Kuhubiri dini kwenye mabasi na standi za umma nao ni uhuru wa kuabudu?

Ukahaba ulikuwepo toka Enzi za Ibrahimu na Yakobo. Hata Yesu alipokuwa kwa Jinsi ya mwili ukahaba na makahaba walikuwepo so auhusiani na Wahubiri. Tafuta sababu nyingine mkuu.
Uhuru wa kuwatoa watu kwenye imani zao halafu unawapeleka motoni,shauri yenu.Hata chanzo cha dhambi ni tamaa na uongo tangu mwanzo nyoka alienda kwa "Eva na kumwuliza Eti Mungu aliwakataza"
 
amani ya nchi hii inatokana na wananchi kuwa mazuzu wala hakuna kingine
 
Makanisa yapo acheni upumbavu na utapeli.
 
Upuuzi..... Neno litahubiriwa popote,kuamini ni maamuzi yako. Katika kundi la watu 100 akiamkni hata mmoja tu ni ushindi mbinguni. Ukiona unakereka kusikia neno la Mungu basi ujue shetani kakukamata.
 
Tindo,"aka "Kinoa Miguu
 
Sasa wimbo kama wameloa sijui kamatia chini, mara weka nikukaze au linanipwelepweta mara una roba hizo zinafundisha nini? Inaonekana mzee una Mapepo dhahiri kabisa. Sema upo wapi tukuwekee mkono yatole hayo.
Mbona album za nyimbo za dini zipo nyingi tu akina Rose Mhando,akina Bukuku,AICT,Moravian,RC,KKKT,Anglikan kwa nini msiwaambie maderva wawekee badala ya kusumbua watu.
 
Kelele tu
Sijui kwanini wanaruhusiwa.
Wafate taratibu wafungue makanisa waeneze injili zao kwa amani sio mabarabarani.

Na maduka kufunga maspika kelele
NEMC sijui wapo wapi.
Ila wasanii kuimba Barabarani ni sawa. Bara kuwa Barabarani hazina kelele. Kuwepo na machangudoa yanayojiuza Barabarani ni swafiiiii? Vipazasauti vya nisikitini navyo swafiiii ila mtu akihubiri ndio vita. Aiseeeeeeee
 
upo sahihi kabisa mkuu, yaani inakera sana unanihubiria habari za mungu wakati nawaza kuchelewa sehemu muhimu? waende makanisani huko wanaotaka wataenda huko siyo kutupigia kelele ili mpate chochote asante kwa konda na dereva wa gari ya posta makumbusho iliyoandikwa {mahubiri na biashara haviruhusiwi humu}
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…