Asante.Hii comment yako naenda kuiwekea lamination kabisa
Hivi wazee wetu huko nyuma walikuwa na michango kama hivi sasa? Huwa nashangaa sana mtu anataka kuoa lakini ametageti michango kutoka kwa watu ili kufanikisha harusi yake utafikiri tutakuwa tunato**** wote.Mkuu,ukiachana na ujima,pia Pressure ya kuridhisha walimwengu ni kubwa mno.Usipofanya makuu utasimangwa,ukijitutumua na michango ndio kadhia kama za mleta mada..
Bila ya msimamo dhabiti,watu wengi hawaishi maisha yao.
Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
Umaskini mbaya, tafuta pesa.
hapo ndoambapo tumeshindwa kuelewana nimesemea kulingana na mleta mada hapo juu kuchangiwa harusi ni jambo la kawaida sababu tumelikuta na tunaendelea kuchangishanaUmesema suala la kuendeleza utamaduni bila kujadili uzuri au ubaya wa utamaduni.
Kama unaweza kula mavi kwa sababu ni utamaduni wenu tu, sina cha kujadiliana nawe zaidi.
Nikijadiliana nawe zaidi unaweza kuniambukiza kipindupindu cha akili buree.
Word[emoji108]Vijana wa sasa, nimegundua kujikweza na kutaka kufanya harusi kubwa kuliko uwezo wao ndio kinacho wagharimu.
Lets say “Ukioa kimya kimya kuna ubaya gani” ukitoka zako kufunga ndoa kanisani alika ndugu wa karibu wa pande zote mbili na marafiki wachache nendeni sehemu tulivu kwa gharama zako binafsi wapige chakula na vinywaji hadi watambae na uhakika ukitenga milioni tano zinatosha kabisa kuwachachafya, baada ya hapo beba mke wako nendeni mkajenge familia.
Mambo ya kutaka kuwekwa instagram page za ma MC maarafu ndio zinawaponza, mbona miaka yetu tulioa huko vijijini na ilikuwa ni mwendo wa wali na nyama ya ng’ombe na mziki wa kawaida mambo yanaisha na leo tupo imara katika ndoa tofouti na hawa wanaofunga ndoa kwa gharama kubwa kisha wanaishia kuacha ndani ya miaka michache.
Na mimi nakwambia hivi, jambo kuwa la kawaida kwa sababu umelikuta, ni utamaduni wetu, si hoja.hapo ndoambapo tumeshindwa kuelewana nimesemea kulingana na mleta mada hapo juu kuchangiwa harusi ni jambo la kawaida sababu tumelikuta na tunaendelea kuchangishana
Hata Mimi ungenipoteza kama Rafiki.Nilikua na washkaji wengi kabla ya kufunga ndoa na ndugu wengi nilikua nawachangia sana kwenye misiba na harusi lakini Mimi nilivotangaza ndoa wakaniunga mkono muda ulipofika nikipiga cm wana hawapokei wala kujibu text
Nikakausha nikakomaa likapita saivi wengine wanaishia kuview status WhatsApp tu na wengine tukionana wanajikanyaga tu
Nimeamua saivi nitachangia misiba tu Teena ila ya moja kwa moja cjui kipaimara harusi cjui nini mwisho na Nina list ya walionichangia ndo nataka tu kuwarudishia michango yao baasi
Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Jamii ikijiongeza utamaduni huu utakufa wenyewe.Hata Mimi ungenipoteza kama Rafiki.
Huu upumbavu Wa kuchangishana Harusi sijui unapaswa ufe Mara moja. Binafsi huwa sichangii mtu Harusi, kwa maana sikuomba mchango kwa mtu pia.
well said,case closedNa mimi nakwambia hivi, jambo kuwa la kawaida kwa sababu umelikuta, ni utamaduni wetu, si hoja.
Tungetumia mantiki hiyo, kusingekuwa na maendeleo yoyote yanayobadilika kwa kubadilisha utamaduni katika jamii.
Tujadili uzuri au ubaya wa jambo, tusijadili jambo ni la kawaida tumelikuta, ni utamaduni wetu, na tunaliendeleza.
After all, kawaida ya jana inaweza kuonekana si kawaida leo, kwa sababu jamii inaenda ikijiongeza na tamaduni zinabadilika.
Ndiyo maana kuna tamaduni za kutahiri wanawake zilionekana kawaida zamani, leo zinaachwa.
Kwa hivyo, kama tunataka kukubali au kukataa kitu, tujadili uzuri au ubaya wa kitu.
Tusiweke hoja ya "huu ni utamaduni wetu, tumeukuta na tutauendeleza".
Kwa sababu, kwanza, kitu kuwa utamaduni haimaanishi automatically ni kizuri.
Tulikuwa na tamaduni Watemi wa makabila wakifa wanazikwa na watu walio hai.
Siku hizi huo utamaduni wa kuwa na watemi tumeuondoa, tumeazimia kujenga nchi isiyo na matabaka ya watemi.
Lakini pia, hata kama ni utamaduni ambao hapo awali ulikuwa mzuri, dunia inabadilika.
Inawezekana utamaduni huo ulikuwa mzuri katika dunia ya ujima huko nyuma, lakini leo katika dunia ya teknolojia ukawa mbaya. Hautuendelezi, unatubwetesha tusiendelee kwenda na dunia ya leo, unatubakisha kwenye ujima.
Kwa hivyo hata kama utamaduni ulikuwa mzuri hapo awali, hiyo si sababu ya kuendelea nao tu kwa sababu tu "huu ni utamaduni wetu tunauendeleza".
Inabidi tuuchunguze na kuangalia kama unatufaa au hautufai.
huu ni umasikini uliopitiliza,,, raha zako wewe iwe tabu kwa wengine!?Nilikua na washkaji wengi kabla ya kufunga ndoa na ndugu wengi nilikua nawachangia sana kwenye misiba na harusi lakini Mimi nilivotangaza ndoa wakaniunga mkono muda ulipofika nikipiga cm wana hawapokei wala kujibu text
Nikakausha nikakomaa likapita saivi wengine wanaishia kuview status WhatsApp tu na wengine tukionana wanajikanyaga tu
Nimeamua saivi nitachangia misiba tu Teena ila ya moja kwa moja cjui kipaimara harusi cjui nini mwisho na Nina list ya walionichangia ndo nataka tu kuwarudishia michango yao baasi
Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Naunga mkono maelezo yako, ila huu utamqduni ambao tumeukita iko hata ya kuubadilisha , hii ni kulingana na mwenendo wa maisha ya sasa. Mfano; mtu atatumia zaidi ya milioni 10 kwa ajili ya sherehe ya harusi, je hebu mpe mtu anae- straggling na maisha hiyo million 10 uone baada ya mwaka atakuwa kwenye level gani. So guys, we have to think about this. Ni bora tuchange ili akaanzie maisha na sio kula na kunywa kwenye li ukumbi la kifahari halafu baada ya siku kadhaa mnaulizana kodi imeisha tukamkope nani. NO si sawa.Na mimi nakwambia hivi, jambo kuwa la kawaida kwa sababu umelikuta, ni utamaduni wetu, si hoja.
Tungetumia mantiki hiyo, kusingekuwa na maendeleo yoyote yanayobadilika kwa kubadilisha utamaduni katika jamii.
Tujadili uzuri au ubaya wa jambo, tusijadili jambo ni la kawaida tumelikuta, ni utamaduni wetu, na tunaliendeleza.
After all, kawaida ya jana inaweza kuonekana si kawaida leo, kwa sababu jamii inaenda ikijiongeza na tamaduni zinabadilika.
Ndiyo maana kuna tamaduni za kutahiri wanawake zilionekana kawaida zamani, leo zinaachwa.
Kwa hivyo, kama tunataka kukubali au kukataa kitu, tujadili uzuri au ubaya wa kitu.
Tusiweke hoja ya "huu ni utamaduni wetu, tumeukuta na tutauendeleza".
Kwa sababu, kwanza, kitu kuwa utamaduni haimaanishi automatically ni kizuri.
Tulikuwa na tamaduni Watemi wa makabila wakifa wanazikwa na watu walio hai.
Siku hizi huo utamaduni wa kuwa na watemi tumeuondoa, tumeazimia kujenga nchi isiyo na matabaka ya watemi.
Lakini pia, hata kama ni utamaduni ambao hapo awali ulikuwa mzuri, dunia inabadilika.
Inawezekana utamaduni huo ulikuwa mzuri katika dunia ya ujima huko nyuma, lakini leo katika dunia ya teknolojia ukawa mbaya. Hautuendelezi, unatubwetesha tusiendelee kwenda na dunia ya leo, unatubakisha kwenye ujima.
Kwa hivyo hata kama utamaduni ulikuwa mzuri hapo awali, hiyo si sababu ya kuendelea nao tu kwa sababu tu "huu ni utamaduni wetu tunauendeleza".
Inabidi tuuchunguze na kuangalia kama unatufaa au hautufai.
Naunga mkono hoja.Naunga mkono maelezo yako, ila huu utamqduni ambao tumeukita iko hata ya kuubadilisha , hii ni kulingana na mwenendo wa maisha ya sasa. Mfano; mtu atatumia zaidi ya milioni 10 kwa ajili ya sherehe ya harusi, je hebu mpe mtu anae- straggling na maisha hiyo million 10 uone baada ya mwaka atakuwa kwenye level gani. So guys, we have to think about this. Ni bora tuchange ili akaanzie maisha na sio kula na kunywa kwenye li ukumbi la kifahari halafu baada ya siku kadhaa mnaulizana kodi imeisha tukamkope nani. NO si sawa.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Hapo ni kweli mkuu, ila ipo haja ya kuliangalia kwa undani jambo hili.Naunga mkono hoja.
Tatizo kuna watu washachanga sana wakisubiri na wao kuchangiwa, na hao ukiwaambia tunaondoa utamaduni huu, wataona umewaonea.
Kwa sababu wao walichangia wengine kwa madhumuni ya kuchangiwa.