Kuishi kwingi kuona mengi: Soma kisa nilichokiona Kawe

Kuishi kwingi kuona mengi: Soma kisa nilichokiona Kawe

Nakumbuka miaka kama kumi na kidogo hivi mjini Arusha, alikuja nabii mmoja mwanamke ambaye alikuja kufungua kanisa jipya na kumuweka wakfu mchungaji mpya wa kanisa hilo.

Nilichoshangaa ni pale mchungaji mpya alipodondoka alipokuwa anawekwa
a wakfu kwa kuombewa na nabii huyo mwanamke.
Nilishangaa sana, sasa kama yule ambaye anakuwa mchungaji anaanguka ikimaanisha ana mapepo sisi wengine itakuwaje??

Imani yetu tuiweke kwa Mungu Baba, Mwana na Roho mtakatifu, na sio kwa watu.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 

Nilichokiona kwa Mwamposa watu wengi wapo na misongo ya mawazo tu, madeni, na wale ambao Koo zao zina mambo ya kishirikina.
Wengine matatizo ya kisaikolojia tu yanawasumbua.
Asante kwa utafiti shirikishi! Nadhani upo sahihi, ulipata relief yoyote?
 
Nishawai kwenda kanisani tukapangwa foleni ya kupakwa mafuta[emoji3][emoji3][emoji3]...ikawa mchungAji anakupaka mafuta kuchwani alafu akaongea maneno yake...Mimi nikawanashangaa Watu wanaanguka TU...mmoja baada ya mwingine.

Kuna Watu nyuma yetu na wamama wamebeba khanga...

Kila mtu akawa anaanguka ..ilivyofika zamu Yangu nami nikaapiga kelele...alafu nikaajiangusha chini[emoji3][emoji3][emoji3]....

Wengine wanajinyonganyonga Kama nyoka nguo zinawavuka wamama wanakuja kuwafunika...

Kwakweli Sijawai kujua Sababu ya Watu kuanguka...Mimi nilifuata mkumbo.
 
Nishawai kwenda kanisani tukapangwa foleni ya kupakwa mafuta[emoji3][emoji3][emoji3]...ikawa mchungAji anakupaka mafuta kuchwani alafu akaongea maneno yake...Mimi nikawanashangaa Watu wanaanguka TU...mmoja baada ya mwingine.

Kuna Watu nyuma yetu na wamama wamebeba khanga...

Kila mtu akawa anaanguka ..ilivyofika zamu Yangu nami nikaapiga kelele...alafu nikaajiangusha chini[emoji3][emoji3][emoji3]....

Wengine wanajinyonganyonga Kama nyoka nguo zinawavuka wamama wanakuja kuwafunika...

Kwakweli Sijawai kujua Sababu ya Watu kuanguka...Mimi nilifuata mkumbo.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Mgf
Umenichekesha sana umeunga tella
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Mgf
Umenichekesha sana umeunga tella
Mgf nlifuata mkumbo tu...nikatoka nimechafuka nguo zote zimejaa vumbi na mafuta ya mzaituni[emoji23][emoji23]..

Alinipeleka mtoto wa mamdogo nlikua namatatizo mengi..Basi akaniambia twende huko Calvary Assembles of God.

Niliyoyashuhudia huko..nlirudi kwenye Imani Yangu Nasijawai Rudi tena.
 
Katika watu 10 ‘wanaoangukaga’ makanisani, 80% ni wanawawake.
Nikweli..wanaume wamesimama nyuma ya wanawake eti wanawadaka na kuwabeba wakianguka..

Kuna Muda wa maombi Huyu Ndugu Yangu alikua TU anaapiga kelele anaanguka ...wanakuja vijana wanambeba wanampleka mbele ya kanisa..

Sijajua kwa undani sababu ya kuanguka..Rashid Gwajima anaweza kuwa na jibu.
 
umenikumbusha mchizi wangu mmoja aliwahi nambia alienda kuombewa wote wana dondoka yeye kakaza tu. yule bwana anamsukuma kwa nguvu yeye kakausha tu

alipozidi sukumwa akaona yaishe tu akaanguka na yeye.

wanamaombi watakuja na ufafanuzi.
Hhhhhhhhh
 
Picha linaanza napokea simu kwa ndugu zangu upande wa mama watoto wangu wanasema, samahani tunakuja kwenye maombezi kwa Mwamposa wewe kama mwenyeji tunaomba utupokee ili utupeleke kwa Mwamposa tukaombewe.

Nikasema ok poa nitawapeleka nyie njooni. Ijumaa wakaingia ndani ya jiji la Dsm nikawapokea, Jumamosi chapu nikawapeleka Kawe kuombewa, mimi nikaamusha kwenye mishe zangu za hapa jijini.

