Wanabodi,
Kuna msemo wa Waswahili usemao, " Mwanzo wa ngoma ni lele" na "Dalili ya Mvua ni Mawingu". Tukubali, tukatae, huu ushindi wa kishindo cha Magufuli, cha asilimia 99.9% kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, ni mawingu tuu ya dalili za mvua, lakini mvua yenyewe ni Uchaguzi Mkuu wa 2020, na kama hizi kelele ni kelele za ngoma, then hii ni lele tuu, ngoma yenyewe ni 2020!.
Leo tena nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa", ambapo makala ya leo inajikita kwenye swali
Je Wajua Kuwa Hiki Kishindo cha Ushindi wa CCM, Kushinda kwa Asilimia 99.9% Kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni Mwanzo Tuuz?, Kazi Yenyewe Haswa Kukamilika Uchaguzi Mkuu wa 2020?. Jee Huu Sasa ni Uthibitisho wa Rais Magufuli na CCM Kukubalika Sana na Wananchi?. Kufuatia Kukubalika Huku, Kweli Kuna Haja ya Kufanya Uchaguzi 2020?, or Lets Just Save Time, Money and Resources Kwa Kutokufanya Uchaguzi? Rais Magufuli na Watakao Teuliwa na CCM watangazwe tuu moja kwa moja?
Au kwa vile kufanya uchaguzi ni takwa la kikatiba, kisheria, kikanuni na kiutaratibu, 2020 tufanyie tuu Uchanguzi Mkuu hata kama ni igizo tuu la uchaguzi lakini as of now tayari mshindi ni CCM kwa precedence ya matokeo ya uchaguzi huu wa serikali za mitaa?.
Naomba kwanza nianze kwa kukipongeza Chama Cha Mapinduzi, CCM kwa ushindi wa kishindo cha asilimia 99.9% kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kishindo hiki mimi nakiita ni "Kishindo cha Kasi ya Magufuli" na ni uthibitisho wa
Kukubalika kwa chama cha siasa kwa wananchi na hupimwa kwa idadi ya kura wananchi wanazokipigia chama fulani, na ushindi hutangazwa mwisho wa mashindano, anayetangazwa mshindi, ndie mshindi halali kwa mujibu wa kanuni ya "the end justifies the means", naomba sote tukubaliane CCM ndie mshindi halali regardless uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, mshindi ni mshindi, "the winner takes it all, the loser standing small" hongera sana CCM, Hongera Rais Magufuli, Hongera Watanzania kuikubali sana CCM, kumkubali Rais Magufuli.
Uchaguzi huru na wa haki ndicho kipimo pekee cha kupima kukubalika huku, lakini pale ambapo chama kimepata ushindi wa kishindo kwa asilimia 99.9%, ila ni kwa ushindi wa mezani, watu hawakupiga kura baada ya timu pinzani kuweka mpira kwapani, hivyo aliyebaki anatangazwa mshindi halali kwa kupitia bila kupingwa kwenye uchaguzi huru na wa haki, sasa sijui kama kule kutopiga kura kuchagua nako ndiko kukubalika kwenyewe lakini maadam kwa matokeo ya mwisho mshindi ni CCM, then CCM imekubalika.
Inaendelea...