Kulingana na ushahidi wa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa uliotolewa, Je unadhani maelezo ya Adamoo aliyoandikisha polisi yatapokelewa kama ushahidi..?

Kwa upande wangu baada ya ufuatiliaji wa mwenendo mzima wa shauri hili dogo,Ninaona upande wa utetezi utatoboa.
 
Ushahidi una mikanganyiko
1. Ushahidi unaonesha waliteswa.
Japo shahidi ameonesha makovu ila ajabu amesema yapo mapya na ya zamani mahakama itachagua.

2. Shahidi ameonesha tena kwa kuhojiwa na wakili wa serkali kuwa alisaini pasipo mateso yapo baadae alisema kwenye Re examination kuwa alitishwa na Kingai, na kitendo cha kuwa na pingu ni mateso.

3. Hatari zaidi ni pale shahidi amedai akili yake haiko sawa kwa ajili ya Battle confusion, na wakili wa serkali kuiita kama mental disoder,iliyosabibishwa na utumiaji wa madawa ya kulevya kupita kiasi. Hivyo kuwa wakati akili yake haikumbuki mambo kisawasawa.
Yote kwa Yote HAKI ITENDEKE
 
Unataka wapigane na kichaa mwenye rungu wakiwa mikono tupu?
Hii kesi ndani ya kesi inawaumbueni!
Labda 'mtashinda' kwa kuvuruga kesi tu. Lakini mbele ya jamii mmeshashindwa na mtalegea zaidi.
 
Jeshi limedhalilishwa vya kutosha...
Polisi wameonesha hawajali cha komandoo wala 92KJ wala nani wa jeshini. Wanawasulubu na kuwapoteza kama kawa.
Alafu; mbona trend inaonesha wakitokea mission zao Tazara inawahusu?
 
Hahahahahh
 
Nilichoelewa ... Shadidi alihojiwa (specifically kuhojiwa) bila mateso lakini ali sign maelezo kwa kutishwa/kuteswa .... maelezo aliyoyatoa bila kutishwa yaliandikwa na kutayarisha pasipo kushuhudia
 
Unataka wapigane na kichaa mwenye rungu wakiwa mikono tupu?
Hii kesi ndani ya kesi inawaumbueni!
Labda 'mtashinda' kwa kuvuruga kesi tu. Lakini mbele ya jamii mmeshashindwa na mtalegea zaidi.
Hahaha! Mnapenda sana ushabiki na kuamini hearsay!! Hata mimi naweza kujitokeza na nikasema NIMETESWA SANA ili kutafuta huruma ya Umma! Kuna jambo rahisi duniani kama kutunga na kusema uongo? And kuna watu waongo, wafitini na wazushi zaidi ya wanaojiita wapinzani TZ? BTW siyo wapinzani wa kweli, ni wasaka tonge tu, siku wakitupiwa hilo tonge basi na kelele zote zinaisha
 
Una utaalamu wowote wa Sheria? Kama huna basi kuwa na subira, muda ndiyo utatoa majibu, sidhani kama hapa JF utapata jibu sahihi zaidi ya mihemko ya ki CCM na CDM.
Hapana, mimi si mwanasheria kitaaluma lakini ninazo basics za sheria and more over, ni kuwa, wote tunafuatilia hatua kwa hatua mwenendo wa kesi yote mpaka hatua hii...

Ninachotaka watu waseme ni siyo kutoa hukumu bali kutoa maoni yao kulingana na walichoona kwa macho yao na kusikia wenyewe kwa masikio yao...

Nadhani hii haihitaji uwe mtaalamu wa sheria...
 
Sasa nimekulewa kuwa kumbe wewe ndiyo tatizo maana unatoa maoni yako ukiongozwa na pressure na emotion za itikadi za kisiasa na bila shaka wewe ni mwanaCCM, au siyo..?

Kumbuka, hili suala linawahusu watu na wako mahakamani. Usitoe maoni yako kuhusu kesi na mambo ya kisheria kwa kuwa na mtazamo wa;

".....hawa si wapinzani tu, au waoinzani wenyewe si lolote wala chochote..."

Ukiwa na mtazamo huu, you will absolutely miss the bull na bila shaka utajifunga mwenyewe kujipatia ufahamu wa baadhi ya mambo kupitia jambo hili...
 

Ni wazi kuwa hali hii:

Utesaji wa Dola - Agenda kubwa Uchaguzi ujao

ilimhusu sana mja wake Mola, bwana Adamoo.

Hakuna asiyeyajua hayo.

Tulipo ule mhimili uliojichimbia zaidi huingilia mingine yote kama utakavyo.

Majaji wetu ni katika wale vigogo wasiolipa kodi. Wanufaika wa zile haramu za ule mhimili mrefu.

Ni kwa sababu hizo hatuna furaha na matokeo yoyote ya hapa mahakamani kwa maana inajulikana ukiukwaji mkubwa wa sheria kwenye kupatikana kwa ushahidi huu ni dhahiri.

Hata hivyo kwa mahakama zetu tenganisha uamuzi sahihi kwa mujibu wa sheria na maamuzi ya mahakama zetu.

Bado si mahakama wala jaji wote hawawajibiki kwa uamuzi wowote watakao ona wao kuwa inafaa na kwa sababu yoyote.

