Kufanya mauzo makubwa sio kupata faida

Kufanya mauzo makubwa sio kupata faida

Nimejaribu kutoa sababu tu kwanini biashara za mitaani hazikui ama kuwapa watu mafanikio tembea mikoa Mingi biashara zipo sehemu za mijini wanakouza zaidi ya wilaya tatu hizi biashara za mitaani hata mamangi wamezikimbia siku hizi

Nimejaribu kutoa muongozo Nini kifanyike kwa hizi biashara za rejareja mitaani nyingi hazikui pia zinafungwa sababu faida ya asilimia 5-10 haijitoshelezi lazima ufunge tu biashara
Ukisoma biashara u uchumi utajua kwanini bei inauzwa hivyo,...
 
Ndomana biashara ya duka la mangi sitokaa niifanye maana itanitia hasira nitatukana wateja bure imagine mtu anataka kibiriti cha sh 100 au kiwembe cha 100...hawa jamaa wanaouza maduka ya mangi wana uvumilivu sana aisee!
Mtoa mada yupo sahihi,faida atleast iwe asilimia 30 apo watu watapata faida na biashara zitakuwa!
 
mtaji alio nao mtu.. ndio una amua akae upande upi.. kuwa muuzaji wa mwiso au kuwa muuzaji wa kati au kuwa msambazaji mkubwa... ila ni vyema sana kuanzia chini na kwenda juu mana ake una jifunza mengi sana kwenye biashara,, biashara ni kukua kila siku.. na mfanyabiashara yoyote ule nia yake yakila siku nikuwa na mauzo makubwa.. hata kama faida kidogo ndio io io ina jaza kibaba!! nyie vijana wa siku izi mnataka mafaida makubwa ghafla bin vuu!
Nilishafanya sana hizo biashara hizo za rejareja miaka hiyo biashara hizo za faida ndogo nilishindwa kukua baadae nikaja kugundua nilikuwa nakosea nachoongea hapa nauhakika nachoongea hapa zinachelewesha mafanikio

Matumizi ya familia yako kila siku yanakuhitaji

Kuna bidhaa utakopesha na wateja hawatolipa ama mteja analipa na kukopa tena hizi ni hasara

Sio kila bidhaa utaiuza kwa faida Kuna
bidhaa zitakaa mpaka kuharibika

Kuna kuumwa huwezi maliza mwaka bila kuuguliwa na mgonywa mtoto au mke

Michango ya familia huwezi kuikwepa

Bado kama mtu ni mtumiaji wa pombe
 
Ukisoma biashara u uchumi utajua kwanini bei inauzwa hivyo,...
Huwezi kutoboa kwa bidhaa zenye faida asilimia 10 huku unauza mtaani kwako tu huku alikuuzia jumla anauza mkoa mzima solution kwa wewe muuzaji wa reja ni kupandisha bei bidhaa au kuikwepa hiyo bidhaa usiweke dukani kwako na ndio mana supermarket bei zao zinakuwa juu kidogo sababu hili walishaliona
 
hapo ulipo unafanya biashara gani?

watu wanataka unafuu afu unataka mtu akomae na bei kubwa..unataka muuzaji afukuze inzi tu dukani.
Hapa siongelei watu wanaotaka unafuu huyo anaetaka unafuu atakaa hapo kwenye biashara hata miaka 20 bado anatafuta unafuu naongea na watu wanaotaka kukua kwa Kasi kwenye biashara
 
Unapaswa kujua kuna fast & slow moving products.

Kiatu cha laki na 40 mweye duka anaweza kupata faida 30000 mpaka 50000 akiuza, lakini kiatu hicho hicho kinaweza kukaa kwenye shelf miaka 4.

Sheria ya faida inaendana na utokaji wa bidhaa.

Vitu vya bei ndogo ndio vinatoka kwa wingi kwasababu watu wengi wanamudu unafuu wa gharama.

Kwa hiyo kuna uhusiano mkubwa kati ya utokaji wa bidhaa na vipato vya watumiaji.
 
Unapaswa kujua kuna fast & slow moving products.

