Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Asset mean take in and liability mean take out! Unawezaje ku gain pesa wakati unaishi nyumba isiyokuingizia chochote?
Cost saving is also a gain, kama unalipa rent ya 300,000 kwa mwezi ukiwa na nyumba yako hiyo gharama haitakuwepo. Naunga mkono wazo la kufanya biashara kwanza lkn napingana na mnaosema nyumba ni liability, sio kweli.
 
Hii mentality ya kiumaskini sijui imetoka wapi..watu ni waoga mnoo.katika hii thread watu walio changia positive hawazid wanne.wengi wanaogopa biashara!
Huenda madhara ya sera za kijamaa bado yametuganda.
 
Najua unataka kusema nafikiria nyumba ya hali ya chini ndio maana nina mawazo haya. Yes.. kwangu mimi nafikiria sehemu ya kulaza ubavu tu sinaga mambo yale mnaita sijui dream house kwa hiyo budget yangu itategemea kwa wakati huo nina kiasi gani na nitaangalia ujenzi wa bei ndogo kwa kadri inavyowezekana...kkama kuna nyumba inaweza kusimama kwa laki mbili I'll go for it
 
Unayosema ni kweli kabisa baba vipaumbele tunatofautiana sana...mtu anayelipa milioni kumi rent sio wa hivihivi ana uhakika na anachokifanya ila mimi kapuku let's say nimebet nikapata milioni kumi uniambie eti nikaiweke hela yote kwenye biashara siwezi kukuelewa hata robo...walau nitaikata nusu nikanunue kiwanja
 
Huwezi kujenga kama huna kiwanja, na pia usinunuwe kiwanja kama kipofu kisa bei chee, angalia access kutoka hapo kwenda city center, ndio sababu wahindi wanazeekea upanga na hawana mpango wa kujenga na si kwamba watafukuzwa hapa ni kwao hakuna wa kuwafukuza lakini hesabu za kukaa mapinga mishe posta ujinga huo mdosi hafanyi kamwe.
 
Inategemea na biashara yako, kama hiyo city center una kazi nayo freshi ila kama shughuli zako hazikuafanyi uwe na safari za kila siku za kwenda huko ukae nayo karibu ya nini?
 
Inategemea na biashara yako, kama hiyo city center una kazi nayo freshi ila kama shughuli zako hazikuafanyi uwe na safari za kila siku za kwenda huko ukae nayo karibu ya nini?
Tukubaliane kutokukubaliana, kuna maeneo ni ya kuishi maisha ya uzeeni au umestaafu kazi kama ni mwajiriwa unakula pensheni yako tu.

Ndio ukiangalia hata washuwa wa zamani unakuta wengi wana nyumba zaidi ya moja, kuna alipoanzia maisha na anapokwenda kumalizia maisha yake.

Utakaaje sehemu ambayo kutoka nyumbani ni lazima upande bodaboda buku mbili, then uunganishe madaladala, kwenda na kurudi kila siku utumie buku 6, huo ni utaahira.

National housing wanapaswa kubeba lawama zote kwa kutoandaa makazi ya bei nafuu low cost, matokeo yake kuna mpumbavu anaitwa Msechu akaigeuza NHC kuwa ni kwa ajili ya watu high profile.

Makazi na kodi ya nyumba haipaswi kuwa ni vitu vya kuumiza kichwa.
 
Ni kweli ni utaahira kama unatumia buku sita kwenda kazini kila siku lakini kuna watu shughuli zao haziwazimishi kwenda mjini kila siku, wanaenda mara moja au mbili kwa mwezi kwa nini wabanane mjini? Au mwenzetu unaamini ili uwe mfanyakazi au mfanyabiashara ni lazima ufanyie city centre?
 
Mkuu, nakuomba uelezee hili jambo kwa kina. Maana nashangaa mno, unakuta mhindi au mwarabu anamabiashara yanamuingizia Mabilioni ila anabanana upanga, kariakoo au masaki kwenye maghorofa ya nhc. Nakuomba uelezee hii kitu kwa kina ili tuelewe hili jambo.


Nb: mimi ni muoga mno. Yaani hela ikinitembelea pap lazima nijenge hata kama ni kibaha ndanindani huko 😂
 
Hapana,
haikuwa nia yangu kukubeza wala kukufedhehesha.
Sina sababu ya kufanya hivyo na ninaheshimu sana mawazo yako.

Nilitaka nikupe wazo linaloendana na pesa utakayowekeza kwenye nyumba ulifanyie kazi hata kama sio leo basi kesho
lakini utafakari kwa kina.
Najua mtu akishaweka vipaumbele vyake kwenye maisha na pesa anatafuta mwenyewe ni vigumu kumbadilisha lkn ushauri ni ushauri you can take it or leave it.

Nisamehe kama nimekukwaza.
 
Nyumba ya kupanga ya taste unayopenda ni gharama

kujenga ni suala la msingi lisipuuzwe
 
[emoji23][emoji23][emoji23]

Umenichekesha sana eti nimebet nikapata milioni kumi hahaha
We si wa kishua lakini acha kutu actia
 
Hebu nipe basi hilo wazo hela yenyewe ya kujenga ninayo basi nabwabwaja tu hapa
 
[emoji23][emoji23][emoji23]

Umenichekesha sana eti nimebet nikapata milioni kumi hahaha
We si wa kishua lakini acha kutu actia
Haha mimi huyo? Wa kishua? Hilo kwangu nahesabu kama tusi ujue...ni sana na kumuita Keisha black beauty
 
Hujaelewa kitu gani hapo? Kaa na calcutor ndio utawaelewa Wahindi na Waarabu na ndio utaelewa kwa nini gari ukinunuwa kwa Muhindi hata kama lina muda mrefu bado ni jipya na halina magumashi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…