Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Lawama zote kwa benchi la ufundi..

Gundu limeletwa na viongozi wa ccm kuanza kujiweka mbele mbele ili wapate mtaji wa kisiasa. Kiongozi yoyote wa ccm asijiingize kwenye hiyo timu ibaki bila mkono wa siasa ili ipate baraka. Kinyume na hapo pelekeni jeshi.
 
Nilikuonya mapema ukajifanya Kunitukana na Kunidhihaki nadhani sasa umeamini kile nilichokuambia. Huyo ' Mtalaam ' wangu kutoka Pemba huwa habahatishi na kuna ' Hirizi ' alinipa na masharti yake ila ' dharau ' zako ndizo zimenikera na nikaitupa na dakika tatu ( 3 ) baadae tukafungwa kama nilivyokuhakikishia. Ukome!

Mafundi wa kipemba wanaheshimika sana khasa wale wa kuwafuata hukohuko kisiwani Pemba.

Wao hutoa maagizo tu na ukiyazingatia basi mambo yako yataenda moja kwa moja.
 
CCM ni adui namba moja wa taifa. Hii mil 50 ukichanganya na nguvu za wananchi tungeweza jenga zahanati 2
 
Ukiangalia kikosi kinachoa anza, ni rahisi hata kubet na kuiua stars. Kocha huyu hajifunzi hata mechi ya kule verde, wachezaji waliobadilisha mchezo bado amewaweka benchi.

Hivi ametumia akili gani kumweka John Boko dk ya 85? Au anatuhujumu anaona tutawasumbua nigeria?

Aisee, mh Rais, tunataka hela zetu, haiwezekani tupoteze hela kwa wajinga hawa. Yaano hata thamani ya ikulu hawajaiona!

Tuna watu ambao siyo wazalendo kabisa.View attachment 938686
 
Sina mengi sana na pia nimejitahidi nisiiseme hii ndoto yangu mbaya nliyoipata Leo usiku juu ya taifa stars.

Nmeona namna tutakavyo pigwa na wenyeji wetu, na hakuna namna ni kukubali tuu matokeo na turudi kujipanga upya kwa awamu inayokuja ila kwa hii hakika hatuna bahati. Lesotho wamecheza mpira vizuri na taifa stars tumejitahidi kucheza vizuri lakin nafasi chache tulizozipata hasa ile ya bocco kutozaa matunda lakin wenzetu wamepata chache na mbili wamefanikiwa....

Najua wengi mtakuja na povu la uzalendo lakin tuyakubali matokeo na kukubali pia ni uzalendo, mtakao kwenda kutazama mpira mjindae mapema Leo tunafungwa na safari yetu inaishia south.

Update.
HATIMAE ILE NDOTO YANGU IMETIMIA.
LESOTHO 1-TAIFA STARS 0

sio kwamba nmefurai sana hapana nlitaka kuwaanda watanzania juu ya ndoto yangu hii. Tumuombe jiwe atumie jeshi kwenye mechi dhidi ya Uganda la sivyo ntakuja na ndoto mbaya tena
Swahibaa, wako wapi sasa
 
Kiukweli kuna makundi mawili yanayoshindanisha dua zao , moja linataka Taifa Stars ishinde lingine linataka ishindwe , katika nchi ya namna hii si rahisi kufanikiwa .

Baada ya Timu yetu kufungwa goli hakuna wananchi wanaosikitika , ni nini kimeikumba nchi hii ?
Usilete siasa za ufipa kwenye michezo.
 
Back
Top Bottom