Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

katika moja ya TAASISI ninazoziheshimu katika nchi hii, hii ni moja wapo lkn wananishangaza sana, nchi inaingia ktk mikataba mibovu, watu wanakwiba mali za umma, EPA, ubazazi wa kijinga unafanywa WAO WANAANGALIA TU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!. nilitegemea hawa wawe ndio wezi wa tech nje ya nchi kama wenzetu (nchi za nje zilizoendelea)wafanyavyo, lkn wapi Bw., nilitegemea wangeweza kuzuia kufanyika hayo kwa maslahi ya umma lkn wapi Bw. HIVI KWAO(TISS) MASLAHI TAIFA NINi YEPI?
 
Waasisi wa TISS ni akina hayati Emil Mzena kwa kweli kipindi chake idara iliweza kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa, leo tatizo na changamoto inayoipata idara ni huu ubazazi wa ajira, waliomo ndani wanawapigia pande ndugu zao,hali hii inapelekea kuajiriwa wa koo fulani tu utadhani ndio warithi wa nchi hii, watu ambao uwezo wao ni mdogo katika kazi hii wakati Mzena alihahakikisha ajira inafanyika kiumakini sana wanatazamwa wenye vipaji vya kazi hii, leo wenye vipaji vya hii kazi wanaachwa nje kwa kuwa hawana ndugu ndani ya idara wa kuwapigia chapua waweze kuajiriwa, kwa muktadha kama tunataka idara irejee katika ile heshima ya mwanzo basi mabadiliko makubwa yafanyike pia Mzena alihakikisha uwiano wa makabila, leo tunaona walio wengi ndani ya idara ni wahehe,wabondei,wabena na wanyakyusa je uko wapi uadilifu? je makabila mengine hayana haki?
 
Kuna tatizo kubwa linaloikabili idara hii ni usiri wa mapendekezo yao, mimi naamini idara hii inafany kazi vizuri kwa kufuata weledi lakini ikumbukwe wao ni watu wa kushauri kwa kutumia vigezo na suala la kuamua lipo mikononi mwa serikali. Mapungufu mengine waliyoyataja wachangiaji nayakubali.
 
Ukiangalia hasa asili ya idara ya usalama wa Taifa utakuta kuwa FIRAUNI (Pharao) ndiyo mwanzilishi mkuu na lengo lake ni kuhakikisha utawala wake unadumu. Hii ni kwa mujibu wa vitabu. Ngoja nitoa hadithi kidogo halafu ntaielezea idara yetu ya TISS kutokana na maelezo yako hapo juu

Chanzo cha Idara ya usalama wa Taifa a.k.a usalama wa kutawala:

'The Israelites were living a life of slavery under the rule of the Pharaoh where hardship and oppression was part and parcel of their life. Once the Pharaoh saw an unusual dream for which he asked his royal wise men to interpret. They gave the meaning that a boy will be born in the family of the Israelites who will liberate them from this slavery and who will destroy the Pharaoh's empire. Not being able to handle this devastating news, he ordered his men that all new born male children must be murdered. His men went to the Israelites' villages and started to brutally murder all the new born male children. Musa (AS) was born at such distressing times. The mother of Musa (AS) fearing the life of her child was very perplexed on what to do. However, Allah had already destined the future of this child and had decreed that he will survive and the same Pharaoh who ordered the killing, will raise him.
The mother upon being inspired by Allah put the child in a basket and set him off in the river. She sent her daughter to look and see what will be the fate of child. The basket went and reached the house of the Pharaoh. The wife of the Pharaoh fell in love with the child as soon as her gazed fell upon him and intended to raise the child.'

