demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Wanajamvi.
Tukijaribu kwa kina kutafakari njama kuu ya kuengua wagombea wa ubunge wa majimbo yaliyo mengi ni moja ya mkakati wa kuhakikisha unalenga kupunguza idadi ya kura atakazo pata Tundu Lissu. CCM wamegundua kuwa idadi ya wapiga kura walio wengi watakaokwenda kwenye sanduku la kura, wataenda kupigia kura kwa kuhamasishwa zaidi na mbunge wa eneo lake, hamasa ya pili ni kumpigia kura Rais.
Wengi tunaamini kwamba hamasa ya kwenda kupiga kura inachochewa na kumuwezesha mbunge wa eneo lako kuweza kupita/kushinda kwa sababu ni mtu anayegusa maisha yako kwa ukaribu sana. Baada ya hapo kipaumbele namba mbili ni kuhakikisha Rais anapigiwa kura. Hivyo basi kwa namna moja CCM wameshinda katika nyanja hiyo kwa sababu hata Upinzano unaonekana hauna mkakati wowote uliopo kupambana na njama za uenguaji.
Tukumbuke kuwa Idadi kubwa ya wabunge wa CCM katika biunge lijalo itawasaidia kupitisha na kubadilisha katiba itakayo muweka madarakani Rais Magufuli kwa Muhula mwingine wa Tatu kwa visingizio kuwa anastahili kwa yale aliyo yafanya.
"Imbombo Jilipo Mwaka Huu"
Tukijaribu kwa kina kutafakari njama kuu ya kuengua wagombea wa ubunge wa majimbo yaliyo mengi ni moja ya mkakati wa kuhakikisha unalenga kupunguza idadi ya kura atakazo pata Tundu Lissu. CCM wamegundua kuwa idadi ya wapiga kura walio wengi watakaokwenda kwenye sanduku la kura, wataenda kupigia kura kwa kuhamasishwa zaidi na mbunge wa eneo lake, hamasa ya pili ni kumpigia kura Rais.
Wengi tunaamini kwamba hamasa ya kwenda kupiga kura inachochewa na kumuwezesha mbunge wa eneo lako kuweza kupita/kushinda kwa sababu ni mtu anayegusa maisha yako kwa ukaribu sana. Baada ya hapo kipaumbele namba mbili ni kuhakikisha Rais anapigiwa kura. Hivyo basi kwa namna moja CCM wameshinda katika nyanja hiyo kwa sababu hata Upinzano unaonekana hauna mkakati wowote uliopo kupambana na njama za uenguaji.
Tukumbuke kuwa Idadi kubwa ya wabunge wa CCM katika biunge lijalo itawasaidia kupitisha na kubadilisha katiba itakayo muweka madarakani Rais Magufuli kwa Muhula mwingine wa Tatu kwa visingizio kuwa anastahili kwa yale aliyo yafanya.
"Imbombo Jilipo Mwaka Huu"