Mabibi na mabwana moja kwa moja kwenye mada. Itifaki yote imezingatiwa.
Shirika la afya Ulimwenguni (WHO), limekuwa likitoa tathmini, mapendekezo na kauli mbalimbali likionya na kushauri kwenye jitihada za kukabiliana na ugonjwa huu hatari.
Kwa bahati mbaya sana hapa nchini kwetu kumekuwa na upotoshwaji wa wazi kwenye baadhi ya jitihada hizo za WHO.
Ushauri wao usipokubaliana na misimamo ya viongozi wetu, utasikia, "wanatumiwa na mabeberu hao". Ushauri ukiangukia tulipo, tunaukumbatia kwa chereko chereko, hata kama ni nje kabisa ya uhalisia (out of context).
Mifano ni mingi ila kwenye uzi huu, itoshe kuangazia kauli yao hii muhimu ya 'kwenye kuishi na Corona.'
Kwa tathmini za wazi na kwa jinsi maambukizi ya ugonjwa huu yalivyo, WHO walisema:
"ugonjwa huu si wa kuondoka leo au kesho." Kwamba, "itabidi tu kujifunza namna ya kuendelea kuishi nao hadi pale tiba au chanjo kamili itakapopatikana".
Kauli hii imekuwa ikinukuliwa hapa nchini nje ya uhalisia (out of context), kuwa WHO wamepata funzo toka kwa rais wetu mpendwa na kuwa eti sasa sisi tuko kwenye mstari wa mbele tayari kuishi na Corona.
Haiyumkiniki hata hizi chereko chereko na mayowe ya ushindi dhidi ya Corona chini ya bwana yule hapo jumapili ni kwa minajili hiyo.
Kauli ya WHO ni kauli sahihi ya kisayansi na iliyokamilika. Kauli ile haitokei hewani bali ina vigezo kamili vilivyo zingatiwa. Kiuhalisia nchi (yenye Corona) haianzi kuishi tu na Corona from nowhere. Kuna pa kuanzia (starting point) kabla ya kufikia kwenye hatua ya kuishi na ugonjwa huu hatari Ila katika hali ya usalama. Hii ikiwa, wakati hatua zingine zikisubiriwa.
Nchi zote tunazozisikia kuwa zinalegeza masharti yao ya udhibiti zilizo kuwa zimejiwekea, huko kulegeza hayo masharti, ndiyo katika kujipanga kuingia sasa salama kwenye awamu hii ya pili ya kuendelea na maisha kwa tahadhari wakati ugonjwa huu ukingalipo. Angalizo la msingi, "lakini ugonjwa ukiwa umedhibitiwa vilivyo kwanza."
Rwanda, Uganda, USA, UK, Australia, New Zealand, Namibia, Italy, Spain nk, ni mfano wa nchi zilizoko kwenye hatua hizo. Kenya wanapambana vilivyo ili nao angalau waweze kufika kwenye hatua hiyo.
Unaweza ishi na mnyama hatari aliyeko kwenye cage au mhalifu hatari aliyeko jela si anayezurura huru mitaani.
Brazil, Tanzania, Sudan kusini, Burundi, Congo nk, tungali na makundi ya simba, chui, fisi, mbwa mwitu, nk yakizurura mitaani mwetu.
Eti kuwa tunataka sasa kujiaminisha na kuwaachia watoto wetu wadogo kabisa wa chekechea wajiendee tu shule peke yao kwamba wanyama hao watawazoea tu muda unavyopita! Mbona itakuwa ni kujidanganya kwa wazi kuliko pitiliza mno?
Brazil na sisi kwa hali ya sasa kimsingi tofauti haiwezi kuwapo. Kiuhalisia maambukizi yangali bado yanaongezeka sana. Tunatofautiana kwa viwango tu na hilo kwa mwendo wetu huu ni suala la muda tu.
Angalia hapa hawa (Brazil). Wanaanza vipi kuishi na Corona katika hali hii waliyomo sasa?
Kilicho wafikisha hapo ni kama hiki hiki cha kwetu - kibri kilicho pitiliza cha kiongozi wao mkuu.
