Uchaguzi 2020 Kufa kwa Sekta Binafsi na Makampuni ya Ujenzi ya ndani ndio kunanifanya nimpe kura Lissu

Uchaguzi 2020 Kufa kwa Sekta Binafsi na Makampuni ya Ujenzi ya ndani ndio kunanifanya nimpe kura Lissu

Sababu kwangu mimi kupiga kura ni haramu hata angekuwa nani sipigi kura, ila kwa hili aisee linanishangaza sana.
Sabb ya imani ya dini, au?!
Watu wasiotaka kuchukua hatua Kama wewe ndo wanasababisha ccm wanatawala miaka na miaka bila tija yoyote
 
Ukweli ni kwamba hakukua na ulipaji kodi sahihi na hii ilipelekea serikali kupoteza kiasi cha kushindwa hata kuboresha miundombinu huku makampuni kupata faida zisizokua za kweli.
Makampuni mengi yaliweza kumudu matumizi mengi yasiyokua ya lazima sababu tuu pesa ilikua nyingi. Sasa kwakuwa kodi zinalipwa sawasawa wenye makampuni wanatakiwa kujipanga upya kwa kuangalia upya gharama za uendeshaji huku wakiongeza ufanisi
Kulalamika hakutusaidii chochote kwa sasa

Sio kweli. Hizi kodi zinazorudiwa kila siku hazikamiliki ? Mfano mdogo tu...2019 TRA inafanya mahesabu na unaambiwa ulipe kodi kiasi fulani. 2020, TRA hao hao wanarudi kwenye yale yale mahesabu na wanakuja tena na kiasi kingine cha kulipa. Is that how it works? Investors wawe wazawa au wa nje wanawaangaliaje kwenye mambo kama hayo? Mtakusanya wapi kodi kama kampuni kinaendelea kufungwa? I think, mnakusanya kodi ambayo wala sio kodi. Ni kula mitaji ambayo wala hamkuwekeza
 
Hakuna haja ya kuendelea kukuelewesha sabab ushachagua kutokusikiliza.

Siasa sio mpira, usikariri
Wenye kupanga tanking ni Moody au world Bank and it's affiliates organisation??
 
Sabb ya imani ya dini, au?!
Watu wasiotaka kuchukua hatua Kama wewe ndo wanasababisha ccm wanatawala miaka na miaka bila tija yoyote
Achilia mbali imani ya dini, ila akili tu iliyo salimika inakataa mchakato wa upigaji kura, watu kuomna uongozi na mfumo mzima wa uendeshaji mambo chini ya Mwamvulo wa Demokrasia.

Kwani hatua tu ni mpaka umpigie yule aliye dhidi ya CCM au hata kutokupiga kura kabida nayo ni kuchukia hatua, au huku si kuchukua hatua ?
 
Sio kweli. Hizi kodi zinazorudiwa kila siku hazikamiliki ? Mfano mdogo tu...2019 TRA inafanya mahesabu na unaambiwa ulipe kodi kiasi fulani. 2020, TRA hao hao wanarudi kwenye yale yale mahesabu na wanakuja tena na kiasi kingine cha kulipa. Is that how it works? Investors wawe wazawa au wa nje wanawaangaliaje kwenye mambo kama hayo? Mtakusanya wapi kodi kama kampuni kinaendelea kufungwa? I think, mnakusanya kodi ambayo wala sio kodi. Ni kula mitaji ambayo wala hamkuwekeza
Sasa nimeelewa😁
Ukiona TRA wamekuongezea kiasi cha kodi rudi kwenye hesabu zako kama sio wewe basi anayekufanyia hesabu kuna mahali alitengeneza mambo ili kupunguza kodi halafu upande wa pili akashindwa kutengeneza. Sasa documents zinapowafikia lazima wataona na kama wamekuambia ulipe tena wamekupendelea, kwa hilo huwa wanakupiga adhabu ya kutosha. Hii imewatokea wengi, hata mimi iliwahi kunikuta kwa kuamini report iliyoandaliwa na mtu wangu kumbe ndani alivuruga
Kama kampuni ni yako jaribu kupata ukweli wa nini kilitokea ili lisijirudie tena
 