Kesho yake jumapili waakambiwa warudi tena kweli jumapili tena nikawarudisha kwenye ibada kama kawida nikasema ibada ikiisha mtanishitua nije kuwachukua.

Mida ya saa nane ibada ikaiisha wakanishitua nikawachukuwe nilipofika kwa Mwamposa mmoja wao akasema kuwa kuna mfanyakazi mwenzake walishawahi kufanya naye kazi miaka ya nyuma kwenye kampuni kampigia simu waonane maeneo ya PICOLO HOTEL kuna maombezi pia.

Basi bwana tukaenda pale Picolo hotel kufika pale wakatupandisha juu kuna ukumbi kule wanasali.

Nilichokikuta kule kinashangaza sana kwa kuwa ilibidi niwasubiri basi nikasema hebu ngoja nikae nisikilizie hapahapo ukumbini.

Kanisa lina waumini 13 tu, wanawake 10 na wanaume 3. Maombi yakaanza nguvu ya upako sijui nini inawashukia wakawa wanadondoka waumini wote hadi ndugu zangu nao wanadondoka.

Nikajisemea moyoni mbona haya majanga. Ikawa kama mchezo sasa wanaombewa watano waliobaki wanasimama nyuma yao kuwashikilia ili wasijibamize sakafuni. Wakizinduka wengine tena wanaombewa halafu waliodondoka wanaamka tena kuwashikilia wenzao.

Nikachoka kuangalia movie ya kitoto nikawambia oya nyie si mnadondoka humu hebu niwaache mkipona mtanishitua nije niwachukue twende nyumbani. Nimeshangaa hivi kipi kinamfanya mtu anadondoka hovyo wakati wa maombezi au ni michezo ya kuigiza?​

[emoji1787][emoji1787][emoji1787]hiyo zamu ya kupokeana wakidondoka wana ushirikiano sana[emoji23]
 
Picha linaanza napokea simu kwa ndugu zangu upande wa mama watoto wangu wanasema, samahani tunakuja kwenye maombezi kwa Mwamposa wewe kama mwenyeji tunaomba utupokee ili utupeleke kwa Mwamposa tukaombewe.

Nikasema ok poa nitawapeleka nyie njooni. Ijumaa wakaingia ndani ya jiji la Dsm nikawapokea, Jumamosi chapu nikawapeleka Kawe kuombewa, mimi nikaamusha kwenye mishe zangu za hapa jijini.

Kesho yake jumapili waakambiwa warudi tena kweli jumapili tena nikawarudisha kwenye ibada kama kawida nikasema ibada ikiisha mtanishitua nije kuwachukua.

Mida ya saa nane ibada ikaiisha wakanishitua nikawachukuwe nilipofika kwa Mwamposa mmoja wao akasema kuwa kuna mfanyakazi mwenzake walishawahi kufanya naye kazi miaka ya nyuma kwenye kampuni kampigia simu waonane maeneo ya PICOLO HOTEL kuna maombezi pia.

Basi bwana tukaenda pale Picolo hotel kufika pale wakatupandisha juu kuna ukumbi kule wanasali.

Nilichokikuta kule kinashangaza sana kwa kuwa ilibidi niwasubiri basi nikasema hebu ngoja nikae nisikilizie hapahapo ukumbini.

Kanisa lina waumini 13 tu, wanawake 10 na wanaume 3. Maombi yakaanza nguvu ya upako sijui nini inawashukia wakawa wanadondoka waumini wote hadi ndugu zangu nao wanadondoka.

Nikajisemea moyoni mbona haya majanga. Ikawa kama mchezo sasa wanaombewa watano waliobaki wanasimama nyuma yao kuwashikilia ili wasijibamize sakafuni. Wakizinduka wengine tena wanaombewa halafu waliodondoka wanaamka tena kuwashikilia wenzao.

Nikachoka kuangalia movie ya kitoto nikawambia oya nyie si mnadondoka humu hebu niwaache mkipona mtanishitua nije niwachukue twende nyumbani. Nimeshangaa hivi kipi kinamfanya mtu anadondoka hovyo wakati wa maombezi au ni michezo ya kuigiza?​

Umenikumbusha kitu. Ilikuwa mwaka 2014, akaja mtumishi wa Mungu mgeni Kanisani kwetu kwa ajili ya huduma ya Ibada ya jioni. Aliposimama madhabahuni, sikusikia anatoa hata sala, na wala hakusoma hata fungu moja kutoka kwenye maandiko matakatifu kipindi chote alichokuwa amesimama madhabahuni, mwanzo mwisho wa Ibada. Zaidi ni kuwa mtumishi huyu alisimulia kisa cha harakati za utumishi wake halafu kikaniacha midomo wazi.