Analysing the story:
  • Pharaoh the Ruler - Presidents
  • Royal wise men to interpret the dream - Political advisors (e.g Kingunge et al)
  • A boy who will be born to liberate Islaelites - Political parties(eg CDM) or Individuals
  • enslaved Islaelites - Citizens who are living in poverty while rulers enrich themselves
  • His men - Intelligence officials to sneaf and spot anyone who threatens the Empire (For this case CCM)
  • Kill the boys - Kill democracy, delegitimize oposition with fake cases and if possible eliminate those who are resistant (In election ensure Chakachua and all techniques to steal elections even scramble the electoral register to prevent enemies from voting)
Idara ya usalama wa Taifa inafanya kazi kwa masilahi ya watawala na hakuna zaidi hizo theory nyingine kuhusu kazi wanazofanya zipo kama zuga lakini lengo kuu na lengo mama ni kuhakikisha usalama wa watawala. Anyone acts contrary will face consequence Where is Imran Kombe?. Idara yetu kama ingekuwa haifanyi kazi kama 'Pharaoh's men' tungeshuhudia maendeleo makubwa sana katika kuzuia uhalifu unaofanywa na watawala na vibaraka wao. Yote yataandikwa lakini majukumu mama ni kuhakikisha CCM haishindwi uchaguzi period.
 
Kwa vyo vyote idara hii ni ya siri na inafanya kazi zake kwa siri po pote duniani, na ofisi zao si za wazi na huwa zimekuwa kampuni hewa na utafanya nao shughuli zako za kibiashara kumbe ni ofisi ya Usalama wa Taifa. Ni ofisi zao kuu ndizo zinazoweza kufahamika zilipo ambapo raia si rahisi kuguza maana utaelekezwa namna ya kuwasilisha ujumbe.

Tatizo kama alivyosema mtoa mada tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi taasisi hii imepotea kana kwamba iko likizoni na inaweza aminika kwamba ni moja ya vyombo vya dola ambavyo chama tawala inavichukulia kama kigozo cha kujiimarisha kisiasa. Hata hivyo dalili zipo wazi kwamba chombo hiki kimeanza kufungua madirisha kiaina na kwa wenye kujua mienendo ya chombo hiki kinavyofanya kazi zake atakubaliana nami. Kwa vile wakati ukuta.
 
Ahsante mkuu, lakini ukweli ni kwamba TISS ni miongoni mwa taasisi
nyeti ambazo wananchi wanaziogopa sana kwa kuamini kuwa huenda
ndio inayohusika kuwafunga midomo wale wanaoonekana kuwa ni
hatari kwa watawala.
Ninachokiona binafsi kwa mtazamo wangu, TISS haijapoteza wazalendo
tu imepoteza pia Uzalendo.
 
Mkuu Mtoa mada/Hoja umetoa maelezo mazuri mno, na umeeleza malengo na kazi hasa za usala wa taifa,
lakini swali linarudi kwako,
1)Je usalama wa taifa unafanya kazi zilizokusudiwa?
2) Usalama wa taifa unaishia wapi?
2a) Kulinda viongozi tu?
2b) kufatilia jirani (Nchi Jirani) kanunua silaha gani?
2c) Kufatilia kama nchi ina hatari za Kuvamiwa?

NASHINDWA KUJUA HAPA
kAMA USALAMA WA TAIFA WAMEPATA UHAKIKA HIKI KITU KINAATARISHA TAIFA NA WAKAFANYIA REPORT, LAKINI SERIKALI HAWAKUIFANYIA KAZI ILE REPORT WAO USALAMA WA TAIFA WATAKAA KIMYA TAIFA LIYUMBE?

kwa mtazamo wangu Usalama wa Taifa ni uwigo mpana sana, na mpaka sasa sijaona mchango wa Usalama wa Taifa kwenye Uchumi, Sayansi na Biashara

1) Uchumi
Sipati picha nchi inaingia kwenye mikataba mibovu na UWT wapo? sipati picha Fraud inafanyika mpaka Bank Kuu na usalama wa Taifa wapo kimya tu, Tuna Noti za aina mbili zinazozunguka kwenye Mzunguko, nini maana ya hiki kitu?
inamaaana hapa UWT hawaingii? Hawana watu wao pale BOT? na kama wapo Hawakuona Fraud ya EPA?, na kama waliona na wakafanya report na serikali ikapuuzia report ya UWT inamaana wao watanyamaza tu Uchafu uendeleee?

KWA KIFUPI UWT IMEMEZWA NA SIASA NA HIPO KISIASA ZAIDI NA INAFANYA KAZI ZA SIASA
 
Inaonekana ni kweli tuna uhuru mpana wa kuchambua mambo kwa kila mwenye uelewa Fulani ili tuwekane sawa kwa ambao hatuna uelewa wa kutosha...

