Kufanya biashara sio Jambo rahisi, mtaji pekee sio lolote

Kufanya biashara sio Jambo rahisi, mtaji pekee sio lolote

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
KUFANYA BIASHARA SIO JAMBO RAHISI, MTAJI PEKEE SIO LOLOTE

Anaandika, Robert Heriel

Watu wengi wanapenda kufanya biashara, kuna wengine huwalaumu Ndugu zao au Wazazi wao au waume zao Kwa kushindwa kuwapa mitaji, Jambo Moja la uhakika ni kuwa, hakuna ambaye atakupa mtaji ilhali akijua utapoteza pesa zake.

Biashara ni ngumu Sana Ila pia ni rahisi Sana ukifwata kanuni Fulani. Kabla ya biashara kuna mambo yanapaswa yatangulie, mtaji ni kitu cha mwisho katika mambo ya biashara,

Leo sitasema Sana, Acha niiweke hivi;

I/ Jenga jina lako watu wakufahamu na kukuamini eneo ulilopo, hakikisha iwe sifa njema ya kuvutia.
Jina ndilo huamua Hatma yako.

ii/ Tumia jina lako kutafuta na kujenga mtandao wa watu hasa washirika kimkakati.

iii/ Jenga wahusika ndani yako zaidi ya mmoja.
Hii kwenye nadharia ya Utawiwishaji katika kitabu changu nilisema Kwa mfano, Mimi Taikon, ninajipachua nakutoa Taikon zaidi ya mmoja. Kam ifuatavyo;
Taikon 1
Taikon 2
Taikon 3
Taikon 4
Kila mmoja anauhusika wake kama unauwezo wa kifedha basi ajiri watu wachukue uhusika wako,
Taikon 1 unaweza MPA uhusika wa utakatifu, mwerevu, mwenye Busara, Msomi na sifa zote nzuri.
Huyu atakutana na watu wakubwa, wenye hadhi kwenye jami

Taikon 2 huyu utampa Sifa za unyenyekevu, mpenda wanyonge na Masikini, mtatua kero za jamii, Msuluhishi n.k. huyu atakutana na Tabaka la chini Kabisa

Taikon 3 huyu atakuwa Mafia, mambo ya sirini iwe ya kimungu au kishetani, huyu ni mtu wa dili zenye michongo mirefu. Huyu usimdhihirishe mbele za watu, isipokuwa wahusika maalumu kulingana na Mazingira na wakati.

Biashara ndivyo ilivyo, wateja wanatofautiana hivyo lazima uwe na uhusika tofauti.

iv/ Kazi inayokutambulisha.
Labda mwandishi, mwalimu, Fundi, n.k.
Mbali na biashara hakikisha iwe na Fani nyingine ambayo watu wanaijua.
Mfano, mwanamuziki lakini unauza Duka la nguo.

V/ Tafuta Kibali
Hapa lazima upewe kibali cha Kuendeshea biashara, iwe ukipate Kwa Mungu au Kwa Waganga.
Huwezi fanya biashara yoyote bila kibali kutoka kwenye moja ya pande hizo. Usijedanganywa.

Kama vile unavyosumbuliwa ukiwa huna kibali(Leseni) ya kufanya biashara na TRA ndivyo utakavyohangaika usipopata kibali cha kiroho.

Hili ni Jambo kubwa Sana kwenye biashara.

VI/ mtaji
Hii huja mwishoni kabisa.

Hata mambo ya sijui location hayana umuhimu Kama ukiwa na hayo mambo hapo juu.

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Biashara ni mtaj na namna ya kuulinda huo mtaji, matumizi mazuri ya fursa (wateja walio kuzunguka), umakini na nidhamu (usimamizi mzuri wa hiyo biashara).

Uchawi/nguvu za giza ni mbwembwe tu.
 
Mimi nauza simu used hakuna uchawi wala nini watu wanafuata mteremko tu,uchawi labda tukuachie wewe mtoa mada unaowatumainia binadamu wenzako [emoji28]hao waganga mbona hawapo kwenye List yeyote ya mabilionea?
 
Mimi nauza simu used hakuna uchawi wala nini watu wanafuata mteremko tu,uchawi labda tukuachie wewe mtoa mada unaowatumainia binadamu wenzako [emoji28]hao waganga mbona hawapo kwenye List yeyote ya mabilionea?

Nimetaja Uchawi na Mungu, unachagua kimoja.
Sasa usiniambie unamakengeza hujaona neno neno Mungu.
 
Mimi nauza simu used hakuna uchawi wala nini watu wanafuata mteremko tu,uchawi labda tukuachie wewe mtoa mada unaowatumainia binadamu wenzako [emoji28]hao waganga mbona hawapo kwenye List yeyote ya mabilionea?
Amekwambia "Mungu au waganga" utachagua wewe.

Kuna mtu huko anakuombea bila wewe kujua ndugu yangu, huendi kanisani au msikitini wala huendi kwa waganga ila kuna mtu anakuweka kwenye maombi...Mambo ya kiroho yanatupa Discipline ndugu yangu, ukubali au ukatae.
 
Biashara ni mtaji. Biashara ujue namna nzuri ya kuzungusha mtaji wako.

Usisahau kupuliza pembeni kujiweka sawa
 
Hapo kwenye kibali yaan Entrance nimeelewa sana mtu achague mwenyewe nyeupe au nyeusi...Entrance kibali ni muhimu maagano mafungamano
 
Kuna mitaa fulanii ukipita waona jamàa anauza nyanya ama mkaaa, kisha waenda Duka jinginee...kumbe pale uendapo walishakamata unyayo wako
 
Kuna mitaa fulanii ukipita waona jamàa anauza nyanya ama mkaaa, kisha waenda Duka jinginee...kumbe pale uendapo walishakamata unyayo wako
Ukiwa muumini wa haya huwezi kutoboa kimaisha muda wote utakuwa unawaza kwenda kwa waganga kuboost .... unfortunately....
 
Si hayo tu hata kuajiliwa pia kwanza Boss anakuangalia!! angalia weeee!! na wale wafanyakazi utakao kutana nao pale wivu! mtupu!....

wateja nao wakikuona shavu dodo wivu tayari oohhoo mara unapendeza weye? humo humo maneno kwa Boss huyu haja niangalia vizuri mara haja nichekea!! heeee!! weye bibi weye!

Lkn ukiona wengine wanachapa kazi kwa kwenda mbele hawasemi!! serikalini napo ivovio!! usifanye kitu mara boss uchwara kamepeleka umbeya!!! hayaa ujiajili sasa ndo km haya hivi tutaishi vepiiii?

Kusoma usome kwa shidaaa weeee!! kazi nazo shiiidaa haya umepata ndo km hivoooo!! ivi haya maisha yakoje??...usiporoga utarogwa tuuu!! namleta mada hapa tuzingatie uchawi tu maana! heee!

mtu hata hakujui lkn wivu debe!
 
KUFANYA BIASHARA SIO JAMBO RAHISI, MTAJI PEKEE SIO LOLOTE

Anaandika, Robert Heriel

Watu wengi wanapenda kufanya biashara, kuna wengine huwalaumu Ndugu zao au Wazazi wao au waume zao Kwa kushindwa kuwapa mitaji, Jambo Moja la uhakika ni kuwa, hakuna ambaye atakupa mtaji ilhali akijua utapoteza pesa zake.

Biashara ni ngumu Sana Ila pia ni rahisi Sana ukifwata kanuni Fulani. Kabla ya biashara kuna mambo yanapaswa yatangulie, mtaji ni kitu cha mwisho katika mambo ya biashara,

Leo sitasema Sana, Acha niiweke hivi;

I/ Jenga jina lako watu wakufahamu na kukuamini eneo ulilopo, hakikisha iwe sifa njema ya kuvutia.
Jina ndilo huamua Hatma yako.

ii/ Tumia jina lako kutafuta na kujenga mtandao wa watu hasa washirika kimkakati.

iii/ Jenga wahusika ndani yako zaidi ya mmoja.
Hii kwenye nadharia ya Utawiwishaji katika kitabu changu nilisema Kwa mfano, Mimi Taikon, ninajipachua nakutoa Taikon zaidi ya mmoja. Kam ifuatavyo;
Taikon 1
Taikon 2
Taikon 3
Taikon 4
Kila mmoja anauhusika wake kama unauwezo wa kifedha basi ajiri watu wachukue uhusika wako,
Taikon 1 unaweza MPA uhusika wa utakatifu, mwerevu, mwenye Busara, Msomi na sifa zote nzuri.
Huyu atakutana na watu wakubwa, wenye hadhi kwenye jami

Taikon 2 huyu utampa Sifa za unyenyekevu, mpenda wanyonge na Masikini, mtatua kero za jamii, Msuluhishi n.k. huyu atakutana na Tabaka la chini Kabisa

Taikon 3 huyu atakuwa Mafia, mambo ya sirini iwe ya kimungu au kishetani, huyu ni mtu wa dili zenye michongo mirefu. Huyu usimdhihirishe mbele za watu, isipokuwa wahusika maalumu kulingana na Mazingira na wakati.

Biashara ndivyo ilivyo, wateja wanatofautiana hivyo lazima uwe na uhusika tofauti.

iv/ Kazi inayokutambulisha.
Labda mwandishi, mwalimu, Fundi, n.k.
Mbali na biashara hakikisha iwe na Fani nyingine ambayo watu wanaijua.
Mfano, mwanamuziki lakini unauza Duka la nguo.

V/ Tafuta Kibali
Hapa lazima upewe kibali cha Kuendeshea biashara, iwe ukipate Kwa Mungu au Kwa Waganga.
Huwezi fanya biashara yoyote bila kibali kutoka kwenye moja ya pande hizo. Usijedanganywa.

Kama vile unavyosumbuliwa ukiwa huna kibali(Leseni) ya kufanya biashara na TRA ndivyo utakavyohangaika usipopata kibali cha kiroho.

Hili ni Jambo kubwa Sana kwenye biashara.

VI/ mtaji
Hii huja mwishoni kabisa.

Hata mambo ya sijui location hayana umuhimu Kama ukiwa na hayo mambo hapo juu.

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Taikon hebu nielekeze kuhusu icho kibali cha kiroho kwa mungu kinapatikana wapi Na je nipite wapi ili niweze kukipata Na nkikipata ntajuaje kama nmeshakimiliki
 
Biashara ni mtaj na namna ya kuulinda huo mtaji, matumizi mazuri ya fursa (wateja walio kuzunguka), umakini na nidhamu (usimamizi mzuri wa hiyo biashara).

Uchawi/nguvu za giza ni mbwembwe tu.
Usidiriki kusema uchawi ni mbwembwe wapo waliodharau wakaanguka kibiashara
 
KUFANYA BIASHARA SIO JAMBO RAHISI, MTAJI PEKEE SIO LOLOTE

Anaandika, Robert Heriel

Watu wengi wanapenda kufanya biashara, kuna wengine huwalaumu Ndugu zao au Wazazi wao au waume zao Kwa kushindwa kuwapa mitaji, Jambo Moja la uhakika ni kuwa, hakuna ambaye atakupa mtaji ilhali akijua utapoteza pesa zake.

Biashara ni ngumu Sana Ila pia ni rahisi Sana ukifwata kanuni Fulani. Kabla ya biashara kuna mambo yanapaswa yatangulie, mtaji ni kitu cha mwisho katika mambo ya biashara,

Leo sitasema Sana, Acha niiweke hivi;

I/ Jenga jina lako watu wakufahamu na kukuamini eneo ulilopo, hakikisha iwe sifa njema ya kuvutia.
Jina ndilo huamua Hatma yako.

ii/ Tumia jina lako kutafuta na kujenga mtandao wa watu hasa washirika kimkakati.

iii/ Jenga wahusika ndani yako zaidi ya mmoja.
Hii kwenye nadharia ya Utawiwishaji katika kitabu changu nilisema Kwa mfano, Mimi Taikon, ninajipachua nakutoa Taikon zaidi ya mmoja. Kam ifuatavyo;
Taikon 1
Taikon 2
Taikon 3
Taikon 4
Kila mmoja anauhusika wake kama unauwezo wa kifedha basi ajiri watu wachukue uhusika wako,
Taikon 1 unaweza MPA uhusika wa utakatifu, mwerevu, mwenye Busara, Msomi na sifa zote nzuri.
Huyu atakutana na watu wakubwa, wenye hadhi kwenye jami

Taikon 2 huyu utampa Sifa za unyenyekevu, mpenda wanyonge na Masikini, mtatua kero za jamii, Msuluhishi n.k. huyu atakutana na Tabaka la chini Kabisa

Taikon 3 huyu atakuwa Mafia, mambo ya sirini iwe ya kimungu au kishetani, huyu ni mtu wa dili zenye michongo mirefu. Huyu usimdhihirishe mbele za watu, isipokuwa wahusika maalumu kulingana na Mazingira na wakati.

Biashara ndivyo ilivyo, wateja wanatofautiana hivyo lazima uwe na uhusika tofauti.

iv/ Kazi inayokutambulisha.
Labda mwandishi, mwalimu, Fundi, n.k.
Mbali na biashara hakikisha iwe na Fani nyingine ambayo watu wanaijua.
Mfano, mwanamuziki lakini unauza Duka la nguo.

V/ Tafuta Kibali
Hapa lazima upewe kibali cha Kuendeshea biashara, iwe ukipate Kwa Mungu au Kwa Waganga.
Huwezi fanya biashara yoyote bila kibali kutoka kwenye moja ya pande hizo. Usijedanganywa.

Kama vile unavyosumbuliwa ukiwa huna kibali(Leseni) ya kufanya biashara na TRA ndivyo utakavyohangaika usipopata kibali cha kiroho.

Hili ni Jambo kubwa Sana kwenye biashara.

VI/ mtaji
Hii huja mwishoni kabisa.

Hata mambo ya sijui location hayana umuhimu Kama ukiwa na hayo mambo hapo juu.

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hujawahi niangusha ila wachache watalielewa bandiko lako
 
-Biashara ni,
A--nidhamu ya pesa .
B--Mahesabu .

Mengine yote mbwembwe tu
 
Back
Top Bottom