Kukosa credibility kwa tuliokuwa tunawapa kusimamia bandari yetu destiny yake ndio haya DP

Kukosa credibility kwa tuliokuwa tunawapa kusimamia bandari yetu destiny yake ndio haya DP

Tuache kuwasingizia uongo wazalendo wetu walioitunza bandari yetu miaka yote pamoja na kwamba wamekuwa wakishibisha matumbo yao hapo hapo, na kingine kingi kilichobakia wakatupatia na sisi walalahoi tusife njaa.

Hili la kuwapa DP world bandari zetu zote bure na milele ni uhuni tu wa watawala na wala halina uhusiano wowote na ufanisi duni wa pale bandarini. Kwanini? Watawala wamedhamiria zaidi kuwapa waarabu wa Dubai umiliki wa milele wa bandari zetu zote na sio kuboresha bandari yetu.
Wanaolaumu uongozi wa TPA au mwekezaji wa awali (Ticts) ataje Shirika lolote la Umma lililofanya kwa ufanisi na tija. Ukweli ni kwamba mfumo wa uteuzi na uwajibishaji wa Wakuu wa mashirika ya umma ndiyo mbovu, au usimamizi wake ni dhaifu.

Hivyo, basi tutegemea bandari kugeuzwa shamba la bibi, DPW itakapoanza kazi, kwa jinsi ile ile madini na maliasili zingine zinavyochotwa.

Nasimamia kumpongeza Mwendazake kwa jinsi alivyosimamia rasimali za Taifa.
 
Haya ni matokeo ya mtu amabye alitakiwa kuwa mama wa nyumbani kupewa urais. Vision zero. Anafikiri kwenye kusaidiwa tu. Inaonekana hata culture ya sehemu alikokulia inamfanya mwanamke ajione ni kiumbe kinachostahili kufanyiwa mambo watu wenye uwezo.

Hoja yako ni sahihi kabisa. Mwanamke hata akiwa na utajiri bado atataka mwenza wake amsaidie.

Mwanamke aliumbwa kuwa msaidizi wa mwanamme na si vinginevyo, kama ilivyoandikwa kwenye Biblia, Kitabu cha Mwanzo 2:18, 21, 22 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
 
Kwani Ticts si wapo miaka 30 hapo ?
TPA unawalaumu Kwa kipi??
TICTS iliingia mkataba wa kimagumashi kwa mtindo huu huu unaotaka kufuatwa na DPW. Hivi ni vita vya vigogo wa kambi ya TICTS wanaonyang'anywa tonge nono dhidi ya kambi mpya ya DPW.
 
Haya ndio ili kuondoa Kunguni ndani ya godoro lako chumbani unaamua kuchoma moto ghorofa zima....; Cha ajabu zaidi wanaokusifia ni baadhi ya wananzengo, ambao na nyumba zao zinaweza kuungua kwa maamuzi yako...
 
TICTS iliingia mkataba wa kimagumashi kwa mtindo huu huu unaotaka kufuatwa na DPW. Hivi ni vita vya vigogo wa kambi ya TICTS wanaonyang'anywa tonge nono dhidi ya kambi mpya ya DPW.
Exactly
 
walipoteuliwa walikuwa na nyuso za uadilifu walipoingia jikoni walibadilika. kuwa mwanamke kuna maana mtu hawezi kuwa kiongozi bora.. wasomi wote nchi ni mali ya rais yeye anateu ndugu zetu ndugu zetu wanatumia uteuzi kujinufaisha na familia zao na kujenga majumba makubwa wengine ndugu zao wakiishi kwenye nyumba za tembe. WAKUNUNIWA SIO RAIS TUWANUNI NDUGU ZETU KWA KUSHINDWA KUTIMIZA WAJIBU WAO. waliaminiwa wameshindwa kuaminika na wametuzamisha na kutufunga mawe tunashindwa kuibuka tuone na watu tuokolewa na wapita njia.. TPA na wafanyakazi wote wa bandari kwa kujua au kwa kutokujua matendo yao wametufikisha tunaoekelekea
Yaani aiseee..kwa kweli kama ingewezekana, ni kuondoa wafanyakazi wote kuanzia menejmenti hadi kibarua( wanaweza bakiza wachache tu) na kuajiri watu wapya wenye uchungu, wasio wabinafsi na wenye tija Kwa nchi kwenye hiyo bandari...bora kuanzia upya kwenye 'clean slate... manake awamu zote ni kama vile zimeshindwa kuondoa tatizo hilo sugu kwa miongo yote.
 
Kwa muda mrefu watanzania wachache walio pewa dhamana ya kuisimamia bandari yetu kuu ya Dar es salaam walikula bila kunawa, mizigo ya watu ilipotea, enzi za uwaziri wa mwakyembe kontena nzima ya vitenge ilidhibitika kupotea kontena ya mama kutoka zambia, waziri alitoa masaa kontena ikapatikana.

Unajiuliza kwa wakati huko na sasa kontena lilinapoteaje lili tembea!!! lakini jibu uaminifu kwa watanzania wenzetu ni sifuri, walisoma kwa gharama za walipa kodi maskini wa nchi hii na return yao kutoka kwale wale waliotumia kodi zao ni kuibia nchi yao.

Leo tunayaona na kuyasikia yanayoendelea waliotufikisha tulipo ni watanzania wenyewe, wakubwa wanafikiri pengine tukiifanya kama wanavyotaka kufanya tutaona tija yake.

Pamoja na tija hiyo tusilidhike na hiyo trilion 26 kwa mwaka. Nilitamani mtafute watu wakuisimamia bandari TPA waadirifu hata sijui mtapata wapi maana na kama kontena linaweza kupotea mbele yao na mifumo kuwepo!!!

Kukosa uaminifu watanzania wenzetu wanatufikisha tunakoelekea.



Kwani hao wanaoamua lazima hii ndo iwe destiny? Basi wabinafsishe Bunge..
 
- Je ile 'ofisi nyeti' ikikosa credibility nayo tuwape wageni milele?
  • Maskini naye mtu hata kama hana kitu.
  • Je unaweza kujisifia ukiwa na 'wanaume' wenzako kuwa kwako kumeendelea ili hali mpaka viunga vya maua wanahudumia wageni? Na umeutangazia umma kuwa 'watoto' wako ni goigoi.
 
Back
Top Bottom