Angalizo
Tuwe Makini katika kutoa maoni ili kuhakikisha tunajenga badala ya kubomoa kwani iko dhana kua katika ukanda huu wa Africa mashariki na kati UWT ndio chombo imara na madhubuti kuliko nchi zinazotuzunguka na hata hii
political stability despite some few recent outcomes , we
should not put ourselves on the criticising side by not
recognising the efforts hiki chombo Kinachofanya

Nimekua nikisikia wenzetu majirani wakitusifia na pia kutuponda haswa UWT kua wameshindwa kudhibitu hata hii platform ambayo inatupa fursa kuchambua na kubadilishana mawazo .

Sasa tujikite katika michango inayotujenga nakutuweka wamoja tusiwe kama wao..

Lakini pia rujiulize ni lazima kazi zao tuzijue kuona wakiwa na vipindi kwenye TV

Je ni hakuna kazi inayofanyika?
 
.......Sasa wanasimamia Usalama wa Taifa gani kama nchi ipo gizani muda wote na waliosababisha giza hilo wapo na wanapeta tu mtaani !
Hii nchi ni ya ajabu sana, Hata Mwakyembe mwenyewe ni mmoja wa watu wa Idara hii waliosababishia nchii hii hasara kwani alikataa kutoa taarifa yote ya Kamati yake ya kufuatilia sakata la Richmond.....................!!
 
Katika nchi yetu (Tanzania) kuna idara kuu tatu zinazoshughulika na kazi ya upelelezi/ uchunguzi. Idara hizo ni idara ya upelelezi wea makosa ya jinai (CID) idara ya Intelijensia ya jeshi (M I) na idara ya usalama wa Taifa. Idara hizi zinajitegemea na kila moja ina majukumu tofauti. Hata hivyo katika mazingila na nyakati maalumu, idara hizo hufanya kazi kwa kushirikiana ili kukamilisha shughuli fulani maalumu.


1. Idara ya upelelezi wa makosa ya jinai (CID).
Kama lilivyo jina lake, idara ya upelelezi wa makosa ya jinai (Criminal Investigation Department) inashughulika na upelelezi wa makosa ya jinai, kama wizi, ujambazi wa kutumia silaha, mauaji, biashara haramu ya madawa ya kulevya, wizi wa kalamu (fraud) na makosa mengine mengi kama yalivyo ainishwa katika 'penel code'. Aidha idara hiyo pia inahusika na ukaguzi wa maeneo ya tukio (crime scene) na inao wataalamu wa kazi hiyo (forensic experts)


Aidha idara hii ndio inayohusika na kufanya uchunguzi wa mashitaka yote yanayofikishwa katika vituo vya polisi kwa ajili ya kupata ushahidi wa kuwafikisha watuhumiwa mahakamani na kuwatia hatiani wavunjao sheria. Kutokana na majukumu ya askari wa CID hulazimika kuwa karibu sana na wananchi kwani kazi ya idara hii haifanywi kwa siri. Maafisa wa CID huwajibika kutoa ushahidi mahakamani kwa kesi zote walizo fanya uchunguzi.


[TABLE="class: tr-caption-container"]
[TR]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]DCI Robert Manumba
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Hata hivyo idara hii inao askari wachache wa kificho (under cover) ambao hufanya kazi ya kujipenyeza katika vikundi vya uhalifu (k.m wauza madawa ya kulevya, wezi wa mabenki n.k) kwa lengo la kupata taarifa za ndani za wahalifu hao. Kwa vile askari hawa pamoja na wengine wote wa idara hii hawavai sare na mara nyingi hubeba silaha (bastola) wananchi wanao wafahamu hudhani kuwa askari hawa pia ni maafisa wa idara ya usalama wa Taifa. Lakini ukweli ni kwamba askari wote wa idara ya upelelezi wa makosa ya jinai (CID) ni waajiliwa wa jeshi la polisi na muda wowote na kwa sababu yoyote askari wa CID wanaweza kuhamishiwa katika idara nyingine za jeshi hilo kama kikosi cha kutuliza ghasia (FFU), kikosi cha usalama barabarani (Trafic Police) au polisi wa kawaida (General duty)


Idara ya upelelezi wa makosa ya jinai inaongozwa na Kamishna wa polisi Robert Manumba ambae katika kipindi chake ameonesha kuimudu ipasavyo kazi yake kwa kuboresha utendaji kazi wa idara hiyo, na kuinua morali wa askari walio chini yake. Makao makuu ya CID yako eneo la posta mpya katika jengo la wizara ya mambo ya ndani mahali yalipo makao makuu ya jeshi la polisi.


