Nimeona sasa baada ya mafuriko (na si mafuriko bali "maji kujaa ktk Barabara na majengo yaliyo kando") baadhi ya watu wameona kuwa hilo ndilo jibu la mafuriko ya Rufiji.
Ukweli ni kwamba mafuriko ya Rufiji kamwe hayawezi kuwa sawa na mengine kwa sababu,
1. Ukubwa wa mafuriko na eneo kubwa ambalo sasa inakwenda kumezwa Rufiji nzima haiwezi kuwa sawa na kujaa kwa maji katika mitaro, barabara na sehemu ndogo jirani na miundo mbinu hiyo, tofauti na huko Rufiji ambako tunaona kimo cha nyumba nzima ikizama majini.
2. Hayo yanayoitwa mafuriko ktk maeneo mengine huchukua muda mfupi usiozidi wiki moja kuisha na kisha shughuli zingine kuendelea na hii hudhihirisha sababu yake kuwa ni mvua, yatofauti na Rufiji ambako yalianza tangu kutangazwa kwa bwawa kujaa na hadi sasa hakuna dalili ya kupungua bali ni kuongezeka kwa namna hii ni wazi Rufiji ipo sababu ya ziada ya mafuriko hayo
3. Kufananisha mafuriko yoyote na yale ya Rufiji ni kuwahadaa wananchi na kuwapa viongozi na watendaji nguvu ya kutowajibika ktk uzembe ambao wamekuwa wakiufanya kwa maksudi wakitufanya sisi wananchi kama wajinga.
4. Ikumbukwe kuwa moja ya hoja za kuhalalisha ujenzi wa bwawa la Rufiji ilikuwa ni kupunguza au kumaliza tatizo la mafuriko lililowahi tokea kwa kujenga miundo mbinu mingine saidizi itakayo weza kutumika kwa uzalishaji pale bwawa litakapo kuwa limezidiwa. Sasa tujiulize hali hii iliyo kinyume nini kimetikea?
5. Wanaodai kuwa mvua ni nyingi mwaka huu kiasi cha husabanisha hayo mafuriko ya Rufiji, nao pia ni uongo kwa sababu bado mvua za mwaka huu hazijawa nyingi kufikia vipimo vya miaka ya nyuma ambayo haikuwahi kushuhudiwa ukubwa wa mafuriko ya eneo kubwa karibia lote la Rufiji likizama.
Ukweli usemwe, kuteleza si kuanguka, viongozi, watendaji na chawa wao wasiendelee kuwafanya wananchi wajinga kwa kulazimisha sisi wananchi tuione nyeupe huku kukiwa ni giza Totoro "nyeusi"
Ukweli ni kwamba mafuriko ya Rufiji kamwe hayawezi kuwa sawa na mengine kwa sababu,
1. Ukubwa wa mafuriko na eneo kubwa ambalo sasa inakwenda kumezwa Rufiji nzima haiwezi kuwa sawa na kujaa kwa maji katika mitaro, barabara na sehemu ndogo jirani na miundo mbinu hiyo, tofauti na huko Rufiji ambako tunaona kimo cha nyumba nzima ikizama majini.
2. Hayo yanayoitwa mafuriko ktk maeneo mengine huchukua muda mfupi usiozidi wiki moja kuisha na kisha shughuli zingine kuendelea na hii hudhihirisha sababu yake kuwa ni mvua, yatofauti na Rufiji ambako yalianza tangu kutangazwa kwa bwawa kujaa na hadi sasa hakuna dalili ya kupungua bali ni kuongezeka kwa namna hii ni wazi Rufiji ipo sababu ya ziada ya mafuriko hayo
3. Kufananisha mafuriko yoyote na yale ya Rufiji ni kuwahadaa wananchi na kuwapa viongozi na watendaji nguvu ya kutowajibika ktk uzembe ambao wamekuwa wakiufanya kwa maksudi wakitufanya sisi wananchi kama wajinga.
4. Ikumbukwe kuwa moja ya hoja za kuhalalisha ujenzi wa bwawa la Rufiji ilikuwa ni kupunguza au kumaliza tatizo la mafuriko lililowahi tokea kwa kujenga miundo mbinu mingine saidizi itakayo weza kutumika kwa uzalishaji pale bwawa litakapo kuwa limezidiwa. Sasa tujiulize hali hii iliyo kinyume nini kimetikea?
5. Wanaodai kuwa mvua ni nyingi mwaka huu kiasi cha husabanisha hayo mafuriko ya Rufiji, nao pia ni uongo kwa sababu bado mvua za mwaka huu hazijawa nyingi kufikia vipimo vya miaka ya nyuma ambayo haikuwahi kushuhudiwa ukubwa wa mafuriko ya eneo kubwa karibia lote la Rufiji likizama.
Ukweli usemwe, kuteleza si kuanguka, viongozi, watendaji na chawa wao wasiendelee kuwafanya wananchi wajinga kwa kulazimisha sisi wananchi tuione nyeupe huku kukiwa ni giza Totoro "nyeusi"