Kukabiliana na upungufu wa Dollar nchini, napendekeza safari za nje kwa watumishi wa umma zifutwe

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Ni zaidi ya mwaka sasa Serikali yetu inalalamika upungufu wa Dollar Kwa ajili ya kuagizia bidhaa na kulipa mikopo na mahitaji mengine muhimu.

Safari za nje Kwa viongozi wa umma, Hazina yetu ya dollar hutumika, hivyo nashauri tuanze na kufuta safari za nje za viongozi Ili kutunza akiba ya pesa za kigeni kiduchu zilizopo.

Wakati hatua za mwanzo zikiendelea kuchukuliwa.

Tuwaombe viongozi wetu wa Dini wawaombe viongozi na wafanyabiashara wanaosemekana wameficha dollar majumbani wazitoe, walioficha ktk mabenki ya nje warudi kuwekeza nchini.

Mikutano na vikao na mataifa ya nje itumike video conference kama kipindi cha corona.

Magu alisema TUTAMKUMBUKA!

Tusione haya kujisahihisha.

KaribunišŸ™
 
Hauwezi kuzuia wizi Serikalini, hata wakati wa mwendazake kulikuwa na wizi. Cha muhimu ni kuelekezwa wanaoiba wawekeze nchini. Nchi nyingi za Afrika ambazo zina rasilimali kutuzidi sisi lakini wametuzidi umasikini kwa sababu wanasiasa wake wamewekeza nchi za nje. Angalia DRC wanasiasa wake wamewekeza Ufaransa na Afrika Kusini.

Nchi za Afrika magharibi wanasiasa wake wamewekeza Ufaransa na Ubelgiji. Kwa hio hawa watu inabidi waambiwe wawekeze nchini. Mtu anapiga hela ananunua nyumba Dubai huo ni ujinga. Wakati anaweza kufungua kiwanda na kuajiri watu wengi hapa nyumbani.
 
Hauwezi kuzuia wizi Serikalini, hata wakati wa mwendazake kulikuwa na wizi. Cha muhimu ni kuelekezwa wanaoiba wawekeze nchini. Nchi nyingi za Afrika ambazo zina rasilimali kutuzidi sisi lakini wametuzidi umasikini kwa sababu wanasiasa wake wamewekeza nchi za nje. Angalia DRC wanasiasa wake wamewekeza Ufaransa na Afrika Kusini.

Nchi za Afrika magharibi wanasiasa wake wamewekeza Ufaransa na Ubelgiji. Kwa hio hawa watu inabidi waambiwe wawekeze nchini. Mtu anapiga hela ananunua nyumba Dubai huo ni ujinga. Wakati anaweza kufungua kiwanda na kuajiri watu wengi hapa nyumbani.
 
Nchi hii haijui ifanye nini kwa wakati gani! Ni mwendo wa kubahatisha tu.

Safari za nje ziliwahi kurabitiwa kwa tija lakini sasa hivi ni mwendo wa kutiririka tu. Hovyo sana
Mwigu pekee ruksa kuzurura akitembeza bakuli.
 
Tuwaombe viongozi wetu wa Dini wawasihi warudi kuwekeza nchini.

Na wale walioiba na kuficha pesa nje ya nchi wazirudishe,

Bila kusahau walioficha pesa kwenye containers wazitoe, inasemekana lakini!!
 
wao hawakutani na changamoto yoyote maana kila kitu ni bure
 
Waogopa wakiwekeza humu pesa za wizi mtawapuna!!
 
Safari za Nje za Watumishi ndio zinamaliza Dola? Bwege wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…