Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Home
broken-heart.jpg
*BAADHI WAGOMEA WASTAAFU, WADAI MAELEZO

Waandishi Wetu

UAMUZI wa kumwondoa Zitto Kabwe kwenye kinyang'anyiro cha nafasi ya mwenyekiti wa Chadema, umeanza kukitikisa chama hicho baada ya wazee waliokutana jana jijini Dar es Salaam kugawanyika katika makundi mawili.


Zitto, 33, alikitingisha chama hicho alipoamua kupambana na mwenyekiti Freeman Mbowe kuwania nafasi hiyo ya juu kwenye chama hicho, lakini akatangaza kujiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho kuheshimu ushauri wa wazee kuwa uamuzi wake ungesababisha chama kuvunjika.


Lakini habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa baadhi ya wazee wanaomuunga mkono mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini wamepinga uamuzi wa kumshauri Zitto ajiondoe kugombea uenyekiti kwa madai kuwa halitambui kikao kinachoitwa cha wazee wastaafu, wakati kundi jingine linaunga mkono uamuzi huo.


Wazee hao jana walikutana jijini Dar es Salaam pamoja na mambo mengine, kumchagua mwenyekiti wa Baraza la Wazee Taifa.


"Mimi na wenzangu hatutambui baraza lililomwengua Zitto kugombee nafasi ya mwenyekiti. Katiba yetu iko hovyohovyo sana kwa kuruhusu suala hilo," alisema mmoja wa wazee wanaopinga uamuzi huo ambaye hakutaka kutajwa jina gazetini.


"Baraza linalotambuliwa kikatiba ni hili linalokutana leo (Baraza la Wazee la Taifa) na sio waasisi na wazee wastaafu wa chama," alieleza.


Taarifa kutoka kwenye mkutano huo zilieleza kuwa kutokana na kutoridhishwa kwao, baadhi ya wazee wakiwamo wa kutoka Ruvuma wameandaa barua kwenda kwa mwenyekiti wa chama hicho siku ya mkutano mkuu baada ya kukosa fursa kutoa dukuduku lao jana.


Kwa mujibu wa habari hizo, wazee hao wanadai kuwa Zitto aliondolewa kimizengwe kwa sababu ya maslahi ya watu wachache wa chama. Wanadai kuwa muundo mzima wa chama kuanzia kwa Mtei hadi kwa Mbowe umefinyanga demokrasia.


Wakati kundi hilo likipinga uamuzi huo, lingine limebariki likisema ni sahihi Zitto kuondolewa kwenye kinyang'anyiro hicho kwa kuwa uamuzi wake kugombea nafasi hiyo ulianza kukigawa chama.


"Ule uamuzi ni sahihi kwani tulishafikia mahali tukagawanyika, lakini sasa tumerudi kuwa wamoja," alisema mzee mwingine anayeunga mkono uamuzi huo.


Hata hivyo, katiba ya Chadema toleo la mwaka 2006, kipengele cha mabaraza haikuwataja wazee wastaafu na waasisi wa chama kuwa sehemu ya jumuiya za chama hicho.


Lakini katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema kuwa kitendo cha baraza la wazee kukaa na kuamua mvutano kati ya Mbowe na Zitto ni kwa mujibu wa katiba hiyo, kifungu cha 5(1)5.

Kwa mujibu wa kifungu hicho wazee wana haki ya kukaa na kuamua maamuzi ya nani agombee uenyekiti kwa maslahi ya chama.


Alisema kuwa kikao kiliongozwa na mwenyekiti wa kwanza wa Chadema, Edwin Mtei, Balozi Christopher Ngaiza, Profesa Mwesiga Baregu, Bob Makani na mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo akisaidiana na ofisi ya katibu mkuu.


Alisema baada ya kukaa katika kikao hicho walimshauri Zitto asigombee kwa ajili ya maslahi ya chama, lakini pia kwa ajili ya kudumisha mshikamano ndani ya chama.


Alisema kwa kuheshimu demokrasia kikao hicho kilifanyika kwa wazi bila mizengwe yoyote na baada ya kikao Zitto aliandika barua kwa katibu mkuu akieleza kuwa ameamua asigombee ili nafasi hiyo ibaki kwa mgombea mmoja ambaye ni Mbowe.


Kwa mujibu wa kikundi kinachounga mkono kuondolewa kwa Zitto, kitendo hicho hakina mkono wowote wa watu kutumiwa bali kimefikiwa kulinda maslahi ya chama.

Wakati wazee hao wakivutana mmoja wa waasisi wa Chadema aliyeshiriki kikao cha kumwondoa Zitto kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti, Bob Makani amekiri kwamba wazee walifinyanga demokrasia katika kufikia uamuzi huo.

Akizungumza na gazeti hili jana, Makani ambaye alikuwa mwenyekiti wa pili wa Chadema, alisema demokrasia ina ukomo wake kwani inaweza kudhibitiwa pale inapoonekana kwamba itasababisha mtafaruku.

"Demokrasia ina ‘limit' (ukomo), huwezi kuiachia pale 'interests' (maslahi) za chama zinaposababisha athari," alieleza Makani ambaye aling'atuka madarakani na kumpisha Mbowe.

Kwa mujibu wa Makani kwa mazingira ilipofikia hoja ya Zitto, ilikuwa lazima wazee kuingilia kati ili kuokoa chama n athari ambazo zingeweza kutokea baadaye.

Alisema jambo lililofanywa na Chadema si la ajabu kwani hata katika tawala za mataifa, serikali haziwezi kuachia mambo yaende kiholela eti kwa sababu ya demokrasia.

Wakati Makani akisema hayo mhadhiri mwandamizi wa Kitivo cha Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma (PSPA) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema Zitto alikurupuka kugombea uenyekiti.

Dk Bana alisema Zitto alitaka kutengeneza joto na presha ya kisiasa kuuhadaa umma kwamba kuna demokrasia ndani ya Chadema.

Naye Profesa Abdallah Safari alisema kitendo cha Zitto kujiondoa kimedhihirisha wazi kuwa sera na utamaduni wa chama hicho ni kuachiana madaraka.

Pia alisema hoja aliyotoa Zitto ya kukinusuru chama ili kisigawanyike ni kudumaza ukuaji wa misingi bora ya demokrasia ya kweli nchini.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Profesa Safari alisema wazee wa chama hicho wameonyesha udhaifu mkubwa katika kukuza demokrasia hiyo.

"Wazee wa Chadema wamekosea, hivyo ni wazi sasa watangaze kuwa sera na utamaduni wa chama chao ni kuachiana madaraka na si vinginevyo," alisema Prof Safari ambaye aliangushwa na Prof Ibrahim Lipumba kuwania uenyekiti wa CUF. Habari hii imeandaliwa na Musa Mkama, Leon Bahati, Salim Said na Sadick Mtulya.




Contact Us DISCLAMEREmail:webmaster@mwananchi.co.tz© Mwananchi Communications Ltd 2006- 2009
 
Nasikitika kusema kuwa kilichotokea ni utoto wa hali ya juu na kukosekana kwa busara kutoka kwa Wazee wa Chadema, Freeman na Zitto mwenyewe.

Kwanza sielewi na hakuleti maana kusikia kuwa Zitto alichukua fomu na kutangaza nia yake ya kugombea Uenyekiti akiwa njiani kwenda Ujerumani. Kama hiki kitendo ni cha kweli, basi kilikuwa cha Kitoto sana na cha kipuuzi ambacho kinaonyesha woga.

Ama baada ya nia yake ya kugombea kujulikana na mkutano mkuu kuanza, kitendo cha yeye kukubali kuwekwa kikaoni na kukimbilia kutoa masharti ambayo tunayasoma humu kama ndio nji pekee ya yeye kusimama mguu pande ni kweli, basi Zitto na Chadema hawafai kupewa dhamana ya kuliongoza Taifa letu.

Mbowe ilisadikika kuwa hatarejea kwenye Uenyekiti, ni kwa nini basi aliamua kubadilisha mawazo na kugombea?

Kilichotokea CHADEMA ni kunyongwa kwa Demokrasia na udhaifu wa kuelewa njia bora ya kujenga chama cha kisiasa.

Chadema na Zitto wamejidhihirisha kwa Watanzania kuwa bado ni watoto sana katika masuala ya siasa na wamejiunga na kundi la TLP, NCCR na vyama vingine ambavyo vimekuwa na migogoro ya kiuongozi na ubinafsi.

Kama kulikuwa na mtu anayetegemea kuwa CHADEMA ni chama madhubuti cha Upinzani, naomba urudie makala zangu za CHADEMA must Reform na Focus 2010!

Zitto alijua wazi tangu mwanzo kuwa kitendo cha yeye kugombea kingeleta vurugu na kukosesha amani chama.

Wazee wa CHadema na Freeman, nao waliposikia hili, kwa nini hawakumpisha Zitto awe mwenyekiti wa Chama kwa kuwa Freeman Mbowe ilishasikika kuwa atastaafu?

Mambo yaliyotokea CHADEMA katika siku hizi 5 zilizopita, yanayapa nguvu yale maneno ya mtaani yanayodai kuwa kuna watu waliotaka kuingia CHADEMA kutoka CCM ambao si safi na walitaka mtu kama Zitto ambaye ni mwepesi wa ku-compromise, awe Mwenyekiti ili yanayosemwa mtaani kuhusu hawa jamaa, yaishe kimya kimya.

Si mara ya kwanza kwa Zitto kutuhumiwa kuwa anatumiwa na kikundi fulani ndni ya CCM.

Yalianza na kamati ya madini, ikaja suala la Dowans, na kila panapokuwa na tuhuma za Zitto kutumiwa kama kibaraka wa CCM na ajenda zake, si Zitto au CHADEMA ambao wamesimaam kidete na kuondoa huo utata, kitu kinachoonekana wazi kuwa tuhuma hizo ama zina ukweli au basi kuna vurugu ndani ya Chama kama vile Chacha Wangwe alivyodai kuwa Zitto adandie basi la CCM aachane na la Chadema!

Kura na heshima yangu mmeipoteza, nyote CHADEMA na Zitto sawa na vile CCM ilivyojiharibia machoni pangu.

Natafuta chama kipya kukipa kura na nguvu zangu!
 
Zitto alitangaza miaka minne iliyopita kuwa hakuwa na mpango wa kuendelea na siasa, bali alitaka ajijengee uzoefu katika profession aliyosomea. Kitendo chake cha kuamua kugombea uenyekiti wa chama chake bila kuwa amewasiliana na wenzake ndani ya chama na kuona uzito wa support yao ikoje ni kama vile alikuwa anatingisha kiberiti tu bila ya kuwa na nia kubwa ya kufanya hivyo. Inawezekana kabisa kuwa Zitto amefikia adhma yake ya kuachana na siasa za upinzani, ili apate muda wa kufanya "shughuli zake katika profession aliyosomea" na baadaye arudi kwenye siasa kwa kutumia mlango tofauti kabisa na CHADEMA.
 
http://www.mwananchi.co.tz/index.asp

“Demokrasia ina ‘limit’ (ukomo), huwezi kuiachia pale 'interests' (maslahi) za chama zinaposababisha athari,” alieleza Makani ambaye aling'atuka madarakani na kumpisha Mbowe.

Yaani hii athari ya U-CCM itatumaliza kwelikweli. Yaani imefikiwa wakati hawa nao wanaongelea limit za demokrasia na maslahi ya chama mbele. Sasa CCM wanaosema kuwa hawawezi kushughulikia MAFISADI wao kwa maslahi ya chama iweje muwazodoe?


Wakati Makani akisema hayo mhadhiri mwandamizi wa Kitivo cha Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma (PSPA) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema Zitto alikurupuka kugombea uenyekiti.

Dk Bana alisema Zitto alitaka kutengeneza joto na presha ya kisiasa kuuhadaa umma kwamba kuna demokrasia ndani ya Chadema.

Sasa kama alikuwa akitaka kujenga presha iweje amekurupuka?

omarilyas
 
Only fools don't change their minds, Zitto being not among them, he has the right to change his minds. He is not the first to do so in the political arena. In fact, it is one of the rules of the game world-wide. His decision seems to surprise many of you coz it is on the tails side of the coin. If it were on the head side, you probably would have not been shocked by the event. We have seen young people like Hon. Zitto (e.g. President Obama) being stirred by the elderly (wazee) to contest for high political positions. Unfortunately, none of you never came out to condemn the wazee for encouraging the young people to take such big positions. I can assure you my friends, if it were not the wazee, Obama would have not reached where he is now. At some stage, he was probably told "NO FOR NOW" by the wazee. In every political party world-wide the decisions of the wazee are highly respected and easily understood by those who have vision (like Zitto). Zitto is hardly six or seven years in the political field, but some of the CHADEMA wazees have been in the field for more than four decades! Don't you think that entering into dispute with them is cursing oneself. I accept ZItto's decision to accept the advice of his political party's elderly. That's what is called being politically matured. I diverge to those who says zitto ina iburi, mijifuno, etc. My assessment is that 9I might wrong also) Hon. Zitto is most of the time well informed and confident, and that's what is required if you want to continue staying in politics.
 
Zitto alitangaza miaka minne iliyopita kuwa hakuwa na mpango wa kuendelea na siasa, bali alitaka ajijengee uzoefu katika profession aliyosomea. Kitendo chake cha kuamua kugombea uenyekiti wa chama chake bila kuwa amewasiliana na wenzake ndani ya chama na kuona uzito wa support yao ikoje ni kama vile alikuwa anatingisha kiberiti tu bila ya kuwa na nia kubwa ya kufanya hivyo. Inawezekana kabisa kuwa Zitto amefikia adhma yake ya kuachana na siasa za upinzani, ili apate muda wa kufanya "shughuli zake katika profession aliyosomea" na baadaye arudi kwenye siasa kwa kutumia mlango tofauti kabisa na CHADEMA.


Pia ningependa kukurekebisha katika hili suala la Zitto kuacha siasa.
Kamwe Zitto hawezi kupumzika na wala kuacha siasa na hajawahi kutamka nia ya kufanya hilo kamwe.

Alichosema yeye na hadi sasa ndio msimamo wake ingawa siku za hivi karibuni amekuwa akitafakari sana, ni kuwa ataacha jukumu la ubunge (hatagombea mwaka 2010) kwa sababu kadhaa.

Moja ni kuwa anaamini aspokuwa mbunge atapana nafasi zaidi ya kufanya kazi za chama kwa ukaribu zaidi na kuhakikisha kuwa anatoa mchango zaidi katika kujenga chama kiasasi na kukiandaa kuwa kama mbadala makini wa chama tawala inapofika hapo mwaka 2015. Kwake yeye muhimu sio mradi chama chake kuchukua madaraka tu ama kuiondoa CCM madarakani tu, bali kuwa na chama chenye nia ya dhati na uwezo wa uhakika wa kuleta mabadiliko ya kweli ambayo yawawezesha watanzania kutumia potentials zilizojaa nchini kuifanya nchi yetu kuwa yenye demokrasia makini na yenye kuleta tija kwa maisha ya mtanzania.

Zitto anaamini kuwa ni muhimu sasa chama chake kujiongezea nguvu katika vyombo vya maamuzi nchini yaani bunge na mabaraza ya serikali za mitaa ili kuwa na nafasi ya kujijenga zaidi kwa wananchi, kuwaexpose wanachama wao katika nafasi za uongozi kwa mapana zaidi na pia kuwa na nguvu za ushawishi za kufanya mabadiliko ya kimfumo ambayo yanahitajika kufanyika sasa wakati wanajiandaa kuchukua jukumu la kuongoza nchi. Ndio maana anaamini uwa endapo hatagombea 2010 ataweza kutumia muda na nguvu zake zote kusaidia shughuli za kampeni kikamilifu na kuwezesha chama chake kupata viti vingi zaidi haswa kwa wagombea vijana na ama kuondoa ukiritimba wa CCM bungeni ama hata kulazimu kuunda serikali ya mseto kwa kulazimisha waziri mkuu kutokea chama pinzani. Zitto ni gradualist inapokuja katika suala la mustakabali wa taifa letu.Kwake yeye muhimu ni mabadiliko bora na sio bora mabadiliko.

Pia anaamini kuwa kujipunguzia majukumu ya ubunge atakuwa na nafasi ya kujenga zaidi uwezo wake kiuongozi. Anaamini ili kuweza kuwa kiongozi mzuri ni lazima awe na upeo mpana wa masuala ya kiuongozi, kiuchumi , kisiasa na kidunia. Hivyo angelipenda kuchukua muda wake kuanzia sasa kujiongezea elimu na pia kufanya selfreflection/tafakuri binafsi ya miaka mitano ya ubunge wake ili kujipambanua na kuongeza ujuvi katika masuala hayo muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu lakini pia chama chake.

Hivyo ni muhimu kutambua tofauti ya kupumzika siasa na kupumzika ubunge kama ambavyo Zitto alionyesha nia mapema kabisa na hadi sasa bado anaamini kuwa nia hiyo ni bora Hata hivyo endapo ataona kuwa UBUNGE ni muhimu ili kufanikisha malengo yake kwa chama na nchi yake ni wazi hataogopa Nyani ngabu kumuita flip-flopper.

omarilyas
 
Rev Kishoka,

Pole kwa kuchoshwa na haya yaliyotokea. Hata mimi nimeudhika sana. Ila tusipoteze lengo la kuleta mabadiliko. Chadema imeonyesha udhaifu, lakini tukiamua kuitupilia mbali nchi itabaki mikononi mwa CCM.

Kuna uwezekano wa baadhi ya watu wa Chadema, hasa Zitto, aidha kutumiwa na CCM au kuwa power hungry mno! But, we must focus on the target, and that is to get rid of CCM. We will not succeed if we dismantle Chadema at this juncture.

The damage done to Chadema is repairable. After all, we have Dr. Slaa there to pick up the pieces. We can count on him.

Tukikihama Chadema sasa, itakuwa tumepigwa bao na CCM. We may have lost a battle, but we have not lost the war.
 
Omarilyas;

Chadema ni NGO ya Mzee mtei. Ukiangalia kwa umakini utaona kuwa hiki chama ni cha watu kama watatu au wanne tu hivi. Bob Makani, Mtei na Ngaiza.

Mbowe anaongoza kwa remote control tu.

Chadema kina umaarufu wa sasa kwa sababu ya Dr Slaa na Zitto, Mbowe hana lolote kwenye kujenga chama.

Ufadhili wa chama unafanywa kwa kiasi kikubwa na Mzee Mtei.

Pamoja na umaarufu wao Dr Slaa na Zitto hawana PESA.

Kwa mantiki hiyo basi chama ni MALI YA MZEE MTEI kiuongozi.

FP
 
My take so far is as follows:

  • I thank Invisible for his update. It makes the point that Zitto was not forced to abandon his move. Advising him to remove himself from the contest was not undemocratic.
  • Chadema has been bruised in this saga. So has Zitto. Both can emerge with minor injuries, but they have given ammunition to many detractors.
  • Tribalists and their CCM manipulators are using this difficulty to claim that Chadema is a tribal party. That is not true. It was founded by a most distinguished Tanzanian (Edwin Mtei) who, through no fault of his, happens to be Mchaga. I hate to see well educated groups of Tanzanians, like the ones we have here, being so tribal in their outlook.
  • It is not a sin for the son in law of a leader to be a leader. Freeman Mbowe was elected Chadema leader. He was not simply given the chairmanship by Mzee Mtei. In fact, Mzee Mtei was succeeded by Bob Makani, and after Makani, Chadema elected Freeman. What is so sinister about that? Freeman’s association with the founder of Chadema may have helped him, but that there is nothing undemocratic about that.
  • Those who would like to see CCM continue to misrule Tanzania some more will do all they can to exploit this episode. They have already began to try to dismantle the support that those who aim for change give to Chadema her at JF. Their argument that what transpired in Chadema was undemocratic has run out of steam, so they have now reverted to naked tribalism.
  • Change must come to Tanzania. As Obama puts it, we cannot continue to do the same things over and over again and expect a different result. We cannot afford to re-elect CCM. We must build up the opposition, and it seems to me, Chadema is the focal point of that.

Lazima tuteee home Mangi au siyo?. Ondoa kidogo uchaga akilini utaona mengi.
 
Omarilyas;

Chadema ni NGO ya Mzee mtei.

Mbona CCM ni NGO ya mafisadi wanajichotea mabilioni wanavyo taka nyie wala vumbi mnapiga domo tu wenzenu wanaoga mavumbi ya ulaya, america, Asia ukipishana nao wananuka fwedha tu toka NGO ya CCM.
 
Omarilyas;
Pamoja na umaarufu wao Dr Slaa na Zitto hawana PESA.
Kwa mantiki hiyo basi chama ni MALI YA MZEE MTEI kiuongozi.
FP

Ni kama Mwalimu Nyerere alivyokuwa hana pesa. CCM ina pesa, tena nyingi, lakini ni za kuchota serikalini. Ni mali ya wizi, na kuna siku wataajibishwa. Mark my words.
 
Zito amejaa kiburi,dharau na amekua mjivuni....analeta dharau hata kwa walio mfikisha hapo, fikiri anaongea na baraza la wazee, kisha amekubaliana nao maswala fulani yeye anatoka mbio katika vyombo vya habari kuelezea yale ambayo yamezungumziwa kwenye vikao halali vya chama, bado kama raia wakawaida wa Tanzania huu ni mwanzo wa mwisho wakija wetu huyu, kama CHADEMA anadhani hawajamtendea haki anapaswa aende mbele kwa mbele akiwaachia vijana wengine wenye moyo....
CHADEMA inawaheshimu wazee, na hao ni nguzo ya nguvu zake...akina Mtei,Bob Makani na wengineo, hata leo hii WANGEKUWEPO HAI WAZEE KAMA mzee Brown Ngwilulupi ,RIP, bado nidhamu ya chama ni muhimu kuliko kumpoteza muasi mmoja....

Papa Sam,
Give us a break!

If Wazee wa Chadema (as well as Papa Sam) believe that the advice given to Zitto was such a great one and that it was given in good faith for the benefit of the Party, why then don’t they want the rest of us to find out about it? Aren't they proud of their collective wisdom?

You for one have castigated Zitto for revealing the whole kit and caboodle to the public, and I am assuming the Wazee wa Baraza didn’t like it either. I have a sneaking hunch that in your heart of hearts you also believe it wasn’t such a great idea either and therefore as a party faithful you did not want the rest of us mere mortals to find out about it. You would rather the whole issue was shoved under the rug never to be heard of again!

You might as well be honest and admit it so you can sleep at night with a clear conscious!
 
Katika hali ya mshangao na kuonyesha kuchanganyikiwa kuna taarifa zinazosema kuwa baadhi ya viongozi wa CHADEMA wameshinikiza kughairishwa kutangazwa matokeo ya uchaguzi ya Baraza la Vijana na Baraza la wazee ambayo yanaonyesha ushindi mkubwa wa wanachama ambao wanaaminiwa kuwa ni wafuasi wa Zitto Kabwe.

Wakati katika uchaguzi wa Baraza la Vijana unaonyesha kuwa Kafulila ambaye ni msaidizi wa Zitto ambaye amekuwa akimtayarisha kugombea ubunge Kigoma Kusini (sio kigoma kaskazini kwa Zitto) amemshinda kwa kura zilizojitosheleza ndugu Henche ambaye ni chaguo la wafuasi wa Mbowe ambao jana baada ya kumlazimu Zitto kujito walihamishia nguvu zao zote dhidi ya wagombea wanaomuunga mkono Zitto.

Katika matokeo ya uchaguzi wa Baraza la Wazee yanaonyesha kuwa bwana Shilungeshela ambaye pia anasemekana ni mfuasi wa Zitto na ambaye jana usiku Zitto alikuwa akitpita kumuombea kura naye pia ameshinda kwa kura nyingi.

Ukweli ni kuwa haya yanaweza kuwa makosa makubwa zaidi kwa upande wa wafuasi wa Mbowe kwani nahofia nguvu hizi za ushindi wa waliokuwa wakimuunga mkono Zitto zikageuka kuwa kura ya HAPANA kwake na kujikuta akikosa kabisa uhalali wa kiuongozi. Hali ambayo jana usiku Zitto alikuwa akijaribu kuizuia kwa kuhofia kuumiza maslahi ya chama chao.

Cha ajabu na kinachoonyesha kupanick ni kuwa wasimamizi wa chaguzi zote mbili wamezuiwa hata kutangaza matokeo kama zilivyo taratibu....Inaelekea siasa za CCM zimeathiri sana psych ya watanzania.....

Ama kweli hawa jamaa wanajua kukabaka kademokrasia ketu....Mwataka tuende wapi....NYUMBANI kumeota magugu na kumejaa many'agau...

omarilyas

Huu sio ukweli, wazee wa chadema hawajakutana wala hamna kikao chochote cha wazee wa chadema kulichokutana jana usiku. Kilichotokea ni mbunge halima mdee na mwera kama returning officers wameahirisha uchaguzi wa vijana kutokana na tuhuma za rushwa. Madai yaliyotolewa na wanajumbe ni kwamba Zitto amehonga wajumbe ili mgombea wake David Kafulila apite. Maelezo hayo yalitolewa ndani ya ukumbi na kuzua tafrani isiyo ya kawaida. Wajumbe wanadai walikuwa wamepewa maelezo na chama wakutane kinondoni makao makuu asubuhi wapewe usafiri kwenda mbezi kwenye kikao. Msafiri mkurugenzi wa uchaguzi na ambaye ndio aliyekuwa kampeni meneja wa zitto aliagiza mabasi hayo yapite nyumbani kwa Zitto kwanza kabla ya kufika ukumbini. Vijana hao wanadai huko kwa Zitto walishawishiwa kumpigia kura Kafulila na kugawiwa kitu kidogo. Kikao cha wazee kimeitishwa usiku na wanakutana asubuhi hii kujadili kilichoendelea.

OmarIlyas unawatuhumu wazee wa chadema kuvuruga uchaguzi wakati walikuwa wamelala hawajui kinachoendelea (na wewe uko macho usiku mzima) una agenda gani?
 
Saidhorizons,

Vyama vya siasa vina wasemaji wake wa kutangaza maamuzi ya vikao. Hukusikia ya Watergate? Kuna baadhi ya maamuzi ya chama yanabaki siri ili wapinzani wao wasiyajue.

Kama Zitto aliharakisha kukianika chama chake kwa waandishi wa habari, basi lazima tujiulize kusudio lake: alitaka kukiangamiza? Alitaka faida gani? Haya yanayotokea sasa ndio yalikuwa kusudio lake? Is he a divisive fellow?
 
Kuhusu mabadiriko ya uongozi katika Vyama vingi vya siasa Afrika,nchi nyingi za dunia ya tatu ikiwemo Tanzania ni tatizo HILI NI GOJWA KUBWA!Tumekua tukitaja au kujaribu kupambana na magonjwa mbalimbali kama ukimwi,maralia n.k.Naona hapa tunapashwa kuongeza gonjwa lingine ili tuunde mkakati wa kupambana nalo "UROHO WA MADARAKA"Imekua kawaida kwa marais kukata kuondoka madaraka hata baada ya kushindwa kama ilivyotokea Kenya na Zimbabwe na matokeoyake kusababisha vurugu na mauaji ya watu wasio na hatia.Kwetu hapa kama nchi nyingine tatizo hili chakusikitisha lipo kwa vyama vyote.Tatizo hapa ni "UROHO WA MADARAKA NA UBINAFSI"Hili tunapashwa kupambana nalo MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Mbowe atakuwa na wakati mgumu sana kwani hawezi kupata kura toka kwa wajumbe wa kutoka mikoa ya Mara kutokana na sakata la Wangwe,
Kigoma kwani mwenyekiti wa huko ni mjomba wake Zitto Kabwe.
Singida huko ni ngome ya KITILA na LISSU ambao wako kwa Zitto.
Iringa ambako Chiku ambwao alinyimwa ubunge wa viti maalum akapewa mtu wa KILIMANJARO.
TUSUBIRI.

Mgombea anayedaiwa kuwa ni wa mbowe na OmarIlyas anatoka tarime kwa Wangwe. Mwenyekiti wa Kigoma ambaye ni "mjomba" wake Zitto ni mmojawapo wa wazee waliomshauri Zitto ajitoe kwenye kinyang'anyiro. Huu utabiri ni wa kina ama wishful thinking?
 
Omarilyas;

Chadema ni NGO ya Mzee mtei. Ukiangalia kwa umakini utaona kuwa hiki chama ni cha watu kama watatu au wanne tu hivi. Bob Makani, Mtei na Ngaiza.

Mbowe anaongoza kwa remote control tu.

Chadema kina umaarufu wa sasa kwa sababu ya Dr Slaa na Zitto, Mbowe hana lolote kwenye kujenga chama.

Ufadhili wa chama unafanywa kwa kiasi kikubwa na Mzee Mtei.

Pamoja na umaarufu wao Dr Slaa na Zitto hawana PESA.

Kwa mantiki hiyo basi chama ni MALI YA MZEE MTEI kiuongozi.

FP

Kweli nakubaliana na wewe Wazee walilipima hili na kugundua ya kua ni vigumu kwa Zitto kua remote control.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom