Kufanya mauzo makubwa sio kupata faida

Kufanya mauzo makubwa sio kupata faida

Usinibishie hichi nilichoandika hapa Nipo kwenye business mwaka wa kumi nauzoefu mkubwa naona jinsi biashara za mtaani zinavyoshindwa kukua au kushindwa kuleta matokeo

Kuna makosa madogo yanayofanyika katika upangaji wa bei za bidhaa

Mfano mkoa niliopo energy ya mo madukani mengi wanauza 500 faida yake ni 10%-15% wafanyabiashara makini ukienda kwenye duka lake anauza energy hiyo hiyo kwa 600 faida ya 20%-25 kaongeza sh 100 mteja hawezi kuondoka sababu ya ongezeko hilo nazani umeona gap hilo la faida hapo utapojifunza kwanini biashara moja lakini wanaofanikiwa ni wachache

Hii shilingi 100 inayoongezeka ni kubwa sana kwa mfanyabiashara anayezingatia mauzo yake ya mwezi mzima au mwaka

Unafanya biashara gani na wapi ulipo??

Kwa ujumla ulichoandika hakitekelezeki kwenye maisha ya mtaani.

Kwanza unatakiwa ufahamu hii rule 1 kuhusu wateja, kwamba WATEJA WANA TABIA YA KUAMBIANA/KUSANUANA/KUPEANA TAARIFA.

Mteja anaweza kuacha duka mtaani kwake akafata bidhaa duka mtaa wa 2 kisa tu punguzo la sh 50
 
Ili uweze kuwa mshaur mzur lazima ww mwenywe kile unachokishaur uwe umesha kifanya au unakiishi
Mkuu ulishawah kufanya biashara yeyote?
Tuanzie hapo kwanza
 
Ninayo app nzuri ya kupiga mahesabu ya duka.Inafaa kutumia wakati wa kufanya stock.
1.Unaweza kujua duka lako limekuingizia sh. kwa mwezi au kwa mwaka.
2. Inaonyesha thamani stock iliyopo dukani
3. Inaonyesha Kila bidhaa unayouza Ina faida ya sh. ngapi
4. Kama Kuna upotevu wa fedha inaonyesha.

INAFAA KUTUMIA KWENYE SMART PHONE AU COMPUTER

Ili kuitumia unatakiwa kuwa na rekodi sahihi za Kila manunuzi na mauzo ya Kila siku. Nicheki Whatsapp 0753546162
 
Biashara ya kupangiwe bei ni ngumu sana kutoboa hasa hizo za akina azam na mo itakuchukua miaka sana
Biashara ili ufanikiwe inabid bei uipange wewe mwenyewe na ndo maana maproducer hawa akina mo azam, wanzidii kukua tu kila siku na wakatii huo nyie wauzaji wadog mnaendelea kufunga tu maduka kila siku na kumtafuta mchawii nanii.
 
Nilishafanya sana hizo biashara hizo za rejareja miaka hiyo biashara hizo za faida ndogo nilishindwa kukua baadae nikaja kugundua nilikuwa nakosea nachoongea hapa nauhakika nachoongea hapa zinachelewesha mafanikio

Matumizi ya familia yako kila siku yanakuhitaji

Kuna bidhaa utakopesha na wateja hawatolipa ama mteja analipa na kukopa tena hizi ni hasara

Sio kila bidhaa utaiuza kwa faida Kuna
bidhaa zitakaa mpaka kuharibika

Kuna kuumwa huwezi maliza mwaka bila kuuguliwa na mgonywa mtoto au mke

Michango ya familia huwezi kuikwepa

Bado kama mtu ni mtumiaji wa pombe
Ulivyoacha ukahamia kwenye biashara gani mkuu
 
Angalia faida inavyopatikana hapa energy ya mo inayojulikana kwa bei ya Tsh 500 katoni moja zipo pisi 10 faida ni Tsh 1000 mfanyabiashara makini atauza energy 600 atakuwa akipata faida 2000 umecheza na faida ya asilimia 20 na wote mtauza mtamaliza kwa wakati mmoja utofauti wa bei hapo ni mdogo sana mteja atanunua tu

Kuna bidhaa nyingine kama vocha sio zakuziweka dukani inategemea na mzunguko mkubwa sana uliyonayo

Ukitembea na faida ya asilimia 20 mafanikio yapo mkuu
Mafanikio ni nini mkuu?
 
Tatizo bongo watu tuna vichwa vigumu sana, mawazo ya kuhisi ukipunguza bei utauza sana ni mawazo ya kijinga sana.
maduka ya mtaani unaweza kuta mtu anuza hata laki 4 kwa siku alafu hata kula yake bado ni ya kusuasua achilie mbali maendeleo.
 
Miaka ya nyuma wakati nilipokuwa nasafiri kibiashara kwenda Dubai, Nilikuja kugundua Bidhaa tunazonunua Dubai kwa jumla Bongo ni rahisi zaidi reja reja kuliko hata huko Dubai kwenyewe. niliishia kuachana na ile biashara tu.
 
Miaka ya nyuma wakati nilipokuwa nasafiri kibiashara kwenda Dubai, Nilikuja kugundua Bidhaa tunazonunua Dubai kwa jumla Bongo ni rahisi zaidi reja reja kuliko hata huko Dubai kwenyewe. niliishia kuachana na ile biashara tu.
Biashara gani hyo boss...?
 
Mleta mada unazungumzi faida ipi hyo...?

-Gross profit

-Net profit

Faida haipigwi kwa staili kama hyo......unasahau kuna manunuzi,stock opening&closing n.k

Uzuri duka la mangi TRA hawalitolei macho..
 
Back
Top Bottom