Mtumishi alisema kuwa kuna kipindi alikuwa anaenda kutoa huduma ya neno la Mungu kwenye haya makabila ya wawindaji yanayoishi porini, ila bahati mbaya watu hao walikuwa hawaitaki na hawaipendi kabisa huduma hiyo.

Kwa hiyo huyu mtumishi alikuwa akifika huko, wawindaji hao wanaamua kuanza kumpiga hadi inafikia hatua wale wanaompiga, wanazimia kwa kukosa nguvu, wanachoka kutokana na namna walivyokuwa wananmpiga mtumishi huyo.

Hata hivyo hali hiyo bado haikumsababisha mtumishi huyo, kuacha kwenda kufanya huduma hiyo kwa watu hao kwa sababu yeye ni mwinjilisti. Sasa mimi nikajiuliza kwamba wale wanaokupiga wanazimia, halafu wewe bvado upo mzima, na kesho tena unakwenda huko, ukiwa unajua kabisa kuwa unaenda kupigwa, wakati wahitaji wa huduma kama hiyo na ambao hawawezi kukupiga wamejaa kila mahali? Hiki kitu kiliwahi kunishangaz sana.

Halafu ukimwangalia yule ambaye alikuwa antaoa kisa hiki, unaona kabisa kwa nje kuwa huyu mtu hawezi kudanganya, wakati alichokuwa anakisema kinapingana kabisa na uhalisia.

Anyway, hata Yoshua na Kalebu walikuta majitu ya miraba minne kule Yeriko, lakini miraba hiyo haikuakisi uhalisia wake mbele za nguvu za Mungu.

Pengine mtumishi huyu anaweza kuwa alikuwa anasema ukweli, ila inahitaji watu waliobobea kiroho kwa kiwango cha juu sana kuweza kuumeza ukweli huu, assming kwamba kweli ulikuwa ni ukweli
 
Umenikumbusha kitu. Ilikuwa mwaka 2014, akaja mtumishi wa Mungu mgeni Kanisani kwetu kwa ajili ya huduma ya Ibada ya jioni. Aliposimama madhabahuni, sikusikia anatoa hata sala, na wala hakusoma hata fungu moja kutoka kwenye maandiko matakatifu kipindi chote alichokuwa amesimama madhabahuni, mwanzo mwisho wa Ibada. Zaidi ni kuwa mtumishi huyu alisimulia kisa cha harakati za utumishi wake halafu kikaniacha midomo wazi.
Mtumishi alisema kuwa kuna kipindi alikuwa anaenda kutoa huduma ya neno la Mungu kwenye haya makabila ya wawindaji yanayoishi porini, ila bahati mbaya watu hao walikuwa hawaitaki na hawaipendi kabisa huduma hiyo. Kwa hiyo huyu mtumishi alikuwa akifika huko, wawindaji hao wanaamua kuanza kumpiga hadi inafikia hatua wale wanaompiga, wanazimia kwa kukosa nguvu, wanachoka kutokana na namna walivyokuwa wananmpiga mtumishi huyo. Hata hivyo hali hiyo bado haikumsababisha mtumishi huyo, kuacha kwenda kufanya huduma hiyo kwa watu hao kwa sababu yeye ni mwinjilisti. Sasa mimi nikajiuliza kwamba wale wanaokupiga wanazimia, halafu wewe bvado upo mzima, na kesho tena unakwenda huko, ukiwa unajua kabisa kuwa unaenda kupigwa, wakati wahitaji wa huduma kama hiyo na ambao hawawezi kukupiga wamejaa kila mahali? Hiki kitu kiliwahi kunishangaz sana. Halafu ukimwangalia yule ambaye alikuwa antaoa kisa hiki, unaona kabisa kwa nje kuwa huyu mtu hawezi kudanganya, wakati alichokuwa anakisema kinapingana kabisa na uhalisia.
Anyway, hata Yoshua na Kalebu walikuta majitu ya miraba minne kule Yeriko, lakini miraba hiyo haikuakisi uhalisia wake mbele za nguvu za Mungu. Pengine mtumishi huyu anaweza kuwa alikuwa anasema ukweli, ila inahitaji watu waliobobea kiroho kwa kiwango cha juu sana kuweza kuumeza ukweli huu, assming kwamba kweli ulikuwa ni ukweli

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23]aisee
 
Mwaka 2011 nilimtembelea ndug yangu maeneo ya Block T, Mbeya. Yeye na familia yake wanasali AGAPE, ni walokole kwelikweli na mkuu wa kaya ni mzee wa kanisa.
Viongozi wengi wakubwa AGAPE hupenda kutembelea kaya ile kwa maombi, mafundisho, maongezi na chakula. Hadi Mr. Fenandez na mkewe, Annie nao huwatembelea kila wafikapo Mbeya.
Wakati nimefika nilikuta wiki ya maombi ya kazi, na msaidizi wa Askofu Fenandez alikuwa Mbeya akiongoza maombi hayo ya wiki. Kulikuwa kile kinaitwa kufunguliwa, ambao hawajampokea Bwana walimpokea, wengi makumi kwa makumi, isipokuwa mimi. Jambo lile halikuwafurahisha wenyeji wangu, walitaka niokoke pia.
Maombi yakawa maombi, kila siku usiku wanatembelea kaya ile na kufanya maombi, kama kawaida waombewaji hudondoka. Wao wakifanya maombi, mim huwa chumbani nikiperuzi FB na Twitter. Ndugu walinishawishi sana, nikaona acha nifanye watakayo kwakuwa nipo kwao, nikiondoka kurudi home, naendelea na kanisa langu.
Kabla ya maombi, ilianza Sara ya toba, nikifuatisha maneno ya yule msaidizi ya Fenandez. Baada ya hapo alinishika kichwani kuniombea. Kwa kweli sikusikia nguvu yoyote ya ajabu, ulikuwa mkono tu, jambo lililofanya niendelee kusimama wima tela mwenye utulivu huku nimefumba macho.
Nahisi alipoona sitetereki, nikaona anaanza kunifinya maeneo ya misuli ya macho, yakaanza maumivu ya kichwa, nikavumilia... Alipoona nimetulia, akaweka mkono wa pili na kuzidi kuomba huku akiniminya zaidi, maumivu yalizidi, nikapata akili kuwa anataka nidondoke, basi taratiiiiiiibu nikaanza kushuka chini. Bro alipoona nanyong'onyea, akaja nyuma yangu na kunidaka, kisha nikalazwa chini na kila mtu akaanza kukemea pepo chafu la kiburi litoke ndani yangu.
Baada ya kuamka, mchungaji akasema pepo aliyekuwa ndani yangu hakuwa wa kawaida, kama angekuwa mchungaji dhaifu, asingetoka hakika.
Nilicheka kimoyomoyo, siku ikaisha
😂😂😂😂dah pole sna
 
Picha linaanza napokea simu kwa ndugu zangu upande wa mama watoto wangu wanasema, samahani tunakuja kwenye maombezi kwa Mwamposa wewe kama mwenyeji tunaomba utupokee ili utupeleke kwa Mwamposa tukaombewe.

Nikasema ok poa nitawapeleka nyie njooni. Ijumaa wakaingia ndani ya jiji la Dsm nikawapokea, Jumamosi chapu nikawapeleka Kawe kuombewa, mimi nikaamusha kwenye mishe zangu za hapa jijini.

Kesho yake jumapili waakambiwa warudi tena kweli jumapili tena nikawarudisha kwenye ibada kama kawida nikasema ibada ikiisha mtanishitua nije kuwachukua.

Mida ya saa nane ibada ikaiisha wakanishitua nikawachukuwe nilipofika kwa Mwamposa mmoja wao akasema kuwa kuna mfanyakazi mwenzake walishawahi kufanya naye kazi miaka ya nyuma kwenye kampuni kampigia simu waonane maeneo ya PICOLO HOTEL kuna maombezi pia.

Basi bwana tukaenda pale Picolo hotel kufika pale wakatupandisha juu kuna ukumbi kule wanasali.

Nilichokikuta kule kinashangaza sana kwa kuwa ilibidi niwasubiri basi nikasema hebu ngoja nikae nisikilizie hapahapo ukumbini.

Kanisa lina waumini 13 tu, wanawake 10 na wanaume 3. Maombi yakaanza nguvu ya upako sijui nini inawashukia wakawa wanadondoka waumini wote hadi ndugu zangu nao wanadondoka.

Nikajisemea moyoni mbona haya majanga. Ikawa kama mchezo sasa wanaombewa watano waliobaki wanasimama nyuma yao kuwashikilia ili wasijibamize sakafuni. Wakizinduka wengine tena wanaombewa halafu waliodondoka wanaamka tena kuwashikilia wenzao.

Nikachoka kuangalia movie ya kitoto nikawambia oya nyie si mnadondoka humu hebu niwaache mkipona mtanishitua nije niwachukue twende nyumbani. Nimeshangaa hivi kipi kinamfanya mtu anadondoka hovyo wakati wa maombezi au ni michezo ya kuigiza?​
Nina dada yangu humwambii kitu kuhusu Mwamposa, kila akija kunitembelea lazima aje na mafuta kwenye kichupa huwa akinipa nachukua akiondoka natupa, nahisi amegundua, jana nilipita nyumbani kwake kumsalimia akanivizia akanipaka kichwani
 
Back
Top Bottom