Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

Hii ni aibu kwa wana-korogwe kwa kumchagua huyu jamaa.Na hata hilo la kushindwa kutofautisha kati ya Polisi, Jeshi, UWT, Mgambo, Sungusungu, Polisi Jamii, Polisi Shirikishi n.k. ni kutokana na elimu yake ndogo ya Std 7.Iwepo sheria ya kudhibiti vilaza kama hawa kuingia bungeni.

.......aliahidi watu wa Korogwe atawapa matibabu ya uganga wa kienyeji bure wakiwa na shida yoyote ile. Kazi mnayo wanakorogwe
 
Tuesday, 23 August 2011

TUNALAZIMIKA leo kutamka pasipo kutafuna maneno kwamba, matatizo makubwa yaliyoikumba nchi yetu katika miezi ya hivi karibuni yasingetokea au yasingeleta madhara makubwa iwapo Usalama wa Taifa ungetimiza wajibu wake kwa uadilifu na weledi. Sote ni mashahidi wa majanga mbalimbali yaliyoisibu na yanayoendelea kuisibu nchi yetu kiasi cha kuibua maswali kuhusu uwajibikaji wa Usalama wa Taifa katika kulinda maslahi ya Taifa letu.

Ni wazi sasa kwamba wananchi wanaona chombo hicho kama vile kimepoteza mwelekeo kwa sababu ya kwenda kinyume na malengo na matamanio ya waasisi wake. Baada ya nchi yetu kupata uhuru, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alianzisha chombo hicho ili kusaidiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama kulinda nchi yetu na watu wake.

Usalama wa Taifa haukuanzishwa kulinda mifumo hasi inayoneemesha makundi ya watu wachache. Wala haukuanzishwa kuwa chombo cha kulinda mafisadi au mifumo ya kisiasa na kiutawala, kwa maana ya kuratibu na kuhakiki chaguzi na teuzi mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha kundi fulani la viongozi linabaki madarakani.

Mbali na kulinda uhuru wa nchi yetu na watu wake, Usalama wa Taifa ulianzishwa kulinda uchumi wetu na kuhakikisha rasilimali za nchi yetu zinatumika tu kunufaisha na kuendeleza vizazi vilivyopo na vijavyo. Usalama wa Taifa ulipewa majukumu hayo ya kulinda uchumi kwa sababu pasipo uchumi imara uhuru, amani na maendeleo haviwezi kupatikana.

Kama tulivyodokeza hapo juu, nchi yetu imepata mitikisiko mikubwa kutokana na matatizo mbalimbali ambayo tunadhani yangemalizika au kupungua iwapo Usalama wa Taifa ungewajibika ipasavyo. Tatizo la uchakachuaji wa mafuta ambalo liliathiri sana uchumi wetu lilikuwa katika uwezo wa chombo hicho kulimaliza, kwani kilipaswa kuwachunguza na kuwakamata wahalifu hao na kuwapeleka katika vyombo vya kisheria. Kutokana na udhaifu wa chombo hicho, Serikali ilikurupuka na kupandisha bei ya mafuta ya taa yanayotegemewa na watu wengi maskini hapa nchini.

Ni jukumu la Usalama wa Taifa kutafiti na kugundua vyanzo na wasambazaji wa madawa ya kulevya yanayoingizwa nchini na kusababisha madhara makubwa kwa afya ya wananchi. Ni chombo hicho pia ambacho kina wajibu na uwezo wa kutafiti na kuchunguza vyanzo vya bidhaa feki vinavyoingizwa na kusambazwa nchini. Vilevile, ni Usalama wa Taifa wenye wajibu na uwezo wa kugundua mitandao ya kusafirisha wahamiaji haramu wanaoingizwa katika nchi yetu kwa viwango vya kutisha. Chombo hicho kinao wajibu wa kuchunguza mitandao ya nje na hapa nchini inayohusika na biashara hiyo haramu lakini kimeshindwa kabisa kufanya hivyo.

Usalama wa Taifa lazima pia ubebe lawama kwa kushindwa kunusa mapema mgomo wa wauza mafuta uliofanyika hivi karibuni ili Serikali iingilie kati. Kwa kushindwa kufanya hivyo, nchi nusra itumbukie katika maangamizi yasiyo kifani. Uchumi wetu uliathirika kwa kiwango kikubwa kama unavyoendelea kuathirika kwa kuchapishwa na kusambazwa kwa noti bandia na wahalifu ambao Usalama wa Taifa umeshindwa kuwang'amua kwa muda mrefu sasa.

Tukiangalia kwa undani tukio la hivi karibuni la utoroshaji wa wanyamapori kwenda nchi za nje, ni vigumu Usalama wa Taifa kuepuka lawama kutokana na wanyama hao kupitishwa mahali nyeti kama Uwanja wa Ndege wa KIA pasipo kugundulika. Ndivyo lilivyo tatizo la ukabila serikalini na katika utumishi wa mashirika ya umma. Na ndivyo lilivyo tatizo la umeme linaloendelea kuua uchumi wetu na hakika ndivyo pia lilivyo tatizo la kufa kwa viwanda vyetu vilivyobinafsishwa kifisadi na kusababisha ukosefu wa ajira kwa wananchi.

Hakika safu hii haina nafasi ya kutosha kuorodhesha udhaifu wote wa chombo hicho katika kukabiliana na maadui wa nchi yetu kiuchumi, nakadhalika. Tunashauri chombo hicho kifumuliwe ili kiundwe upya na kupewa mwelekeo na majukumu mapya. Tunasisitiza kwamba mfumo wa Usalama wa Taifa uliopo sasa hautufai, ufumuliwe.



Source: Mwananchi - Usalama wa Taifa uvunjwe, umeshindwa majukumu
 
Hawa jamaa wanafanya kila MTZ ajifanye na yeye usalama wa taifa coz wanajulikana na wanajiachia sana hamna siri tena.
 
Labda tujue usalama wa Taifa wao wanaishia wapi kwenye kufuatilia mambo
1) Wanatoa report kwa serikali na wao kazi yao inakuwa imeisha?
2) wana uwezo wa kusimamia utekelezaji wa waliyoyafanyia uchunguzi?
3) Kama kitu kinaatarisha Taifa Kiuchumi (Ufisadi EPA, Meremeta nk ), wao wamekitolea report na serikali ikaendelea na uchafu, Usalama wa Taifa wana Nguvu gani ya Kisheria Kuzuia hayo?
4) Usalama wa Taifa wa Tanzania ni wa kusimamia Usalama wa Viongozi, Siasai na Uvamizi tu ama ni wa kusimamia pia Uchumi, Technologia, Afya, nk?
 
jamani mfumo wanaofanyia kazi mnaujua au mnaropoka tu. waoneeni huruma wao ni wazalendo kweli kweli
 
Katika historia za nchi hii miaka ya nyuma idara hii ilitaka kuvunjwa maana ilianza kupoteza mwelekeo na kuendeshwa kimajungu zaidi kama magazeti ya udaku lakini mwalimu akawasihi wenzake akasema mapungufu yarekebishwe na Idara iendelee kuwepo maana kila nchi lazima iwe na idara hii kwa ya ujasusi na walijirekebisha na maisha kuendelea.

Na ndiyo waliompa mwalimu taarifa kuwa Kikwete hafai na Mwalimu akaja na kigezo cha ki diplomasia zaidi na kumwambia kuwa umri wake bado na maagizo kwa mkapa ni kwamba huyu jamaa hakutakiwa kabisa kunusa magogoni ila walishachelewa maana jamaa alishapenyeza wahuni kila mahali kwa kushirikiana na Lowassa na hivyo kufanya kazi ya kumwengua kuwa ngumu.

