Kufuturishana Wabunge Dodoma ni rushwa, ni nchi gani nyingine ina huu utaratibu?

Kufuturishana Wabunge Dodoma ni rushwa, ni nchi gani nyingine ina huu utaratibu?

Yaani unaweza kumfuturisha mtu mwenye mshahara wa 12+... Wakati Kuna waislam wasiojiweza?. Ni upuuzi uliopita kiwango.
Shida sio mishara wanayo lipwa shida ni aina ya taasisi inayo futurishwa na umuhimu wao kwa jamii, hii nibsawa na majaji nao waanze kufuturishwa,
 
We ni mjinga kubali, make kwa comment yako kosa unalo ona ni kufuturishwa juu ya meza, basi, hilo ndio kosa hizo taasisi zinafanya.

Unaweza kukuta ww sio muislam chakula hakiliwi mezani tena si kwa kijiko wala kuwa juu ya meza muwe mnasoma mandiko

Halafu hiyo benk mnayoishambulia imetoa chakula kwa wateja pia waliwaandalia ukiachana na wabunge kwa hiyo nayo ni rushwa?

Nimekwambia wapi unanioneshe sehemu nipost KOSA unabaki kulazimisha nikubali ujinga wako kuwa wangu muwe mnasoma post za watu kwa umakini mimi nimetoa maoni namna futari inatakiwa iliwe hayo ya nani kaandaa hayanihusu
 
Wabunge waache huu utaratibu wa kufuturishwa kule Dodoma, Bunge linazidi kuwa too low sana, Juzi niliona Benki ya CRDB inawafuturisha, sasa chukulia kwamba Benki ikajikuta kwenye kashifa kubwa za pesa, hawa Wabunge wataanza kuona aibu ya kuishughurikia kisa inawafuturishaga.
Naongana na ww mkuu kuna wanaohitaji hiyo huduma ya kufuturishwa kama mayatima na watu maskini .unaende kumfuturisha mtu mwenye mshahara wa 11m kweli si kitutoka jamani
 
Imeandikwa wapi futari ni kwenye jamvi au zuria?

Una mlivyo weupe hata chakula hamjui taratibu zake za kidini na namna ya kula. Shuka nayo hapo chini nimeweka kwa uchache

[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]

ADABU / TARATIBU ZA KULA/ KUNYWA

Muislamu hukiangalia chakula na kinywaji kwa jicho la kukizingatia kuwa ni wasila/chombo cha kumfikishia katika malengo ya maisha yake ya siku hata siku.

Muislamu hakitazami chakula/kinywaji kwa dhati yake kama ndio upeo wa makusudio na malengo yake.

Kwa hiyo basi, Muislamu haishi ili ale na kunywa bali anakula na kunywa ili aishi. Anakula na kunywa kwa ajili ya kuhifadhi usalama wa afya ya mwili wake, kwani ni kupitia mwili huu ndio huweza kumuabudu Mola wake. I

bada hii ndio humfanya astahiki kupata utukufu, mafanikio na neema za maisha ya milele ya akhera.

Muislamu hali au kunywa kwa dhamira ya kula na kunywa tu, au kwa matamanio, bali hali ila kwa kusikia njaa na kadhalika hanywi ila kwa kiu.

Na hii ni kanuni muhimu ya afya aliyotuwekea Bwana Mtume – Rehma na Amani zimshukie – aliposema :

“ Sisi ni watu hatuli mpaka tusikie njaa na tukila basi hatushibi (kupita kiasi)”.

Lau watu wa leo tungejilazimisha kuifuata kanuni hii, basi tungeliepukana na maradhi mengi. Kwani asilimia kubwa ya maradhi yanayomsibu huanzia tumboni, kutokana na kula na kunywa ovyo ovyo.

