Kufanya biashara ya ubia partnership na mbongo bora pesa yako ujenge nyumba ya wapangaji

Kuhusu hao ambao hawajajengwa tangu wadogo ni ngumu sana lakini kama kungekuwa na sheria ngumu katika mahakama zetu
Ambao ndio chanzo cha wala rushwa

Mimi nimeishi na kutembea sehemu nyingi duniani
Kuna nchi zingine nimekaa miaka mpaka 10 huko middle east ambapo ukiiba unakatwa mkono

Kwa kweli unaacha gari milango wazi unaingia shopping na kurudi hukuti hata paka kaingia

Sisemi na sisi tuwakate mikono ingawa mnawachoma moto waizi wa kuku na kuwashangilia waizi wa billions

Kama mahakama wataacha rushwa na kufuata sheria na kuwafunga kila wanapopata ushahidi wa kuwaweka jela basi na iwe hivyo

Angalia suala la majizi ya bandari TPA mahakama bado wanavutana ili mwisho wawafutie kesi

Hawa ndugu wanaoiba pia nao ni mtihani mkubwa yaani unamtumia hela akujengee yeye anazila tu na kukupigia picha ya jengo la mtu huyo sijui utamfanya nini

Taumbeane tu mema ila kuamini hata ndugu huko ni ngumu labda muwe na uelewa mmoja
 
Na hao wapangaji labda wawe wahindi.

Mtu akifiwa hata na shemeji yake asiyeishi naye ni excuse ya kutokulipa kodi kwa wakati.
 
Pole sana mkuu yalimkuta mzee wangu na sisi tukarudia kosa
Wafugaji wengi wana tamaa sana yaani ikizaa tu anatamani

Sitaki hata kuwasikia [emoji1]
Kuna mmoja alimpa ndugu yake ng'ombe wa naziwa akakaanae miaka 5. Siku aliyoenda kumchukua alimruka wakaaanzisha kesi, sijui mwisho wao ulikuwaje maana nilihama kile kijiji.
 
Mkuu umegusia TPA. Vipi suala la kubinafsisha, ni sahihi?
 
Sio mbongo tu, Mwafrika kwa ujumla Uaminifu hasa katika mambo ya Pesa na ustaarabu ni sifuri Kabisa.
 
Bongo bahati mbaya chief!
 


Serikali yenyewe partnership haiwezi? Sio issue ya Serikali, parnership ni Jambo gumu.

Kwa case ya jamaa issue sio partnership problem, issue ni jamaa ni mwizi kamwibia.
 
Mimi niko kwenye partnership, mimi ndie niko jikon, naeshirikoana nae wala hajawah fika hapa and we are doing soooo good
 
Hii ni kweli, ila pia tatizo lipo kwenu nyie wabia/partners pia.

Engage lawyer, engage Accountant, engage tax consultant, engage corporate intelligence analist fuata ushauri wao uone kama kuna shida itatokea. (Wataalamu wote hao wapo Tz)

Tatizo kubwa wengi wetu tunafanya mambo hasa biashara kienyeji sana, unaweza kukuta kampuni imesajiliwa na ina operate lakini haijawahi kukaa kikao hata siku moja, unajiuliza how?

Sasa mtu anakimbiaje na mtaji wa $35,000 uliopo kwenye biashara?, hiyo biashara ni lazima inaendeshwa kienyeji tu.

Lakini, pole sana Mkuu.
 
Sijadharau mtu mkuu ila huo ni ukweli biashara na mbongo maelezo ni mengi sana na mengi ni uongo ili akupige tu.
Biashara ya kibongo inaendeshwa kienyeji sana, makubaliano ni ya mdomo tu hakuna maandishi wala lo lote kwa hivyo ni rahisi kwa partner kukimbia na fedha.

Jengine ni kuwa mtu hana 'enterpreneurship skills' (mbinu za ujasiriamali) lakini bado unakwenda kumkabidhi duka la milioni 100 halafu kwa makubaliano ya mdomo tu ati akupe (mfano) milioni mbili kila mwezi. Hakuna mahesabu yanayoeleweka na baada ya muda mfupi duka limepotea.

Tatu ni kwamba baada ya muda mfupi anaona kama vile anakupa fedha za bure amesahau kuwa ule mtaji ni wako.
 
Umenena kweli mkuu,kakimbia nazo Bado atakuwa maskini!
 
Umesema ukweli mswahili ukimkabidhi mali zako au pesa akilala nazo siku mbili tu zinabadilika kua zake, sasa wewe unabadilika kua mdai wake, nayeye anaanza kujipa mwoyo huyu ntampoza tu...loh mbogo ni shida ndo maana mpaka leo hari zetu ni zile zile.
 
Umeongea kweli tupu. Mimi naongezea, hata waliovuka mipaka nao wengi wao ni wale wale tu!

Mfano tu, Mwijaku na baba levo wameenda sana ughaibuni, sasa unadhani kwenda ughaibuni kumewabadili lolote kimtazamo?

Sisi ngozi nyeusi shida sana. Ndio maana hatuwezi kusimamia hata biashara ya familia. Yaani huwezi kukuta familia moja inaendeaha biashara kwa pamoja kama walivyo wahindi, waarabu, wazungu n.k.

Sisi ni majungu tu ndio tunaweza
 
Kwanu huyu mwijaku hajawahi kuenda kuka kule kutafuta maisha zaidi ya tour ya mwezi au wiki, hapo bado hawajabadilika tabia, ila kuna waswahili tumeka zaidi ya miaka 10 mpaka 20 tabia zako zina badilika na kukifunza mengi bila hata kujua unaanza kuwaza kwamba na wenzako wako hivyo loh dhubutu mtu anakuja kwako na shida kukopa 50k kwamba atarudisha kesho, kesho yako ile anaisahau anakuja umuazime 100k eti amefiwa hata haya hawana wapumvavu sana.
 
Pole
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…