Ndicho tunachovuna maana ameingia madarakani ameshafanya mabadiliko mengi na kuwapandikiza watoto wa vigogo na hivyo hakuna Idara tena bali ni chipukizi wa uvccm. Na walio safi wanaogopa kuripoti maana kazi zitakuwa mashakani.

Kifupi hawa jamaa hawapo kwa sasa wamebaki masalia ya mbali na ndiyo wanaovujisha siri ili kuinusuru nchi lakini bado umelala hatutaki kutoka mbele tuwange mkono hawa masalia ya Nyerere.
 
Tuesday, 23 August 2011

TUNALAZIMIKA leo kutamka pasipo kutafuna maneno kwamba, matatizo makubwa yaliyoikumba nchi yetu katika miezi ya hivi karibuni yasingetokea au yasingeleta madhara makubwa iwapo Usalama wa Taifa ungetimiza wajibu wake kwa uadilifu na weledi. Sote ni mashahidi wa majanga mbalimbali yaliyoisibu na yanayoendelea kuisibu nchi yetu kiasi cha kuibua maswali kuhusu uwajibikaji wa Usalama wa Taifa katika kulinda maslahi ya Taifa letu.

Ni wazi sasa kwamba wananchi wanaona chombo hicho kama vile kimepoteza mwelekeo kwa sababu ya kwenda kinyume na malengo na matamanio ya waasisi wake. Baada ya nchi yetu kupata uhuru, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alianzisha chombo hicho ili kusaidiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama kulinda nchi yetu na watu wake.

Usalama wa Taifa haukuanzishwa kulinda mifumo hasi inayoneemesha makundi ya watu wachache. Wala haukuanzishwa kuwa chombo cha kulinda mafisadi au mifumo ya kisiasa na kiutawala, kwa maana ya kuratibu na kuhakiki chaguzi na teuzi mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha kundi fulani la viongozi linabaki madarakani.

Mbali na kulinda uhuru wa nchi yetu na watu wake, Usalama wa Taifa ulianzishwa kulinda uchumi wetu na kuhakikisha rasilimali za nchi yetu zinatumika tu kunufaisha na kuendeleza vizazi vilivyopo na vijavyo. Usalama wa Taifa ulipewa majukumu hayo ya kulinda uchumi kwa sababu pasipo uchumi imara uhuru, amani na maendeleo haviwezi kupatikana.

Kama tulivyodokeza hapo juu, nchi yetu imepata mitikisiko mikubwa kutokana na matatizo mbalimbali ambayo tunadhani yangemalizika au kupungua iwapo Usalama wa Taifa ungewajibika ipasavyo. Tatizo la uchakachuaji wa mafuta ambalo liliathiri sana uchumi wetu lilikuwa katika uwezo wa chombo hicho kulimaliza, kwani kilipaswa kuwachunguza na kuwakamata wahalifu hao na kuwapeleka katika vyombo vya kisheria. Kutokana na udhaifu wa chombo hicho, Serikali ilikurupuka na kupandisha bei ya mafuta ya taa yanayotegemewa na watu wengi maskini hapa nchini.

Ni jukumu la Usalama wa Taifa kutafiti na kugundua vyanzo na wasambazaji wa madawa ya kulevya yanayoingizwa nchini na kusababisha madhara makubwa kwa afya ya wananchi. Ni chombo hicho pia ambacho kina wajibu na uwezo wa kutafiti na kuchunguza vyanzo vya bidhaa feki vinavyoingizwa na kusambazwa nchini. Vilevile, ni Usalama wa Taifa wenye wajibu na uwezo wa kugundua mitandao ya kusafirisha wahamiaji haramu wanaoingizwa katika nchi yetu kwa viwango vya kutisha. Chombo hicho kinao wajibu wa kuchunguza mitandao ya nje na hapa nchini inayohusika na biashara hiyo haramu lakini kimeshindwa kabisa kufanya hivyo.

