Kufundisha Watu Kura ya Ndiyo (Serikali), Hapana (Maaskofu,UKAWA) ni Sahihi?

Kufundisha Watu Kura ya Ndiyo (Serikali), Hapana (Maaskofu,UKAWA) ni Sahihi?

Not_Yet_Uhuru

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2010
Posts
1,304
Reaction score
432
Wadau wa JF Great Thinkers,

Kwa wale wanaotaka kuutambua ukweli ili ukweli uwaweke huru na wadumu ktk nuru hiyo daima wataafikiana na uwazi na wataukubali ukweli hata kama unawaumiza saana, watajua ndio mwelekeo wa haki.

Tangu mwaka jana, mara baada ya kumalizika kwa bunge maalumu la katiba, serikali ya ccm ilifanya matamasha, kuhamasisha na kusherehekea 'katiba pendekezwa' kuwa 'ccm wameshinda' dhidi ya 'wapinga rasimu ya 2 ya katiba' kama ilivyowasilishwa na jaji joseph sinde warioba. Hii ikimaanisha kuwa ccm walianza kusherehekea [hadi kucheza taarabu bungeni waziwazi] hata kabla ya kuanza kunadi kwa wananchi ili waelewe kilichoandikwa ndani ya chapisho hilo waliloliita 'katiba pendekezwa' na pia mikakati iliwekwa kuhakikisha kuwa chapisho hili halisambazi mapema sana, halichapishwi nakala nyingi sana, na haliwafikii wengi saana [tofauti na walengwa wa ccm], hii yote ni kuhakikisha kuwa mikakati ya watawala kuelekeza watu waipigie kura ya ndio inafanikiwa siku na wakati utakapofika. Siyo hivyo tu:

* Kikwete mwenyewe na makamu wake kupitia serikali yake yote iliandaa bajeti ya mabilioni ili kuhakikisha vyombo vya habari [hasa vinavyomilikiwa na serikali, na hasa tbc1, magazeti, radio na vile vingi vya binafsi ila vinavyoendeshwa 'kinjaa njaa' kuwa upande wa kuwaelekeza na kuwafundisha wananchi la kufanya] vinaandaa programu kabambe kuhamasisha na kuwaelekeza wananchi popote waipigie katiba pendekezwa kura ya ndiyo!!! Toka mwaka jana hadi leo hii 'mafundisho' hayo na 'maelekezo' hayo ya kupiga kura ya ndiyo yanaendelea!! Ukweli ni uhuru na hatuwezi kufumbia macho unafiki au woga utokanao na watawala, au wapambe wao wanaohemea ktk meza zao ili kushibishwa na kusahau utu wao.

Je, hayo yote yaliyofanyika kwa aidi ya miezi 7, hayakuwa mafundisho, maelekezo na kuingilia uhuru wa mwananchi kusema ndiyo au hapana?? Kwa nini serikali haikuwaelekeza kuwa wasome machapisho hayo ili siku ya kura 'waamue watakavyo'?? Bali inasema wazi wazi kuwa waipigie kura ya ndiyo?? Unafiki! Mhashamu kardinali pengo hakupata ufahamu wa 'matenddo haya maovu' ya serikali na ccm kuingilia 'akili au dhamira' za wananchi [ambao ndio waumini wake pia] kuwaelekeza wapige kura ya ndiyo badala ya kujiamulia wenyewe? Upofu huo!

* Baraza la maaskofu na jumuiya za makanisa ya kikristo yaliyotoa tamko rasmi hivi karibuni la kuwaelimisha waumini na watanzania wote waiosome katiba pendekezwa [ambayo hata hivyo imefichwa-fichwa, tena wasioielewa, na imevurugwa mambo muhimu] na kuipigia kura ya hapana ili 'kuikataa' ni tamko na fundisho sahihi kabisha ni la haki, elimu sahihi, na iliyojaa ukweli na unayoutenga unafiki pembeni na kueneza nuru itawale ili taifa lipate chombo sahihi, na kamilifu kinachoitwa katiba ya wote. Maaskofu na viongozi hawa wa dini walichelewa sana kutoa tamko au mafundisho yao maana serikali ilianza toka mwaka jana, ndipo ukawa nao wakaikabili serikali na ccm kwa kuwaelekeza wafuasi wa wasiipigie kura! Lakini ukweli ni kuwa baraza la maaskofu na jumuiya za makanisa ya kikristo tanzania, wapo sahihi, wapo ktk haki na tunawaomba wasimamie waliyoyasema na kuyaelekeza makanisa yote tanzania nzima, waumini wao wasimame imara kupiga kuwa ya 'hapana'!

Haki inajibiwa kwa haki, na sio dhuluma! Kama serikali imetumia miezi zaidi ya 7 kuwafundisha wananchi wapige kuwa ya 'ndiyo' basi viongozi wetu wa dini wapo sahihi kuwafundisha waumini wao wapige kura ya 'hapana' angalau kwa hizi wiki chache zilizobakia, ili haki ikamilike! Kuwakemea maaskofu kwa tamko lao ni unafiki, upofu na woga wa kuukwepa ukweli, au 'kujipendekeza kwa kaisari'. Mh askofu mkuu kardinali pengo angetambua kuwa kushirikiana na 'kaisari' [serikali] kuwapokonya watauwa haki, 'kuwanyima kauli' au kuwaingiza wtu ktk giza nene kama la kuipa nchi katiba mbovu...hii dhambi haitafutika usoni pako daima!! Hii ni kwaresma...tutende haki-kwa-haki.

Nawasilisha kwa mjadala!
 
vote-no.jpg
vn.jpg
I_AM_VOTING__NO_2_t266x200.gif
 
Baba Askofu Cardinali Pengo alipotoka na naamini hadi sasa atakuwa ameshagundua kosa lake kwenye hili na naamini ataliachia baraza la maaskofu na na Jukwaa la wakristo wafanye vyema kazi yao iliyotukuka. ukitaka kujua kuhusu hili hutamsikia tena Cardinali Pengo akiuongelea suala hili hadharani !!
 
Waumini tutafuata mwongozo na maelekezo ya Wachungaji wetu kama yalivyoainishwa katika waraka wa baraza la kikristo; serikali na wahafidhina wa CCM wapende wasipende. period
 
ilitakiwa tuanze kushangaa waliotupendekezea katiba mara baada ya kuwashambulia waliopiga kura ya hapanna kuanza kusakamwa.
 
Watu wahamasishwe tu kujitiokeza kwa wingi kupiga kura na viongozi watendaji wa serikali na dini.

Lakini viongozi wa vyama vya siasa ruksa kueleza wanataka watu wapige upande gani.

Ila nadhani kuna tatizo la viongozi hasa wa dini kuchanganya mambo kisa eti wamemsikia raisi kasema watu wapige kura ya ndiyo.Raisi ni mwenyekiti wa CCM taifa.Akiongea mambo ya kutaka watu wapige kura ya ndiyo anaongea msimamo wa chama chake yeye akiwa kiongozi wa chama.

Lakini inapofika askofu ambaye anaongoza kanisa lenye wanachama wa UKAWA ,CCM na wasio na vyama naye akajitosa eti kupigia debe eti kura ya ndiyo au hapana hapo anakuwa hajui vizuri kazi yake kama kiongozi wa dini kwa waumini wake wenye vyama tofauti na misimamo tofauti ya kisiasa.Maaskofu ni vizuri wabakie kwenye majoho yao siasa wawaachie waumini.Askofu awaambie tu waende kupiga kura kwa kadri ya dhamiri zao kisha aendelee kuwaswalisha wakishatoka kupiga hiyo kura sawasawa na dhamiri zao.
 
Baba Askofu Cardinali Pengo alipotoka na naamini hadi sasa atakuwa ameshagundua kosa lake kwenye hili na naamini ataliachia baraza la maaskofu na na Jukwaa la wakristo wafanye vyema kazi yao iliyotukuka. ukitaka kujua kuhusu hili hutamsikia tena Cardinali Pengo akiuongelea suala hili hadharani !!