2. Idara ya Intelijensia ya jeshi la wananchi (Millitary Intelligence).
Hii ni idara ya usalama ya jeshi la wananchi wa Tanzania. Ingawa idara hii haitajwi tajwi sana, na wala haifahamiki sana miongoni mwa wananchi wengi, Idara hii ndio idara kubwa zaidi ya usalama PENGINE kuliko idara nyingine yoyote ile nchini. Idara hii hufanya kazi zake kwa usiri wa hali ya juu kama ilivyo idara ya usalama wa Taifa, na mara nyingi maafisa wa idara hii hushirikiana na maafisa wa Idara ya usalama wa Taifa katika kazi mbali mbali.


[TABLE="class: tr-caption-container"]
[TR]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Mkuu wa Majeshi Jenerali Mwamnyange
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Kazi kubwa ya idara hii ni kuangalia usalama wa nchi ndani na nje ya jeshi, kuangalia usalama wa mipaka, kugundua njama za maadui wanaotaka kuvamia nchi yetu kijeshi, kufuatilia viashilia mbali mbali vinavyo onesha kuwepo kwa hali ya uadui kati ya nchi yetu na nchi jirani. Aidha katika kipindi cha migogoro, idara hii huwajibika kuchunguza na kujua uwezo wa adui ili kuwasaidia makamanda kuweka mikakati ya ushindi.
Idara hii pia huhusika na kufuatilia mwenendo wa maafisa wa jeshi na wapiganaji ili kulinda nidhamu ya jeshi, na kuwapasha makamanda habari kuhusu hatua za kuchukua ili kuinua morali kwa maafisa na wapiganaji.


Kwa sababu maafisa wa idara hii wako ndani na nje ya vikosi vya jeshi, mara nyingi wananchi wa kawaida hudhani maafisa wa idara hii pia ni maafisa wa idara ya usalama wa Taifa kwa sababu hawavai sare (walio nje ya vikosi vya jeshi) na mara nyingi hufanya kazi zinazo fanana na zile za idara ya usalama wa Taifa, na mara nyingine kwa kushirikiana na maafisa wa idara ya usalama wa Taifa.


(c) Idara ya usalama wa Taifa (TISS)


ITAENDELEA...


Angalizo: Mwandishi wa makala hii HANA UHUSIANO wowote na Idara ya Usalama wa Taifa
wala idara nyingine zilizotajwa katika makala hii.
Kwa maswali au maoni bofya kisanduku cha maoni.

Tembelea www.mwana-dikala.blogspot.com upate uhondo zaidi!
 
Kuna tatizo kubwa linaloikabili idara hii ni usiri wa mapendekezo yao, mimi naamini idara hii inafany kazi vizuri kwa kufuata weledi lakini ikumbukwe wao ni watu wa kushauri kwa kutumia vigezo na suala la kuamua lipo mikononi mwa serikali. Mapungufu mengine waliyoyataja wachangiaji nayakubali.
Nakubaliana na wewe Mzee wa Rula.
Wananchi wengi huwa hawaelewi kuwa TISS inakusanya habari , inazichambua lakini mtekelezaji ni Serikali yenyewe.Inabeba lawama isiyostahili kwa vile haina mdomo kisheria ya kujitangaza kwa yote inayoshughulikia.
Hata hivyo kwa wale wapenzi wa kufuatilia shughuli za CIA, MI5 na nyinginezo mtajua kuwa usiri katika shughuli zao ni nguzo muhimu sana.
Nakupongeza mkuu Rungwe kwa kuanzisha hii mada yenye info ya kuelimisha.
 
Wakurugenzi wake alianza hayati Mzena kisha hayati Gama kisha kitine kisha Dakta MAHIGA kisha Kombe kisha Apson[Huyu ndio chanzo cha mporomoko wa idara] na sasa yuko Rashid Othman[RO] anasuasua kidogo kwa mbali anajitahidi tahidi tatizo lake mpenda straehe mzee wa kujilusha.
 
Waasisi wa TISS ni akina hayati Emil Mzena kwa kweli kipindi chake idara iliweza kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa, leo tatizo na changamoto inayoipata idara ni huu ubazazi wa ajira, waliomo ndani wanawapigia pande ndugu zao,hali hii inapelekea kuajiriwa wa koo fulani tu utadhani ndio warithi wa nchi hii, watu ambao uwezo wao ni mdogo katika kazi hii wakati Mzena alihahakikisha ajira inafanyika kiumakini sana wanatazamwa wenye vipaji vya kazi hii, leo wenye vipaji vya hii kazi wanaachwa nje kwa kuwa hawana ndugu ndani ya idara wa kuwapigia chapua waweze kuajiriwa, kwa muktadha kama tunataka idara irejee katika ile heshima ya mwanzo basi mabadiliko makubwa yafanyike pia Mzena alihakikisha uwiano wa makabila, leo tunaona walio wengi ndani ya idara ni wahehe,wabondei,wabena na wanyakyusa je uko wapi uadilifu? je makabila mengine hayana haki?


Mkuu naona ni ujinga kusema kuna wanyakyusa wengi, wahehe, wabondei, wabena etc, cha muhimu ni kuangalia ni jinsi gani waliingia huko. Kama waliingia kwa kubebwa hilo ndio tatizo. Kabila lolote wanaweza kuwa TISS as long as waliingia kwa utaratibu sahihi na kuwa na sifa.

Kwa mtu mwenye akili timamu kwa sasa hawezi kuwa na imani kabisa na TISS, kwa kuwa kama kweli TISS ingekuwepo na ingekuwa effective na efficient mengi tunayolalamikia leo yasingekuwepo. Sasa hivi viongozi hawana maadili kabisa na TISS inaangalia tu (bila kushauri cha kufanya), viongozi wanaiba na wanakuwa wezi TISS inachekelea tu, kuna mambo ambayo hayakutakiwa kutokea lakini yanatokea na yanaendelea kutokea.

Whether the weakness is with our political leadership to manage and make a full use of TISS, or whether it is internal problems ( old definition ya kazi yao kuua wapinzani na dissidents na kulinda chama na kuilinda serikali na kutoijali Tanzania, nepotism and favoritism, incompetence hasa watu kukaa kwenye madawati wasiyotakiwa kukaa kuwa na uwezo mdogo kichwani kuliko nyadhifa zao, corruption na uswahili+undugunization) within TISS, still the end product is the same.

Haiwezekani sasa hivi uhalifu nchini kuwa tacitly torrelated, hakuna hatua za maana zinazochukuliwa. Usalama maana yake nini? Uchumi wa nchi uko kwenye jeopardy, umeme kitu ambacho ni centre ya usalama wa taifa lolote unaendelea kuwa Tatizo nchini kwa miaka karibu 10 sasa, and we are fooled that we have TISS. Kuna tatizo kubwa sana ambalo linahitaji utatuzi wa haraka sana.
 
Nimepitia kila mchango humu ndani. wapo walionifurahisha, wapo walioniboa. Nimeamua niwaunge mkono walinifurahisha na kuwapotezea walioniboa.

Tatizo la watengeneza sera, sheria na wanaozipitisha, wameshindwa kujua maana ya maneno yanayotumika katika mambo waliyoyaunda. Kwa mfano.

Wizara ya mambo ya ndani ya nchi, wana idara inayohusika na USALAMA WA RAIA NA MALI ZAO. Wengi serikalini, au wamepuuzia usalama wa raia, au hawajui usalama wa raia ni nini. Hali hii imepelekea pia kuwa na askari wa aina hiyohiyo ambao mwisho wa siku hajui majukumu yao katika kazi wazifanyazo. Wengi wa viongozi na watendaji wanafahamu usalama wa raia na mali zao, ni kupambana na ujambazi, wizi na the like. Nje ya hilo, hawajui lolote. Wamechukua suala moja tu, na kuyatelekeza mengine mengi tena ya msingi. Mwisho wa siku, wanajikita na wanaamini wapo ili uhalifu utendeke ili wao waonekane wapo kazini. Na wengi wanaamini kwa mfano, ujambazi, wizi wa mtu-kwa mtu ukimalizika, basi na kibarua chao kitaota nyasi. Ndiyo maana matatizo ya namna hiyo hayaishi, kwani watendaji wamejitambua kuwa ajira yao, inategemea uwepo wa makosa hayo. Hakuna nia ya dhati mioyoni mwao ya kuyazuia.