Kiatu cha laki na 40 mweye duka anaweza kupata faida 30000 mpaka 50000 akiuza, lakini kiatu hicho hicho kinaweza kukaa kwenye shelf miaka 4.

Sheria ya faida inaendana na utokaji wa bidhaa.

Vitu vya bei ndogo ndio vinatoka kwa wingi kwasababu watu wengi wanamudu unafuu wa gharama.

Kwa hiyo kuna uhusiano mkubwa kati ya utokaji wa bidhaa na vipato vya watumiaji.
Kuuza mauzo makubwa unaweza sana tena sana lakini lengo la faida usilifikie inategemea labda hizo fast moving kama unaweza kutumia wilaya zaidi ya mbili kufanya mauzo faida unaipata vizuri

Ila kuuza bidhaa bei kubwa wewe utalenga zaidi wateja wanaohitaji huduma na sio punguzo la bei unakuwa na wateja wachache lakini unawatumia wakuzalishie faida inayopatikana ni kubwa njia hii Mimi naipenda sana sababu wateja wanaofuata huduma wao wanapenda kuona unawajali na kauli nzuri na ndio mana Kuna biashara watu wanauza vitu bei ya juu lakini bado wanapata wateja
 
Nilishafanya sana hizo biashara hizo za rejareja miaka hiyo biashara hizo za faida ndogo nilishindwa kukua baadae nikaja kugundua nilikuwa nakosea nachoongea hapa nauhakika nachoongea hapa zinachelewesha mafanikio

Matumizi ya familia yako kila siku yanakuhitaji

Kuna bidhaa utakopesha na wateja hawatolipa ama mteja analipa na kukopa tena hizi ni hasara

Sio kila bidhaa utaiuza kwa faida Kuna
bidhaa zitakaa mpaka kuharibika

Kuna kuumwa huwezi maliza mwaka bila kuuguliwa na mgonywa mtoto au mke

Michango ya familia huwezi kuikwepa

Bado kama mtu ni mtumiaji wa pombe
Bado kama mtu ni mtumiaji wa pombe🤣🤣
.
kiukweli mkuuu, kutoka kibiashara akili inabidi itulie sana, na ujuwe wapi uwekeze uweze kupata faida na kuwa na mafanikio! siyo kupata hela ya kula.
 
Unavyosema inatakiwa mfanyabiashara apandishe bei ili apate faida unamaanisha nini?


Ninachojua bei ya vitu vingi vya maduka haya ya mtaani bei zake zinajulikana.
 
Mfuko wa 40k anauza 41k mkoa gani huo mkuu hebu toa uongo wako

Halafu unaongelea theoretically na sio practically hebu jaribu kuanzisha duka lako halafu uuze kibiriti kimoja kwa Tshs 500 kama hujaishia kufukuza nzi tu dukani Mc Eddie

Unaongelea bei za supermarket na kucompare na maduka ya mtaani haimake sense angalia Location ya hizo supermarket imezungukwa na watu wa aina gani

Mbna huku kwetu Mburahati kisiwani hawaweki hayo masupermarket???
 
Unavyosema inatakiwa mfanyabiashara apandishe bei ili apate faida unamaanisha nini?


Ninachojua bei ya vitu vingi vya maduka haya ya mtaani bei zake zinajulikana.
Angalia faida inavyopatikana hapa energy ya mo inayojulikana kwa bei ya Tsh 500 katoni moja zipo pisi 10 faida ni Tsh 1000 mfanyabiashara makini atauza energy 600 atakuwa akipata faida 2000 umecheza na faida ya asilimia 20 na wote mtauza mtamaliza kwa wakati mmoja utofauti wa bei hapo ni mdogo sana mteja atanunua tu

Kuna bidhaa nyingine kama vocha sio zakuziweka dukani inategemea na mzunguko mkubwa sana uliyonayo

Ukitembea na faida ya asilimia 20 mafanikio yapo mkuu
 
Nilikuwa najiuliza kwa muda mrefu kwanini hizi biashara za mtaani kwanini hazikui kwanini watu hawatajiriki nyingi zinakufa

Biashara hizi zilizopo mtaani
Maduka ya vitu vya rejareja
Maduka ya vipodozi
Wachoma chips
Migahawa
Maduka ya dawa nk

Kwanini sasa biashara hizi watu hawatajiriki au kupata mafanikio makubwa sababu kubwa ni kuwa kutokuwa na elimu

Biashara za mtaani hazihitaji mauzo makubwa zinazohitaji faida kubwa

Kuna jambo moja wafanyabiashara wa mitaani hawafahamu unavyofanya biashara ni lazima ujue upo kwenye level gani

Ipo hivi kwenye biashara kama biashara yako kila bidhaa unayouza inakupa faida ya asilimia 5-10 biashara yako itakutaka uuze zaidi ya wilaya 2 ili upate faida na wengi wamefanikiwa wafanyabiasha na Mo na Azam wanasambaza energy nchi nzima kila enery faida haizidi sh 100

Jibu nikaja kupata hapa kwanini wafanyabiashara wa mtaani hawafanikiwi wanatafuta faida ndogo sawa na mtu kama Azam huku wao wanauza mtaa mmoja

Maduka ya rejareja energy inapatikana kwa 700 lakini kwa mfanyabiashara makini atauza energy 1000 sababu ukiuza 700 kwenye katoni ya juisi 12 faida 500 ni faida ndogo sana haitokufikisha popote

Anaetengeneza vocha anauza nchi nzima huku wewe unauza mtaani kwako tu vocha za shilingi elfu 20 faida haizidi 1000 kuna kutajirika hapa wadau ebu tujiongeze

Makampuni ya soda yanawataka muuze soda 700 lakini kiuhalisia soda inatakiwa iuzwe 1000 ili upate faida ukiuza soda 700 ni kama unawafanyia wenye makampuni faida utayoipata ni mbuzi

Nimekuja kujifunza kwanini ukienda supermarket bei zinaongezeka kidogo nimegundua biashara wanaifanya kisomi na ndio mana wanazidi kutajirika kama biashara hakuna wateja mtu anaona Bora afunge kuliko kuendelea kupoteza muda muuzaji wa rejareja ni lazima upandishe vitu bei ukiuza bei Ile ya soko linavyotaka ni kama kupoteza muda tu
Mkuu ulishawahi hata kufanya biashara yoyote?!! Bei ya bidhaa inategemea na uwezo wa wanunuzi, kwa uswahilini soda uuze 1000!!??eti utake faida kubwa?! Mtu yupo ladhi kutembea km 1 kuokoa sh. 100 tu. Eti mfanya biashara makini!! Mtu akienda supermarket /hotel kubwa tayari amejiandaa kwa bei za huko, wananchi hawa ni wa kuhurumia tu maisha ni kama wanaigiza kumbe ndio real life hilo!!
 
Mfuko wa 40k anauza 41k mkoa gani huo mkuu hebu toa uongo wako

Halafu unaongelea theoretically na sio practically hebu jaribu kuanzisha duka lako halafu uuze kibiriti kimoja kwa Tshs 500 kama hujaishia kufukuza nzi tu dukani Mc Eddie

Unaongelea bei za supermarket na kucompare na maduka ya mtaani haimake sense angalia Location ya hizo supermarket imezungukwa na watu wa aina gani

Mbna huku kwetu Mburahati kisiwani hawaweki hayo masupermarket???
Bahati nzuri Nina usoefu wa hizi biashara za mitaani nimeanza kuona watu wanamiaka zaidi ya 10 lakini biashara zao hazikui wengi wameshindwa hawajapata mafanikio asilimia 10 ya faida inaishia kula tu

Kama unaona supermarket hawafungui mtaani tayari wenzio ni wajanja walishajua huko mauzo yanapatikana lakini faida haipatikani

Biashara zinazoshamili nchi mzima ni Hawa wafanyabiashara wanafungua biashara town center wanapata faida 10 lakini sababu wapo town center wanahudumia mkoa mzima
 
Nilikuwa najiuliza kwa muda mrefu kwanini hizi biashara za mtaani kwanini hazikui kwanini watu hawatajiriki nyingi zinakufa

Biashara hizi zilizopo mtaani
Maduka ya vitu vya rejareja
Maduka ya vipodozi
Wachoma chips
Migahawa
Maduka ya dawa nk

Kwanini sasa biashara hizi watu hawatajiriki au kupata mafanikio makubwa sababu kubwa ni kuwa kutokuwa na elimu

Biashara za mtaani hazihitaji mauzo makubwa zinazohitaji faida kubwa

Kuna jambo moja wafanyabiashara wa mitaani hawafahamu unavyofanya biashara ni lazima ujue upo kwenye level gani

Ipo hivi kwenye biashara kama biashara yako kila bidhaa unayouza inakupa faida ya asilimia 5-10 biashara yako itakutaka uuze zaidi ya wilaya 2 ili upate faida na wengi wamefanikiwa wafanyabiasha na Mo na Azam wanasambaza energy nchi nzima kila enery faida haizidi sh 100

Jibu nikaja kupata hapa kwanini wafanyabiashara wa mtaani hawafanikiwi wanatafuta faida ndogo sawa na mtu kama Azam huku wao wanauza mtaa mmoja

Maduka ya rejareja energy inapatikana kwa 700 lakini kwa mfanyabiashara makini atauza energy 1000 sababu ukiuza 700 kwenye katoni ya juisi 12 faida 500 ni faida ndogo sana haitokufikisha popote

Anaetengeneza vocha anauza nchi nzima huku wewe unauza mtaani kwako tu vocha za shilingi elfu 20 faida haizidi 1000 kuna kutajirika hapa wadau ebu tujiongeze

Makampuni ya soda yanawataka muuze soda 700 lakini kiuhalisia soda inatakiwa iuzwe 1000 ili upate faida ukiuza soda 700 ni kama unawafanyia wenye makampuni faida utayoipata ni mbuzi

Nimekuja kujifunza kwanini ukienda supermarket bei zinaongezeka kidogo nimegundua biashara wanaifanya kisomi na ndio mana wanazidi kutajirika kama biashara hakuna wateja mtu anaona Bora afunge kuliko kuendelea kupoteza muda muuzaji wa rejareja ni lazima upandishe vitu bei ukiuza bei Ile ya soko linavyotaka ni kama kupoteza muda tu
hiz biashara za maduka ya mitaan kufanikiwa ni ngumu Sana labda zkupe hela ya kula2 swala la kufanikiwa znahitaji nidham ya hali ya juu Sana au uwe na sehem nyingne ambayo itakua inaendesha maisha yako bila kugusa hela ya biashara
 
hiz biashara za maduka ya mitaan kufanikiwa ni ngumu Sana labda zkupe hela ya kula2 swala la kufanikiwa znahitaji nidham ya hali ya juu Sana au uwe na sehem nyingne ambayo itakua inaendesha maisha yako bila kugusa hela ya biashara
Nilikuwa na kiwanda kidogo Cha mikate miaka mikumi iliyopita tulikuwa tunafanya delivery madukani niliona tatizo hili la biashara nyingi za mitaani kushindwa kukua na mwisho wake kufungwa nikagundua makosa hayo yanayofanyika

Mfanyabiashara mwenye mtaji wa million 3-5 anaona ni sawa kupata faida ya laki 3- 6 kwa mwezi kwake ni sawa

Lakini kwa kawaida kwa mtaji huo wa million 3-5 ili biashara yako ikuwe ni lazima upate faida ya kuanzia
mil 1 - 1.5 kwa miezi 10 tu utakuwa umefunga faida ya million 10
 
Nilikuwa na kiwanda kidogo Cha mikate miaka mikumi iliyopita tulikuwa tunafanya delivery madukani niliona tatizo hili la biashara nyingi za mitaani kushindwa kukua na mwisho wake kufungwa nikagundua makosa hayo yanayofanyika

Mfanyabiashara mwenye mtaji wa million 3-5 anaona ni sawa kupata faida ya laki 3- 6 kwa mwezi kwake ni sawa

Lakini kwa kawaida kwa mtaji huo wa million 3-5 ili biashara yako ikuwe ni lazima upate faida ya kuanzia
mil 1 - 1.5 kwa miezi 10 tu utakuwa umefunga faida ya million 10
Noted.
 
Back
Top Bottom