Kuhubiri dini kwenye mabasi na standi za umma nao ni uhuru wa kuabudu?

Kuhubiri dini kwenye mabasi na standi za umma nao ni uhuru wa kuabudu?

Una hoja, Ila binafsi sioni Tatizo la kuhubiri habari za Mungu mitaani.

Mimi ni muislam, Ila kamwe sijawahi kuchukizwa na mahubiri ya wanaomtangaza Mungu.

Hakuna dini inayohamasisha matendo mabaya. Dini zote zinatuhimiza kutenda wema na kuacha mabaya.

Kwa jamii yetu ilipofikia, watu wengi ni wakatili ni vyema neno la Mungu likasambazwa bila kujali kukereka Kwa watu wachache.
Neno la Mungu ni tiba, Kwa mioyo yenye visasi, mioyo yenye husda, mioyo yenye kukata tamaa, mioyo yenye choyo,roho mbaya na mauaji.
Mtu yeyote mwenye hofu ya Mungu ni mtu mwema kuishi nae.
Waende kwenye mabaa ili tuwaone kuwa ni watu wa kweli siyo kwenye mabasi na masokoni.
 
Wacha tuhubiri watu wamjue Mungu. Usidanganyike bro, amani ya nchi hii haitokani na kuwa na jeshi zuri juridical mataifa mengine yenye vita ila ni kutokana na hofu ya Mungu ambayo watu wanayo. Na hofu hii huja pale tunapowahubiria na kuwaombea Watanzania. Tuache tuhubiri kama ambavyo kuna Bongo flavor na Sinema kwenye mabasi.
Kwa hiyo nchi zenye vita kama DRC, Somali, Israel, Ukraine, Gaza n,k hawafanyi maombi??
 
Kuna siku nillitaka kumuambia mmoja aache kelele na usumbufu nikishangaa dakika chache baadaye robo ya bus wakaanza kumpa sadaka!
Wanaendekezwa na wenye mahaba zaidi na dini zao.
Unaona eh!Je hapo pana utakatifu kweli?
 
sidhani .maana unakuta umesafiri na mwanao wa kike na wakiume gafla unashangaa Diamondi anasema eti legeza kidogo .........sasa wengine tumeokoka hatuitaji kusikia legeza kidogo
Katika nchi zilizostaaribika zaidi huwa hawaweki muziki, movies, maubiri au mawaidha katika usafiri wa umma.
 
Kwa hiyo nchi zenye vita kama DRC, Somali, Israel, Ukraine, Gaza n,k hawafanyi maombi??
Wapi nimesema hawafanyi maombi mkuu? Nilichosema ni kuwa na hofu ya Mungu kwenye mioyo yao. Hiyo ndiyo chanzo cha amani na hofu hii huja kwa kuhubiriwa/kufundishwa kuhusu Mungu na Maombi juu ya hofu ya Mungu itawale kwenye mioyo ya wanadamu.
 
Upuuzi..... Neno litahubiriwa popote,kuamini ni maamuzi yako. Katika kundi la watu 100 akiamkni hata mmoja tu ni ushindi mbinguni. Ukiona unakereka kusikia neno la Mungu basi ujue shetani kakukamata.
Mbona kwenye mabaa na guest hamwendi?
 
Waende kwenye mabaa ili tuwaone kuwa ni watu wa kweli siyo kwenye mabasi na masokoni.
Mbona wengi tu huku vijijini huwa tunaenda kuhubiri kwenye mikusanyiko including kwenye vilabu. Hii ni kwanini? Kwa sababu Neno la Mungu lina nguvu kuliko mazingira. Sijui kwanini unapinga kwa so called ustaarabu ila Neno la Mungu linahubiriwa kila sehemu. Hata huko nchi zilizostaarabika usemazo, wapo watu wanahubiri mitaani. Bro, kuna watu wanashida na kutamani kupata amani kwa kusikia Neno la Mungu tu. Ebu tusipige vita vitu hivi vizuri bro. Wanadamu wana dhiki na shida mioyoni mwao. Hawana wa kuwaeleza zaidi ya Mungu wa kweli ila hawajui namna ya kumfikia. Jambo hili ni jema na linatakiwa lienziwe na sio kuzuiwa na kupigwa vita.
 
Au Bar, kwenye mahotelini.
Kuna comment hapo juu niliona umeandika kwenye nchi zilizostaarabika hakuna hilo jambo. Nafikiri umeifuta.

Suala la kuhubiri mitaani lipo Dunia nzima mkuu na sio Tanzania japo kuhubiri kwenye vyombo vya usafiri Mahali pengine halifanyiki. Injili ni lazima ihubiriwe kila mahali hapa Duniani mkuu.
 
Mbona wengi tu huku vijijini huwa tunaenda kuhubiri kwenye mikusanyiko including kwenye vilabu. Hii ni kwanini? Kwa sababu Neno la Mungu lina nguvu kuliko mazingira. Sijui kwanini unapinga kwa so called ustaarabu ila Neno la Mungu linahubiriwa kila sehemu. Hata huko nchi zilizostaarabika usemazo, wapo watu wanahubiri mitaani. Bro, kuna watu wanashida na kutamani kupata amani kwa kusikia Neno la Mungu tu. Ebu tusipige vita vitu hivi vizuri bro. Wanadamu wana dhiki na shida mioyoni mwao. Hawana wa kuwaeleza zaidi ya Mungu wa kweli ila hawajui namna ya kumfikia. Jambo hili ni jema na linatakiwa lienziwe na sio kuzuiwa na kupigwa vita.
Mnapenda mijini tena miji mikubwa,vijijini hamwendi na huo ndiyo ukweli.
 
Mnapenda mijini tena miji mikubwa,vijijini hamwendi na huo ndiyo ukweli.
Inaonekana u maskini sana wa fikra bro samahani kwa hilo. Toka mwanzo sijajua nini hasa logic yako. Ulianzia kelele, ukaja utapeli, ukaitaja CCM, ukahukumu wanajifanya watakatifu, ukautaja ukahaba n.k.
 
Hawa wahubiri holela mabasini wanakera sana,kila mtu katoka nyumbani kwake ana imani yake,basi sio kanisa ndo maana hakuna madhabahu,duuh mpaka mnatuhubiria visogoni kweli,tunashindwa kusikia vituo vya kushukia kutokana na mipayuko yenu,mnapunguza pocket money zetu japo hamtulazimishi kutoa sadaka zetu lakini mnatia huruma mno midomo imewakauka kama mwala chakula juzi yatulazimu kutoa,basi iwe bora tu katika mabasi jiiteni watu yatima ombeni msaidiwe,kibaya zaidi mwingine unakutana nae usiku katika maeneo ya starehe je,hayo ndio matumizi sahihi ya mlichopewa
 
Back
Top Bottom