Kukamilika Ikulu Chamwino Dodoma, Rais Samia Kuandika Historia Nyingine

Kukamilika Ikulu Chamwino Dodoma, Rais Samia Kuandika Historia Nyingine

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Wakati uzinduzi wa Ofisi za Rais Ikulu, Chamwino jijini Dodoma, ukitarajiwa kufanyika Mei 20 Mwaka huu Serikali imesema serikali imesema inajivunia mchango wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, katika ujenzi huo, ambao utaandika historia nyingine.

Rais Samia ataingia katika Historia ya Tanzania kwa kuwa Rais wa Kwanza kuhamia na kuanza kutumia Ikulu ya Chamwino Dodoma baada ya kukamilika tangu wimbo wa Serikali kuhamia Dodoma uanze kuimbwa enzi za Hayati Mwalimu Nyerere

Akizungumza jana baada ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus, kutoa video fupi kuelekea uzinduzi wa Ikulu mpya, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alisema kukamilika kwa ujenzi huo, Rais Dk. Samia ameonesha ushujaa.

Msigwa alisema ujenzi wa Ikulu hiyo umekuwa wa kihistoria kutokana na kutumia fedha za ndani, huku vijana wazalendo wa jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wakitumika kuufanikisha.

"Ofisi ya Ikulu Dodoma imekamilika...ofisi hii ndiyo ambayo Rais Dk. Samia ataitumia kwa kazi zake za kila siku, tunafahamu Ikulu ya Dar es Salaam ilijengwa wakati wa ukoloni, hivyo hatua ya ujenzi huu kujengwa kwa fedha za ndani kwa kutumia vijana wetu wa JKT na kukamilika hadi kufikia kuzinduliwa mapema mwezi huu, serikali tutaendelea kutambua mchango wa Rais Samia kama shujaa katika kuandika historia hii muhimu," alisema.

Alisema ujenzi huo unakwenda pamoja na ujenzi wa mji wa serikali jijini Dodoma, ambao umefikia asilimia 60 hadi 70, ukiwa ni utekelezaji wa llani ya Uchaguzi ya CCM na Katiba ya Tanzania ya mwaka 1973 kuhusu serikali kuhamia mkoani humo.
 
..msifikiri huo uzinduzi unafanyika bure.

..kuna mamilioni ya kodi zetu yanatumika kufanya sherehe ya kuzindua ikulu.

..Na Raisi tulishamuona ktk Ikulu ya Dodoma sasa sherehe za ufunguzi zina msaada gani kwa Watanzania masikini?
 
..msifikiri huo uzinduzi unafanyika bure.

..kuna mamilioni ya kodi zetu yanatumika kufanya sherehe ya kuzindua ikulu.

..Na Raisi tulishamuona ktk Ikulu ya Dodoma sasa sherehe za ufunguzi zina msaada gani kwa Watanzania masikini?
Roho mbaya tu inakusumbua, Chadema mlivyoenda kumpokea Lissu mlitumia mamilioni mangapi?
 
Wakati uzinduzi wa Ofisi za Rais Ikulu, Chamwino jijini Dodoma, ukitarajiwa kufanyika Mei 20 Mwaka huu Serikali imesema serikali imesema inajivunia mchango wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, katika ujenzi huo, ambao utaandika historia nyingine.

Rais Samia ataingia katika Historia ya Tanzania kwa kuwa Rais wa Kwanza kuhamia na kuanza kutumia Ikulu ya Chamwino Dodoma baada ya kukamilika tangu wimbo wa Serikali kuhamia Dodoma uanze kuimbwa enzi za Hayati Mwalimu Nyerere

Akizungumza jana baada ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus, kutoa video fupi kuelekea uzinduzi wa Ikulu mpya, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alisema kukamilika kwa ujenzi huo, Rais Dk. Samia ameonesha ushujaa.

Msigwa alisema ujenzi wa Ikulu hiyo umekuwa wa kihistoria kutokana na kutumia fedha za ndani, huku vijana wazalendo wa jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wakitumika kuufanikisha.

"Ofisi ya Ikulu Dodoma imekamilika...ofisi hii ndiyo ambayo Rais Dk. Samia ataitumia kwa kazi zake za kila siku, tunafahamu Ikulu ya Dar es Salaam ilijengwa wakati wa ukoloni, hivyo hatua ya ujenzi huu kujengwa kwa fedha za ndani kwa kutumia vijana wetu wa JKT na kukamilika hadi kufikia kuzinduliwa mapema mwezi huu, serikali tutaendelea kutambua mchango wa Rais Samia kama shujaa katika kuandika historia hii muhimu," alisema.

Alisema ujenzi huo unakwenda pamoja na ujenzi wa mji wa serikali jijini Dodoma, ambao umefikia asilimia 60 hadi 70, ukiwa ni utekelezaji wa llani ya Uchaguzi ya CCM na Katiba ya Tanzania ya mwaka 1973 kuhusu serikali kuhamia mkoani humo.
Na Washindi ndio huandika historia.Kwenye Jiwe la uzinduzi itakaa alama ya Dr.Samia
 
Roho mbaya tu inakusumbua, Chadema mlivyoenda kumpokea Lissu mlitumia mamilioni mangapi?

..nazungumzia matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za umma.

..sherehe za ufunguzi wa Ikulu Dodoma zinamsaidia nini mlipakodi au mwananchi masikini?

..kwani Raisi angehamia humo --nadhani ameshahamia--, bila kufanya hiyo sherehe hataitwa Raisi?
 
Back
Top Bottom