Usalama wa Taifa lazima pia ubebe lawama kwa kushindwa kunusa mapema mgomo wa wauza mafuta uliofanyika hivi karibuni ili Serikali iingilie kati. Kwa kushindwa kufanya hivyo, nchi nusra itumbukie katika maangamizi yasiyo kifani. Uchumi wetu uliathirika kwa kiwango kikubwa kama unavyoendelea kuathirika kwa kuchapishwa na kusambazwa kwa noti bandia na wahalifu ambao Usalama wa Taifa umeshindwa kuwang'amua kwa muda mrefu sasa.

Tukiangalia kwa undani tukio la hivi karibuni la utoroshaji wa wanyamapori kwenda nchi za nje, ni vigumu Usalama wa Taifa kuepuka lawama kutokana na wanyama hao kupitishwa mahali nyeti kama Uwanja wa Ndege wa KIA pasipo kugundulika. Ndivyo lilivyo tatizo la ukabila serikalini na katika utumishi wa mashirika ya umma. Na ndivyo lilivyo tatizo la umeme linaloendelea kuua uchumi wetu na hakika ndivyo pia lilivyo tatizo la kufa kwa viwanda vyetu vilivyobinafsishwa kifisadi na kusababisha ukosefu wa ajira kwa wananchi.

Hakika safu hii haina nafasi ya kutosha kuorodhesha udhaifu wote wa chombo hicho katika kukabiliana na maadui wa nchi yetu kiuchumi, nakadhalika. Tunashauri chombo hicho kifumuliwe ili kiundwe upya na kupewa mwelekeo na majukumu mapya. Tunasisitiza kwamba mfumo wa Usalama wa Taifa uliopo sasa hautufai, ufumuliwe.



Source: Mwananchi
 
Naamini usalama wa taifa yamebakia mabaki tu. Iliyopo sasa ni walinzi wa mageti ya Ikulu, Takukuru na CAG. Hawathaminiwi kabisa. Naamini wanatoa taarifa zote muhimu ktk vyombo husika.

Hebu tujikumbushe kisa cha afande Mwema kumpigia simu mtuhumiwa na kumweleza kuwa fulani kakutaja kuwa unafanya hili na hili!

Dawa ya watendaji wetu iwekwe wazi na bunge, UKITUHUMIWA hakuna cha tume ila ujiuzuru. Mbona tumeshuhudia afande kule London akijiuzuru kufuatia fujo za vijana hivi majuzi, kwetu inashindikana nini?
 
Ukipita mitaa ya wanayoishi usalama wa taifa, ukiangalia maisha yao na watoto wao ni sawa na maisha ya wananchi wanaolia kila siku ugumu wa maisha. Wanaishi kwenye lindi la umasikini na karaha. Hata wakati mwingine wanagandamizwa na sheria wanazozilinda au kuzifanyia kazi. Wananyanyaswa kimaisha na kujikuta wanatumikia tumbo badala ya taaluma zao. Ukiwauliza wengi wamekata tamaa, wanafanya kazi kwa maelekezo kwa sababu waliapa kufuata mlolongo wa amri.

Sisi ndio usalama wa taifa sisi ndio tunatumika sisi ndio wananchi sisi ndio tunaadhirika. Umefika wakati chombo hiki muhimu kijitambue. Tuelezane kuwa maisha haya magumu ni kushindwa kwa taasisi zetu nyingi kwa kumtumikia mjomba. Hakuna sababu ya usalama wa taifa kukubali kutumika kuiba kura ya mwanao, mjomba , mke au mume. Kuiba kura na haki ya baba yako na mama yako kisa tu wewe usalama wa taifa. Kuiba kura ya daktari halafu kesho unahitaji matibabu bora, kuiba kura ya mwalimu halafu kesho unadai elimu bora kwa mwanao. Usalama wa taifa semini sasa basi tumechoka kuzulumu watu wetu na ndugu zetu, semeni tunataka kufanya kazi kwa heshima na mujibu wa mafunzo yetu.

