Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
CHADEMA tudhihirishieni kama nyie sio chama cha kaskazini mbona mna woga kiasi hicho,eti mpaka kwenye press conference ndo suluhu au ukuu wa chama ni wa watu flaflani..,sikutegemea.....MNATUPA WASIWASI VIPI MKITWAA NCHI???? JIREKEBISHENI TUWAAMINI TENA
 
Invisible,
Mkuu wangu yaani wee niache tu..sina pumzi hapa nilipo..
 
Emotional Intelligence is lacking in some person that's why all this happen.
 
Kwangu network imekatika katika ubongo... Sielewi nini kinaendelea mkuu Mkandara!
Mkuu Invisible, nimeshasema hapo juu kuwa kama Mheshimiwa hajapiga ulabu (mvinyo) kabla ya kuandika post hiyo, basi something wrong somewhere. Acha Mkandara achukie kiasi hicho! na sidhani kuwa ni yeye tuu, wako wengi ambao ni kama wamepigwa ngumi ya utosi ghafla na kuona kiza kimetanda mchana kweupe
 
This is part of spinning. Uwongo, uzushi nk. Tatizo wanaopanga haya wanasahau kuwa tuliyapanga wote dhidi ya marehemu Chacha Wangwe. Unatengeneza uwongo, unausambaza, na hatimaye wewe mwenyewe unauamini kuwa ni kweli.

Kama kuna kitu kilimuuma marehemu wangwe na alikufa nacho ni kile cha kumsema kuwa alikuwa anatumiwa na mafisadi. Namshukuru Mungu kuwa nilimwomba radhi Chacha kabla na baada ya kifo chake siku ya postmorterm kwa kumzushia uwongo.

Asha ni mmoja wa wenzangu tulioshiriki kumtenda Chacha. Wanatumia mtindo ule ule na wanapita njia zile zile. Rashidi wa Kuli alisema, YANA MWISHO HAYA!

Asha, (ninakujua wewe ni nani) kuwa mkweli wa nafsi yako! Utalipwa hapa hapa duniani kwa uzushi wako na wenzako.

To put record clear - Kasisiko sio ndugu yangu wa damu. Ni mwenyekiti wangu tu wa Mkoa Kigoma. Pili, Baregu hajahudhuria kikao hata kimoja cha wazee toka ajue ukweli wa mambo.
Tatu, chama jana kimechagua rasmi Baraza la Wazee na mgombea aliyekuwa ananiunga mkono waziwazi ameshinda. Inakuwaje bado vikao vya wazee vya chama vinaendeshwa na Mtei na Ndesamburo?

Pili, vyombo vyote vya habari vilikuwapo katika hotuba ya Mtei. Imekuwaje NIPASHE peke yake ndio ione alisema kuna ufisadi kwenye chaguzi za chama? Mhariri mtendaji wa Nipashe ni jesse kwayu kutoka Machame. Mmiliki wa Nipashe ni Reginald Mengi kutoka Machame.

Spinns sio sustainable. Acheni tujenge chama chetu.


Kwa maneno haya Zitto unakiri kwamba CHADEMA in ukabila ndo kisa cha kukutosa?? Naomba ufafanuzi hapa tafadhali mimi kama mwanachama.
 
Nina mashaka kama Post hii kaandika Zitto mwenyewe ninayemfahamu. Nahisi kuna mtu ana Password yake ndio kaweka haya maneno hapa.
Ila kama niyeye mwenyewe na hajapiga mvinyo (NAJUA HUU NI MWEZI MTUKUFU) basi something wrong somewhere.

Kaamuwa kutubu mbele ya wananchi ,sasa mnachoshangaa ni nini.

Mtikila alitwaambieni ukweli lakini kwa ugumu wa nyoyo zetu tukamuona hafai tukamponda na mawe kama Yesu vile.

Hakika hakuna jiwe lilo fanya uovu juu ya marehemu litabaki bila kupinduliwa,tuliwaambia tangu mwanzo mkatuona sie wahuni ,tumetumwa lakini ukweli unabaki palepale hakika damu ya maremu inawalilia.