Ni makwetu tu ambako huwezi kulalia mlango wazi.
 
PGO haikufuatwa wakati Police wanatekeleza kazi yao
Ushahidi umedhihirisha pasi na shaka kwamba washitakiwa waliteswa kabla ya kusign maelezo yao
Udhalilishaji mkubwa wa haki kwa washtakiwa & kuwaondolea manhood yao (utu)

Mangai hatoboi - ushahidi wake una mashaka makubwa !!
 

Mkuu rejea case ya uhaini miaka ya 80s mashahidi wa serikali wakiwa kina Mabere Marando na kina Dr. Mahiga. Washitakiwa kina Hatty MacGhee, na kina Hans Poppe.

Kulikuwa na mawakili wa utetezi wazuri tu (first class) kama kina Murtaza Lakha na kina Muccaddam.

Ushahidi ulikuwa umepatikana kwa mateso kama hivi hivi. Ushahidi ulipokelewa na kutumika mahakamani dhidi ya watuhumiwa pamoja na mapingamizi kama hivi hivi.

Karibu Tanzania ambako bila katiba mpya mihimili mingine inawajibika kwa ule mmoja uliojichimbia zaidi.

Bila katiba mpya hatupaswi kuwa na matumaini, kushangilia au hata kusikitika kwa uamuzi wowote utakaotolewa.

Hata hapa pamoja na facts zote usishangae historia ikijirudia.
 
Vyema sana...

Observation yako iko vizuri na inaonesha unafuatilia hatua kwa hatua shauri hili...

Hata mimi ndivyo hivyo nionavyo...

More over, ushahidi wa upande Wa utetezi kwa mashahidi wao wote uko very consistent na unapatana vizuri. Na kama kuna variation, basi ni ndogo sana...

Hata shahidi wa leo nwanamke (mke wa Adamoo) amethibitisha hili kuwa kila wanachoeleza ni uhalisia na siyo vitu vya kutunga mahali kisha afundishwe kuja kusema uongo. Hili hata asiyesomea psychology anaweza kujua mara moja....

Hii ni tofauti sana na upande wa washitakiwa katika kesi hii ndogo ktk kesi kubwa yaani POLISI....

Hawa wameonesha dhahiri shahiri kuwa wanafanya shughuli zao kwa kutofuata sheria na kutumia madaraka yao vibaya kunyanyasa watu (RAIA) kwa kuwatengenezea makosa kwa malengo yao mabaya na kisha kufungua kesi za uongo. Huu ni uhujumu uchumi 100%....

Hili linathibitishwa na maelezo ya ushahidi wao kukosa consistency kutoka kwa askari huyu hata kwa yule kwa mambo ya kila siku yahusuyo taratibu za kisheria na kikanuni ktk ku - execute majukumu yao ya kipolisi...

Na kwa sababu ya kutozingatia sheria, kila kitu walichokitenda hawa polisi kuanzia ktk kuanzisha shauri hili, ukamataji wa watuhumiwa, kuwahoji, kuwa - detain, kuwapeleka mahakamani na namna walivyofanya juhudi kubwa kutaka shauri hili lisikilizwe gizani ni ishara kuwa everything is vanity (ubatili mtupu) na kwa hiyo hii inathibitisha kuwa MSINGI WA KESI HII NI UONGO na HILA ZA KUKOMOANA TU isikusukumwa na misukumo ya kisiasa nyuma yake....!

Hivi ndivyo nianavyo Mimi na kama maamuzi yatafanyika kwa mujibu wa sheria na siyo "kwa mujibu wa maelekezo toka juu", basi kesi hii imeshakwisha kufikia mwisho mpaja hatua hii...!!!
 
Kama maamuzi yata andikiwa Ikulu/ Lumumba basi ushahidi wa kubumba wa polisi uta pokelewa. Lakini kama Jaji ana maamuzi yake binafsi, basi hakuna ushahidi utapokelewa.. Na hakuna kesi...
 
Kuweka rekodi sahihi Adamoo ni mshtakiwa namba2 sio 1 na Lingwenya ni mshtakiwa namba 3 sio 2

Mshtakiwa namba 1 ni Bwire
 
Ndiyo brazaj, mimi nakubaliana na wewe kabisa, kuwa hilo linaweza kutokea bila shaka....

Hata ikitokea watu hawa wakifungwa kwa kuonewa tu kwa sababu "wenye mamlaka na nguvu za kiserikali" wameamua hivyo, basi hiyo haitaondoa ukweli kuwa HAWA WATU HAWAKUWA NA HATIA...!!

Lakini kubwa ni hili, lazima tujue na kuzingatia kuwa NYAKATI na MAJIRA zimebadilika sana. Nyakati za kesi hiyo ya uhaini ni tofauti kabisa na nyakati hizi tulizopo hizi...

Nakuhakikishia jambo moja kuwa, kesi hakutakuwa na mashinikizo ya kuamua kunyume cha mwenye haki dhidi ya asiyekuwa na haki hata kama Jaji ni CCM kijani kupita majani yenyewe halisi...

Mazingira yatamlazimisha kusimama upande wa haki. Kama huamini, subiri utashuhudia kwa masikio na macho yako...

HAKUNA KESI HAPA hata mtoto mdogo anajua hili...!!
denoo J dudus
 
Hii ilikua ni lini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…