Kufuta namba ya simu ya marehemu inauma sana

Kufuta namba ya simu ya marehemu inauma sana

Baba yangu alifariki 2017 Mama yangu alifariki may mwaka jana,namba zao zote bado sijazifuta,hali ya kuondokewa na wapendwa uisikie tu usiombe ikukute kwani maumivu yake hayasemeki
 
Awe mume, mke, mtoto, mzazi babu au bibi hata rafiki au mpenzi. Marehemu akisha kufa inauma sana kufuta namba zake za simu. Wakati ule wa simu za mezani za Shirika la Posta na Simu, jirani zetu walifiwa na mama yao ambae ndiye alikua na akaunti ya simu.

Walikaa miaka mingi wakilipa ankara kwa jina lile mpaka siku ilitokea matatizo, Posta walimuomba mwenye ankra aende ofisini. Baba alikwenda, alijibiwa tunamtaka mwenye jina. Aliwajibu kuwa mwenye jina ni mke wangu alifariki miaka mitano iliyopita.

Waliomba kuona cheti cha kifo na kujiridhisha, mzee aliambiwa ni kosa la jinai kuendelea kutumia jina la marehemu. Ilibidi jina la ankra kubadilishwa.
Daah inauma sana.
Age imeenda but still i cant delete my Father's number...
Na technology ilivyo sikuhizi ,numbe ipo synchronised kwenye devices zangu mbali mbali.
Iache tu ibaki[emoji17][emoji17][emoji17]
 
Namba baba nimeifuta mwaka huu, baada ya kufariki mwaka jana, Mana kila nikiwa napitia majina pindi niwapo na shida ,naiona namba yake na mtu ambae alikuwa na mwitikio wa Hali ya juu Sana, kwa hasira nikaona bora nifute, kupunguza maumivu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Imenigusa kama ndiye mfiwa[emoji17][emoji17][emoji17]nimeshindwa kuvivaa viatu vyenu
 
Back
Top Bottom