Mkuu Invisible, nimeshasema hapo juu kuwa kama Mheshimiwa hajapiga ulabu (mvinyo) kabla ya kuandika post hiyo, basi something wrong somewhere. Acha Mkandara achukie kiasi hicho! na sidhani kuwa ni yeye tuu, wako wengi ambao ni kama wamepigwa ngumi ya utosi ghafla na kuona kiza kimetanda mchana kweupeKwangu network imekatika katika ubongo... Sielewi nini kinaendelea mkuu Mkandara!
This is part of spinning. Uwongo, uzushi nk. Tatizo wanaopanga haya wanasahau kuwa tuliyapanga wote dhidi ya marehemu Chacha Wangwe. Unatengeneza uwongo, unausambaza, na hatimaye wewe mwenyewe unauamini kuwa ni kweli.
Kama kuna kitu kilimuuma marehemu wangwe na alikufa nacho ni kile cha kumsema kuwa alikuwa anatumiwa na mafisadi. Namshukuru Mungu kuwa nilimwomba radhi Chacha kabla na baada ya kifo chake siku ya postmorterm kwa kumzushia uwongo.
Asha ni mmoja wa wenzangu tulioshiriki kumtenda Chacha. Wanatumia mtindo ule ule na wanapita njia zile zile. Rashidi wa Kuli alisema, YANA MWISHO HAYA!
Asha, (ninakujua wewe ni nani) kuwa mkweli wa nafsi yako! Utalipwa hapa hapa duniani kwa uzushi wako na wenzako.
To put record clear - Kasisiko sio ndugu yangu wa damu. Ni mwenyekiti wangu tu wa Mkoa Kigoma. Pili, Baregu hajahudhuria kikao hata kimoja cha wazee toka ajue ukweli wa mambo.
Tatu, chama jana kimechagua rasmi Baraza la Wazee na mgombea aliyekuwa ananiunga mkono waziwazi ameshinda. Inakuwaje bado vikao vya wazee vya chama vinaendeshwa na Mtei na Ndesamburo?
Pili, vyombo vyote vya habari vilikuwapo katika hotuba ya Mtei. Imekuwaje NIPASHE peke yake ndio ione alisema kuna ufisadi kwenye chaguzi za chama? Mhariri mtendaji wa Nipashe ni jesse kwayu kutoka Machame. Mmiliki wa Nipashe ni Reginald Mengi kutoka Machame.
Spinns sio sustainable. Acheni tujenge chama chetu.
Nina mashaka kama Post hii kaandika Zitto mwenyewe ninayemfahamu. Nahisi kuna mtu ana Password yake ndio kaweka haya maneno hapa.
Ila kama niyeye mwenyewe na hajapiga mvinyo (NAJUA HUU NI MWEZI MTUKUFU) basi something wrong somewhere.
Wakina Zitto Mnatutia aibu kubwa sana, Sikidhani kama watu kama nyinyi mtafanya mambo ya ajabu sana katika kipindi kama hiki. Jaribuni kuwa makini na mambo haya kuyamaliza ndani na sio kama mnavyofanya. Tunahuzuni kubwa sananiliombwa kujitoa na nikajitoa kama ilivyotangazwa.
Asha ni mmoja wa wenzangu tulioshiriki kumtenda Chacha. Wanatumia mtindo ule ule na wanapita njia zile zile. Rashidi wa Kuli alisema, YANA MWISHO HAYA!
Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa. Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG
Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!
Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.
wachaga ni kansa inayotafuna hii nchi taratibu.Zitto kabwe kajaribu kuwa tiba ya hii kansa lakini wamemzuia.nasikitika CHADEMA kina wapenzi na mashabiki wengi bila hao mashabiki kujua nini dhamira ya waasisi wa chama hiki,Zitto kabwe anajua ndio maana akajaribu kuweka ushindani lakini wasiojua na wenye agenda zao wamemzuia
Mkuu Zitto, hakika hii inakuondolea sifa ya Kugombea Uenyekiti automatic yaani hufai!..maelezo yako ni dhahiri yanaonyesha wazi huna Hekima wala Busara kuongoza chama, kifupi hujakomaa kisiasa kabisaaa. Una papara, mwenye hasira na mwepesi kuropoka..Mkuu hukutakiwa kabisa kubwabwaja ovyo hapa kijiweni maneno haya kwani yanazidi kukufunga wewe ikiwa umeshakubali kujitoa ktk kugombea.
Maneno haya yalitakiwa kutangulia na hasa siku ya kikao cha chama. Na nakuomba sana ktk mkutano mkuu wa chama hii September, zungumza yote yaliyoko moyoni mwako, kuwa muwazi, mkweli na bayana tuhoji utendaji kazi wa hao wazee ama watu ambao unawafahamu kuhusika na mbinu hizi chafu za kupakaza.