Polisi, chokeni: wamefikia mahala sasa wanaowaona vikaragosi, kila mwenye shati la kijana anawaona hamnazo, matusi yamekuwa chakula chenu. Wanawatumia pale wanapotaka kama taulo, wanawatumia pale wanapotaka kama choo. wakisha maliza haja zao wanawatukana, hawajali maslahi yenu, mna maisha duni na ya kusonesha, hamna uhakika wa kesho. Msiposaidia kwenye wimbi hili la demokrasia na vita vya kiuchumi, matusi yataongezeka kwani mashati ya kijani yanawakumbuka tu kwenye kuiba kura.

Polisi kumbukeni ninyi ni sisi, tunaishi sote kwa taabu na familia zetu, kwanini mfie watu wasio wathamini. Simamieni haki semeni imetosha, jitokezeni wajasiri mtakumbukwa daima.

chief Mkwawa wa kalenga
Uhuru ni pamoja na kujua aliyekuweka utumwani
 
Unaweza kutolea ushahidi hayo unayoyasema au unabwabwaja tu?
 
unaweza kutolea ushahidi hayo unayoyasema au unabwabwaja tu?

angalia kota za police zilivyo kama magofu mfano k.koo yanapopaki magari ya mbezi na kimara, buguruni sokoni ukiziona utadhani magofu yaliyotelekezwa na wenyewe kabla ya uhuru kumbe zinatumika na wasimamia sheria wa tz
 
Ccm mnawatumia hawa jamaa kama toiletpaper na nyie police na usalama wa taifa ni wakati sasa yafaa mbadilike ili maisha yenu nayo yabadilike
 
Umeonyesha uzalendo wako kwa kulitumia jukwaa hili kama ilivyokusudiwa, asante kwa fikra sahihi mahali sahihi mkuu
 
Bwana eeh labda polis tu ila naskia usalama wa taifa wanakula mishahara minono sana hawa watu ndiomana wanajitahd kuwaweka ccm madarakan by any way
 
Chief Mkwakwa wa Kalenga, umetumia vizuri jina lako kuwakilisha ujumbe muhususi, wenye mantiki, na wenye ukweli usiopingika.

Ni kawaida unapokutana na Chief, basi tunategemea Busara zaidi. Kwa hilo ujumbe umefika tutake, tusitake, na nina hakika watu walishaanza kubadilika na tumeshuhudia tukipewa habari nyingine toka ndani kabisa ya vikao vizito. Hiyo inadhihirisha kuchochwa na mwenendo wa uongozi.

Ahsante Chief.
 
Hakuna mitaa ya Usalama wa Taifa. Usalama wa Taifa wanakaa katika gated community, sasa wewe sijui ulipita vipi kule.

Kuhusu wao kuwa na maisha magumu, sijui kuhusu polisi, lakini kuhusu Usalama wa Taifa siyo rahisi outright kwangu mimi kusema kwamba wanaishi maisha magumu. In fact,I am tempted to say kwamba they are filthy rich [yaani matajiri sana], but I could be wrong;inawezekana kwamba wanaishi kwa matabaka;kwamba wengine ni matajiri kuliko wengine.

You are calling for them to rebel, [or something like that].

Mimi nadhani military rule imekuwa na sifa mbaya duniani,;lakini nadhani,kimsingi,there is nothing wrong with military rule, militaristic rule. Musharraf Pakistan alikuwa na Serkali ya Kijeshi lakini Bunge lilikuwepo.

In fact, kule Pakistan kuna Brigade maalum ambayo kazi yake ni hiyo tu ya Kupindua Serikali [if the need arises]
Mimi nadhani there is a place for military governance katika siasa za Dunia.

