Kuhamishwa kwa Wamisai Ngorongoro, tumechelewa lakini tumpongeze Rais Samia. Tujifunze Canada na tusahihishe

Kuhamishwa kwa Wamisai Ngorongoro, tumechelewa lakini tumpongeze Rais Samia. Tujifunze Canada na tusahihishe

Mzungu hapendi ujue kuvua samaki anataka akuvulie akupatie. Kitendo Cha kuhamisha wazawa ni siri ya utalii endelevu. Binadamu anahatarisha maisha ya viumbe hai hifadhini ambavyo kimsingi vikitoweka hakuna utalii. Sasa unataka Siri hiyo upewe na wazungu?

Waliwafukuza kwanza waliopona hifadhi zimejaa viumbe wanavyotaka wakawarejesha lakini wamepewa elimu za uhifadhi na zaidi hawafanyi shughuli zozote za uzalishaji kama kilimo au ufugaji ndani ya hifadhi zaidi ya kuendeleza tamaduni zao.
Dunia itambue kwamba, Ndugu zetu Wamasai Wanateseka.

Wamasai ni wahanga wa Serikali ambayo imeshindwa kuwapa haki ya kumiliki na kuishi katika ardhi yao. Ni muhimu kuwawajibisha wale walio madarakani kwa matendo yao na kutetea haki za Jamii zilizotengwa.
 
Ndio nimesema wewe mleta mada ni Magaidi. Itoshe, badala ya kutetea hoja yenu mnaanza kunishambulia. Mtashindwa na mtalegea.

Narudia, Nyie ni magaidi, hamna tofauti na Magaidi na madhalimu wengine hapa Duniani.

Roho zenu zinaungua na mtaendelea kuungua mbeleni. Mlegee.
Maamuzi ya miaka 100 ijayo huwaga sio maamuzi ya kucheka na nyani. Kilichofanywa na Rais Samia ni urithi wa Tanzania.
 
Ni muda muafaka wa kumpongeza Rais Samia kwa kuwahamisha Wamasai na wakazi wengine ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kulingana na maamuzi kama hayo yaliyowahi kufanyika Canada na Marekani...
Na "SIASA TUNAIGA CANADA???....
 
Mambo ya kuiga sijui Canada, sijui India sijui Cuba sijui Dubai nk...yanatoka wapi.

Kama tunaiga tuige na siasa zao pia na demokrasia yao.

Sio nusunusu....
 
Mambo ya kuiga sijui Canada, sijui India sijui Cuba sijui Dubai nk...yanatoka wapi.
Kama tunaiga tuige na siasa zao pia na demokrasia yao.
Sio nusunusu....
Demokrasia sio chupa ya Coca-cola lazima ifanane kila mahali. Demokrasia inatakiwa kufuata utamaduni wa eneo husika. Demokrasia ya mzungu ushoga unaruhusiwa ,je kwako ni sawa?
 
Kuandika uongo nikazi ngumu sana, inabidi ushushe gazeti Ili kujaribu kueafanya wasomaji wauine kama unafanana na ukweli lakini haiwezekani.
 
Ndio nimesema wewe mleta mada ni Magaidi. Itoshe, badala ya kutetea hoja yenu mnaanza kunishambulia. Mtashindwa na mtalegea.

Narudia, Nyie ni magaidi, hamna tofauti na Magaidi na madhalimu wengine hapa Duniani.

Roho zenu zinaungua na mtaendelea kuungua mbeleni. Mlegee.
Mara moja hii umeshachanganyikiwa na kupwagaza maneno namna hiyo ?!!! [emoji1787][emoji1787]

Kweli NGO's zimeshikwa pabaya.....mkuu hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho....

Serikali iko sahihi kuangalia maslahi mapana zaidi ya wachache humo Ngorongoro [emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Stop the Genocide
[emoji15][emoji15][emoji15]
Umeanza na "personality disorder" na kugeuka haraka kuwa na "psychosis" ?!!! [emoji1787][emoji1787]

Genocide gani ambayo the so called "perpetrators" wanawaacha wamasai wa maeneo mengine ?!!!

Genocide gani ambayo "perpetrators" wanawahamisha wengine kwenda kuishi MSOMERA HANDENI?!! [emoji1787]

Mirembe vitanda havitoshi na wengine kuzagaa humu mitaani ?!! [emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Ni muda muafaka wa kumpongeza Rais Samia kwa kuwahamisha Wamasai na wakazi wengine ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kulingana na maamuzi kama hayo yaliyowahi kufanyika Canada na Marekani.

