Kufuta namba ya simu ya unaempenda akifariki ni Jambo kubwa, omba yasikufike

Tunza hao mapacha kama full dedication kwa legacy ya shangazi yako.
 
Mimi juzi nimefuta ya mama yangu aliefariki miaka 7 iliyopita. Kabla sijaifuta nilipiga, akapokea mshikaji, nikamwambia nimepiga one more last time kwa sababu namba alikua anaitumia mama. Jamaa very understanding, akanipa pole tukaongea sana kisha nikaifuta once and for good.

Hata medical reports zake zote za hospitali kama x rays, mri na vipimo vingine vyote nilivyi distroy baadae sana.

Pumzika kwa amani mama yangu. Kijana wako bado nakukumbuka kila siku na naendelea kupambana.
 
Poleni sana.
Ni ngumu sana kufuta.
Mimi nilikaa na namba ya simu ya marehemu baba yangu kwa miaka zaidi ya 10 mpaka hapo nilipoona namba hiyo inatumika kwa mtu mwingine ndo nikaifuta.
 
inauma sana mkuu, ila tuseme huduma zetu za upasuaji bado hazijawa za uhakika, mtu alienda kujifungua, njia ya kawaida ikashindikana, ikabidi afanyiwe op,ameruhusiwa siku 5 hali ikawa mbaya,wakarudi hosp. Wamekaa kama 6days wakasema wameshndwa wakapewa rufaa to nkinga, kisha walipofika huko wakaongezewa drip 4 za damu na ule mshono ukarudiwa kutengenezwa upya,wamekaa takribani 6days hali ikazidi kuwa mbaya,kupumulia milija, badae ndo hali ikazidi kuwa mbaya na kufariki dunia,kiukweli kama wangejua wangeenda moja kwa moja kwenye hosp. Ya rufaa kuliko hizi tiamajitiamaji. Marehemu shangazi kaacha watoto mapacha wenye umri wa mwezi mmoja. Lala salama shangazi
 
Mimi nina namba ya Binamu yangu aliyefariki kwa ajali mwaka jana juzi nimeshindwa kufuta, pamoja na picha 2 alizonitumia kwa WhatsApp kabla ya kufa
 
Pole sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…