Kwa hivyo basi, muislamu anapaswa kujilazimisha kufuata taratibu za kisheria katika kula na kunywa kwake. Taratibu/adabu hizi tutazigawa katika mafungu/sehemu tatu zifuatazo :

a) ADABU/TARATIBU ZA KUFUATWA KABLA YA KUANZA KULA :

1. Kwanza kabisa Muislamu ahakikishe anaandaa na kukipata chakula chake kwa njia za halali, kwa kuitekeleza kauli ya Mola Mtukufu

“ENYI MLIOAMINI ! KULENI VIZURI TULIVYOKURUZUKUNI …” [2:172]

Muradi na mapendeleo ya chakula kizuri ni chakula cha halali na sio uzuri wa ladha.

Kwani ladha hutofautiana baina ya mtu na mtu.

2. Anuie kwa kula na kunywa kwake kupata afya na nguvu ya kumuabudu Mola wake ili apewe thawabu kwa atachokila au kukinywa cha nia hiyo. Kwani jambo la MUBAAH hugeuka kwa nia njema kuwa TWAA ambayo Muislamu hulipwa thawabu kwa kulitenda.

3. Aoshe mikono yake kabla ya na baada ya kula.

4. Akiweke chakula chake kwenye sahani/sinia chini na sio mezani, ka kuwa hili la kulia chini hupelekea zaidi unyenyekevu. Na haya ni kwa mujibu wa kauli ya swahaba Anas bin Malik –Allah amuwie Radhi – Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehema na Amani zimshukie – hakupata kula juu ya meza.

ZINDUKA: Si haramu kula chakula juu ya meza, bali SUNA ni kula chini ukiwa umeketi mkekani/jamvini au katika busati na vitu kama hivyo.

5. Akae kwa unyenyekevu wakati wa kula. Akalie matumbo ya nyayo zake, mguu wa kulia aunyooshe wima na nyayo yake juu ya ardhi, na aukalie ule wa kushoto kama alivyokuwa akikaa Bwana Mtume. {kielelezo}Bwana Mtume anatueleza namna ya ukaaji wake wakati wa kula, anasema : “Sili hali ya kuchegemea (kitu), hakika si vinginevyo mimi ni mja (Mtumwa wa Allah) ninakula kama alavyo mja na ninakaa kama akaavyo mja” Abu Dawuud na Tirmidhiy.

6. Aridhie na kutosheka na chakula kilichopo na wala asikitie kasoro/aibu. Kikimpendeza akile na kama hakikumridhia basi na akiache bila ya kutoa maneno yasiyo mazuri. Haya ni kwa mujibu wa hadithi iliyopokelewa na Abuu Hurayrah – Allah amuwie radhi – : “Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehema na Amani zimshukie – kamwe hakupata kukitia aibu/kasoro chakula akipendezewa hukila na kisipompendeza basi hukiacha” Abu Dawuud na Tirmidhiy.

7. Asile peke yake bali ale pamoja na wenziwe; mgeni, mkewe, wanawe, au hata mtumishi wake. Hii haimaanishi kwamba kula peke yake ni haramu, la hasha bali ni vyema kula pamoja na wengine. Hili linatokana na kauli ya Nabii Muhammad –Rehema na Amani zimshukie – aliposema : “Kusanyikeni pamoja katika chakula chenu mtabarikiwa ndani yake” Bukhariy na Muslim. Kwa hivyo utaona chakula cha pamoja hubarikiwa, kinyume na chakula cha mtu mmoja peke yake.

b) ADABU/TARATIBU ZA KUFUATWA WAKATI WA KULA :

1.Muislamu anatakiwa aanze kula kwa kupiga BISMILLAH kwa kuitekeleza kauli ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie –

“Atakapoanza kula mmoja wenu basi na alitaje jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu, akisahau kulitaja jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu mwanzoni mwake (huko kula) basi aseme (pale atakapokumbuka) BISMILLAHI FIY AWWALIHI WA AKHARIHI (Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzoni na mwisjoni)” Bukhariy na Muslim.

2.Amalizapo kula amshukuru Mwenyezi Mungu aliyemruzuku. Kufanya hivyo ni kuitekeleza kauli ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie – aliposema :
 
MURUSI !
Uko sahihi kabisa kuhusiana na hili.