Tarehe 20 ya mwezi wa 7 kila mwaka nchini Canada wanasherehea ' National Park Day" sherehe ambayo Wacanada wanapewa ruhusa ya kutembelea hifadhi za Taifa bure.

Inasemwa kwamba furaha ya uwepo wa siku hii unachagizwa na maamuzi magumu na mazito yaliyochukuliwa miaka ya 1880 na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Taifa hilo la kuwahamisha wazawa na wakazi kwenye hifadhi za Taifa.

Mwaka 1887 hifadhi ya kwanza Canada na ya Tatu duniani inayoitwa "Banff National Park" ilianzishwa Kwa wazawa kuhamishwa tena kwa kutumia nguvu kubwa. Maamuzi hayo leo ndio yamesadia kukuza utalii ndani ya Canada na utalii unachangia pakubwa sana katika Pato la Taifa la pili kwa ukubwa Marekani ya Kaskazini.

Mchakato wa kuwahamisha wazawa kwenye hifadhi haukuishia hapo bali uliendelea kwenye hifadhi nyingine ndani ya Canada na Marekani.

Faida zilizopatikana/zinazopatika a maeneo husika Kwa kuwahamisha wakazi kwenye hifadhi:
Kwanza, kukuza utalii wa ndani na wa nje. Utalii kama chanzo kikubwa Cha mapato na fedha za kigeni kwa mataifa mengi, mataifa mengi yameangalia suala la kukuza utalii Kwa namna hii. Kama ilivyokuwa kwa hifadhi ya 'Banff' nchini Canada na hapa Tanzania utalii Ngorongoro utakua sana.

Pili, kulingana na mtazamo wa wahifadhi, Moja ya njia ya uhifadhi ni kuwatenganisha binadamu na viumbe wengine. Kwenye hifadhi Kuna viumbe vingi ambavyo ni urithi wa dunia, viumbe hivyo kuwa karibu na binadamu ni kuhatarisha uwepo wao. Ndio maana yanafanyika maamuzi ya kuwahamisha.

Hasara za kuwahamisha wazawa kwenye maeneo ya hifadhi:
Kwanza, kupotea kwa utamaduni wa wazawa na asili yao.

Pili, kama itatumika nguvu inawezekana wakapanga kurudi tena baadae Kwa hoja za kurejesha utamaduni na asili yao.

The way forward: Wazawa kama wahifadhi:
Ili kuepukana hasara za hapo juu nchini Canada walifanya makubaliano mbalimbali na wazawa na wazawa wakawa ni wahifadhi namba moja na haya ni baadhi ya makubaliano hayo:

Mwaka 1984 kulifanyika "Inuvialuit Final Agreement" ya kuruhusu wazawa kuwepo hifadhini Kwa kutengenewa eneo dogo ndani ya hifadhi ili waweze kudumisha mila, desturi na tamaduni zao.

Vivyo hivyo mwaka 1993 kulifanyika "Gwaii Haanas Agreement" kati ya Haida Nation na nchi ya Canada juu ya uhifadhi wa maliasili na utamaduni katika " Gwaii National Park Reserve"

Makubaliano kama hayo yanaendelea kwenye nchi nyingine nyingi mpaka Leo katika hoja kwamba WAZAWA NI WAHIFADHI.

The way forward: Hoja ya wazawa ni wahifadhi na suala la Ngorongoro:
Nadhani nasi pia tunaweza kwenda na hoja hiyo ya wazawa ni wahifadhi kwenye suala la Ngorongoro na Wamasai lakini iendane na mazingira ya kwetu.

Pawepo na makubaliano maalumu na wazee wa kabila la kimasai na Serikali, watengewe eneo kidogo ndani ya hifadhi ambalo watakuwa wanaishi humo. Hoja ya msingi ya kutengewa eneo hilo ni kuendeleza na kudumisha utamaduni wao na sio vinginevyo

Hitimisho,
Kama kichwa Cha mada kinavyosema uamuzi wa kuwahamisha Wamasai Ngorongoro ni sahihi na Rais Samia apongezwe Kwa hilo.