Kulitumia jina la wangwe na uchafu wote mlofanya dhidi yake hakika umenichefua kichizi yaani kumbe kweli Zitto mlimfanyia Wangwe roho mbaya makusudi?..Hukuona ubaya wa kutenda ulotenda Ukajisafisha hadharani hadi siku ambayo umetendewa wewe ndipo unakuja na habari hizi za Wangwe tena ktk gazeti!..
Well itakuwa vizuri ukimalizia kabisa kutufahamisha maanake hakuna kitu ambacho sisi wananchi tunataka kuelewa zaidi ya Kifo CHA WANGWE kama kuna mkono wa mtu..Ikiwa wewe mkweli na unataka tukuamini basi tueleze yote mlomtendea Marehemu Wangwe ambayo wewe mwenyewe unakiri na ulikwenda simama mbele ya maiti na Kutubu..What real happen? wewe mwenyewe pamoja na Bi Asha ,mlifanya nini au mlicheza part gani mkuu come clean leo hii hapa hapa JF.
Duh, ama kweli mkuu wangu najua ulikuwa na haki ya kugombea kiti hicho lakini leo hii na maelezo haya yaonyesha wazi kwamba hufai kabisa... Na wala usije fikiria kuwa Wangwe alikuwa mtu mzuri vile vile..ila kwa walalahoi wasojua kwamba a sneetch ni Liability ktk taasisi yoyote na hafai kabisa..isipokuwa kwetu sisi Ndivyo Tulivyo (Watumwa wa akili), kumbe ktk jumuiya kama zetu nchi za nje watu hawa hamalizwa vibaya vibaya na hawapokelewi mahala popote.
Kifupi Zitto hakuna sifa hata kidogo unapokipaka chama chako na sidhani hata ukiondoka ama kwenda chama chochote utapokelewa kwa mikono miwili, laa utatumiwa tu na hakuna mtu wala chama kitakachokuamini. Watu kama Wangwe na wewe ni wa kuogopwa na kukaliwa mbali sana na sii kwa sababu unasema ukweli wako ila Mropokaji ni Liabiility ktk chama..Usifikirie unajenga mkuu wangu yaani duh! ama kweli Umri ni moja ya kigezo kikubwa sana ktk CV ya mtu..
Wakina Zitto Mnatutia aibu kubwa sana, Sikidhani kama watu kama nyinyi mtafanya mambo ya ajabu sana katika kipindi kama hiki. Jaribuni kuwa makini na mambo haya kuyamaliza ndani na sio kama mnavyofanya. Tunahuzuni kubwa sana
Hakuna napingana na wewe.
Sauli leo paulo alitubu na akawa kiongozi mzuri,mtu anayetenda mabaya na kuja kuyakiri huyu twamhitaji.
Hii move ni sahihi kabisa kwa Zitto hatujui watakuja kufanya nini na plan C baad ya plan B.
Si sahihi kwa zitto kukaa kimya saizi kama anaona dalili za kumwoondoa kutokuwa mwenyekiti bado kuna harakati za kwenda mbali zaidi.
Wewe Mkandara kaa kimya muonja, asali haonji mara moja hujikita na kuchonga mzinga.
Pole sana ndugu yangu. Naelewa feelings zako na za wengine humu ndani. Ninawahakikishia kuwa tutainuka, tutajipakusa vumbi na kukimbia tena pamoja. Mchakato huu waweza kuwa na matokeo ya kukikuza na kukikomaza chama sana. Tunajifunza katika changamoto hizi. Hatuwezi kukubali kuingia katika historia ya kuua CHADEMA. Kuna masuala fulani fulani ya msingi kabisa kuhusu mahusiano yetu na marafiki zetu ambayo lazima tuyashughulikie asap.
Deep in my heart i believe truth will prevail and the party will come up strong.
Hivi ukiwa kama Kiongozi Mkuu kwenye Ukatibu Mkuu Makamu hivi huoni kuwa umeingilia huo uchaguzi kwa kusema wewe mwenyewe kuwa ulifanya kampeni wazi wazi kwa vijana hawa wadogo huoni kuwa ukutenda kosa??
Hivi mtu ukishakuwa naibu katibu mkuu unakosa haki ya kumpigia kampeni mgombea unayemwamini hata kama umejivua majukumu yote ya kusimamia uchaguzi? Hivi hawa vijana wadogo kwa Zitto mwenye umri wa miaka 33 ni wapi hao? Kama Zitto alijitoa katika shughuli za kusimamia uchaguzi na yeye ni mjumbe wa mkutano wa vijana ni wapi amekosea? Na kati ya Zitto na ninyi ni kina nani ambao wamo katika timu ya kusimamia uchaguzi lakini pia wanakuwa mbele kupiga kampeni chafu dhidi ya Zitto na sasa mmekimbilia kwa watu wanaomuunga mkono?
Kwa taarifa yenu Zitto hakuwa na nia ya kufanya kampeni zaidi yakumsaidia kimawazo Kafulila hadi mlipojikusanya wote na baadhi yenu mkiwa wasimamizi wa uchaguzi kuenda kuanza kumfanyia kampeni mtu "wenu" eti kumuonyesha siasa Zitto. Hapo ndipo mlipo likoroga. Zitto alishakuwa tayari kujishusha na kum-approach Mbowe for genuine reconciliation lakini kwa utoto wenu mkajiona kuwa mmemshinda na mtaweza "kummaliza". That wa a big mistake kwenu lakini pia kwa maslahi ya chama chenu.
Mh Zitto! kwenye kipindi kama hiki kizito kwa chama kwanini usiwe na moyo kama wa mwenyekiti wako Mbowe ukakaa kimya kwa masrahi ya chama kwanza, unapoanza kusema mambo ya Fedha (CAG) huoni kuwa hapo kuna mushkeli,
Hivi Mbowe amekaa kimya? Yaani mtu anayeongea nyumba ya pazia ndio amekaa kimya na huyu anayeongea bila ya kujificha ndiye amekuwa mbaya. Tatizo vijana mnakurupukia profession za watu. Unaibuka huko ulipo unajidanganya kuwa unajua spining bia ya kutambua uwezo na uthubutu wa unayemfanyia spining katika kujibu mashambulizi. Ulitaka uj umwage sumu yako halafu Zitto anyamaze afe kisabuni? Tena hapa Zitto amejicontroal sana maana ninyi ndio mnaojua ni nani na kutoka upande gani wamekuwa wakitumia rushwa katika uchaguzi huu.
Pia kuja hapa kwenye JF forum kumwaga razi lote hilo ambalo kuna utitiri wa wanaCCM kibao, huoni kuwa unavujisha siri??
Siri, yaleyale wtu wanatoka ndani ya CCM kushutumu ufisadi kina Makamba wanasema washugulikiwa kwa kuvuja siri za chama. Uozo na uvundo hauwezi kuwa siri na kuuficha ni kuwalaghai watanzania.
Mimi sina chama ila picha unayoonyesha ni ile ya mapindikizi ya CCM tuliyozoea kuona!!!
Yale yale, wanatokea watu wanawaeleza uovu wa MASIHA FEKI wenu wanaonuka ufisadi na kujidai kuwa wanapiga vita ufisadi huohuo, mnakimbilia kusema kuwa wanaosema uchafu wao watakuwa wametumwa na mafisadi. Hivyo hivyo ndani ya chama chenu mnapofanya mambo ya maovu yaliyopita kiwango cha uvumilivu wakitokea wenzenu kuyasema mabaya hayo mnakimbilia kutafuta mchawi nje ya nyumba...Hapa CCM msiwahusishe kwani ni wenyewe mmeamua kujigeuza asusa yao.
Kubalini makosa yenu, jifunzeni kujisahihisha halafu muanze upya na sio kutaka kushambulia mliowkosea ili kuhalalisha makosa mliyoyafanya na mnaendelea kuyafanya kama spining hii mliyoleta hapa
omarilyas
Ndugu zangu,
Katika kipindi hiki sikutaka kabisa kuingia na kujibu hoja yeyote ndani ya JF kuhusiana na uchaguzi wa vijana Taifa. Hata hivyo mtaniwia radhi kujibu hili ili kuweka rekodi sahihi kutokana na upotoshaji ambao unafanyika kwa makusudi kabisa ili kushusha heshima yangu katika jamii.
Moja, mimi ni mumbe wa Baraza la Vijana la CHADEMA kwa nafasi yangu ya kuwa mjumbe wa Kamati Kuu wa kuchaguliwa kuwakilisha vijana na nikiwa Mbunge mwenye umri wa ujana (miaka 33). Hivyo kushiriki kwangu kwenye vikao ni jambo la kawaida kabisa kwani nina haki ya kupiga kura. Vile vile nina haki ya kuamua mgombea gani wa kumuunga mkono katika uchaguzi. Niseme waziwazi kuwa David Kafulila ndiye mgombea niliyemwunga mkono na kumfanyia kampeni waziwazi bila kificho chochote kile. Hii inatokana na tabia yangu ya kutokuwa mnafiki. Nilimwunga mkono David Kafulila na alishinda kwa kupata kura 99 dhidi ya kura 73 ambazo alipata mgombea mwingine John Heche ambaye alikuwa anaungwa mono na kundi lililonipinga kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.
Huyu aliyeandika post hii ni mmoja wa vijana wa makao makuu ya CHADEMA ambaye amekuwa akinipinga siku zote kwa chuki tu ya kuwa mimi nimepaata umaarufu wa kisiasa kuliko yeye na kundi lake.
Mama yangu mzazi ni mwanachadema. Ni kiongozi mwandamizi wa CHADEMA kutoka mkoa wa Kigoma na amekuwa msaada mkubwa wa chama katika Manispaa ya Kigoma. Ninaomba sana masuala yangu ya kisiasa na mahasimu wangu wasimhusishe mama yangu mzazi. Ninaomba sana sana mumuweke mama yangu pembeni. Mwandishi wa post hii tafadhali naomba usimhusishe mama yangu na tofauti zetu za kisiasa. Ninaomba sana hili liheshimiwe.
Pili, ni dhahiri kulikuwa kuna makundi katika uchaguzi wa BAVICHA. Mimi niliweka wazi msimamo wangu wa kumwunga mkono kafulila. Wakurugenzi wa Makao makuu ya chama kuanzia Katibu Mkuu mpaka wakurugenzi kama John Mnyika, John Mrema na hata maafisa kama Halima Mdee walikuwa wanampinga David Kafulila. Hawa wanaogopa uwezo wa Kafulila wa kukataa kutumika na kuwa independent katika maamuzi yake.
Hii sio mara ya kwanza kwa Kafulila kuzuiwa haki yake. Kijana huyu alipitishwa kugombea Ukurugenzi wa vijana na jina lake kwenda katika Kamati Kuu. Ajenda ya uteuzi wake ikasitishwa baada ya kuhofia kuwa atashinda. Mtindo huo huo wameutumia sasa kufuta uchaguzi na kuupeleka mbele mpaka baada ya miezi 6. Mimi nimekataa
1. Uchaguzi umefanyika.
2. Matokeo hayakutangazwa
3. Hakuna aliyekata rufaa
Hivyo, wazee wanapata wapi 'locus' ya kufuta uchaguzi?
Hata hivyo wenye mamlaka ya kufuta uchaguzi ni Kamati Kuu ya chama maana kuna taratibu za rufaa ndani ya chama chetu. Nimetaka Kamati Kuu iitishwe ili taratibu zifuatwe.
Huyu mtu aliyeleta post hii hapa anataka kuspin ili kupinda ukweli bila aibu.
David Kafulila kashinda round ya kwanza zaidi ya 50%. Wamekataa kutangaza matokeo na kuleta fujo kwenye mkutano.
Kuna tuhuma dhidi yangu kuwa nimetoa rushwa. Huku ni kutapatapa kwani tuhuma hizi zinatolewa bila ushahidi. Hivi huyu mwandishi na akili zake timamu anaweza kuweka akilini kwake kuwa mimi naweza kutoa rushwa hadharani? Eti nimevuta kiti na kuita watu kutoa rushwa. Bila adabu anamhusisha mama yangu mzazi.
Mama yangu ana maamuzi yake binafsi na mfano dhahiri ni uchaguzi wa chaha wangwe ambapo mimi nilimwunga mkono arfi na yeye akamwunga mkono Chacha wangwe waziwazi na bila kificho.
Uchaguzi wa vijana haukua na rushwa. Uchaguzi wa vijana wa chadema umefanyika kwa amani kabisa na matokeo hayakutangazwa kwa kuwa mgombea 'wao' hakushinda.
Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa. Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG
Katika spirit ya umoja na mshikamano wa chama tutamaliza suala hili katika Kamati Kuu ya chama.
Ninaomba sana vijana wa Makao Makuu - hasa Mrema, Mnyika na wengineo waache spinning za kipumbavu ambazo hazijengi umoja na mshikamano wa chama. Waache kuchafua jina langu. Wakumbuke kuwa kuna maisha mbele yetu na kuna kazi ya kujenga chama chetu.
Vijana hawa wakumbuke kuwa majungu hulipwa hapa hapa duniani. Wasubiri nao watakuwa wabunge na watapata ajenda zao za kuwafanya kuwa maarufu.
Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!
Haya ambayo nimeyaandika hapa JF nimewaambia vijana hawa 'face to face' ili waache uwongo, uzandiki, majungu, fitna na chuki.
Kafulila kashinda uenyekiti wa vijana. Mpeni ushindi wake. Msibake demokrosia.
Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.