Zitto kaamuwa kutubu kwa nini munamwandama ,mwacheni aseme anayoyajuwa kama kweli mwatafuta demokrasia ama damu za watu.
 
niliombwa kujitoa na nikajitoa kama ilivyotangazwa.
Wakina Zitto Mnatutia aibu kubwa sana, Sikidhani kama watu kama nyinyi mtafanya mambo ya ajabu sana katika kipindi kama hiki. Jaribuni kuwa makini na mambo haya kuyamaliza ndani na sio kama mnavyofanya. Tunahuzuni kubwa sana
 
Mimi bado naomba Zitto tafadhali nijibu thread yango hapo juu ili nirudishe kadi, kwani CHADEMA siyo mama yangu.
 
Nawashangaa sana CHADEMA kwa uamuzi wa kumuondoa Zito kwenye ugombea na kumuacha Mbowe kama mgombea pekee. Nina maswali mengi:
1. Hivi wao hawataki kiongozi bora?
2. Kama wangegombea Zito na Mbowe, nadhani yule aliye bora kati yao ndiye angechaguliwa. Au labda wenzangu hawa wasingefanya hivyo?
3. Na kama kati ya Zito na Mbowe kuna mmojawao ambaye ndiye angependwa na wengi hivyo kuibuka mshindi, wanaona shida gani kupata kiongozi kwa mtindo huo, yaani yule aliyekubalika kwa wengi katika kura?
4.Na maswali mengine mengi tu, naona hii CHADEMA sasa sijui imefuliaaa?
 
Asha ni mmoja wa wenzangu tulioshiriki kumtenda Chacha. Wanatumia mtindo ule ule na wanapita njia zile zile. Rashidi wa Kuli alisema, YANA MWISHO HAYA!

Zitto,

Can you please "Put the records clear" on the paragraph above?
 
Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa. Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG

Duh, Zitto haya ungemezea ingekuwa powa sana. Anyway akina Makamba ndo usiseme. Hapa wakulaumiwa ni wewe na Slaa kama sikosei. Anyway sijui katiba yenu inasemaje ila simply kuna UFISADI CHADEMA. Kesho magazetini watakunukuu.

Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!

Eehh, Malizeni halafu Zitto usisahau kuangalia pia friends and advisors wako. at this stage you should have advisors in sectorial. Your future is bright and people especially your friends wanakutumia kama ngazi. si kwa matakwa yao ila kwa priorities zao. Review wote ikiwezekana piga wote chini. Katika kipindi cha miaka mitatu hii wakubomoa ila naamini umejijenga wewe binafsi. cheki ishu ya DOWANS, kugombea tena ubunge, afrika mashariki na sasa uenyekiti. People have these in their mind. they will judge you.....Hizi siasa za upepo ni kwasababu tu watu wamechoka ila zikija siasa za kimarekani utakuwa kama vumbie, waaa haupo.

Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.

Mimi binafsi nakuelewa but tusifikishane kutoelewana.
 
wachaga ni kansa inayotafuna hii nchi taratibu.Zitto kabwe kajaribu kuwa tiba ya hii kansa lakini wamemzuia.nasikitika CHADEMA kina wapenzi na mashabiki wengi bila hao mashabiki kujua nini dhamira ya waasisi wa chama hiki,Zitto kabwe anajua ndio maana akajaribu kuweka ushindani lakini wasiojua na wenye agenda zao wamemzuia

Wewe kwa nini unaropoka tu bila kufanya utafiti,inamaana baraza zima la wazee ni wachaga na viongozi wengine waliopo kwenye uongozi chadema ni wachaga.Huu ni upotoshwaji tuu na sio bure umepewa hela na mafisadi ili uchafue hewa hapa jamvini.Kama huna ka kusema si ukae kimya uache wenye data wazungumze.
 
Mkuu Zitto, hakika hii inakuondolea sifa ya Kugombea Uenyekiti automatic yaani hufai!..maelezo yako ni dhahiri yanaonyesha wazi huna Hekima wala Busara kuongoza chama, kifupi hujakomaa kisiasa kabisaaa. Una papara, mwenye hasira na mwepesi kuropoka..Mkuu hukutakiwa kabisa kubwabwaja ovyo hapa kijiweni maneno haya kwani yanazidi kukufunga wewe ikiwa umeshakubali kujitoa ktk kugombea.

Maneno haya yalitakiwa kutangulia na hasa siku ya kikao cha chama. Na nakuomba sana ktk mkutano mkuu wa chama hii September, zungumza yote yaliyoko moyoni mwako, kuwa muwazi, mkweli na bayana tuhoji utendaji kazi wa hao wazee ama watu ambao unawafahamu kuhusika na mbinu hizi chafu za kupakaza.

