Kuhusu Kusafiri Usiku; Waziri Mkuu awaagiza ama RC, DC

Kuhusu Kusafiri Usiku; Waziri Mkuu awaagiza ama RC, DC

Super Handsome

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2013
Posts
3,844
Reaction score
6,448
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameliagiza Jeshi la Polisi kupitia kamati za ulinzi na usalama za mikoa na wilaya ziendelee kufanya tathimini juu ya utoaji wa vibali vya mabasi ya abiria kusafiri usiku.

Majaliwa alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Sophia Mwakagenda katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo bungeni.

Mbunge huyo alitaka kufahamu nini Serikali inafanya ili kuruhusu mabasi ya abiria yasafiri usiku na mchana, hatua ambayo italiingizia mapato Taifa.

Akijibu swali hilo, Majaliwa amesema agizo la mabasi kutosafiri usiku lilitolewa kwasababu mara nyingi mabasi yalikuwa yanatekwa wakati yanaposafiri usiku na Serikali ilikuwa ikilazimika kuweka askari kwa kila basi linaposafiri ili kuhakikisha usalama kwa wasafiri.

“Ni kweli kuwa usalama umeimarika nchini na Serikali inaendelea kuimarisha zaidi usalama. Umuhimu wa hilo jambo upo lakini tutaendelea kuwasiliana na vyombo vya ulinzi na usalama na kama je wamejiridhishaje na usalama huo ili turuhusu mabasi kusafiri wakati wote ili kuboresha uchumi,”amesema.

Majaliwa amesema pia hatua hiyo ya kuruhusu mabasi kusafiri usiku itawezesha wafanyabiashara kuweka mipango yao ya kutoka eneo moja hadi nyingine katika kuendesha biashara zao kwa uhuru mkubwa.

Chanzo: Habari Kuu za Tanzania, Siasa, Afya, Uhalifu na zaidi - TanzaniaWeb
 
safi sana haswa kwa mabasi yanayo toka Dar kuelekea Mkoa wa Kigoma ni shida......yaani safari siku 2, watu wanalala njiani kisa hakuna Askari wa ku escort!!
hili halikubaliki, nashuri kauli hii ya Waziri Mkuu utekelezaji wake uanzie kwa mabasi yaendayo Mkoa wa Kigoma kuna chngamoto kubwa sana.
 
safi sana haswa kwa mabasi yanayo toka Dar kuelekea Mkoa wa Kigoma ni shida......yaani safari siku 2, watu wanalala njiani kisa hakuna Askari wa ku escort!!
hili halikubaliki, nashuri kauli hii ya Waziri Mkuu utekelezaji wake uanzie kwa mabasi yaendayo Mkoa wa Kigoma kuna chngamoto kubwa sana.
Kigoma
Kagera
Mara
Huko Shida Ibaki Mchana, Ulale Kaliua Ama Kahama
Kagera Utapitaje Mbuga Ya Burigi ~Chato
 
safi sana haswa kwa mabasi yanayo toka Dar kuelekea Mkoa wa Kigoma ni shida......yaani safari siku 2, watu wanalala njiani kisa hakuna Askari wa ku escort!!
hili halikubaliki, nashuri kauli hii ya Waziri Mkuu utekelezaji wake uanzie kwa mabasi yaendayo Mkoa wa Kigoma kuna chngamoto kubwa sana.
Nyie wa kigoma msahau suala la kusafiri usiku, Yale mapori bado sio salama kabisa hata mchana tu ndio iwe usiku???
 
Kigoma
Kagera
Mara
Huko Shida Ibaki Mchana, Ulale Kaliua Ama Kahama
Kagera Utapitaje Mbuga Ya Burigi ~Chato
Huu ni ukweli usiopingika, hakuna anayependa watu wasafiri siku mbili lakini kiusalama hakuna atakayeruhusu wapige usiku.

Yawezekana kwa sasa panaonekana hali ni shwari Ila kuna mambo yanaendelea na itakapotolewa ruhusa ya mabasi ya abiria kusafiri usiku majangili wataona fursa imerudi.

So hayo maeneo ambako yapo mbele ya Kahama kuelekea BK au KG wawe wapole tu wakubaliane na hali halisi.
 
nauli ya ndege kwenda Bukoba, kigoma na Musoma iwe ya kizalendo ili ikiwezekana abiria wengi wasafiri na mwewe kwenye hayo maeneo hatari..

Serikali inaweza kuagiza maantonov ya kirusi bei rahisi, yaruke kwenda hayo maeneo kwa nauli hata ya 100k ( go and return), one way 50k
 
Mimi naona bado swala la Usalama bado hasa hasa kwa Kigoma na Kagera! Utaratibu ulipo uendelee mpaka hapo vyombo vya ulinzi na usalama vitakapojilidhisha!
 
nauli ya ndege kwenda Bukoba, kigoma na Musoma iwe ya kizalendo ili ikiwezekana abiria wengi wasafiri na mwewe kwenye hayo maeneo hatari..

Serikali inaweza kuagiza maantonov ya kirusi bei rahisi, yaruke kwenda hayo maeneo kwa nauli hata ya 100k ( go and return), one way 50k
Akili yako hiyo mmh yaani nauli ya Basi itoshe kuhudumia ndege?
Bus dar-kigoma unapendekeza nauli sh ngapi?
 
Mimi naona bado swala la Usalama bado hasa hasa kwa Kigoma na Kagera! Utaratibu ulipo uendelee mpaka hapo vyombo vya ulinzi na usalama vitakapojilidhisha!
Swala la usalama siyo shida
Mfano bukoba

Gari inaanza safari ubungo saa 4 usiku hivyo kunakucha bado iko mazingira salama. Inakuja kufika mazingira hatarishi mchana saa 6 hivyo inakuwa haina tatizo

Kurudi

Gari inaanza safari asubuhi kuja kufika usiku iko mazingira ya dodoma hivyo inatembea bila shida
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameliagiza Jeshi la Polisi kupitia kamati za ulinzi na usalama za mikoa na wilaya ziendelee kufanya tathimini juu ya utoaji wa vibali vya mabasi ya abiria kusafiri usiku.

Majaliwa alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Sophia Mwakagenda katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo bungeni.

Mbunge huyo alitaka kufahamu nini Serikali inafanya ili kuruhusu mabasi ya abiria yasafiri usiku na mchana, hatua ambayo italiingizia mapato Taifa.

Akijibu swali hilo, Majaliwa amesema agizo la mabasi kutosafiri usiku lilitolewa kwasababu mara nyingi mabasi yalikuwa yanatekwa wakati yanaposafiri usiku na Serikali ilikuwa ikilazimika kuweka askari kwa kila basi linaposafiri ili kuhakikisha usalama kwa wasafiri.

“Ni kweli kuwa usalama umeimarika nchini na Serikali inaendelea kuimarisha zaidi usalama. Umuhimu wa hilo jambo upo lakini tutaendelea kuwasiliana na vyombo vya ulinzi na usalama na kama je wamejiridhishaje na usalama huo ili turuhusu mabasi kusafiri wakati wote ili kuboresha uchumi,”amesema.

Majaliwa amesema pia hatua hiyo ya kuruhusu mabasi kusafiri usiku itawezesha wafanyabiashara kuweka mipango yao ya kutoka eneo moja hadi nyingine katika kuendesha biashara zao kwa uhuru mkubwa.

Chanzo: Habari Kuu za Tanzania, Siasa, Afya, Uhalifu na zaidi - TanzaniaWeb
Pale pori la kasindaga vp??
 
Back
Top Bottom