Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Ila hii post ingewekwa kwenye jukwaa husika la sports and entertainment ingependeza sana!
Siku muhimu kama hizi kwa nchi hili ni jukwaa sahihi. Hata redio za dini leo habari ni hii.
 
Wakuu,

Leo Tanzania inaweza kuingia kwenye historia muhimu sana kwenye ulimwengu wa michezo. Tunatakiwa kuishinda Lesotho kwa namna yeyote ili tuweze kushiriki michuano mikubwa kabisa barani Africa ambayo tulishiriki Zaidi ya miaka 38 iliyopita.

Watanzania wote tusimamishe kila kitu na kuonesha kila namna ya kuiunga mkono timu yetu ya Taifa. Masaa haya machache tuchafue mitandao ya kijamii na mitaani kuonesha mshikamano wetu nyakati muhimu kama hizi.

Hii mechi ya leo si ya kawaida bali ni vita ambayo tukishindwa ni taifa limeshindwa na tukishinda ni taifa limeshinda. Heshima ya ushindi wa leo itaiweka nchi kwenye ramani kubwa Zaidi kimichezo na Zaidi itabadili uelekeo wa michezo na hasa nafasi ya wachezaji wetu kupata fursa Zaidi kwenye Nyanja za kimataifa.

Kila lakheri timu ya taifa ya Tanzania, nendeni mkapiganie nchi kwa nguvu zenu zote. Wanajeshi wetu wengi wamemwaga damu zao kuipigania heshima ya taifa letu na nyie mtambue mnawajibu sawa na huo kwaajili ya Tanzania.

Taifa zima leo limeweka matumaini yote mikononi mwenu, kaipiganieni Tanzania na mlete heshima ambayo vizazi vyote vitawakumbuka kuwa nyie ndio mliorudisha heshima ya nchi baada ya miaka 38 kushindwa kushiriki michuano hii mikubwa.

"We will stand and fight here. If we can't stay here alive, then let us stay here dead." General Sir Bernard Montgomery

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Taifa Stars ….
Wakuu,

Leo Tanzania inaweza kuingia kwenye historia muhimu sana kwenye ulimwengu wa michezo. Tunatakiwa kuishinda Lesotho kwa namna yeyote ili tuweze kushiriki michuano mikubwa kabisa barani Africa ambayo tulishiriki Zaidi ya miaka 38 iliyopita.

Watanzania wote tusimamishe kila kitu na kuonesha kila namna ya kuiunga mkono timu yetu ya Taifa. Masaa haya machache tuchafue mitandao ya kijamii na mitaani kuonesha mshikamano wetu nyakati muhimu kama hizi.

Hii mechi ya leo si ya kawaida bali ni vita ambayo tukishindwa ni taifa limeshindwa na tukishinda ni taifa limeshinda. Heshima ya ushindi wa leo itaiweka nchi kwenye ramani kubwa Zaidi kimichezo na Zaidi itabadili uelekeo wa michezo na hasa nafasi ya wachezaji wetu kupata fursa Zaidi kwenye Nyanja za kimataifa.

Kila lakheri timu ya taifa ya Tanzania, nendeni mkapiganie nchi kwa nguvu zenu zote. Wanajeshi wetu wengi wamemwaga damu zao kuipigania heshima ya taifa letu na nyie mtambue mnawajibu sawa na huo kwaajili ya Tanzania.

Taifa zima leo limeweka matumaini yote mikononi mwenu, kaipiganieni Tanzania na mlete heshima ambayo vizazi vyote vitawakumbuka kuwa nyie ndio mliorudisha heshima ya nchi baada ya miaka 38 kushindwa kushiriki michuano hii mikubwa.

"We will stand and fight here. If we can't stay here alive, then let us stay here dead." General Sir Bernard Montgomery

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Taifa Stars ….
Weka na muda wa watch sio maneno tu
 
Lawama na maneno yote itakuwa vyema baada ya mechi. Nchi ikiwa vitani huwezi kuanza kubeza jeshi lako na hasa majenerali kuwa hawakujiandaa vizuri kwa vita.

Mkiwa vitani mtatoka na mlichonacho hata kijiko na mwiko lakini lengo kuu ni kushinda alafu mengine yatafata.

Leo tuwatakie kheri wenzetu tuliowapa jukumu zito kutuwakilisha.
Lesotho wamekuja hapa bongo tumefungana 1-1, unategemea tukienda kule kwao kuna muujiza?
 
Lesotho wamekuja hapa bongo tumefungana 1-1, unategemea tukienda kule kwao kuna muujiza?
Kwa hesabu hizo hizo, cape Verde walitupiga ngapi kwao alafu hapa kikatokea nini? Kwasasa hizo hesabu hazisaidii bali ni kuitakia kheri vijana tuliowatwisha jukumu hili kwa niaba yetu.
 
Siku muhimu kama hizi kwa nchi hili ni jukwaa sahihi. Hata redio za dini leo habari ni hii.
Sema kwenye jukwaa husika uchangiaji ni mdogo mno. Ushindi hautapatikana kwa maombi wala kwa kuweka akili zetu huko. Kushinda au kushindwa itakuwa ni matokeo tu ya maandalizi endelevu. We can only keep our fingers crossed!
 
Umesema "Tanzania kwenye vita muhimu" iweje tbc hawaonyeshi badala yake ni azam!!!
 
nipo kwenye mtanziko kwenye hili
1.tukipita ccm wataongeza kwenye mafanikio ya jiwe
2.tukitolewa roho itaniuma
ila bora namba 1 itokee halafu tutapambana na ccm humu wakisema ni mafanikio yao
yes,siasa kila mahali😀😀
 
nipo kwenye mtanziko kwenye hili
1.tukipita ccm wataongeza kwenye mafanikio ya jiwe
2.tukitolewa roho itaniuma
ila bora namba 1 itokee halafu tutapambana na ccm humu wakisema ni mafanikio yao
yes,siasa kila mahali😀😀
Great. Positive vibes only, Tanzania mbele
 
Kwa hesabu hizo hizo, cape Verde walitupiga ngapi kwao alafu hapa kikatokea nini? Kwasasa hizo hesabu hazisaidii bali ni kuitakia kheri vijana tuliowatwisha jukumu hili kwa niaba yetu.
Kwahiyo kumbe ugenini Tz hatuna matokeo mazuri???
 
Wanachokipigania Lesotho ndicho hichohicho tunachokipigania sisi, nawaunga mkono wote katika vita yao. Mmoja ashinde tusonge nae mbele....
 
Kwahiyo kumbe ugenini Tz hatuna matokeo mazuri???
Kwahiyo mpira unaamuliwa kwa ubashiri huo? Basi tungewaweka mbao fc ile mechi ya marudio tuone. Tuwatakie kheri wenzetu tuache maneno maneno kwasasa.
 
Back
Top Bottom