Kwa uelewa Zaidi, pitia hapa https://www.google.com/url?sa=t&sou...AQFnoECCsQAQ&usg=AOvVaw2TYKY4LSgGKHllgAjlsyQQ
Njaa imekupanda kichwani wewe
 
Wakati Nchi zilizofanya maangamizi dhidi ya Watu bara la Marekani kaskazini na Canada wakitafuta suluhu na Kuanza kutubu na kuomba misamaha ya kufanya Uangamizaji huko kwa karne na karne, leo hii anatokea mtu Kumpongeza Raisi wa Tanzania kufanya Uangamizaji wa watu wa Maasai.

Sijawahi kusema haya,..
Raisi Samia hastahili pongezi lelote lile likija suala la Wamasai.

Wanaangamia.

This is Pure Terrorism
Huyo mleta mada ni zaidi ya zwazwa
 
[emoji15][emoji15][emoji15]
Umeanza na "personality disorder" na kugeuka haraka kuwa na "psychosis" ?!!!
Ati ndi hoja hiyo?
[emoji1787][emoji1787]

Genocide gani ambayo the so called "perpetrators"
Hamna cha the so called hapa. Ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ikiongozwa na Rais wake
wanawaacha wamasai wa maeneo mengine ?!!!
Usijifanye mbumbumbu
Genocide is happening!
Genocide gani ambayo "perpetrators" wanawahamisha wengine kwenda kuishi MSOMERA HANDENI?!!
Watu wa Handeni nao wameanza kurudisha kadi za CCM huko kwa "perpetrators"
[emoji1787]

Mirembe vitanda havitoshi na wengine kuzagaa humu mitaani ?!
So what, people won't notice the difference? We acha, kama Kusema Serikali ya Tanzania inahusika katika maangamizi ya wamasai loliondo na morogoro inafungua vitanda mirembe, so let it be.
! [emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
STOP THE GENOCIDE.
 
Ukweli ni kwamba Uhifadhi wa Serengeti wa leo hauwezi kulinganishwa na uhifadhi wa Canada au nchi yeyote ile kati ya karne hizo za 17 na 18, au kwa mantiki ya mleta mada, kuwafurusha Wamasai huko.
Kuna tofauti.

Uhifadhi wa Serengeti unatokana na kutambua thamani ya ecolojia ambayo ni makazi ya jamii ya Wamasai. Itoshe, mradi wa uhifadhi ulilenga kulinda usawa wa asili wa mazingira, kuzuia ujangili(ambao sasa ni kinyume au kinzani na baadhi ya malengo; umepewa kibali sasa kufanya ujangili), haijalishi-uhifadhi huo ulilenga kusaidia maendeleo endelevu na elimu kwa watu wa eneo hilo, yaani Wamasai. Serikali imeahindwa kufanya hivyo, sasa inawaangamiza. Waingereza na Wafaransa walipora na kuangamiza kila kitu huko.....

Pia, Historia inatuambia Canada katika karne ya 17 na 18 iligibikwa na unyonyaji wa maliasili na kuhamishwa kwa watu wa asili na walowezi wa Ulaya. Wakoloni hao wa kutoka ulaya walifika huko sio kwa uhifadhi bali kuanzisha biashara, mashamba ya kulima na vituo vya kijeshi kwa malengo ya kutawala-sawa na wanaofanya Waarabu Ngorongoro sasa na mawakala wake Serikalini.

kwa hiyo,
historia ya ukoloni wa Canada ulisukumwa zaidi na maslahi ya wachache na yaliharibu mazingira na watu wa Asili wa huko, they commited Gonocide. Hii haina tofauti na hawa wa sasa kufanya hayo hayo, sasa unawezaje kudai tuwaige Waingereza na Wafaransa waliovamia Canada na kusababisha maafa ya mazingira, maafa ya watu asili wa Canada?
 
Anawahamisha ili wafanye nini ? Kwangu mimi the End might Justify the means kama wanapunguzwa / Sio kumaliza wote ili watunza mazingira well and good ila kama wanahamishwa ili The highest bidder afanye yake watu wapate 10% hilo halina tofauti na wale jamaa waliokuwa wanauza ndugu zao kama watumwa...
 
Demokrasia sio chupa ya Coca-cola lazima ifanane kila mahali. Demokrasia inatakiwa kufuata utamaduni wa eneo husika. Demokrasia ya mzungu ushoga unaruhusiwa ,je kwako ni sawa?
Utamaduni wa TZ yenye makabila zaidi ya 100 ni upi?
Tunataka Katiba mpya!
 
Back
Top Bottom