Imeandikwa wapi futari ni kwenye jamvi au zuria?
Una mlivyo weupe hata chakula hamjui taratibu zake za kidini na namna ya kula. Shuka nayo hapo chini nimeweka kwa uchache
[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
ADABU / TARATIBU ZA KULA/ KUNYWA
Muislamu hukiangalia chakula na kinywaji kwa jicho la kukizingatia kuwa ni wasila/chombo cha kumfikishia katika malengo ya maisha yake ya siku hata siku.
Muislamu hakitazami chakula/kinywaji kwa dhati yake kama ndio upeo wa makusudio na malengo yake.
Kwa hiyo basi, Muislamu haishi ili ale na kunywa bali anakula na kunywa ili aishi. Anakula na kunywa kwa ajili ya kuhifadhi usalama wa afya ya mwili wake, kwani ni kupitia mwili huu ndio huweza kumuabudu Mola wake. I
bada hii ndio humfanya astahiki kupata utukufu, mafanikio na neema za maisha ya milele ya akhera.
Muislamu hali au kunywa kwa dhamira ya kula na kunywa tu, au kwa matamanio, bali hali ila kwa kusikia njaa na kadhalika hanywi ila kwa kiu.
Na hii ni kanuni muhimu ya afya aliyotuwekea Bwana Mtume – Rehma na Amani zimshukie – aliposema :
“ Sisi ni watu hatuli mpaka tusikie njaa na tukila basi hatushibi (kupita kiasi)”.
Lau watu wa leo tungejilazimisha kuifuata kanuni hii, basi tungeliepukana na maradhi mengi. Kwani asilimia kubwa ya maradhi yanayomsibu huanzia tumboni, kutokana na kula na kunywa ovyo ovyo.
Kwa hivyo basi, muislamu anapaswa kujilazimisha kufuata taratibu za kisheria katika kula na kunywa kwake. Taratibu/adabu hizi tutazigawa katika mafungu/sehemu tatu zifuatazo :
a) ADABU/TARATIBU ZA KUFUATWA KABLA YA KUANZA KULA :
1. Kwanza kabisa Muislamu ahakikishe anaandaa na kukipata chakula chake kwa njia za halali, kwa kuitekeleza kauli ya Mola Mtukufu
“ENYI MLIOAMINI ! KULENI VIZURI TULIVYOKURUZUKUNI …” [2:172]
Muradi na mapendeleo ya chakula kizuri ni chakula cha halali na sio uzuri wa ladha.
Kwani ladha hutofautiana baina ya mtu na mtu.
2. Anuie kwa kula na kunywa kwake kupata afya na nguvu ya kumuabudu Mola wake ili apewe thawabu kwa atachokila au kukinywa cha nia hiyo. Kwani jambo la MUBAAH hugeuka kwa nia njema kuwa TWAA ambayo Muislamu hulipwa thawabu kwa kulitenda.
3. Aoshe mikono yake kabla ya na baada ya kula.
4. Akiweke chakula chake kwenye sahani/sinia chini na sio mezani, ka kuwa hili la kulia chini hupelekea zaidi unyenyekevu. Na haya ni kwa mujibu wa kauli ya swahaba Anas bin Malik –Allah amuwie Radhi – Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehema na Amani zimshukie – hakupata kula juu ya meza.
ZINDUKA: Si haramu kula chakula juu ya meza, bali SUNA ni kula chini ukiwa umeketi mkekani/jamvini au katika busati na vitu kama hivyo.
5. Akae kwa unyenyekevu wakati wa kula. Akalie matumbo ya nyayo zake, mguu wa kulia aunyooshe wima na nyayo yake juu ya ardhi, na aukalie ule wa kushoto kama alivyokuwa akikaa Bwana Mtume. {kielelezo}Bwana Mtume anatueleza namna ya ukaaji wake wakati wa kula, anasema : “Sili hali ya kuchegemea (kitu), hakika si vinginevyo mimi ni mja (Mtumwa wa Allah) ninakula kama alavyo mja na ninakaa kama akaavyo mja” Abu Dawuud na Tirmidhiy.
6. Aridhie na kutosheka na chakula kilichopo na wala asikitie kasoro/aibu. Kikimpendeza akile na kama hakikumridhia basi na akiache bila ya kutoa maneno yasiyo mazuri. Haya ni kwa mujibu wa hadithi iliyopokelewa na Abuu Hurayrah – Allah amuwie radhi – : “Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehema na Amani zimshukie – kamwe hakupata kukitia aibu/kasoro chakula akipendezewa hukila na kisipompendeza basi hukiacha” Abu Dawuud na Tirmidhiy.
7. Asile peke yake bali ale pamoja na wenziwe; mgeni, mkewe, wanawe, au hata mtumishi wake. Hii haimaanishi kwamba kula peke yake ni haramu, la hasha bali ni vyema kula pamoja na wengine. Hili linatokana na kauli ya Nabii Muhammad –Rehema na Amani zimshukie – aliposema : “Kusanyikeni pamoja katika chakula chenu mtabarikiwa ndani yake” Bukhariy na Muslim. Kwa hivyo utaona chakula cha pamoja hubarikiwa, kinyume na chakula cha mtu mmoja peke yake.
b) ADABU/TARATIBU ZA KUFUATWA WAKATI WA KULA :
1.Muislamu anatakiwa aanze kula kwa kupiga BISMILLAH kwa kuitekeleza kauli ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie –
“Atakapoanza kula mmoja wenu basi na alitaje jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu, akisahau kulitaja jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu mwanzoni mwake (huko kula) basi aseme (pale atakapokumbuka) BISMILLAHI FIY AWWALIHI WA AKHARIHI (Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzoni na mwisjoni)” Bukhariy na Muslim.
2.Amalizapo kula amshukuru Mwenyezi Mungu aliyemruzuku. Kufanya hivyo ni kuitekeleza kauli ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie – aliposema :