Kufanyike nini sasa ili Hayati Magufuli achukiwe na wote? Naona waliokuwa wanamchukia wanabaki kuwa walewale

Kufanyike nini sasa ili Hayati Magufuli achukiwe na wote? Naona waliokuwa wanamchukia wanabaki kuwa walewale

Wanashindana na kivuli cha Magufuli lakini bado kinawabwaga chini!! Magufuli alipendwa sana na watanzania walio wengi!! Ila kuna sehemu ndogo ya watanzania hasa mafisadi na jamaa zao, wakwepa kodi, na wale waliotaka kuleta ugaidi huko kibiti na rufiji na familia zao, hao kwa kweli hatuwezi kuwalaumu wakimchukia, aliwashughulikia vilivyo ila ni kwa manufaa ya Tanzania!
Hivi ile mbuga ya chato burigi inaendeleaje mkuu bila kusahau ile international airport kule porini chato

Vipi ule uwanja wa kisasa wa mpira huko chato ambako hamna hata timu ya kijiji nao umekamilika?? Vp chato kuwa miongoni mwa majiji makubwa Afrika mashariki bado unaendelea au ndio imeisha hiyo
 
Kwangu mimi nitamchukia milele kwa mauaji yaliyofanyika katika utawala wake. Lissu aliponywa na Mungu. Alikuwa katili sana mwenye ushetani mwingi tu.
 
wengi tulikuwa hatumpendi lakini si kwa kiwango cha kutaka afe. we miss our President.
 
Sitakaa nisahau ile tr 1.5

Sitakaa nisahau ujenzi wa air port Chato bila kuidhinishwa na bunge (ufisadi) sitakaa nisahau hospital kubwa kuliko kcmc kujengwa porini chato badala hata kujengwa Mwanza jijini.

Sitasahau manunuzi ya ndege bila kuidhinishwa na bunge wala kutangazwa zabuni kama sheria zinavyotaka

Sitasahau watu wanatoa ushauri kuambiwa wanawashwawashwa

Sitasahau maiti za watz wenzetu kuokotwa kwenye sandarusi

Sitasahau watumiaji wa kivuko kigamboni kuambiwa wapige mbizi

Sitasahau watu wa kimara kuvunjiwa nyumba kwamba wamejenga kwenye hifadhi ya barabara lakini wa mwanza ikazuiwa wasivunjiwe ilhali wamejenga eneo la barabara kisa eti ndio waliompigia kura

Sitasahau gharama iliyotumika kununua wapinzani eti wanaunga mkono juhudi

Sitasahau watu kupigwa risasi mchana kweupe kisa ana mawazo tofauti na ya mtawala

Sitasahau wakurugenzi kupewa maagizo eti "nikupe kazi, nikupe gari, nikupe mshahara na nyumba halafu umtangaze mpinzani kashinda huna kazi"

Yapo mengi, kwa leo naishia hapa
Lile lilikuwa ni Meo, limekata moto bila machafuko, safi sana. Halita pumzishwa chizi lile, tutalinanga mpaka basi. Maana sasa tuna uhuru.
Binadamu kosa kila kitu kasoro uhuru. Yule chizi alikuwa na fix siyo za karne hii.
 
Alikuwa mwamba, lala salama baba. Alifuta Ile kauli "unanijua Mimi ni nani?" Huenda upigaji unakuja kwa Kasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo ndiyo upuuzi. "Unanijua mimi" maana yake watu waliwekwa ndani/magereza bila sababu za msingi. Fuatilia kipindi cha yule chizi, ndio utajua. Watu wanapewa kesi hazina mbele wala nyuma, hadi ndugu zako wanashangaa. Hiyo ndiyo maana ya unanijua mimi. Mtu alikuwa aki challenge Madudu ya system, ndani ya mwezi unakutana na kesi ya ajabu. Hapo unajua kuwa unanijua mimi maana yake nini?
Leo watu tupo huru, tena huru kweli. Yule mwamba wa Kifala alidanja. Subiri ukazikwe pembeni yake kule Chato.
 
Tusifichane,

Imebaki kuwa wale wale wenye chuki na Hayati JPM, tena ni wale wale ambao yeye aliwaita wakwamishaji wa maendeleo ya nchi, na aliwashughurikia kisawasawa

Waliokuwa wakila pesa za walipakodi Kwa mgongo wa wafanyakazi hewa, ndio hao hao wana chuki naye mpaka leo, kwa sababu mirija yao ilizibwa!

Wenzangu na Mimi waiba majina ya watu ili tu waajiriwe bila kupita shule, ndio hao hao wameendelea kumchukia, lakini majuzi kuna rafiki yangu mmoja alimshukuru JPM baada ya yeye kutimliwa akiwa na cheti feki kipindi hiko, aliamua kuingia shule kwa hasira, amehitim majuzijuzi na akaajiriwa idara ya Maji Dawasa, alimshukuru saana JPM kwa kumfanya awe na elimu bora!

