Kukaa Kijijini ni kufeli maisha

Kukaa Kijijini ni kufeli maisha

Upo sahihi kabisa,kijiji kizima hamna mwenye tv au radio ya maana utapata saa ngap mzuka wa kununua hio tv na kijiji kizima hakina umeme,kuna wakati niliishi Handeni kijiji kwa Kwakonje kuna jamaa mmoja alikuwa na tv kijiji kizima na toyo basi ndio anaonekana tajiri kwenye kile kijiji
 
Unakaa mjini halaf unakaa sehem ka mbagala au gongo la mboto au kigambon shida tupu kuanzia usafir mpk maisha unapanga chumba kimoja kwa tabu halaf kijijin watu wanaishi maisha mazur tu bora nn ss
Unamfananisha mtu wa Mbagala na kijijini , Jitathmini mkuu , Mjini ni Mjinj tu,Kijijini unatakiwa kwenda kuangalia Fursa na sio kuishi
 
Kijijini ni kwa wazee zaidi, wastaafu na pia wakulima na wafugaji.
Daaah sa nikizeeka ndio nikakae Kijijini?🤔 hospital mbali,bank mbali, shopping mpaka uende wilayani daaah kichwa kinauma
 
We acha tu ukiamka asubuh kila utembeapo unapishana na miembe na nyumb za nyasi tu
Mkuu siyo vijiji vyote vipo kama vya huko kwenu, Jaribu kutembea uone. Kuna vijiji vina mazingira mazuri na fursa pia
 
Habari wana jf napenda kutanguliza huu uzi kama ulivyoandikwa hapo juu. Najua kuna baazi ya watu hawawezi kunielewa. Ila ukweli upo hivi kukaa kijijin kwa kijana unaejitafuta kimaisha ni kufeli na nasema hivi kwasbabu nazoziona mimi.

1. KUZUNGUKWA NA WATU WASIOSAHIHI NA WENYE MITAZAMO HASI
Kijijini watu wengi hawaamin kuish ndoto zao na wanaamin kila aliyefanikiwa ni mchawi, freemason,jambazi.. na kila ukijaribu kufanya kitu tofaut na mila za hapo kijijin. Wengi hawaamin unaweza kufanikiwa watakukatisha sana tamaaa

2. KUDUMAA AKILI NA KULIZIKA MAPEMA
Kijijni ukimilki pikpik tu wanaanza kukuita boss kitu ambacho kinalufanya ujionee umefanikiwa na kulizika mapema. Pia hata mazingira hayaruhusu mtu ukue kiuchumi unakosa sehem ya kutizamia au role model tofaut na mjin

3. MZUNGUKO WA PESA NI MDOGO SANA
Kijijni ni rahis sana kuuwa pesa ukifungua biashara kutokana na mzunguko. Pesa huja mara moja tu wakat wa mavuno na kuna baazi ya biashara kama nguo baazi ya wanakijij huwa na dhana kwamba kununua nguo mpka sikukuu au safari. Na ukinunua nguo bila kuzingatia hivo vitu husema unaharibu pesa au unatumia pesa ovyo.

4. KUKOSA NDOTO ZOZOTE
Kijijini mtu akiamka asubuh anaenda shamba na akirud shamb anawaza aoge akae kijiweni apige stori bas siku imeisha. Na kubishana na vitu visivokuwa na msingi na kupiga umbea.

Kiufupi yapo mengi yanayomzuia mtu kukua na kuwa na mtazamo chanya ila kwa machache ndo hayo

NB. Ushauri wangu kama unajitafuta kimaisha usikae kijijini sana ni bora uanze na level za wilaya
ILA KUKAA VIJIJINI VIJANA WENZANGU NI KUFELI KIJIJINI HAKUNA MAENDELEO NA NDO MAANA HAKUNA AFSA BIASHARA WALA MASOKO

KIJIJINI SHUGHULI KUBWA NI KILIMO NA NDO MAANA KUNA AFSA KILIMO

Kama una maoni unaweza ukashare ila mi kwa mtazamo wangu upo hivyo
Inategemea unatokea kijiji gani? Nimeishi Mara kipindi hicho Nyamongo na Nyamwaga ni kijijini. Lakin palikuwa na Baadhi ya watu wewe wa Buzuruga, Sanawari,Majengo na Tabata wala humsogelei hata kidogo.
 
Dont conclude in that, kila mtu panamfaa mahali anapoishi kulingana na mtazamo wake (Vision)
Kuna watu ukiwaangalia mjini wanaishi maisha ya tabu sana. Usikae mjini kama huna akili ya kimaisha.

Wapo watu wanaishi mijini wala haisaidii bali wanajitengenezea umaskini tu
Bora umesema ukweli,nikiwahi kukaa Kwa mda mjiwmema kigamboni aisee Kuna watu wanaishi Kwa kuunga unha sana nyumba mbovu Ile mbaya ila ukimwambia aende kijijin hataki but ukoangalia life yake hata mie wa kijijin hanifikii hata nusu ya mali nilizonazo
 
Kwa sasa hivi vijijini Kuna fulsa nyingi kupita mjini.
Kama hujui.
Hasa vijiji vyenye Rutuba na Ardhi ya kutosha.
 
Habari wana jf napenda kutanguliza huu uzi kama ulivyoandikwa hapo juu. Najua kuna baazi ya watu hawawezi kunielewa. Ila ukweli upo hivi kukaa kijijin kwa kijana unaejitafuta kimaisha ni kufeli na nasema hivi kwasbabu nazoziona mimi.