In Japan after the war, General MacAuthour ndiye aliyeijenga Japna ikawa great economic power[after which MacArthur almost wanted to run for president when he went back home to the US.
 
Ukipita mitaa ya wanayoishi usalama wa taifa, ukiangalia maisha yao na watoto wao ni sawa na maisha ya wananchi wanaolia kila siku ugumu wa maisha. Wanaishi kwenye lindi la umasikini na karaha. Hata wakati mwingine wanagandamizwa na sheria wanazozilinda au kuzifanyia kazi. Wananyanyaswa kimaisha na kujikuta wanatumikia tumbo badala ya taaluma zao. Ukiwauliza wengi wamekata tamaa, wanafanya kazi kwa maelekezo kwa sababu waliapa kufuata mlolongo wa amri.

Sisi ndio usalama wa taifa sisi ndio tunatumika sisi ndio wananchi sisi ndio tunaadhirika. Umefika wakati chombo hiki muhimu kijitambue. Tuelezane kuwa maisha haya magumu ni kushindwa kwa taasisi zetu nyingi kwa kumtumikia mjomba. Hakuna sababu ya usalama wa taifa kukubali kutumika kuiba kura ya mwanao, mjomba , mke au mume. Kuiba kura na haki ya baba yako na mama yako kisa tu wewe usalama wa taifa. Kuiba kura ya daktari halafu kesho unahitaji matibabu bora, kuiba kura ya mwalimu halafu kesho unadai elimu bora kwa mwanao. Usalama wa taifa semini sasa basi tumechoka kuzulumu watu wetu na ndugu zetu, semeni tunataka kufanya kazi kwa heshima na mujibu wa mafunzo yetu.

Polisi, chokeni: wamefikia mahala sasa wanaowaona vikaragosi, kila mwenye shati la kijana anawaona hamnazo, matusi yamekuwa chakula chenu. Wanawatumia pale wanapotaka kama taulo, wanawatumia pale wanapotaka kama choo. wakisha maliza haja zao wanawatukana, hawajali maslahi yenu, mna maisha duni na ya kusonesha, hamna uhakika wa kesho. Msiposaidia kwenye wimbi hili la demokrasia na vita vya kiuchumi, matusi yataongezeka kwani mashati ya kijani yanawakumbuka tu kwenye kuiba kura.

Polisi kumbukeni ninyi ni sisi, tunaishi sote kwa taabu na familia zetu, kwanini mfie watu wasio wathamini. Simamieni haki semeni imetosha, jitokezeni wajasiri mtakumbukwa daima.

chief Mkwawa wa kalenga
Uhuru ni pamoja na kujua aliyekuweka utumwani

What are you trying to imply, ni kwamba huko waliko hawana watu wanao ona matatizo yaliyopo! I think you are probably wrong! Hao wote ni watu wenye akili zao.

Kuwa na akili nzuri hakuna uhusiano na kuhamasisha vurugu. They are probably fighting their battle while standing on their positions. Not all problems can be solved politically. Take your part in solving the problems surrounding us siyo kuhamasisha vurugu.

One thing you should understand history shows that all immediate changes have never been sustained. Smooth changes however have always been fruitful and can be sustained.
 
Mawazo mazuri ya kizalendo haya. Taasisi hizi zinatakiwa zifanye kazi kwa uaminifu na haki ili ziheshimike katika jamii.

Makamanda wa majeshi yote na taasisi nyingine za usalama, wanatakiwa waelewe kwamba wataheshimika zaidi kuliko viongozi wa kisiasa pale watakapojiepusha na upendeleo katika utoaji haki.

Makamanda na wanajeshi wenye uhuru wa mawazo ni lazima waelewe kwamba, hakuna wanachopoteza wanapohakikisha haki imetendeka,ila wakishiriki kunyang'anya haki basi wanapoteza heshima na imani ya wananchi kwao.
 
Back
Top Bottom