Wale waliokuwa wakishirikiana na mabeberu ili kukwamisha ujenzi wa Bwawa la Umeme Rufiji na mazungumzo ya wamiliki wa migodi mbalimbali nchini ndio hao kila leo kelele na bahati mbaya wako mpaka huko juu, na ndiyo maana hata mradi huo hauendi utadhani anayekomolewa ni JPM, kumbe tunakomolewa wananchi! Hizo hasira zingine hazifai bhana!!

Mashoga wenyewe wanajulikana, bishara zao walizifanya kwa taaabu mno kiasi kwamba wakaingia kinyongo na JPM

Hata hivyo, Raia wema na wapenda nchi, wote walimwelewa huyu mwamba na bado wako upande wake lije jua au inyeshe Mvua, wataendelea kumtetea kila kunapotokea uhuni!

Na cha kushangaza, hao hao 2025 wataomba kura kwa kutumia jina na mifano yake ya uchapa kazi!
Magufuli angekuwa Bora sana kama angeshika kipaji chake Cha uchapakazi na ufuatiliaji wa viongozi nyoro nyoro, lakini Magufuli alikosa thamani kwa kuwabagua raia kivyama, yeye akawafanya CCM daraja la kwanza. Hakujali kufuata katiba, lolote analosema saa hiyo hiyo linakuwa sheria. Akaamuru Wakurugenzi maeneo yao akishinda mpinzani Mkurugenzi huyo atafute Cha kumueleza. Sanduku la kura likawa haliheshimiwi, matokeo yakawa yanatolewa Kama atakavyo yeye. Matendo haya yaliondoa kabisa thamani yake.
 
Mshamba tu yule.....a covid denial pesdaa? hahahahhh MUNGU HADHIHAKIWI
 
Akifa itakaa poa.Lakini ninyi huu ni muda muafaka mkajilaze pembeni ya shimo lake huku mnajiliza kwa kwikwi.Fuateni ushauri hata dhambi mtafutiwa.
JPM ni best president ever baada ya wazalendo Nyerere na Sokoine! JPM alikuwa reincarnation yao
 
Hata akipendwa na watu wote,haiondoi ukweli kwamba hakua mtu sahihi kuongoza nchi
 
Wezi walioiba CCM na Serikalini ndio vinara wa kumsema vibaya Magufuli.Mungu yupo hajafa

Wezi wa mali za CCM na waliokwapua Pesa za umma kwa njia mbalimbali ziwe za moja kwa moja au tenda sasa hivi ndio vinara wa kuponda marehemu Magufuli

Wanaweza kujifanya kujisafisha waonekane wazuri mbele ya wananchi kwa laghai zao wakati ni uozo mtupu

Wakumbuke kitu kimoja Mungu hajafa kama Magufuli yuko hai anajua uovu wao vizuri sana na anajua cha kufanya

Waweza laghai wananchi na wakamdhihaki sana marehemu Magufuli huku wakikenua meno ila wakumbuke kitu kimoja Mungu.yuko hai hafi leo wala Kesho ambaye halaghaiwi wala hadhihakiwi na ndie mshika hatima za leo na Kesho na za kizazi vyao vya leo na Kesho.Awezae kujua awafanyie nini majizi na walaghai na vizazi vyao vya leo na Kesho

Kifupi wezi wote na walaghai mnaojitia kumponda Magufuli kesi zenu tunamwachia Mungu
 
Wezi walioiba CCM na Serikalini ndio vinara wa kumsema vibaya Magufuli.Mungu yupo hajafa

Wezi wa mali za CCM na waliokwapua Pesa za umma kwa njia mbalimbali ziwe za moja kwa moja au tenda sasa hivi ndio vinara wa kuponda marehemu Magufuli

Wanaweza kujifanya kujisafisha waonekane wazuri mbele ya wananchi kwa laghai zao wakati ni uozo mtupu

Wakumbuke kitu kimoja Mungu hajafa kama Magufuli yuko hai anajua uovu wao vizuri sana na anajua cha kufanya

Waweza laghai wananchi na wakamdhihaki sana marehemu Magufuli huku wakikenua meno ila wakumbuke kitu kimoja Mungu.yuko hai hafi leo wala Kesho ambaye halaghaiwi wala hadhihakiwi na ndie mshika hatima za leo na Kesho na za kizazi vyao vya leo na Kesho.Awezae kujua awafanyie nini majizi na walaghai na vizazi vyao vya leo na Kesho

Kifupi wezi wote na walaghai mnaojitia kumponda Magufuli kesi zenu tunamwachia Mungu
Membe alisema nchi ilitekwa na warundi, vetting system ilikuwa paralysed.
Hao mamluki viongozi wameingiza mamluki wenzao wengi katika uongozi wa nchi
Na walileta ya kutoka huko kwao kuuana na kutekana.

Sasa hao unaowaita CCM na serikali, kina Bashiru na Magufuli, inajulikana walikotoka.
Nchi hii ina wenyewe.
 
Membe alisema nchi ilitekwa na warundi, vetting system ilikuwa paralysed.
Sasa hao unaowaita CCM na serikali, kina Bashiru na Magufuli, inajulikana walikotoka.
Nchi hii ina wenyewe.
Membe huyo mwizi aliyeiba hela za Libya kuwa zinaenda kujenga kiwanda kusini akazifisadi au Membe yupi unayemuongelea?
 
Back
Top Bottom