Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Umeishi Zanziba? Kuna baadhi wana chuki sana kwa wale wanaowaita machogo. Na wengine dhidi ya wapemba. Kisiwa kimejaa sana chuki kile.

Amandla...
 
kweli lumumba imekuharibu,huyu ni mwanasheria na anajua nn anachoongea kama ZNZ ni nchi kwann iliondolewa OIC ?????
 
Kesho kutwa tutapofika December kutakuwa na sherehe ya UHURU.
uhuru upi ? Watanzania au watanganyika?

Maana Tanzaina haikupata uhuru imezaliwa tarehe 26 April 1964.
Lakini hiyo sherehe ni ya Uhuru wa Tanganyika.
Pia isitoshe angalia katiba ya mwanzo ya Tanzania ilivyo undwa. Ilichukuliwa katiba ya Tanganyika na kubadilishwa. Kila pahala panasomeka Tanganyika ikawekwa neno Tanzania.

kwa maana hiyo ni kama Tanganyika imebadili jina kutoka Tanganyika kuja Tanzania. Sawa Na Rhodesia kuitwa Zimbabwe.

Kwa hivyo Zanzibar hapo haipo.

Na sasa hakuna jambo Zanzizibar wanaloweza kufanya bila kupitia Katika Serikali Ya muungano Tanzania which is Tanganyika.

Samahani sana huwezi kumuita kiongozi muongo.
Kuna lugha unatumia ya watu wenye hekima na busara
 
Jidanganye mwenyw
 
Huu ni muungano wa kisanii fullstop
 
Ukwel lazma usemwe japo mchungu,zama za ulaghai na usanii zmekwisha
 
Kwa maono yangu Zanzibar walibaki na Serikali yao! Serikali ya Tanganyika iko wapi? Paschal pamoja na usomi ulio nao hulioni hilo?

Tusiwekeane mabanzi kwenye macho jamani! Kwenye Muungano bado kuna mambo hayako sawa! Wazanzibar ruhusa kugombea uongozi huku Bara! Wabara hawaruhusiwi! Paschal hilo hulioni hilo? Wala halihitaji elimu ya PHD. Mfano mzuri ni Rais wa sasa wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar! Amewahi kuwa Mbunge huku Bara, akatoka akaenda Zanzibar, miaka mitano akarudi Bara, akalamba uwaziri JMT na sasa Rais wa Zanzibar! Je kuna uwiano hapo?
 
Wajitenge waone!
Zitarushwa fighter jets 38 usawa wa mapaa ya mji mkongwe kama China kwa Taiwan, alafu tuone ataenda kumlilia nani @#$&+*#@!
 
Unauliza chuki ya wabara kwa wazenji mbna ipo wazi tu,au Lukuvi alipotamka maneno yake kuhusu ZNZ ulikuwa mtoto?????
 
Muungano wetu una walakini kuanzia day one..hakuna terms zinazoeleweka, ndo mana upo fragile chama kimoja tu ndo kinaupgania. Siku chama kingine upande wowote kikachukua full authority ndo itakua mwisho wa huu muungano. Binafs sijawahi kuupenda, sijaona sababu ya kuungana nao kabsa..
 

Ugomvi wa familia ya Al Said siyo ugomvi wa watu wote wa Zanzibar na Oman. Wazanzibari na Waomani wana undugu mzuri tuu. Halafu kama unaona Wazanzibari ni wapenda dezo, kwa nini bado tunaung'ang'ania Muungano? Waache wafanye vyao ili wakupunguzie mzigo.
 
Hlo jibu lake lipo wazi kwa kila mwnye akili timamu,nchi ambayo hata kiongozi wake hatambulik kmataifa c usanii huo?????
Na vipi kuhusu sie wa bara, mbonà huku bara wa pemba wengi wana miliki ardhi tena na majumba lkn hukonznz mbara hata kibaraza tu hana haki ya kumiliki ?
 
Unadhani wananchi wa Oman ndio wangewapa mafuta? Kama masultan hawaelewani hamna namna Zanzibar ingepewa mgao wa mafuta yao.
Wanaolalamikia Muungano ni wazanzibari kwa hiyo ni wajibu wao kuuvunja kama wanaona hauwafai. Wewe mume anakutesa, anakupiga, anakudhalilisha, anawatesa watoto lakini hautaki kuondoka mpaka akupe talaka. Zanzibar si nchi? Wana Rais, wana bunge lao na serikali yao, wanashindwa nini kuiambia JMT kuwa Muungano hawautaki? Kama kweli hawautaki, wawatume wawakilishi yao wakadai talaka. Kama wanaona CCM watawasiliti wawatume ACT Uzalendo wadai talaka na sio huu upuuzi wa kusema wanataka serikali tatu au serikali ya mkataba. Hivi unadhani mtanganyika gani anafaidika na huu Muungano moja kwa moja? Wangapi wana mashamba au biashara Zanzibar? Wangapi wanapeleka watoto wao wakasome Zanzibar? Wangapi wanapeleka wagonjwa wao Zanzibar? Wangapi ndugu zao wamehamia Zanzibar? Huu Muungano ukivunjika watakaoguswa zaidi ni wazanzibari kuliko mtanganyika wa Newala. Ndio maana hawataki kuuvunja bali wanataka watanganyika wauvunje ili mambo yakiwaharibikia wawatupie lawama machogo.

Amandla...
 
Nakuhakikishia wazanzibar walio bara wapige kura ya maoni wao tu kwa niaba ya wazanzibar wote .basi wataukataa muungano na Mali zao watakao ziacha zitapelekea WATANGANYIKA kuwana sanaaaa
 
Mayala unamzidi nn othman masoud kuhusu Sheria wewe jarib kumuheshim hata kidogo inakuonesha waziwazi muungano huujui
 

Kwani Waomani wangapi wamepewa mafuta? Hata Wazanzibari wasingepewa mafuta wangefaidika tuu na utajiri ulioletwa na mafuta kama Waomani wengine wenzao ambao nao hawajapewa hayo mafuta. Halafu kwa jinsi unavyoiponda Zanzibar unaonyesha ni jinsi gani huo Muungano umeshindwa kuwaletea faida Wazanzibari. Hawana shule nzuri, hospitali nzuri, biashara haziendi wamebaki na umasikini. Ndiyo maana wameuchoka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…