Kwa kweli inasikitisha kuona mambo ya kipuuzi kama haya yakipewa nafasi tena kutoka kwenye mhimili muhimu kama Bunge la Jamhuri ya Nchi.

Kwamba wabunge wanafuturishwa kwa kushindana,tena wafuturishaji wakiwa ni wale ambao ni watuhumiwa kwenye ripoti ya CAG iliyoko mezani kwa spika wa hilo hilo Bunge.

Na ukakasi zaidi ni pale ambapo,shirika kama TTCL ambalo liko taaban,na huku likiwa mojawapo ya mashirika yaliyoorodheshwa kuitia hasara kubwa serikali.

Kwamba TTCL inaandaa futari na mgeni rasmi anakuwa ni waziri wa habari Ambaye mimi simtambui tena kama mheshimiwa bali Ndugu Nape Moses Nnauye!
Kwamba shirika liko hoi kimapato,lakini linaweza kuandaa iftal tena kwenye hotel ya hadhi ya nyota ***

Hii ni Rushwa,huu ni mtego wa kutafuta ukaribu na wajumbe wa kamati husika za Bunge.
Na kutumia nafasi hiyo kuweka miadi ya kukutana eneo tofauti na kuweza kujadili au kupanga jinsi ya kulihujumu zoezi la mjadala na uchunguzi wa ripoti ya CAG utakaofanywa na hizo kamati.

Na ndio sababu,binafsi jana niliandika kuhusu umuhimu wa kubadili utaratibu sasa!
Ili vikao vya hizo kamati viweze kuonyehwa live,ili kuzuia uwezekano mkubwa wa kupindisha ukweli...kwa huu mtindo wa sasa wa kujifungia faragha na kuwahoji watuhumiwa kimya kimya!
Pia soma hii
KUNA UMUHIMU KAMATI ZA BUNGE KUANZA KUONYESHWA LIVE[emoji116]
 
Hizi pesa ni mara mbili wangewapa taasisi za kiislamu zinazolea yatima.
Ni kweli kabisa. lakini si taasisi za kiislamu tu. wangewapa yatima. hii ni sura nyingine ya ufisadi. Bunge linapokuwa na upofu wa kiwango hiki, tutarajie linaishupalia serikali au wabadhirifu wa mali za umma?
 
Una mlivyo weupe hata chakula hamjui taratibu zake za kidini na namna ya kula. Shuka nayo hapo chini nimeweka kwa uchache


[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]

ADABU / TARATIBU ZA KULA/ KUNYWA


Muislamu hukiangalia chakula na kinywaji kwa jicho la kukizingatia kuwa ni wasila/chombo cha kumfikishia katika malengo ya maisha yake ya siku hata siku.

Muislamu hakitazami chakula/kinywaji kwa dhati yake kama ndio upeo wa makusudio na malengo yake.

Kwa hiyo basi, Muislamu haishi ili ale na kunywa bali anakula na kunywa ili aishi. Anakula na kunywa kwa ajili ya kuhifadhi usalama wa afya ya mwili wake, kwani ni kupitia mwili huu ndio huweza kumuabudu Mola wake. I

bada hii ndio humfanya astahiki kupata utukufu, mafanikio na neema za maisha ya milele ya akhera.

Muislamu hali au kunywa kwa dhamira ya kula na kunywa tu, au kwa matamanio, bali hali ila kwa kusikia njaa na kadhalika hanywi ila kwa kiu.

Na hii ni kanuni muhimu ya afya aliyotuwekea Bwana Mtume – Rehma na Amani zimshukie – aliposema :

“ Sisi ni watu hatuli mpaka tusikie njaa na tukila basi hatushibi (kupita kiasi)”.

Lau watu wa leo tungejilazimisha kuifuata kanuni hii, basi tungeliepukana na maradhi mengi. Kwani asilimia kubwa ya maradhi yanayomsibu huanzia tumboni, kutokana na kula na kunywa ovyo ovyo.

Kwa hivyo basi, muislamu anapaswa kujilazimisha kufuata taratibu za kisheria katika kula na kunywa kwake. Taratibu/adabu hizi tutazigawa katika mafungu/sehemu tatu zifuatazo :

a) ADABU/TARATIBU ZA KUFUATWA KABLA YA KUANZA KULA :

1. Kwanza kabisa Muislamu ahakikishe anaandaa na kukipata chakula chake kwa njia za halali, kwa kuitekeleza kauli ya Mola Mtukufu



“ENYI MLIOAMINI ! KULENI VIZURI TULIVYOKURUZUKUNI …” [2:172]

Muradi na mapendeleo ya chakula kizuri ni chakula cha halali na sio uzuri wa ladha.

Kwani ladha hutofautiana baina ya mtu na mtu.

2. Anuie kwa kula na kunywa kwake kupata afya na nguvu ya kumuabudu Mola wake ili apewe thawabu kwa atachokila au kukinywa cha nia hiyo. Kwani jambo la MUBAAH hugeuka kwa nia njema kuwa TWAA ambayo Muislamu hulipwa thawabu kwa kulitenda.

3. Aoshe mikono yake kabla ya na baada ya kula.

4. Akiweke chakula chake kwenye sahani/sinia chini na sio mezani, ka kuwa hili la kulia chini hupelekea zaidi unyenyekevu. Na haya ni kwa mujibu wa kauli ya swahaba Anas bin Malik –Allah amuwie Radhi – Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehema na Amani zimshukie – hakupata kula juu ya meza.

ZINDUKA: Si haramu kula chakula juu ya meza, bali SUNA ni kula chini ukiwa umeketi mkekani/jamvini au katika busati na vitu kama hivyo.

5. Akae kwa unyenyekevu wakati wa kula. Akalie matumbo ya nyayo zake, mguu wa kulia aunyooshe wima na nyayo yake juu ya ardhi, na aukalie ule wa kushoto kama alivyokuwa akikaa Bwana Mtume. {kielelezo}Bwana Mtume anatueleza namna ya ukaaji wake wakati wa kula, anasema : “Sili hali ya kuchegemea (kitu), hakika si vinginevyo mimi ni mja (Mtumwa wa Allah) ninakula kama alavyo mja na ninakaa kama akaavyo mja” Abu Dawuud na Tirmidhiy.

6. Aridhie na kutosheka na chakula kilichopo na wala asikitie kasoro/aibu. Kikimpendeza akile na kama hakikumridhia basi na akiache bila ya kutoa maneno yasiyo mazuri. Haya ni kwa mujibu wa hadithi iliyopokelewa na Abuu Hurayrah – Allah amuwie radhi – : “Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehema na Amani zimshukie – kamwe hakupata kukitia aibu/kasoro chakula akipendezewa hukila na kisipompendeza basi hukiacha” Abu Dawuud na Tirmidhiy.

7. Asile peke yake bali ale pamoja na wenziwe; mgeni, mkewe, wanawe, au hata mtumishi wake. Hii haimaanishi kwamba kula peke yake ni haramu, la hasha bali ni vyema kula pamoja na wengine. Hili linatokana na kauli ya Nabii Muhammad –Rehema na Amani zimshukie – aliposema : “Kusanyikeni pamoja katika chakula chenu mtabarikiwa ndani yake” Bukhariy na Muslim. Kwa hivyo utaona chakula cha pamoja hubarikiwa, kinyume na chakula cha mtu mmoja peke yake.



b) ADABU/TARATIBU ZA KUFUATWA WAKATI WA KULA :

1.Muislamu anatakiwa aanze kula kwa kupiga BISMILLAH kwa kuitekeleza kauli ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie –

“Atakapoanza kula mmoja wenu basi na alitaje jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu, akisahau kulitaja jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu mwanzoni mwake (huko kula) basi aseme (pale atakapokumbuka) BISMILLAHI FIY AWWALIHI WA AKHARIHI (Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzoni na mwisjoni)” Bukhariy na Muslim.

