Kujenga miundombinu na kuruhusu wamachinga wasibughudhiwe ndio kusema kunafuta madoa ya utawala wa hayati Magufuli?

Kujenga miundombinu na kuruhusu wamachinga wasibughudhiwe ndio kusema kunafuta madoa ya utawala wa hayati Magufuli?

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Halina ubishi hata kiduchu kwa miaka yote tangu mwaka 1995 hayati JPM amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha barabara za Tanzania zinaunganika. Na kweli sasa hivi nchi imepiga hatua kwa kuwa na miundo mbinu mizuri. Pia alipokuwa rais wa JMT aliwakingia kifua wamachinga wasiwekewe kiwingu na kufanya biashara kwa uhuru wao.

Lakini hii pekee ndio inakuwa sababu ya kusema hakuna madoa yaliyowekwa na uongozi wake au utawala wake?

Muamar Ghadafi alitengeneza taifa lililokuwa na miundo mbinu mizuri tena ya kisasa kuliko hata nchi za ulaya. Alihakikisha watu wanapata elimu bure,ndoa bure na chakula bure, lakini doa pekee lilimfanya mpaka akauliwa kwa fedheha ni ukatili dhidi ya binadamu, tena alioufanya kwenye gereza maarufu la Abu salim. Maana alikuwa hataki kukosolewa.

Ni kweli kabisa hayati JPM alikuwa mfuatiliaji na msimamizi mzuri ndio maana alifanikisha nchi ikawa na miundo mbinu mizuri, ndio kusema alitawala bila dosari?

image_search_1616834634042.jpg
 
Mama Samia wewe ni mtoto wa kiislam aliefundwa akafundika.
Achilia mbali wengine wasiofundika kidini.
Wewe ulifundwa ukafundika.
Nakupenda sana
 
Naomba kuuliza itifaki inasemaje makamu wa raisi alivyoenda kumtembelea Lisu aliomba ruhusa kwa hayati Magu?
 
Angalau we unakiri Kuna mambo yamefanyika mengine hayo ni makosa ya kibinaadamu maana hamna binaadam aliyekamilka. Na hamna uongoz ambao watu hawajapotea kwa awamu zote
 
Angalau we unakiri Kuna mambo yamefanyika mengine hayo ni makosa ya kibinaadamu maana hamna binaadam aliyekamilka. Na hamna uongoz ambao watu hawajapotea kwa awamu zote
Hayo makosa nayo tuyajadili.
 
Hata Yesu hakukubaliwa na waisrael wote huo ndio utashi wa kibinaadamu hivyo hata JPM wapo wanao mkubali na wapo wasio mkubali hilo lazima liwepo kwa kuwa ndio hulka ya kibina adamu
 
Angalau we unakiri Kuna mambo yamefanyika mengine hayo ni makosa ya kibinaadamu maana hamna binaadam aliyekamilka. Na hamna uongoz ambao watu hawajapotea kwa awamu zote
Ndugu yangu sasa wazidi kudhihirisha kuwa huko kwenu shetani ndio anaetawala.
Kutwa eti washindana, kumwimba Mungu mdomoni
Kumbe hasa mwawindana, kwa chuki hila Moyoni

Kweli Mungu kaamua kutuepusha na mengi ambayo yangetokea mpaka kuja kumaliza 'mitano' tena.
 
Angalau we unakiri Kuna mambo yamefanyika mengine hayo ni makosa ya kibinaadamu maana hamna binaadam aliyekamilka. Na hamna uongoz ambao watu hawajapotea kwa awamu zote
Yaani Kutesa na Kuua watu mnaita ni "makosa ya kibinadamu?" Ubinadamu gani wa kuamuru watu wateswe wauawe? Kama huo ndo ubinadamu Unyama ukoje sasa? Utetezi wa kijinga Kama huu ndo unazidisha hasira za wapenda haki. Tafuteni maana halisi ya makosa ya kibinadamu lakini siyo kuhalalisha mauaji. Nyie mnalia mtu wenu kaondoka duniani, lakini wengine wameondolewa uhai na vibaraka wa mtu huyohuyo mkashangilia.
 