Kardinali Pengo amewazuga tu. Kama alikuwa hakubaliani na baraza la Wakristo mbona alikuwa na uwezo wa kuzuia tamko lisisomwe kwenye Jimbo Kuu la Dar er Salaam?
 
Baba Askofu Cardinali Pengo alipotoka na naamini hadi sasa atakuwa ameshagundua kosa lake kwenye hili na naamini ataliachia baraza la maaskofu na na Jukwaa la wakristo wafanye vyema kazi yao iliyotukuka. ukitaka kujua kuhusu hili hutamsikia tena Cardinali Pengo akiuongelea suala hili hadharani !!

Ukishakunywa maji ya bendera ya kijani siyo rahisi kuacha!! plus kuangalia ule Mwenge wenye makafara ni hatari!
 
not_yet_uhuru tambua kwamba serikali ni kaizari na maaskofu ni watumishi wa bwana.

serikali kufundisha wananchi wapige kura ya ndio wako sahihi kabisa kwa kuwa katiba ni mtoto wao waliyemuasisi na wanataka kumhalalisha lakini ikitokea watumishi wa bwana wanaingilia serikali na kuwadanganya waumini kwamba ati watapata dhambi wakipiga kura ya ndio hapo unapaswa kutia shaka uadilifu wa hao watumishi wa bwana kwani wameenda kinyume na usemi wa "ya kaizari mpe kaizari na ya Mungu mpe Mungu".

watuache tuisome kwani dunia yetu chaguo letu sisi ndio tutaamua tupige kura ya ndiyo au hapana
 
Kardinali Pengo amewazuga tu. Kama alikuwa hakubaliani na baraza la Wakristo mbona alikuwa na uwezo wa kuzuia tamko lisisomwe kwenye Jimbo Kuu la Dar er Salaam?

Hakutaka kuleta vurugu ndani ya kanisa sababu kuna mapadri UKAWA ambao kutwa ni kuhubiri habari za UKAWA wangezisoma hizo barua kwa nguvu kwa maana wamepotoka kiasi kuwa wanawaza siasa kuliko dini walizokabidhiwa.Pia kuna waumini vichaa kanisani ambao wangeleta vurugu kanisani kama zisingesomwa.
Mzee pengo ni mtu mzima katulia aliona atafute wakati muafaka wa kutoa tamko.
 
Watu wahamasishwe tu kujitiokeza kwa wingi kupiga kura na viongozi wa serikali na dini.

Lakini viongozi wa vyama vya siasa ruksa kueleza wanataka watu wapige upande gani.

Ila nadhani kuna tatizo la viongozi hasa wa dini kuchanganya mambo kisa eti wamemsikia raisi kasema watu wapige kura ya ndiyo.Raisi ni mwenyekiti wa CCM taifa.Akiongea mambo ya kutaka watu wapige kura ya ndiyo anaongea msimamamo wa chama chake yeye akiwa kiongozi wa chama.

Lakini inapofika askofu ambaye anaongoza kanisa lenye wanachama wa UKAWA ,CCM na wasio na vyama naye akajitosa eti kupigia debe eti kura ya ndiyo au hapana hapo anakuwa hajui vizuri kazi yake kama kiongozi wa dini kwa waumini wake wenye vyama tofauti na misimamo tofauti ya kisiasa.Maaskofu ni vizuri wabakie kwenye majoho yao siasa wawaachie waumini.Askofu awaambie tu waende kupiga kura kwa kadri ya dhamiri zao kisha aendelee kuwaswalisha wakishatoka kupiga hiyo kura sawasawa na dhamiri zao.

Rais pia ni kiongozi wa nchi na yeye alipaswa kusisitiza watu wajitokeze kupigia kura katiba pendekezwa kwa kadri ya uelewa wao na c kusema wapigie kura ya ndio mkuu
 
Serikali si ndo CCM? Kwani hawataiba kura au kuchakachua matokeo?
 
Viongozi wa dini wanatoa unabii kwa mambo yajayo na kutoa ushauri nini cha kufanya
 
Back
Top Bottom