Uandishi ni taaluma mtambuka, mnaweza kuwafungia gazeti na wakaendelea kuishi. Hii ni tofauti na nyie LB7 ambao mnategemea mwenyekiti ameamkaje!
Sio kwa Sasa hivi kawamwagia kitumbua kwenye mchanga yeye huyo anaendelea kula Bata
Waandishi wa habari wawe makini lakini yawezekana kabisa Kuna waandishi mahiri Tanzania Daima Ila yawezekana Ni hujuma wamehujumu gazeti lifungiwe kwa makusudi sababu ya kutolipwa mishahara au stahiki zao na Chadema wakati miruzuku chadema inapata kibao
Yaweza kuwa Ni internal wars za ndani ya chadema.Haiwezekani mwandishi mahiri anaandika habari ya askofu kuitisha maandamano nchi nzima wakati yeye Ni Askofu tu wa kidayosisi kidogo Tena maskini cha karagwe
Ki protocol hata kama Askofu angeitisha maandamano alitakiwa kuwa Askofu mkuu wa KKKT Tanzania nzima Askofu shoo
Ki protocol Bagonza eneo lake Ni karagwe tu sio nchi nzima!!
Sasa Tanzania Daima hata walishindwa kuchuja kuwa huyo Bagonza judistriction powers zake mwisho area ipi sio kweli ona Sasa kilichosukwa
Binafsi naamini kuhujumiana ndani ya Chadema kumeanza hasa kipindi hiki wanagombana Nani awe mgombea uraisi Chadema.Tanzania Daima lilikuwa linamjenga mtia Nia fulani sasa Kama humo ndani ya chumba Cha habari Kama Kuna makundi ya wagombea mahasimu kutakuwa na mmoja kaamua kuzima switch ya umeme ya Tanzania Daima lisiendelee kuwaka kwa kuchapisha habari hiyo ya kinyume na maadili ya uandishi ya Askofu Bagonza ili Tanzania Daima ifungiwe
My advice waandishi wazingatie taaluma na kuepuka makundi ndani ya vyama
Gazeti laweza kuwa limefungiwa kupitia inside Job ya kundi la Askofu Bagonza ambaye labda Yuko upande wa mgombea uraisi fulani lakini asiyeelewana na mgombea aliyekuwa akibebwa na Tanzania Daima!! Askofu akawaagiza wachapishe hiyo habari gazeti lifungiwe ili huyo wasiyekubaliana naye akose forum ya ku ji nafasi kurasa za mbele za gazeti
Kuna mtu katia Nia Kugombea uraisi kupitia Chadema Askofu Bagonza alikutana naye Marekani wakaongea Sana tu naona kuna faulo wagombea uraisi Chadema wameanza kuchezeana.Askofu Bagonza ana mgombea wake Chadema nitamtaja siku ingine sitaki kuvuruga michakato Yao ya Chadema kumpata ila napiga tu filimbi kuwa wagombea wameanza kuchezeana faulo ndani ya Chadema wao na wapambe wao