Sasa nimeelewa[emoji16]
Ukiona TRA wamekuongezea kiasi cha kodi rudi kwenye hesabu zako kama sio wewe basi anayekufanyia hesabu kuna mahali alitengeneza mambo ili kupunguza kodi halafu upande wa pili akashindwa kutengeneza. Sasa documents zinapowafikia lazima wataona na kama wamekuambia ulipe tena wamekupendelea, kwa hilo huwa wanakupiga adhabu ya kutosha. Hii imewatokea wengi, hata mimi iliwahi kunikuta kwa kuamini report iliyoandaliwa na mtu wangu kumbe ndani alivuruga
Kama kampuni ni yako jaribu kupata ukweli wa nini kilitokea ili lisijirudie tena
Shida ni kwamba hata uki appeal bado unatakiwa ulipe aslimia fulani kubwa tu wakati ukisubiria majibu ya rufaa yako.
 
Achilia mbali imani ya dini, ila akili tu iliyo salimika inakataa mchakato wa upigaji kura, watu kuomna uongozi na mfumo mzima wa uendeshaji mambo chini ya Mwamvulo wa Demokrasia.

Kwani hatua tu ni mpaka umpigie yule aliye dhidi ya CCM au hata kutokupiga kura kabida nayo ni kuchukia hatua, au huku si kuchukua hatua ?
Mkuu, hatua inayosaidia kuangusha mfumo mbovu ni nzuri zaidi
 
Sasa nimeelewa😁
Ukiona TRA wamekuongezea kiasi cha kodi rudi kwenye hesabu zako kama sio wewe basi anayekufanyia hesabu kuna mahali alitengeneza mambo ili kupunguza kodi halafu upande wa pili akashindwa kutengeneza. Sasa documents zinapowafikia lazima wataona na kama wamekuambia ulipe tena wamekupendelea, kwa hilo huwa wanakupiga adhabu ya kutosha. Hii imewatokea wengi, hata mimi iliwahi kunikuta kwa kuamini report iliyoandaliwa na mtu wangu kumbe ndani alivuruga
Kama kampuni ni yako jaribu kupata ukweli wa nini kilitokea ili lisijirudie tena
Mara nyingi Tra wanakulainisha tu kwa Kodi kubwa ili rushwa itoke kirahisi
 
Mkuu, hatua inayosaidia kuangusha mfumo mbovu ni nzuri zaidi
Si kweli na hili huwezi kuthibitisha. Tunaweza kusema ya kuwa serikali inafanya uonezi kwa makampuni binafsi hasa hasa madogo ila kuna makampuni haiwezi kuyaondoa sababu nchi haina mpango huo na haiwezi kufanya baadhi ya kazi.

Ngoja nikupe mfano, serikali yenyewe inadai imekuja kubaini ya kuwa kwenye hii miradi kuna upigaji mkubwa sana. Sasa kama ni kweli,hapa kunaonyesha udhaifu mkubwa wa serikali yenyeww kupitia watendaji wake. Mkandarasi au mtu binafsi huwa hapigi deal mwenyewe bali anapiga deal na serikali husika. Kwahiyo serikali ilitakiwa kwanza iwaajiri watu ambao hawana tamaa na kuweka mfumo mzuri juu ya hilo.

Kinachokuja kutokea ni miradi mingi inayofanywa na serikali yenyewe ina kuja kuwa na ubora mdogo sana, na hapa kuna sababu za kumridhisha mtawala na si uhaslisi. Mifano iko mingi katika hili.

Lakini labda nikuulize,ni mfumo gani huo unao ukusudia na ni hatua zipi ?
 
Unafungua biashara survival strategy yako ufanye kazi na serikali tu, sio kwamba umefanya demand analysis ya soko zima. Wakati unasoma biashara ukufundishwa effect za changes in consumption trends za wateja na jinsi ya kujikinga?

Biashara ya namna hiyo zife tu hakuna creativity. Kungekuwa na high streets retails leo kweli nchi za wenzetu zama hizi za online shopping bila ya maduka makubwa ku adapt mazingira ya leo.

Serikali imeamua hela yake inataka iende mbali value for money na miradi yake iishe on time; hata hizo taasisi za serikali zinazo sua sua miradi wananyang’anywa with minimal legal consequences za kupelekana mahakamani for breach of contract.

Zama zimebadilika tatizo sio Magufuli isipokuwa wafanyabiashara wasiotaka kubadilika; fungua biashara nyingine sio lazima ufanye kazi na serikali tu.
 
Unafungua biashara survival strategy yako ufanye kazi na serikali tu, sio kwamba umefanya environmental analysis ya soko zima. Wakati unasoma biashara ukufundishwa effect za changes in consumption trends za wateja na jinsi ya kujikinga?

Biashara ya namna hiyo zife tu hakuna creativity. Kungekuwa na high streets retails leo kweli nchi za wenzetu zama hizi za online shopping bila ya maduka makubwa ku adapt mazingira ya leo.

Serikali imeamua hela yake inataka iende mbali value for money na miradi yake iishe on time; hata hizo taasisi za serikali zinazo sua sua miradi wananyang’anywa with minimal legal consequences za kupelekana mahakamani for breach of contract.

Zama zimebadilika tatizo sio Magufuli isipokuwa wafanyabiashara wasiotaka kubadilika; fungua biashara nyingine sio lazima ufanye kazi na serikali tu.
Uchumi wa vitabuni huo ndiyo yale boss wa tra akistaafu anafungua biashara mwaka anafilisika
 
Uchumi wa vitabuni huo ndiyo yale boss wa tra akistaafu anafungua biashara mwaka anafilisika
Ni kwa sababu hawana survival strategy (sina uhakika ntaingia google nirudi na takwimu rasmi) hila wanadai katika biashara laki moja zinazofunguliwa nchi za mabeberu karibu 2/3 hufa ndani ya miaka miwili, zilizobaki kama 3/5 hufa ndani ya miaka 5 na katika miaka 10 unakuta zimebaki biashara kama 5000 tu kati ya laki zilizoanzishwa pamoja. kati ya hizo 5000 zilizobaki kama 100 ndio ukuwa kuelekea kuitwa biashara za kati.

Tatizo kubwa linatajwa ni poor planning and the ability to adapt to changing external environment, yaani mtu anafungua biashara kwa lengo la kuhudumia serikali tuu. Hizo ndio akili gani, serikali ikibadili mfumo wake wa manunuzi wanakuja kulia.

Shughuli anayofanya Magufuli leo sio optional ni lazima nchi aiwezi chochea speed ya ukuaji wa uchumi bila ya miundombinu in 10 years time ndio watu watakuja faidika na kuelewa kinachofanywa leo.
 
Uchumi wa vitabuni huo ndiyo yale boss wa tra akistaafu anafungua biashara mwaka anafilisika
Kampuni za ujenzi mubadirike tunategemea sasa muingie mikataba na sisi wananchi wakawaida mtujengee nyumba kwa bei nafuu maana mlikimbilia serikalini kwakuwa mlipiga hela sasa rudini nyumbani kazi zipo tu
 
Kampuni za ujenzi mubadirike tunategemea sasa muingie mikataba na sisi wananchi wakawaida mtujengee nyumba kwa bei nafuu maana mlikimbilia serikalini kwakuwa mlipiga hela sasa rudini nyumbani kazi zipo tu
Si ndio hapo yaani wao mteja ni serikali tu. Wanunue viwanja na kuanza kujenga nyumba za bei nafuu mteja sio serikali tu.
 
Mpaka 2015 private sectors zilikuwa zinashamiri. Jakaya aliacha mazingira mazuri na bora kabisa kwa sekta binafsi kukua na kuboreka. Ila tokea 2016 makampuni ambayo idadi yake haijulikani yamefungwa katika nchi hii, na bado yanaendelea kufungwa. Vijana lukuki wamepoteza ajira katika makampuni hayo.... na wale ambao walijiajiri kwa kufungua makampuni kwa sasa wanalia kilio cha kusaga meno, baada ya kuwindup makampuni yao....

Nilikuwa naongea na Mwanasheria moja jana anasema kazi nyingi anazopata kwa sasa ni kuwindup makampuni. Kwa mwezi anawindup makampuni 46-50 na kwa upande mwingine anafungua 2-3 tu. Sasa cheki hiyo ratio mwenyewe uone.. The private sector is tottaly dead!. Na ndio sector ambayo ingechukua vijana wengi hasa wahitimu wa vyuo. UD inamwaga kila mwaka, UDOM inamwaga kila mwaka, Mzumbe, Tumaini, Muhimbili, TIA na wengine wengi. zaidi ya vyuo 40.... Sasa vijana hao wote hawawezi kuajiriwa sijui na SUMA JKT, TBA,NHC ambao kwa sasa ndio wanafanya kazi zote mpaka za kufagia barabara wakati hizo zilikuwa ni kazi za vikundi vya wanawake na vijana katika mitaa chini ya usimamizi wa Halmashauri.

Jakaya kipindi anatoka aliacha makampuni ya ujenzi ya ndani yalioweza kushindana na Wachina kibao. But look now they are all dead. Kivipi, TRA Kuwabambikizia kesi za madeni, kazi kubwa zote wamechukua makampuni ya nje, kazi za ndani zote za serikali anafanya SUMA JKT, TBA, NHC, mpaka na Magereza. Is simpe local contractors can not survive in that circumstance. Ok!.. Mpaka yale maujenzi ya Halmashauri wameleta mfumo wa Force Account ambao ni ulaji wa watu wa manunuzi bila kujua wanauwa private sekta... Tuliona enzi za Jakaya akipambana kuweka mazingira bora, ndio maana tukaona wazawa wakiflourish kama vile SKOL (now is dead), DELEMONTE (now is dead), MILEMBE (now is dead), MECCO (now id dead), CASPIAN (is almost dead kabaki na kazi za Barrik tu)... the list is endless..

Sasa kwa hali kama hiyo how can You dare to vote for this man again!. No, way unless atuambie kuwa atabadilika na kubadili mfumo wake wa kuuwa makampuni ya ndani. Wahenge wanasema kuuwa uchumi ni suala la siku 2 au tatu ila kuujemga ni miaka 10 t0 20... Hii miaka 5 uchumi umekufa kabisa, mpaka kuja kusimamisha uchumi is not now and haitatokkea kama hatobadilika au kama wananchi tusipoamua kumpa kura Lisu
Tra walifanya sifa kutangaza mapato kila mwezi.
Walitamani kila mwezi uwe na makusanyo ya juu kuliko mwezi uliopita..
Ule mchezo wa halmashauri za mikoa kushindana mapato .
(Wahusika ili kupata sifa za ukusanyaji wanambana mfanya biashara kupita kiasi)

Haya mambo yamewaumiza sana wafanya biashara na kupelekea mitaji yao kuanguka.
 
Kampuni za ujenzi mubadirike tunategemea sasa muingie mikataba na sisi wananchi wakawaida mtujengee nyumba kwa bei nafuu maana mlikimbilia serikalini kwakuwa mlipiga hela sasa rudini nyumbani kazi zipo tu
Mkuu una nyumba ?
Namaanisha nyumba uliyojenga kwa kutumia mafundi wa kawaida mitaani.
Gharama zake umezionaje?
 
Sasa nimeelewa[emoji16]
Ukiona TRA wamekuongezea kiasi cha kodi rudi kwenye hesabu zako kama sio wewe basi anayekufanyia hesabu kuna mahali alitengeneza mambo ili kupunguza kodi halafu upande wa pili akashindwa kutengeneza. Sasa documents zinapowafikia lazima wataona na kama wamekuambia ulipe tena wamekupendelea, kwa hilo huwa wanakupiga adhabu ya kutosha. Hii imewatokea wengi, hata mimi iliwahi kunikuta kwa kuamini report iliyoandaliwa na mtu wangu kumbe ndani alivuruga
Kama kampuni ni yako jaribu kupata ukweli wa nini kilitokea ili lisijirudie tena
Matokeo ya hizo kodi yanareflect kwenye kushamiri kwa hiyo biashara. Ikiwa makadirio yanapelekea kufungwa kwa biashara ,hayo hayawezi kuwa makadirio sahihi kwa maana mfanya biashara analipa kodi nyingi kuliko faida anayotengeneza.
 
Back
Top Bottom