Kulitumia jina la wangwe na uchafu wote mlofanya dhidi yake hakika umenichefua kichizi yaani kumbe kweli Zitto mlimfanyia Wangwe roho mbaya makusudi?..Hukuona ubaya wa kutenda ulotenda Ukajisafisha hadharani hadi siku ambayo umetendewa wewe ndipo unakuja na habari hizi za Wangwe tena ktk gazeti!..

Well itakuwa vizuri ukimalizia kabisa kutufahamisha maanake hakuna kitu ambacho sisi wananchi tunataka kuelewa zaidi ya Kifo CHA WANGWE kama kuna mkono wa mtu..Ikiwa wewe mkweli na unataka tukuamini basi tueleze yote mlomtendea Marehemu Wangwe ambayo wewe mwenyewe unakiri na ulikwenda simama mbele ya maiti na Kutubu..What real happen? wewe mwenyewe pamoja na Bi Asha ,mlifanya nini au mlicheza part gani mkuu come clean leo hii hapa hapa JF.

Duh, ama kweli mkuu wangu najua ulikuwa na haki ya kugombea kiti hicho lakini leo hii na maelezo haya yaonyesha wazi kwamba hufai kabisa... Na wala usije fikiria kuwa Wangwe alikuwa mtu mzuri vile vile..ila kwa walalahoi wasojua kwamba a sneetch ni Liability ktk taasisi yoyote na hafai kabisa..isipokuwa kwetu sisi Ndivyo Tulivyo (Watumwa wa akili), kumbe ktk jumuiya kama zetu nchi za nje watu hawa hamalizwa vibaya vibaya na hawapokelewi mahala popote.

Kifupi Zitto hakuna sifa hata kidogo unapokipaka chama chako na sidhani hata ukiondoka ama kwenda chama chochote utapokelewa kwa mikono miwili, laa utatumiwa tu na hakuna mtu wala chama kitakachokuamini. Watu kama Wangwe na wewe ni wa kuogopwa na kukaliwa mbali sana na sii kwa sababu unasema ukweli wako ila Mropokaji ni Liabiility ktk chama..Usifikirie unajenga mkuu wangu yaani duh! ama kweli Umri ni moja ya kigezo kikubwa sana ktk CV ya mtu..

Hakuna napingana na wewe.
Sauli leo paulo alitubu na akawa kiongozi mzuri,mtu anayetenda mabaya na kuja kuyakiri huyu twamhitaji.

Hii move ni sahihi kabisa kwa Zitto hatujui watakuja kufanya nini na plan C baad ya plan B.

Si sahihi kwa zitto kukaa kimya saizi kama anaona dalili za kumwoondoa kutokuwa mwenyekiti bado kuna harakati za kwenda mbali zaidi.

Wewe Mkandara kaa kimya muonja, asali haonji mara moja hujikita na kuchonga mzinga.
 
Wakina Zitto Mnatutia aibu kubwa sana, Sikidhani kama watu kama nyinyi mtafanya mambo ya ajabu sana katika kipindi kama hiki. Jaribuni kuwa makini na mambo haya kuyamaliza ndani na sio kama mnavyofanya. Tunahuzuni kubwa sana

Tell them please. Mambo hayo ya mnayaleta hapa JF kwani JF ni forum ya chamema bana? Mbona mnaharibu sasa? I want to strongly believe that sisiM strategist wanaelekea kufanikiwa kukibomoa na kukimaliza hiki chama. Hatutafika popote kwa style hizi alizoanza mweshimiwa. Suppose JJ nae aje, Mbowe nae aweke yake,Slaa aandike si ndio itakua kwishnei? Mliobaki plz msije kujibu hizi hoja hapa. Kaeni kama kamati fanyeni vikao vya ndani malizeni mambo haya. Msitutie aibu kama mwenzenu Zitto alivyotutia aibu ya karne hii!
 
Hakuna napingana na wewe.
Sauli leo paulo alitubu na akawa kiongozi mzuri,mtu anayetenda mabaya na kuja kuyakiri huyu twamhitaji.

Hii move ni sahihi kabisa kwa Zitto hatujui watakuja kufanya nini na plan C baad ya plan B.

Si sahihi kwa zitto kukaa kimya saizi kama anaona dalili za kumwoondoa kutokuwa mwenyekiti bado kuna harakati za kwenda mbali zaidi.

