Kuhusu walimu kupanda madaraja kwa Mseleleko

Kuhusu walimu kupanda madaraja kwa Mseleleko

F4B

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2022
Posts
336
Reaction score
429
Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza serikali ya mhe Samia Suruhu Hassan kwa kujali na kusikiliza kero mbalimbali za walimu.Lakini pia nikipongeze Chama Cha walimu Tanzania CWT kwa yale mliyoafikiana na serikali.

Hoja yangu ni hii CWT imesema serikali imeridhia kuwapa madaraja ya Mseleleko walimu takribani elfu 50,hawa ni wale waliopaswa kupanda madaraja 2016/2017, ni jambo jema na la kupongezwa.

Lakini serikali na CWT wasisahau kuna walimu waliopaswa kupanda madaraja mwaka 2018 hawakupanda badala yake walikuja kupandishwa mwaka 2021, yaani takribani miaka Saba wametumikia cheo kimoja mfano halisi ni watu waliopanda daraja mwaka 2015 mara ya mwisho wamekuja kupandishwa tena mwaka 2021.

Kwa maoni yangu CWT na Serikali wanapaswa kuwajali watumishi hao pia.
 
Kweli Kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake, wakati Mimi nalia na ajira mwenzangu unalia na kupanda madaraja.
 
Huu ndo ukweli unaouma.Nao hao waliopaswa kupanda 2018 wawape haki yao.Na wengi ni ajira ya 2015.Ambao walipaswa kupanda 2018 but hawakupanda mpaka 2021.Inasikitisha na kukatisha tamaa kwa watumishi hao.
Huu ndo Ukweli ndugu yangu, Kuna hatari mtu aliyeajiliwa nyuma kuwa mbele ya yule aliyetangulia kuajiliwa ikiwa hili jambo halitafanyiwa kazi na itakuwa dhuluma kwa baadhi ya wafanyakazi.
 
Hongera sana mama unaupiga mwingi sana, lakini kuna waalimu walitakiwa wapande 2018 hawakupanda badala yake wakaja kupanda 2021 na wengi wao niwale walioajiriwa 2014 ,kidumu chama cha mapinduzi
 
HAO watakaopanda 2016/2017 ni ajira ya mwaka GANI?halafu kwa sheria ya miaka mingapi mitatu au minne kazini!??maana kuna sheria mbili Hadi Sasa za kupanda madaraja!!ile ya zamani miaka mitatu na ile ya jiwe miaka minne Sasa ipi ni ipi!!
 
Mkianza kusema hivyo basi kuna wa 2014 ambao walikuja kupanda kwa mara ya kwanza 2019 BADALA ya 2017, nao wapate la mserereko ili hali itendeke sawa!
 
Hongera sana mama unaupiga mwingi sana, lakini kuna waalimu walitakiwa wapande 2018 hawakupanda badala yake wakaja kupanda 2021 na wengi wao niwale walioajiriwa 2014 ,kidumu chama cha mapinduzi
Na Mimi ndiyo hoja yangu kuwa Kuna walimu wengi wanapaswa kutendewa haki.
 
Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza serikali ya mhe Samia Suruhu Hassan kwa kujali na kusikiliza kero mbalimbali za walimu.Lakini pia nikipongeze Chama Cha walimu Tanzania CWT kwa yale mliyoafikiana na serikali...

Je Idara nyingine km ,AFYA,KILIMO & MIFUGO waliokua na tatizo kama Hilo wao HAWAGUSWI na huo mchakato wa mseleleko wa kila dishes madaraja?nafikiri waangaliwe wafanyakazi wote walioguswa kwenye hili
 
  • Thanks
Reactions: F4B
Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza serikali ya mhe Samia Suruhu Hassan kwa kujali na kusikiliza kero mbalimbali za walimu.Lakini pia nikipongeze Chama Cha walimu Tanzania CWT kwa yale mliyoafikiana na serikali...
Hii kweli ingeenda kwa watumishi wote hasa ukizingatia huu mfumoko wa bei
 
Je Idara nyingine km ,AFYA,KILIMO & MIFUGO waliokua na tatizo kama Hilo wao HAWAGUSWI na huo mchakato wa mseleleko wa kila dishes madaraja?nafikiri waangaliwe wafanyakazi wote walioguswa kwenye hili
Kwanza watumishi wa umma hapa Tanzania licha ya mishahara yao kuwa midogo mno,serikali ya CCM imejitahidi kuwagawa ili iwatawale kirahisi kimaslahi-Divide ana Rule.Mifano ipo mingi kuthibitisha hilo.
 
Je Idara nyingine km ,AFYA,KILIMO & MIFUGO waliokua na tatizo kama Hilo wao HAWAGUSWI na huo mchakato wa mseleleko wa kila dishes madaraja?nafikiri waangaliwe wafanyakazi wote walioguswa kwenye hili
Watumishi wengine kwa mfano idara ya afya halmshauri fulani wao wameambiwa kuwa watapanda .Maafisa utumishi wamejenga hoja kwa katibu mkuu utumishi watu hao walidhurumiwa hivyo wamepewa kibari
 
Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza serikali ya mhe Samia Suruhu Hassan kwa kujali na kusikiliza kero mbalimbali za walimu.Lakini pia nikipongeze Chama Cha walimu Tanzania CWT kwa yale mliyoafikiana na serikali.
Hoja yangu ni hii CWT imesema serikali imeridhia kuwapa madaraja ya Mseleleko walimu takribani elfu 50,hawa ni wale waliopaswa kupanda madaraja 2016/2017, ni jambo jema na la kupongezwa.Lakini serikali na CWT wasisahau kuna walimu waliopaswa kupanda madaraja mwaka 2018 hawakupanda badala yake walikuja kupandishwa mwaka 2021,yaani takribani miaka Saba wametumikia cheo kimoja mfano halisi ni watu waliopanda daraja mwaka 2015 mara ya mwisho wamekuja kupandishwa tena mwaka 2021.Kwa maoni yangu CWT na Serikali wanapaswa kuwajali watumishi hao pia.
Siyo walimu tu, ni watumishi wote wanatakiwa kutazamwa kwenye suala hili
 
Je Idara nyingine km ,AFYA,KILIMO & MIFUGO waliokua na tatizo kama Hilo wao HAWAGUSWI na huo mchakato wa mseleleko wa kila dishes madaraja?nafikiri waangaliwe wafanyakazi wote walioguswa kwenye hili
Hao Afya,mifugo hawana platform yenye nguvu ya kuwasemea
 
  • Thanks
Reactions: F4B
Back
Top Bottom