2.Amalizapo kula amshukuru Mwenyezi Mungu aliyemruzuku. Kufanya hivyo ni kuitekeleza kauli ya Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie – aliposema :
Wewe jamaa post yangu haihusu muundo wa kufuturisha hata kama ingekuwa ni kufuturisha watu wakiwa wamelala mimi nazungumzia Bunge sizungumziii aina
 
Walengwa wale mayatima na wasiojiweza hawapo kabisa wote wapo.. Hapo ni kukutanisha wanasiasa na matajiri wa nchi ..
 
Unaweza kukuta ww sio muislam chakula hakiliwi mezani tena si kwa kijiko wala kuwa juu ya meza muwe mnasoma mandiko

Halafu hiyo benk mnayoishambulia imetoa chakula kwa wateja pia waliwaandalia ukiachana na wabunge kwa hiyo nayo ni rushwa?

Nimekwambia wapi unanioneshe sehemu nipost KOSA unabaki kulazimisha nikubali ujinga wako kuwa wangu muwe mnasoma post za watu kwa umakini mimi nimetoa maoni namna futari inatakiwa iliwe hayo ya nani kaandaa hayanihusu
Mkuu maada yangu haihusu muundo au aina ya kufuturisha, inahusu Wabunge kufuturishwa bila kujalisha walilala, walikaaa juu meza, walisimama walikuwa wanarukaruka wakati wanafuturu,
 
Hiyo futari ya kuwafuturisha wasio funga kama Tulia na Msukuma ndio nzuri na inapendwa zaidi na shetani
Ni maajabu waziri mkuu atafuturishaje walio funga wakati yeye nyumbani anapikiwa na asio muislamu asio funga manaake ana zini kila siku, kwa kulala na mke na ndoa asie tambuliwa na sheria za dini .......bora asafishe nyumbani kwake kabla ya kufuturisha watu.
 
Ukweli ni kuwa ni vile imeshakuwa brand tu lakini crdb ni benki moja ya hovyo sana hata huduma zao ni mbovu sana kwa sasa. kama mtu haamini unaweza ukatembelea hata matawi yao makubwa utashangaa.

Kama tawi lao la mlimani city, dar, ndiyo hovyo kabisa. limejaza wapumbavu watupu hata hawajui namna ya kuwahudumia wateja.

Sishangai kuona benki iko bize kuwafuturisha mafisadi na waporaji wa kura za watu
 
ZINDUKA: Si haramu kula chakula juu ya meza, bali SUNA ni kula chini ukiwa umeketi mkekani/jamvini au katika busati na vitu kama hivyo.
Nakusalimia tu bahati nzuri umekopi kama ilivyo. Kwa hiyo sema hapa sasa wamekosea wapi kula kwenye meza? Au ndo unasoma ila huelewi?
 
ukweli ni kuwa ni vile imeshakuwa brand tu lakini crdb ni benki moja ya hovyo sana hata huduma zao ni mbovu sana kwa sasa. kama mtu haamini unaweza ukatembelea hata matawi yao makubwa utashangaa.

kama tawi lao la mlimani city, dar, ndiyo hovyo kabisa. limejaza wapumbavu watupu hata hawajui namna ya kuwahudumia wateja.

sishangai kuona benki iko bize kuwafuturisha mafisadi na waporaji ya kura za watu
Hio ndio njia pekee kwa sasa wanayo itegemea
 
Sasa wapo kazini waje kufuturishwa nanani Sasa?? Na nyie basi mbona nyie ni mazwazwa
 
Baadala kupeleka hizo pesa za kufuturishana kwenye kaya masikini wanaendelea kujaza maji kwenye bahari
 
Mkuu maada yangu haihusu muundo au aina ya kufuturisha, inahusu Wabunge kufuturishwa bila kujalisha walilala, walikaaa juu meza, walisimama walikuwa wanarukaruka wakati wanafuturu,
Hao ndio ma- chawa wao wanajaribu kupindisha mada!
 
Waziri mkuu ashughulikiwe kwa lipi? Acha uchawi wewe, wa kushughulikiwa ni yule bibi pale juu
 
Back
Top Bottom