ya kwa makusudi kabisa katika hii habari yako kuzidi kutengeneza mgawanyiko katika Chama kwa kuwaelezea watu kama Wafuasi wa Mbowe na Wafuasi wa Zitto.

Na mbona matokeo ya Baraza la Wazee yalikuwa yameshatangazwa na sehemu pekee ambayo ilikuwa na walakini ni BAVICHA. Ama hizo taarifa nazo hukupewa? Kaka jaribu kuweka personal interest pembeni unapojaribu kumtumikia Boss wako kwa maslahi ya Wanachadema na Taifa kwa Ujumla.

Poti Lusajo..vipi na wewe umepewa mke kule?
 
Zitto,
Umemjeruhi sana Mh Mbowe na Mzee Mtei. Hata kama umeondoa jina kwenye kugombea usidhani utafanya kazi naye kwa kuaminiana, kuelewana na kuheshimiana kama ilivyokuwa kabla haujachukua fomu na kuijaza kwa nia ya kutaka kugombea nafasi hii.
Binafsi ningekushauri upumzike SIASA kwa sasa. Utakaporudi, uje na msimamo usioyumba kwa mambo muhimu kama haya. JK alikatishwa tamaa sana kugombea Uraisi wa Nchi hii tangu 1995. Hakuyumba.
Kwa sasa kaa mbali kidogo na vyombo vya habari.
 
Kibanda na Ngurumo wamejadili hoja kwa kupitia matukio ya Zitto, Mbowe na CHADEMA.
Endeleza mkondo huo wa fikra na mtindo ya kujadili hoja;si watu na ushabiki.
Wakhtanabahu,
 
Rafiki yangu hiyo ndio inaitwa SIASA. Ukishaingia huko uwe tayari na mambo kama haya. Haya yanatokea hata huko CCM, walivyomwambia John Cigwiyemisi ajitoe haikuwa kwenye kikao, bali aliitwa na kushurutizwa kuchomoa fomu yake.

Nadhani Zito ameshayaona mengi kwenye siasa (hasa uozo ndani ya ChaDeMa) lakini njia anayotaka kukimbilia kuyatatua anafanya haraka. Atafute political analysts wamsaidie. You cant fight alone, you need commandas, battalion, section, volunteers etc. He should be strategic rather than opportunist.
 
Mkuu Kanda2 mbona hii makala ipo tayari hapa, kulikuwa na sababu ya kuipost upya mkuu? ipo kwenye thread ya Invisible tayari kuhusu chadema na Zitto
 
CHADEMA bwana! mara hii Zitto keshakuwa mtoa rushwa? Kweli hii Tanzania mtu mdogo hutakiwi kugusa maslahi ya wakubwa.

ZITTO umeambiwa ni fisadi, njoo CCM kwenye chama cha mafisadi uje ule kuku zako. Siasa za Kaskazini mtu wa bara huko Kigoma utaziweza? Mwishowe watakuambia wewe ni Mkongo.
 
Katika hali ya mshangao na kuonyesha kuchanganyikiwa kuna taarifa zinazosema kuwa baadhi ya viongozi wa CHADEMA wameshinikiza kughairishwa kutangazwa matokeo ya uchaguzi ya Baraza la Vijana na Baraza la wazee ambayo yanaonyesha ushindi mkubwa wa wanachama ambao wanaaminiwa kuwa ni wafuasi wa Zitto Kabwe.

Wakati katika uchaguzi wa Baraza la Vijana unaonyesha kuwa Kafulila ambaye ni msaidizi wa Zitto ambaye amekuwa akimtayarisha kugombea ubunge Kigoma Kusini (sio kigoma kaskazini kwa Zitto) amemshinda kwa kura zilizojitosheleza ndugu Henche ambaye ni chaguo la wafuasi wa Mbowe ambao jana baada ya kumlazimu Zitto kujito walihamishia nguvu zao zote dhidi ya wagombea wanaomuunga mkono Zitto.