1. KUZUNGUKWA NA WATU WASIOSAHIHI NA WENYE MITAZAMO HASI
Kijijini watu wengi hawaamin kuish ndoto zao na wanaamin kila aliyefanikiwa ni mchawi, freemason,jambazi.. na kila ukijaribu kufanya kitu tofaut na mila za hapo kijijin. Wengi hawaamin unaweza kufanikiwa watakukatisha sana tamaaa

2. KUDUMAA AKILI NA KULIZIKA MAPEMA
Kijijni ukimilki pikpik tu wanaanza kukuita boss kitu ambacho kinalufanya ujionee umefanikiwa na kulizika mapema. Pia hata mazingira hayaruhusu mtu ukue kiuchumi unakosa sehem ya kutizamia au role model tofaut na mjin

3. MZUNGUKO WA PESA NI MDOGO SANA
Kijijni ni rahis sana kuuwa pesa ukifungua biashara kutokana na mzunguko. Pesa huja mara moja tu wakat wa mavuno na kuna baazi ya biashara kama nguo baazi ya wanakijij huwa na dhana kwamba kununua nguo mpka sikukuu au safari. Na ukinunua nguo bila kuzingatia hivo vitu husema unaharibu pesa au unatumia pesa ovyo.

4. KUKOSA NDOTO ZOZOTE
Kijijini mtu akiamka asubuh anaenda shamba na akirud shamb anawaza aoge akae kijiweni apige stori bas siku imeisha. Na kubishana na vitu visivokuwa na msingi na kupiga umbea.

Kiufupi yapo mengi yanayomzuia mtu kukua na kuwa na mtazamo chanya ila kwa machache ndo hayo

NB. Ushauri wangu kama unajitafuta kimaisha usikae kijijini sana ni bora uanze na level za wilaya
ILA KUKAA VIJIJINI VIJANA WENZANGU NI KUFELI KIJIJINI HAKUNA MAENDELEO NA NDO MAANA HAKUNA AFSA BIASHARA WALA MASOKO

KIJIJINI SHUGHULI KUBWA NI KILIMO NA NDO MAANA KUNA AFSA KILIMO

Kama una maoni unaweza ukashare ila mi kwa mtazamo wangu upo hivyo
Ni mtazamo wako tu huu.

Kuna watu wanaishi kijijini washatoboa maisha. Yupo jamaa mmoja anamiliki magari kwa ajili ya biashara ya usafiri kutoka kijijini hadi mjini. Ameanza tangu 2002, ambapo alianzia kwenye uuzaji wa kuku miaka ya late 1990, then akafungua Duka, ikafuatia gari aina ya Landrover kwa wakati huo mwaka 2002, Biashara ikawa inakua. Kila ikifika msimu wa kilimo anaingia shambani kulima vitunguu kwa kutumia faida kutoka kwenye biashara ya Duka na usafiri.

Hadi sasa biashara zake zimeinuka na zinaendelea kupiga hatua, ni tegemeo kwenye usafiri kijijini. Wengi waliowahi kufanya biashara ya usafishaji hawakudumu kama yeye, wengine wanaanza na kumuacha yeye hatetereki.

Binafsi naona ni ile commitment ha mtu kufanya anachokiamini kwa usahihi na kutokata tamaa
 
Sikupingi ndgu, hata madogo waliotoka bush kuja town hawatamani kurudi, town kushika vichenji ni kawaida.

Ubaya wa bush ni watu wengi kama sio wote kua level moja, tajiri ni yule anaemiliki duka tu pale kijiji cha pili.
Kijijiji kunadumaza na kuzeesha haraka.

Watu wanasema kuna wadau waliopiga mamilioni kwa kilimo, bila shaka hao watu wameishi town na wakasoma gape baada ya kupata maarifa wakiwa town wakaridi bushi kupiga ambush wakaondoka na kitita.

Na ni wengi hufanya hivyo, ila ukulie bush uje usuke mchongo wa kupiga 50M em tuache utani aisee, bush hata ujanja ujanja unakua huna.
 
Ni mtazamo wako tu huu.

Kuna watu wanaishi kijijini washatoboa maisha. Yupo jamaa mmoja anamiliki magari kwa ajili ya biashara ya usafiri kutoka kijijini hadi mjini. Ameanza tangu 2002, ambapo alianzia kwenye uuzaji wa kuku miaka ya late 1990, then akafungua Duka, ikafuatia gari aina ya Landrover kwa wakati huo mwaka 2002, Biashara ikawa inakua. Kila ikifika msimu wa kilimo anaingia shambani kulima vitunguu kwa kutumia faida kutoka kwenye biashara ya Duka na usafiri.

Hadi sasa biashara zake zimeinuka na zinaendelea kupiga hatua, ni tegemeo kwenye usafiri kijijini. Wengi waliowahi kufanya biashara ya usafishaji hawakudumu kama yeye, wengine wanaanza na kumuacha yeye hatetereki.

Binafsi naona ni ile commitment ha mtu kufanya anachokiamini kwa usahihi na kutokata tamaa
Hiyo bishara ya usafirishaji angeijulia wapi bila kufika town na kusoma gap??

Sio watu wasiishi kijijini ila ile kuishi bush maisha yako yote ndo tatizo kubwa.
Watu wanatoka town wamesoma gape la kupiga pesa hapo kijijini kwenu, nyie wenyeji sio rahisi kuiona hiyo pesa maana hamna exposure.
 
Tusipangiane wewe Piga pesa huko mjini wengine tupige huku kijijini, kila mtu ashinde mechi zake
 
Back
Top Bottom