Zitto
Zitto
has no status.
JF Senior Expert Member
Join Date: Fri Mar 2007
Posts: 541
Thanks: 160
Thanked 1,431 Times in 324 Posts
Rep Power: 64
Re: Zitto na Mama yake wawazidi kete vijana CHADEMA
Ndugu zangu,
Katika kipindi hiki sikutaka kabisa kuingia na kujibu hoja yeyote ndani ya JF kuhusiana na uchaguzi wa vijana Taifa. Hata hivyo mtaniwia radhi kujibu hili ili kuweka rekodi sahihi kutokana na upotoshaji ambao unafanyika kwa makusudi kabisa ili kushusha heshima yangu katika jamii.
Moja, mimi ni mumbe wa Baraza la Vijana la CHADEMA kwa nafasi yangu ya kuwa mjumbe wa Kamati Kuu wa kuchaguliwa kuwakilisha vijana na nikiwa Mbunge mwenye umri wa ujana (miaka 33). Hivyo kushiriki kwangu kwenye vikao ni jambo la kawaida kabisa kwani nina haki ya kupiga kura. Vile vile nina haki ya kuamua mgombea gani wa kumuunga mkono katika uchaguzi. Niseme waziwazi kuwa David Kafulila ndiye mgombea niliyemwunga mkono na kumfanyia kampeni waziwazi bila kificho chochote kile. Hii inatokana na tabia yangu ya kutokuwa mnafiki. Nilimwunga mkono David Kafulila na alishinda kwa kupata kura 99 dhidi ya kura 73 ambazo alipata mgombea mwingine John Heche ambaye alikuwa anaungwa mono na kundi lililonipinga kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.
Huyu aliyeandika post hii ni mmoja wa vijana wa makao makuu ya CHADEMA ambaye amekuwa akinipinga siku zote kwa chuki tu ya kuwa mimi nimepaata umaarufu wa kisiasa kuliko yeye na kundi lake.
Mama yangu mzazi ni mwanachadema. Ni kiongozi mwandamizi wa CHADEMA kutoka mkoa wa Kigoma na amekuwa msaada mkubwa wa chama katika Manispaa ya Kigoma. Ninaomba sana masuala yangu ya kisiasa na mahasimu wangu wasimhusishe mama yangu mzazi. Ninaomba sana sana mumuweke mama yangu pembeni. Mwandishi wa post hii tafadhali naomba usimhusishe mama yangu na tofauti zetu za kisiasa. Ninaomba sana hili liheshimiwe.
Pili, ni dhahiri kulikuwa kuna makundi katika uchaguzi wa BAVICHA. Mimi niliweka wazi msimamo wangu wa kumwunga mkono kafulila. Wakurugenzi wa Makao makuu ya chama kuanzia Katibu Mkuu mpaka wakurugenzi kama John Mnyika, John Mrema na hata maafisa kama Halima Mdee walikuwa wanampinga David Kafulila. Hawa wanaogopa uwezo wa Kafulila wa kukataa kutumika na kuwa independent katika maamuzi yake.
Hii sio mara ya kwanza kwa Kafulila kuzuiwa haki yake. Kijana huyu alipitishwa kugombea Ukurugenzi wa vijana na jina lake kwenda katika Kamati Kuu. Ajenda ya uteuzi wake ikasitishwa baada ya kuhofia kuwa atashinda. Mtindo huo huo wameutumia sasa kufuta uchaguzi na kuupeleka mbele mpaka baada ya miezi 6. Mimi nimekataa
1. Uchaguzi umefanyika.
2. Matokeo hayakutangazwa
3. Hakuna aliyekata rufaa
Hivyo, wazee wanapata wapi 'locus' ya kufuta uchaguzi?
Hata hivyo wenye mamlaka ya kufuta uchaguzi ni Kamati Kuu ya chama maana kuna taratibu za rufaa ndani ya chama chetu. Nimetaka Kamati Kuu iitishwe ili taratibu zifuatwe.
Huyu mtu aliyeleta post hii hapa anataka kuspin ili kupinda ukweli bila aibu.
David Kafulila kashinda round ya kwanza zaidi ya 50%. Wamekataa kutangaza matokeo na kuleta fujo kwenye mkutano.
Kuna tuhuma dhidi yangu kuwa nimetoa rushwa. Huku ni kutapatapa kwani tuhuma hizi zinatolewa bila ushahidi. Hivi huyu mwandishi na akili zake timamu anaweza kuweka akilini kwake kuwa mimi naweza kutoa rushwa hadharani? Eti nimevuta kiti na kuita watu kutoa rushwa. Bila adabu anamhusisha mama yangu mzazi.
Mama yangu ana maamuzi yake binafsi na mfano dhahiri ni uchaguzi wa chaha wangwe ambapo mimi nilimwunga mkono arfi na yeye akamwunga mkono Chacha wangwe waziwazi na bila kificho.
Uchaguzi wa vijana haukua na rushwa. Uchaguzi wa vijana wa chadema umefanyika kwa amani kabisa na matokeo hayakutangazwa kwa kuwa mgombea 'wao' hakushinda.
Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa.
Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG
Katika spirit ya umoja na mshikamano wa chama tutamaliza suala hili katika Kamati Kuu ya chama.
Ninaomba sana vijana wa Makao Makuu - hasa Mrema, Mnyika na wengineo waache spinning za kipumbavu ambazo hazijengi umoja na mshikamano wa chama. Waache kuchafua jina langu. Wakumbuke kuwa kuna maisha mbele yetu na kuna kazi ya kujenga chama chetu.
Vijana hawa wakumbuke kuwa majungu hulipwa hapa hapa duniani. Wasubiri nao watakuwa wabunge na watapata ajenda zao za kuwafanya kuwa maarufu.
Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!
Haya ambayo nimeyaandika hapa JF nimewaambia vijana hawa 'face to face' ili waache uwongo, uzandiki, majungu, fitna na chuki.
Kafulila kashinda uenyekiti wa vijana. Mpeni ushindi wake. Msibake demokrosia.
Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.