Wewe Mkandara kaa kimya muonja, asali haonji mara moja hujikita na kuchonga mzinga.

Unamaana hiyo plan C ni ya kutaka kumuwangwe zitto?
 
Pole sana ndugu yangu. Naelewa feelings zako na za wengine humu ndani. Ninawahakikishia kuwa tutainuka, tutajipakusa vumbi na kukimbia tena pamoja. Mchakato huu waweza kuwa na matokeo ya kukikuza na kukikomaza chama sana. Tunajifunza katika changamoto hizi. Hatuwezi kukubali kuingia katika historia ya kuua CHADEMA. Kuna masuala fulani fulani ya msingi kabisa kuhusu mahusiano yetu na marafiki zetu ambayo lazima tuyashughulikie asap.

Deep in my heart i believe truth will prevail and the party will come up strong.


Mh. Zitto nafikiri kama ni kweli ulikuwa na nia ya kuchukuwa uwenyekiti ili kuimalisha chama halfu badaye ugomebee ukuu wa nchi nafikiri timing haikuwa nzuri. Sababu yangu ni kwamba umri wako ni mdogo kwa hiyo mpaka ufikie umri wa kugombea urais unahitaji miaaka 12 zaidi. Sasa kama ungechukua leo hakika katika kipindi cha miaka 10 ijayo ungeweza kufanya makosa mambayo angekuharibia. Timing is very important kwenye politics, hiyo jaribu kuangalia when is the right time for you!!! Ila hii haikuwa wakati mzuri kwa mtizamo wangu!!
 
Hivi ukiwa kama Kiongozi Mkuu kwenye Ukatibu Mkuu Makamu hivi huoni kuwa umeingilia huo uchaguzi kwa kusema wewe mwenyewe kuwa ulifanya kampeni wazi wazi kwa vijana hawa wadogo huoni kuwa ukutenda kosa??

Hivi mtu ukishakuwa naibu katibu mkuu unakosa haki ya kumpigia kampeni mgombea unayemwamini hata kama umejivua majukumu yote ya kusimamia uchaguzi? Hivi hawa vijana wadogo kwa Zitto mwenye umri wa miaka 33 ni wapi hao? Kama Zitto alijitoa katika shughuli za kusimamia uchaguzi na yeye ni mjumbe wa mkutano wa vijana ni wapi amekosea? Na kati ya Zitto na ninyi ni kina nani ambao wamo katika timu ya kusimamia uchaguzi lakini pia wanakuwa mbele kupiga kampeni chafu dhidi ya Zitto na sasa mmekimbilia kwa watu wanaomuunga mkono?

Kwa taarifa yenu Zitto hakuwa na nia ya kufanya kampeni zaidi yakumsaidia kimawazo Kafulila hadi mlipojikusanya wote na baadhi yenu mkiwa wasimamizi wa uchaguzi kuenda kuanza kumfanyia kampeni mtu "wenu" eti kumuonyesha siasa Zitto. Hapo ndipo mlipo likoroga. Zitto alishakuwa tayari kujishusha na kum-approach Mbowe for genuine reconciliation lakini kwa utoto wenu mkajiona kuwa mmemshinda na mtaweza "kummaliza". That wa a big mistake kwenu lakini pia kwa maslahi ya chama chenu.

Mh Zitto! kwenye kipindi kama hiki kizito kwa chama kwanini usiwe na moyo kama wa mwenyekiti wako Mbowe ukakaa kimya kwa masrahi ya chama kwanza, unapoanza kusema mambo ya Fedha (CAG) huoni kuwa hapo kuna mushkeli,

Hivi Mbowe amekaa kimya? Yaani mtu anayeongea nyumba ya pazia ndio amekaa kimya na huyu anayeongea bila ya kujificha ndiye amekuwa mbaya. Tatizo vijana mnakurupukia profession za watu. Unaibuka huko ulipo unajidanganya kuwa unajua spining bia ya kutambua uwezo na uthubutu wa unayemfanyia spining katika kujibu mashambulizi. Ulitaka uj umwage sumu yako halafu Zitto anyamaze afe kisabuni? Tena hapa Zitto amejicontroal sana maana ninyi ndio mnaojua ni nani na kutoka upande gani wamekuwa wakitumia rushwa katika uchaguzi huu.


Pia kuja hapa kwenye JF forum kumwaga razi lote hilo ambalo kuna utitiri wa wanaCCM kibao, huoni kuwa unavujisha siri??

Siri, yaleyale wtu wanatoka ndani ya CCM kushutumu ufisadi kina Makamba wanasema washugulikiwa kwa kuvuja siri za chama. Uozo na uvundo hauwezi kuwa siri na kuuficha ni kuwalaghai watanzania.

Mimi sina chama ila picha unayoonyesha ni ile ya mapindikizi ya CCM tuliyozoea kuona!!!

Yale yale, wanatokea watu wanawaeleza uovu wa MASIHA FEKI wenu wanaonuka ufisadi na kujidai kuwa wanapiga vita ufisadi huohuo, mnakimbilia kusema kuwa wanaosema uchafu wao watakuwa wametumwa na mafisadi. Hivyo hivyo ndani ya chama chenu mnapofanya mambo ya maovu yaliyopita kiwango cha uvumilivu wakitokea wenzenu kuyasema mabaya hayo mnakimbilia kutafuta mchawi nje ya nyumba...Hapa CCM msiwahusishe kwani ni wenyewe mmeamua kujigeuza asusa yao.

Kubalini makosa yenu, jifunzeni kujisahihisha halafu muanze upya na sio kutaka kushambulia mliowkosea ili kuhalalisha makosa mliyoyafanya na mnaendelea kuyafanya kama spining hii mliyoleta hapa

omarilyas
 
MH,Zitto

Poleni na mambo ya uchaguzi,Ila nina mambo kadha nataka kukueleza,kwanza usilalamike sana kuhusu mama yako mzazi kuongelewa kwenye mambo yaliondelea inavyonekana na kwa jinsi ulivyoandika inaonyesha dhairi kabisa mama yako anashiriki kwa karibu saana kwenye mambo yako yakisiasa kwa hiyo ujue kama anajiusisha basi iko siku hata mbeleni atazungumziwa tu,hilo huwezi kulikataa,mpaka labda siku ikiamua kutojiusisha na mambo ya siasa kiundani saana.


Mifano tunayo kama pale tulipoona wakati wa uchaguzi kule marekani ,wakati Obama alipolalamika kuwa wamuache kuongelea familia yake ,ndipo watu walipoibuka nakusema kama hutaki tusimuongelee mkeo basi asipande majukwaa,kwa hiyo bwana mkubwa vumilia tu.

Mh, punguza mambo ya kumwaga data za mambo yanayoendelea kwenye chama chenu !!. yani umeamua hata kutangaza matokeo humu wakati ulitakiwa utulie mpaka wahusika watangaze halafu wewe ndio labda uibuke na kutueleza unachojua ,ila nimegundua kila kikitokea kitu kwenye chama chenu wewe unaibuka na ka breaking News kako, anagalia saana hiyo ni siasa na unapambana na wanene wa hicho chama !!

Hayo mambo ya chuki na fitna inabidi uyazoee ndio siasa usianze kulilia mapema mambo bado saana kama ni bado utakua unania ya kuusaka uonngozi wa juu zaidi ''you have not seen nothing yet''

politics is a dirty game

Take care
Ndugu zangu,

Katika kipindi hiki sikutaka kabisa kuingia na kujibu hoja yeyote ndani ya JF kuhusiana na uchaguzi wa vijana Taifa. Hata hivyo mtaniwia radhi kujibu hili ili kuweka rekodi sahihi kutokana na upotoshaji ambao unafanyika kwa makusudi kabisa ili kushusha heshima yangu katika jamii.

Moja, mimi ni mumbe wa Baraza la Vijana la CHADEMA kwa nafasi yangu ya kuwa mjumbe wa Kamati Kuu wa kuchaguliwa kuwakilisha vijana na nikiwa Mbunge mwenye umri wa ujana (miaka 33). Hivyo kushiriki kwangu kwenye vikao ni jambo la kawaida kabisa kwani nina haki ya kupiga kura. Vile vile nina haki ya kuamua mgombea gani wa kumuunga mkono katika uchaguzi. Niseme waziwazi kuwa David Kafulila ndiye mgombea niliyemwunga mkono na kumfanyia kampeni waziwazi bila kificho chochote kile. Hii inatokana na tabia yangu ya kutokuwa mnafiki. Nilimwunga mkono David Kafulila na alishinda kwa kupata kura 99 dhidi ya kura 73 ambazo alipata mgombea mwingine John Heche ambaye alikuwa anaungwa mono na kundi lililonipinga kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.
Huyu aliyeandika post hii ni mmoja wa vijana wa makao makuu ya CHADEMA ambaye amekuwa akinipinga siku zote kwa chuki tu ya kuwa mimi nimepaata umaarufu wa kisiasa kuliko yeye na kundi lake.

Mama yangu mzazi ni mwanachadema. Ni kiongozi mwandamizi wa CHADEMA kutoka mkoa wa Kigoma na amekuwa msaada mkubwa wa chama katika Manispaa ya Kigoma. Ninaomba sana masuala yangu ya kisiasa na mahasimu wangu wasimhusishe mama yangu mzazi. Ninaomba sana sana mumuweke mama yangu pembeni. Mwandishi wa post hii tafadhali naomba usimhusishe mama yangu na tofauti zetu za kisiasa. Ninaomba sana hili liheshimiwe.

Pili, ni dhahiri kulikuwa kuna makundi katika uchaguzi wa BAVICHA. Mimi niliweka wazi msimamo wangu wa kumwunga mkono kafulila. Wakurugenzi wa Makao makuu ya chama kuanzia Katibu Mkuu mpaka wakurugenzi kama John Mnyika, John Mrema na hata maafisa kama Halima Mdee walikuwa wanampinga David Kafulila. Hawa wanaogopa uwezo wa Kafulila wa kukataa kutumika na kuwa independent katika maamuzi yake.
Hii sio mara ya kwanza kwa Kafulila kuzuiwa haki yake. Kijana huyu alipitishwa kugombea Ukurugenzi wa vijana na jina lake kwenda katika Kamati Kuu. Ajenda ya uteuzi wake ikasitishwa baada ya kuhofia kuwa atashinda. Mtindo huo huo wameutumia sasa kufuta uchaguzi na kuupeleka mbele mpaka baada ya miezi 6. Mimi nimekataa

1. Uchaguzi umefanyika.
2. Matokeo hayakutangazwa
3. Hakuna aliyekata rufaa

Hivyo, wazee wanapata wapi 'locus' ya kufuta uchaguzi?

Hata hivyo wenye mamlaka ya kufuta uchaguzi ni Kamati Kuu ya chama maana kuna taratibu za rufaa ndani ya chama chetu. Nimetaka Kamati Kuu iitishwe ili taratibu zifuatwe.

Huyu mtu aliyeleta post hii hapa anataka kuspin ili kupinda ukweli bila aibu.

David Kafulila kashinda round ya kwanza zaidi ya 50%. Wamekataa kutangaza matokeo na kuleta fujo kwenye mkutano.

Kuna tuhuma dhidi yangu kuwa nimetoa rushwa. Huku ni kutapatapa kwani tuhuma hizi zinatolewa bila ushahidi. Hivi huyu mwandishi na akili zake timamu anaweza kuweka akilini kwake kuwa mimi naweza kutoa rushwa hadharani? Eti nimevuta kiti na kuita watu kutoa rushwa. Bila adabu anamhusisha mama yangu mzazi.

Mama yangu ana maamuzi yake binafsi na mfano dhahiri ni uchaguzi wa chaha wangwe ambapo mimi nilimwunga mkono arfi na yeye akamwunga mkono Chacha wangwe waziwazi na bila kificho.

Uchaguzi wa vijana haukua na rushwa. Uchaguzi wa vijana wa chadema umefanyika kwa amani kabisa na matokeo hayakutangazwa kwa kuwa mgombea 'wao' hakushinda.

Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa. Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG

Katika spirit ya umoja na mshikamano wa chama tutamaliza suala hili katika Kamati Kuu ya chama.

Ninaomba sana vijana wa Makao Makuu - hasa Mrema, Mnyika na wengineo waache spinning za kipumbavu ambazo hazijengi umoja na mshikamano wa chama. Waache kuchafua jina langu. Wakumbuke kuwa kuna maisha mbele yetu na kuna kazi ya kujenga chama chetu.

Vijana hawa wakumbuke kuwa majungu hulipwa hapa hapa duniani. Wasubiri nao watakuwa wabunge na watapata ajenda zao za kuwafanya kuwa maarufu.

Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!


Haya ambayo nimeyaandika hapa JF nimewaambia vijana hawa 'face to face' ili waache uwongo, uzandiki, majungu, fitna na chuki.

Kafulila kashinda uenyekiti wa vijana. Mpeni ushindi wake. Msibake demokrosia.

Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom