Kufuta namba ya simu ya marehemu inauma sana

Kufuta namba ya simu ya marehemu inauma sana

Kufuta unajiskia vibaya unaona kama unampotezea ama unajaribu kumfuta kicgwani marehemu
Kuiacha nayo ni kujiongezea machungu.

Nilibaki na namba za swahiba wangu na kaka yangu kwenye simu kwa miaka takribani miaka mi3 toka umauti wao uwafike.

Allah awasamehe madhambi yao, hakika nao ni waja si wakamilifu, kukosea ni sehemu ya maisha ya mwanadamu, awapunguzie adhabu za kaburi.
Inauma saana, ni mara chache saana mwanaume kumwaga chozi[emoji24], inatokea mara chache mnoo
kama umepitia hali hii unaelewa.
Miaka 3 mm nina namba ya swahiba wangu mkubwa huu ni mwaka wa 10 sasa
Alifariki mwaka 2010 lkn chakushangaza miaka yote hiyo mpk sasa hiyo namba tigo hawajawahi kumpa mtu mana nikiwa na huzuni napigaga lkn najibiwa haipatikani

Kwa mm siwezi kufuta namba ya marehemu aisee
Tangu nianze kumiliki simu sijawahi futa namba za marehemu nina namba za ndugu zaidi ya 7 kila nikijaribu kufuta nashindwa aisee
Mm namba muhimu nasave kwenye laini hata nikiwa na kitochi nakuwa nayo namba yako so katika hiyo phonebook ya SIMCARD nina namba za marehemu si chini ya 7
 
Yeah upo sawa maybe I will see her again ...in heaven I hope so [emoji17][emoji17][emoji853]
Utamuona[emoji4]
Hakuna namna tutafika Mbinguni pasipo kufa ..

Jitahidi Sasa utengeneze njia zako ili uweze kufika Mbinguni kumuona..I hope yupo huko.. swali wewe je ntafanikiwa kwenda njia aliyopo?

Mungu hakosei ..yatupasa kushukuru
 
Mimi ninazo mbili hata text message sijafuta na za mwisho zote zilikuwa ni kunishukuru 🙏🏾🙏🏾🙏🏾
Awe mume, mke, mtoto, mzazi babu au bibi hata rafiki au mpenzi. Marehemu akisha kufa inauma sana kufuta namba zake za simu. Wakati ule wa simu za mezani za Shirika la Posta na Simu, jirani zetu walifiwa na mama yao ambae ndiye alikua na akaunti ya simu.

Walikaa miaka mingi wakilipa ankara kwa jina lile mpaka siku ilitokea matatizo, Posta walimuomba mwenye ankra aende ofisini. Baba alikwenda, alijibiwa tunamtaka mwenye jina. Aliwajibu kuwa mwenye jina ni mke wangu alifariki miaka mitano iliyopita.

Waliomba kuona cheti cha kifo na kujiridhisha, mzee aliambiwa ni kosa la jinai kuendelea kutumia jina la marehemu. Ilibidi jina la ankra kubadilisha even.
 
Namba ya mzee sijaifuta hadi leo na simu yake ninayo mpaka sasa naitumia ikiwa na line yake. Naitumia kulipia dstv, luku na maji kama ambavyo alipendelea enzi za uhai wake.
 
Sijafuta namba ya marehemu baba. Mwaka wa pili hii unaisha toka mauti yamkute. Ni siifuti kabisa. Acha ikae tu maana kuna wakati naona kabisa "Baba calling...."
 
Namba ya marehemu dada yangu nimeifuta mwaka jana.
Ni baada ya miaka mi4 kupita.

Kuna muda nilikuwa naiangalia na kujipa matumaini ya kusadikika kwamba itaita.

Siku naifuta nililia sana Sana.
Nililia mno.
Very sorry,
 
Mimi nilikua na simu ya Marehemu Baba sikuwahi kuizima... Wiki Moja baada ya Mzee kufariki, baadhi ya marafiki zake mshua wakawa wanapiga sasa, nikawa naogopa hata kupokea nikazani labda hawana taarifa au wanatest kma ipo hewani.
End of the day, line nilitoa... Namba ipo mpaka kichwani
 
poleni sana wote mlio poteza wapendwa wenu inauma sana.

nilimpoteza rafiki yangu wa shule mpaka leo naumia,maana alikuwa hawezi pitisha siku ajani text wasap,fb ama text za kawaida.
 
Awe mume, mke, mtoto, mzazi babu au bibi hata rafiki au mpenzi. Marehemu akisha kufa inauma sana kufuta namba zake za simu. Wakati ule wa simu za mezani za Shirika la Posta na Simu, jirani zetu walifiwa na mama yao ambae ndiye alikua na akaunti ya simu.

Walikaa miaka mingi wakilipa ankara kwa jina lile mpaka siku ilitokea matatizo, Posta walimuomba mwenye ankra aende ofisini. Baba alikwenda, alijibiwa tunamtaka mwenye jina. Aliwajibu kuwa mwenye jina ni mke wangu alifariki miaka mitano iliyopita.

Waliomba kuona cheti cha kifo na kujiridhisha, mzee aliambiwa ni kosa la jinai kuendelea kutumia jina la marehemu. Ilibidi jina la ankra kubadilishwa.
Dani.eniumiza sana hii.
 
Poleni sana!
Mimi huwa na delete Kabisa,maisha inatakiwa yaendelee huku tukiwaombea walale pema peponi.
Sitaki stress.
 
Sitaki kukumbuka maana nitaumia zaidi,,nafutaga mapema sana,,
 
Back
Top Bottom