Katika matokeo ya uchaguzi wa Baraza la Wazee yanaonyesha kuwa bwana Shilungeshela ambaye pia anasemekana ni mfuasi wa Zitto na ambaye jana usiku Zitto alikuwa akitpita kumuombea kura naye pia ameshinda kwa kura nyingi.

Ukweli ni kuwa haya yanaweza kuwa makosa makubwa zaidi kwa upande wa wafuasi wa Mbowe kwani nahofia nguvu hizi za ushindi wa waliokuwa wakimuunga mkono Zitto zikageuka kuwa kura ya HAPANA kwake na kujikuta akikosa kabisa uhalali wa kiuongozi. Hali ambayo jana usiku Zitto alikuwa akijaribu kuizuia kwa kuhofia kuumiza maslahi ya chama chao.

Cha ajabu na kinachoonyesha kupanick ni kuwa wasimamizi wa chaguzi zote mbili wamezuiwa hata kutangaza matokeo kama zilivyo taratibu....Inaelekea siasa za CCM zimeathiri sana psych ya watanzania.....

Ama kweli hawa jamaa wanajua kukabaka kademokrasia ketu....Mwataka tuende wapi....NYUMBANI kumeota magugu na kumejaa many'agau...

omarilyas

Yangu Macho, inawezekana Kibanda yuko sahihi, na Ngurumo je? anyway maswali magumu mara nyingi majibu yake ni Muda tu. Tutasikia mengi mwaka huu. Ni mwaka ambao Kondoo watajipambanua na Mbwa Mwitu hali kadhalika.
 
CHADEMA bwana! mara hii Zitto keshakuwa mtoa rushwa? Kweli hii Tanzania mtu mdogo hutakiwi kugusa maslahi ya wakubwa.

ZITTO umeambiwa ni fisadi, njoo CCM kwenye chama cha mafisadi uje ule kuku zako. Siasa za Kaskazini mtu wa bara huko Kigoma utaziweza? Mwishowe watakuambia wewe ni Mkongo.

Tukiwa na Wahandisi wa Fikra Ndogo kama zako Basi hatutaweza kujenga hata visima.

Wakaskazini wanakutisha sana ee, Usiwaogope ndugu yangu, they are just aggressive na si kingine
 
Jembe Ulaya,na wanachadema wenzako,kwa hakika sasa mmefikia mahali pabaya,chadema kama vyama vyote vya upinzani tanzania sio maarufu bila ya kuweposome figures amazo wananchi wanazikubali,,,kama mnafanya character assassination ya kumuuwa zitto ,kitila etc soon mtakosa mvuto wa kisiasa na mtakuwa chama dhaifu....chadema kigoma ilidhoofishwa sana na mbowe as ugomvi wake na kabouru ulipelekea hata alipoenda kigoma asipande kumnadi kwenye mkutano wa hadhara.matokeo yake jama akarudi ccm.zitto kajitoa sasa mnadai kuwa anatoa rushwa....chadema mnahitaji mabadiliko walau mpunguze ata idadi ya madereva wachaga makao makuu yenu.

Umejuaje kama ni Wachagga, Unajua mtu mzima na Familia yako unapokuwa Mbeya ni jambo la aibu hata kwako mwenyewe.

Wachagga ni NOMA, kila sehemu wapo, na watu wanawahara si mchezo
 
Kakwangu ni kajiswali kwa Dr. Hosea,Boss wa TAKAKURU:Kwa kuwa CHADEMA ni Taasisi ya Kitaifa,na kwa kuwa sio siri tena chaguzi nyingi nchini mwetu zinahusishwa na rushwa,je ni jitihada gani ofisi yako ilifanya/inafanya ili kudhibiti vitendo vya rushwa au vinavyoashiria rushwa katika uchaguzi unaoendelea CHADEMA?Nauliza hivi kwa sababu Taasisi yako ndio inatakiwa iwe msemakweli katika masuala nyeti kama haya kwani bila ya hivyo Watanzania tutakuja kutoana ngeu kwa tuhuma ambazo hazina ushahidi wa kitaalam kama ule ambao Taasisi yako imekuwa equiped na pesa za walipa kodi kuutafuta.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom