Uchaguzi 2020 Kuelekelea Uchaguzi mkuu 2020: Tupe tetesi na maoni yako, unapendekeza nani agombee wapi na nafasi gani?

Leo umewamaliza, kabisaaaaa! Polepole kiuno cha kukatika mbona hakipo? Bashite Kishitobe kipo poa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu nasikia sikia hivi karibuni kulitokea msiba wa mtu mmoja maarufu kule Kiomboi Iramba Mwigulu baada ya kusikia Prof. Kitila na Kilimba wapo akaingia mitini.
 
Huyo Mhandisi anaitwa nani? ni vizuri tu atajwe hapa na hata kuendelea kuwachambua hawa waonesha nia sio mbaya sana. Kwa mfano Mwigulu Vs Kitila Mkumbo vipi?
au Mwigulu Vs Juma Kilimba - hapo vipi?
Mnambua nikushauri uibadilishe username isomeke "munaambûâ"

Usijihusishe kabisaa na wanaoita "kisiriri" maana wanyiramba "anaambûâ" inclusive hawana "R" hata kabila lao inapaswa liitwe wanilyamba.

Mwigulu ni raia mnilyamba pasi na shaka, likewise kétiilâ Mùkúmbo na J. Kêlímbâ.
Tutasikiliza ahadi zao nasi tutawauliza maswali.
 
Asante kwa kuboresha. Hapo Jogi ni kifupi cha Joginda ama? Halafu unafikiri utakuwa na nafasi ya kuwauliza maswali?
 
Huyo Mhandisi anaitwa nani? ni vizuri tu atajwe hapa na hata kuendelea kuwachambua hawa waonesha nia sio mbaya sana. Kwa mfano Mwigulu Vs Kitila Mkumbo vipi?
au Mwigulu Vs Juma Kilimba - hapo vipi?
Hii ni nzuri:
Mie nikiambiwa kati ya Prof. Kitila na Mwigulu naona km Prof pamoja na kuwa anaweza asishinde kutokana na kutokuwa na taarabu kama Mwigulu lkn anafaa zaidi kwa sababu Mwigulu from the beginning aliingia akiwa na ambition za Uraisi na kujali zaidi siasa za nchi kuliko kuangalia jimbo.
Ila kuhusu Mwigulu na Juma Kilimba, naona hapo Mwigulu bado ni nafuu kubwa sana. Juma Kilimba sikuwahi kuona kabisa km ana cha kujivunia katika kipindi chake cha ubunge. Halafu anaonekana ni mtu wa majungu majungu hivi.
 
Halo JF siasa.

Nimekuja na Uzi maalumu wa tetesi za wagombea majimboni mkoa kwa mkoa. Tunaanza na Alphabet, Mkoa wa Arusha alafu itafuatiwa na Dar es salaam na mtiririko huohuo.

1. Mkoa wa Arusha.
Jimbo la Arusha mjini wagombea kupitia CCM ni Monabana au Philimon Mollel, RC Mrisho Gambo na mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya Asia. Wengine wakiongezeka nitawajuza.

Jimbo la Arumeru Magharibi ni Stephen Zelote, Daniel Ole Njoolay, Elsa Mollel (Mbunge wa zamani) Goodluck Olemedeye (Mbunge wa zamani)na kijana moja machachari jina nalisaka.

Arumeru Mashariki ni Joshua Nassari na Mbunge wa sasa. Nassari anahamia CCM hivi punde.

Ngorongoro: Ole Nasha, Ole Telele na Mhadhiri moja wa chuo cha SAUT.

Monduli: Julius Kalanga MB, Joseph Sokoine, Namelok Sokoine, Fredy Lowassa na Loota Ole Sanare RC Morogoro. Huenda familia ya Sokoine wakafanya kikao ili mmoja ajitoe.

Karatu: Nafanya mawasiliano.

Longido: Dr Stephen Kiruswa MB, na Daniel Marari.

NB: Kama una tetesi za mkoa wowote nifuate inbox.
 
Mhe. Mwigulu Nchemba amekuwa akituhubiria kila siku TUJIAJIRI...nadhani sasa anatakiwa kuonyesha kwa vitendo dhana ya KUJIAJIRI baada ya kupigwa chini Ubunge

Sent using Jamii Forums mobile app

Nondo mtoto wa mlalahoi alionewa na nani? Ni nani alitangaza bungeni kuwa mtoto wa masikini kijana Nondo Abdul kajipaka mafuta ya maarashi na poda na kujiteka mwenyewe? Yote aliachiwa Muumba!
 
Asante kwa kuboresha. Hapo Jogi ni kifupi cha Joginda ama? Halafu unafikiri utakuwa na nafasi ya kuwauliza maswali?
Usihamishe goli mnilyamba, kukosa nafasi ya kuwauliza maswali means hawataniwakilisha kama ambavyo hawaniwakilishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…