Kufanyike nini sasa ili Hayati Magufuli achukiwe na wote? Naona waliokuwa wanamchukia wanabaki kuwa walewale

Hivi ile mbuga ya chato burigi inaendeleaje mkuu bila kusahau ile international airport kule porini chato

Vipi ule uwanja wa kisasa wa mpira huko chato ambako hamna hata timu ya kijiji nao umekamilika?? Vp chato kuwa miongoni mwa majiji makubwa Afrika mashariki bado unaendelea au ndio imeisha hiyo
 
Kwangu mimi nitamchukia milele kwa mauaji yaliyofanyika katika utawala wake. Lissu aliponywa na Mungu. Alikuwa katili sana mwenye ushetani mwingi tu.
 
wengi tulikuwa hatumpendi lakini si kwa kiwango cha kutaka afe. we miss our President.
 
Lile lilikuwa ni Meo, limekata moto bila machafuko, safi sana. Halita pumzishwa chizi lile, tutalinanga mpaka basi. Maana sasa tuna uhuru.
Binadamu kosa kila kitu kasoro uhuru. Yule chizi alikuwa na fix siyo za karne hii.
 
Alikuwa mwamba, lala salama baba. Alifuta Ile kauli "unanijua Mimi ni nani?" Huenda upigaji unakuja kwa Kasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo ndiyo upuuzi. "Unanijua mimi" maana yake watu waliwekwa ndani/magereza bila sababu za msingi. Fuatilia kipindi cha yule chizi, ndio utajua. Watu wanapewa kesi hazina mbele wala nyuma, hadi ndugu zako wanashangaa. Hiyo ndiyo maana ya unanijua mimi. Mtu alikuwa aki challenge Madudu ya system, ndani ya mwezi unakutana na kesi ya ajabu. Hapo unajua kuwa unanijua mimi maana yake nini?
Leo watu tupo huru, tena huru kweli. Yule mwamba wa Kifala alidanja. Subiri ukazikwe pembeni yake kule Chato.
 
Magufuli angekuwa Bora sana kama angeshika kipaji chake Cha uchapakazi na ufuatiliaji wa viongozi nyoro nyoro, lakini Magufuli alikosa thamani kwa kuwabagua raia kivyama, yeye akawafanya CCM daraja la kwanza. Hakujali kufuata katiba, lolote analosema saa hiyo hiyo linakuwa sheria. Akaamuru Wakurugenzi maeneo yao akishinda mpinzani Mkurugenzi huyo atafute Cha kumueleza. Sanduku la kura likawa haliheshimiwi, matokeo yakawa yanatolewa Kama atakavyo yeye. Matendo haya yaliondoa kabisa thamani yake.
 
Mshamba tu yule.....a covid denial pesdaa? hahahahhh MUNGU HADHIHAKIWI
 
Akifa itakaa poa.Lakini ninyi huu ni muda muafaka mkajilaze pembeni ya shimo lake huku mnajiliza kwa kwikwi.Fuateni ushauri hata dhambi mtafutiwa.
JPM ni best president ever baada ya wazalendo Nyerere na Sokoine! JPM alikuwa reincarnation yao
 
Hata akipendwa na watu wote,haiondoi ukweli kwamba hakua mtu sahihi kuongoza nchi
 
Wezi walioiba CCM na Serikalini ndio vinara wa kumsema vibaya Magufuli.Mungu yupo hajafa

Wezi wa mali za CCM na waliokwapua Pesa za umma kwa njia mbalimbali ziwe za moja kwa moja au tenda sasa hivi ndio vinara wa kuponda marehemu Magufuli

Wanaweza kujifanya kujisafisha waonekane wazuri mbele ya wananchi kwa laghai zao wakati ni uozo mtupu

Wakumbuke kitu kimoja Mungu hajafa kama Magufuli yuko hai anajua uovu wao vizuri sana na anajua cha kufanya

Waweza laghai wananchi na wakamdhihaki sana marehemu Magufuli huku wakikenua meno ila wakumbuke kitu kimoja Mungu.yuko hai hafi leo wala Kesho ambaye halaghaiwi wala hadhihakiwi na ndie mshika hatima za leo na Kesho na za kizazi vyao vya leo na Kesho.Awezae kujua awafanyie nini majizi na walaghai na vizazi vyao vya leo na Kesho

Kifupi wezi wote na walaghai mnaojitia kumponda Magufuli kesi zenu tunamwachia Mungu
 
Membe alisema nchi ilitekwa na warundi, vetting system ilikuwa paralysed.
Hao mamluki viongozi wameingiza mamluki wenzao wengi katika uongozi wa nchi
Na walileta ya kutoka huko kwao kuuana na kutekana.

Sasa hao unaowaita CCM na serikali, kina Bashiru na Magufuli, inajulikana walikotoka.
Nchi hii ina wenyewe.
 
Membe alisema nchi ilitekwa na warundi, vetting system ilikuwa paralysed.
Sasa hao unaowaita CCM na serikali, kina Bashiru na Magufuli, inajulikana walikotoka.
Nchi hii ina wenyewe.
Membe huyo mwizi aliyeiba hela za Libya kuwa zinaenda kujenga kiwanda kusini akazifisadi au Membe yupi unayemuongelea?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…