Vivyo hivyo, usalama wa Taifa, wameacha mambo ya msingi yanayoweza kutuletea usalamawa mda mrefu, wakajikita katika kuhakikisha mtu mwenye ndoto ya kuwaletea maisha mazuri wataifa hafanikiwi. Kwao huyu anahesabika kama hatari kwani anaingilia mamlaka ya watawala waliopo madarakani. Watafanya kila kitu kuhakikisha kuwa, mtu anayekuja na njia mbadala za kuboresha hali za watu hafanikiwi ili wale waliopo madarakani waendelee kula pasipo kuhojiwa. wamekuwa USALAMA WA WANASIASA WEZI na sio Usalama wa Taifa. Ndiyo chimbuko la ufisadi/fraudi kufanyika wao wakiwa kimya tu.

Maoni yangu. Maneno haya usalama wa raia na mali zao na usalama wa taifa, yafanye kazi kwa kuhakikisha kuwa
1. kunakuwa na ustawi wa watu na taifa.
2. kuwe na uhakika wa kila mwananchi kupata mahtaji yote ya msingi yaani chakula, elimu, mavazi, usalama na yafananoyo.
3. Wahakikishe kila mtu kwenye jamii ana fursa sawa ya kufaidika kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni
4. wafanye kazi kwa mjibu wa katiba ya zamani(inayosema......."mamlaka yoyote, yanatokana na wananchi....." ) na hivyo ikiwa wananchi hawaridhiki na utendeja wa vyombo vyote vilivyopo ndani ya jamii yao, wakiamua kuwaondoa, basi usalama wa raia na mali zao-POLISI na usalama wa Taifa, wawasimamie wananchi kufanikishe kile wakitakacho. Hata hivyo, KATIBA MPYA, itoe mwongozo kwa vyombo hivyo kulinda wananchi wanapodai haki zao na sio kuwazuia.

Pia, viongozi wa idara hizo, pamoja na hao wa jeshi la wananchi, KAMWE WASITOKANE na wanasiasa, bali wachaguliwe na maofisa wenzao ndani ya chombo husika, au zitangazwe nafasi za kazi na watu ndani ya idara hizo wanaomba, wanaitwa kwenye usahili wapewe uongozi huo ndani ya idara kwa mchujo maalumu ili wawe na nguvu ya kuwasimamia viongozi wa kisiasa, na wakuu wengine wa idara za serikali.

Kwangu mie, ufisadi uliofanyika ndani ya nchi yetu, na wahusika kuachwa bila kuchukuliwa hatua kali, ndiyo chanzo cha maisha magumu ya wananjamii, na kwa sababu hiyo, wizi, ujambazi, unyang'anyi, maandamano na harakati zote za kudai ukombozi hazitakoma mpaka pale tu tutakapofanikiwa kuhakikisha usalama wa jamii katika CHAKULA, ELIMU, AFYA, MALAZI na mambo mengine ya msingi binadamu anaypyahitaji mtu.

Sheria ziundwe ili wasiishie tu kutoa ushauri, bali kama mtu amefanya madudu, ashtakiwe mara moja bila kupoteza na hukumu yake iwe ya haraka na kubwa. hii itarejesha nidhamu ya watumishi wengine wa umma.
 
Mkuu, ninakugongea THANKS kwa angalizo lako.
Ukichukulia Idara ya Usalama wa Raia na Mali zao, na Idara ya Usalama wa Taifa, ni kweli kuwa (baadhi ya) Watendaji wametoka katika maadili ya kazi zao na kujishughulisha na mbwembwe, sifa na hata uhalifu. Tumeona wanajeshi wakivamia wananchi eti kwa sababu mwenzaokwa sababu alinyimwa bia ya bure katika baa, akaanza kurusha makonde na wananchi wakarjitetea. Nimewahi kumwona Usalama wa Taifa mmoja ambaye kwa kuwa alikuwa hataki kutoa nauli kwenye daladala, ulitoa pingu na kumwonyesha kondakta. Raia mwema anaogopa kwenda kushitaki polisi au kutoa ripoti kwani wanaweza kumgeuza shamba la bibi. Hii ni aibu na kuidhalilisha Idara ya Usalama wa Taifa. Usalama wa Taifa wamekuwa usalama wa kulinda maslahi yao na baadhi ya viongozi. Hata ukupitia sheria ya kuanzishwa kwa Idara ya TISS, utagundua kuwa uteuzi wa Mkuu wa Idara unafanywa kisiasa kuliko kiutendaji. Ikiwa Rais ndie anayeteua Mkuu wa Idara, siku akija rais mwengine anateua mtu wake, kwa mujibu wa utashi wake.
Ukweli utabaki pale pale kuwa nchi inahitaji walinzi, inahitaji wapiganaji, inahitaji habari za kuisaidia nchi kujilinda, lakini kwa kukosa maadili katika shughuli zao (hapa nasisitiza neno "baadhi yao"), wamekuwa kero, aibu na hatari kwa taifa.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mkuu, ninakugongea THANKS kwa angalizo lako.
Ukichukulia Idara ya Usalama wa Raia na Mali zao, na Idara ya Usalama wa Taifa, ni kweli kuwa (baadhi ya) Watendaji wametoka katika maadili ya kazi zao na kujishughulisha na mbwembwe, sifa na hata uhalifu. Tumeona wanajeshi wakivamia wananchi eti kwa sababu mwenzaokwa sababu alinyimwa bia ya bure katika baa, akaanza kurusha makonde na wananchi wakarjitetea. Nimewahi kumwona Usalama wa Taifa mmoja ambaye kwa kuwa alikuwa hataki kutoa nauli kwenye daladala, ulitoa pingu na kumwonyesha kondakta. Raia mwema anaogopa kwenda kushitaki polisi au kutoa ripoti kwani wanaweza kumgeuza shamba la bibi. Hii ni aibu na kuidhalilisha Idara ya Usalama wa Taifa. Usalama wa Taifa wamekuwa usalama wa kulinda maslahi yao na baadhi ya viongozi. Hata ukupitia sheria ya kuanzishwa kwa Idara ya TISS, utagundua kuwa uteuzi wa Mkuu wa Idara unafanywa kisiasa kuliko kiutendaji. Ikiwa Rais ndie anayeteua Mkuu wa Idara, siku akija rais mwengine anateua mtu wake, kwa mujibu wa utashi wake.
Ukweli utabaki pale pale kuwa nchi inahitaji walinzi, inahitaji wapiganaji, inahitaji habari za kuisaidia nchi kujilinda, lakini kwa kukosa maadili katika shughuli zao (hapa nasisitiza neno "baadhi yao"), wamekuwa kero, aibu na hatari kwa taifa.

Si huko tu idara zote hazifai sasa hivi kama huna mjomba,shangazi huna kazi na graduate wengi wanakimbilia jeshini na hao wanachukia serikali yao sababu wameingia huko kwa kulazimishwa na hali ya sasa,unategemea badae kitatokea nini? Muulizeni gadafi na wengine kama yeye! Na ndiko tunakoelekea
 
Tuwe wakweli sio tunadanganyana mchana jamani Kuwa kuna Afisa usalama alimtolea mtu pingu kwenye daladala jamani Hawa watu hawana pingu na sio kazi Yao kutia watu pingu tuache kuchangia kwa hisia na kusema alimradi tumepata nafasi..
 
asanteni kwa taarifa muhimu kama hizi ni kweli na mm naboreka sana na hii hali ya watu kujitapa mitaani me uwt na kutuchukulia warembo wetu kisa utanifanya nn nitakupa skendo
kwani wao wako juu ya sheria? Ni wakati sasa wananchi kutambua haki zao, hawawezi kukunyanyasa tu eti ni usalama wa taifa kwa mambo binafsi. Sasa usalama wa taifa na kuingilia social life wapi nawapi bwana!
 
Back
Top Bottom