Shirika la afya Ulimwenguni (WHO), limekuwa likitoa tathmini, mapendekezo na kauli mbalimbali likionya na kushauri kwenye jitihada za kukabiliana na ugonjwa huu hatari.
Kwa bahati mbaya sana hapa nchini kwetu kumekuwa na upotoshwaji wa wazi kwenye baadhi ya jitihada hizo za WHO.
Ushauri wao usipokubaliana na misimamo ya viongozi wetu, utasikia, "wanatumiwa na mabeberu hao". Ushauri ukiangukia tulipo, tunaukumbatia kwa chereko chereko, hata kama ni nje kabisa ya uhalisia (out of context).
Mifano ni mingi ila kwenye uzi huu, itoshe kuangazia kauli yao hii muhimu ya 'kwenye kuishi na Corona.'
Kwa tathmini za wazi na kwa jinsi maambukizi ya ugonjwa huu yalivyo, WHO walisema:
"ugonjwa huu si wa kuondoka leo au kesho." Kwamba, "itabidi tu kujifunza namna ya kuendelea kuishi nao hadi pale tiba au chanjo kamili itakapopatikana".
Kauli hii imekuwa ikinukuliwa hapa nchini nje ya uhalisia (out of context), kuwa WHO wamepata funzo toka kwa rais wetu mpendwa na kuwa eti sasa sisi tuko kwenye mstari wa mbele tayari kuishi na Corona.
Haiyumkiniki hata hizi chereko chereko na mayowe ya ushindi dhidi ya Corona chini ya bwana yule hapo jumapili ni kwa minajili hiyo.
Kauli ya WHO ni kauli sahihi ya kisayansi na iliyokamilika. Kauli ile haitokei hewani bali ina vigezo kamili vilivyo zingatiwa. Kiuhalisia nchi (yenye Corona) haianzi kuishi tu na Corona from nowhere. Kuna pa kuanzia (starting point) kabla ya kufikia kwenye hatua ya kuishi na ugonjwa huu hatari Ila katika hali ya usalama. Hii ikiwa, wakati hatua zingine zikisubiriwa.
Nchi zote tunazozisikia kuwa zinalegeza masharti yao ya udhibiti zilizo kuwa zimejiwekea, huko kulegeza hayo masharti, ndiyo katika kujipanga kuingia sasa salama kwenye awamu hii ya pili ya kuendelea na maisha kwa tahadhari wakati ugonjwa huu ukingalipo. Angalizo la msingi, "lakini ugonjwa ukiwa umedhibitiwa vilivyo kwanza."
Rwanda, Uganda, USA, UK, Australia, New Zealand, Namibia, Italy, Spain nk, ni mfano wa nchi zilizoko kwenye hatua hizo. Kenya wanapambana vilivyo ili nao angalau waweze kufika kwenye hatua hiyo.
Unaweza ishi na mnyama hatari aliyeko kwenye cage au mhalifu hatari aliyeko jela si anayezurura huru mitaani.
Brazil, Tanzania, Sudan kusini, Burundi, Congo nk, tungali na makundi ya simba, chui, fisi, mbwa mwitu, nk yakizurura mitaani mwetu.
Eti kuwa tunataka sasa kujiaminisha na kuwaachia watoto wetu wadogo kabisa wa chekechea wajiendee tu shule peke yao kwamba wanyama hao watawazoea tu muda unavyopita! Mbona itakuwa ni kujidanganya kwa wazi kuliko pitiliza mno?
Brazil na sisi kwa hali ya sasa kimsingi tofauti haiwezi kuwapo. Kiuhalisia maambukizi yangali bado yanaongezeka sana. Tunatofautiana kwa viwango tu na hilo kwa mwendo wetu huu ni suala la muda tu.
Angalia hapa hawa (Brazil). Wanaanza vipi kuishi na Corona katika hali hii waliyomo sasa?
Kilicho wafikisha hapo ni kama hiki hiki cha kwetu - kibri kilicho pitiliza cha kiongozi wao mkuu.