Ndugu yangu sasa wazidi kudhihirisha kuwa huko kwenu shetani ndio anaetawala.
Kutwa eti washindana, kumwimba Mungu mdomoni
Kumbe hasa mwawindana, kwa chuki hila Moyoni

Kweli Mungu kaamua kutuepusha na mengi ambayo yangetokea mpaka kuja kumaliza 'mitano' tena.
Na Mimi nawashangaa hawa Watanzania Wanyarwanda ambao wanahalalisha mauaji kwa kisingizio cha kutawala.?
 
Yaani Kutesa na Kuua watu mnaita ni "makosa ya kibinadamu?" Ubinadamu gani wa kuamuru watu wateswe wauawe? Kama huo ndo ubinadamu Unyama ukoje sasa? Utetezi wa kijinga Kama huu ndo unazidisha hasira za wapenda haki. Tafuteni maana halisi ya makosa ya kibinadamu lakini siyo kuhalalisha mauaji. Nyie mnalia mtu wenu kaondoka duniani, lakini wengine wameondolewa uhai na vibaraka wa mtu huyohuyo mkashangilia.
Waliuwawa ni wangap hebu waorodheshe Basi,
Waliteswa wangapi,
Tupe na source ya taarifa.
Halafu mbona awmu zote zilipita watuwengi tu walipotea ila mmemkomalia jpm tu,
Na nyie mnaojua ubinaadam mbona mlimpoteza wangwe kwa usalama wa uwenykiti wa milele
 
Mbona yeye mwenyewe anasema ameacha kuvaa suruali na kuanza kuvaa shungi juzi tu ili apate ubunge Sasa hizo sifa wewe umetoa wapi...wabongo bhana.
Mama Samia wewe ni mtoto wa kiislam aliefundwa akafundika.
Achilia mbali wengine wasiofundika kidini.
Wewe ulifundwa ukafundika.
Nakupenda sana
 
Angalau we unakiri Kuna mambo yamefanyika mengine hayo ni makosa ya kibinaadamu maana hamna binaadam aliyekamilka. Na hamna uongoz ambao watu hawajapotea kwa awamu zote
Lakini wengine walikuwa wanatumia akili kubwa kuwapoteza wale waliokuwa tishio kwa usalama wa nchi, lakini sio utawala ule uliokuwa ukiwapoteza watu ki jinga jinga tu, hata mjinga anafahamu nini kinaendelea!!yaani ukimkosoa tu hata katibu kata tayari, unaanza kuishi kwa mashaka!!na ukipotea hakuna anayeguswa na kupotea kwako?!!!
 
Lakini wengine walikuwa wanatumia akili kubwa kuwapoteza wale waliokuwa tishio kwa usalama wa nchi, lakini sio utawala ule uliokuwa ukiwapoteza watu ki jinga jinga tu, hata mjinga anafahamu nini kinaendelea!!yaani ukimkosoa tu hata katibu kata tayari, unaanza kuishi kwa mashaka!!na ukipotea hakuna anayeguswa na kupotea kwako?!!!
Njoo na mifano ili tujue hii akili kubwa na ndogo ikoje.
 
SIO kweli ndugu yangu.
Huo ni msemo unaopendwa na wenye hulka za kidhalimu kama marehemu na washirika wao ambao kwao demokrasia na haki za binadamu kama vilivyo kwenye Katiba yetu na utawala sheria kwao vilikwisha poteza maana.
Uhuru wa habari kwao ni kumsifu Jiwe. Usipojipendekeza WAGENDA.
Ilibidi hata ma Propesa wengine ambao wanastahili kuheshimika, bila aibu walijivunia kujigalagaza miguuni pa Jiwe; sijui eti " ... niliokotwa jalalani...." ; ".......jina lake la kwanza ni zuri sana, tena la kitakatifu....". Wengine (kama MB wa mpakani kusini magharibi) wakijivunia kununuliwa na ambae aliwahi kutishia hadharani 'kushughulikia' Mashangazi wa wabunge waliyotofautiana nae kuhusu uendeshaji wa mfuko wa korosho.
Yaonekana nawe bado hujijui vizuri, ila siku ukijapenya ukaukwaa uongozi wa nchi utaishia kuwa kama marehemu.
Tukiwa bado twamsoma Mama, tumwombe Mungu atuepushe na wenye mitazamo hasi kama ya kwako.
Amen
Nchi zote unazoona zimesimama duniani zimemwga damu hasa kuwandoa wasaliti Rwanda leo mnapenda kuitolea mfano ila fuatilia historian take miaka 10 nyuma. utajua kwamba hakuna mamlaka takatifu.
 
Back
Top Bottom