Kulingana na ushahidi wa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa uliotolewa, Je unadhani maelezo ya Adamoo aliyoandikisha polisi yatapokelewa kama ushahidi..?

Mkuu hii naichukua kama reference ntaangalia Jaji atatoa maamuzi gani sijasoma sheria lakini naona kama iko wazi haki ni ipi na batili ni ipi

Nitashangaa tu iwapo maamuzi ya jaji yatakuwa vinginevyo mana hii nchi hii kuna "inavyotakiwa kuwa na ilivyo" Ni vitu viwili tofaut kabisa.
 
Nitashangaa sana mahakama ikijivua nguo mbele ya umma wa watanzania na serikali ikijivua nguo mbele ya uso wa dunia (mabalozi wa nje wanaohudhuria kesi).

Hii dunia ya leo sio ile ya 1980's.

Ukiangalia mlolongo wa matukio kwenye hii kesi uliotolewa na watuhumiwa pamoja na mke wa mtuhumiwa Lin'gwenya leo, utaona wazi kuna unyama mwingi zaidi waliotendewa watuhumiwa zaidi hata ya kile kilichofikiriwa mwanzo.

Haki za washtakiwa, na haki za binadamu kwa ujumla wake vyote vilikiukwa wakati wa kuwakamata mpaka baada ya kuwakamata, polisi kukiepuka kikombe hiki hata kwa katiba hii tuliyonayo litakuwa ni ajabu la dunia.
 

Mkuu ninakusoma na ningekwambia ni maombi yangu yasiyokoma kwa Mola ikapate kuwa kama ulivyo andika.

Niweke wazi kuwa hakuna asiyeuona ukweli huo uliouandika. Hii ni kutokea Samia, Sirro, ma W.S, Jaji, Kingai, Mahita na hata mtoto mdogo kama ulivyo sema.

Shida iko hapa:

1. Kuna mhimili unaoingilia mingine kwa mujibu wa katiba hii hii,
2. Majaji ni wanufaika wa moja kwa moja kwenye mhimili huu uliojichimbia zaidi,
3. Majaji ni wateuliwa wa moja kwa moja wa mhimili huu mrefu,
4. Majaji hawawajibiki kwa lolote katika hukumu zao.

Zaidi sana ngoma iko hapa:

Utesaji wa Dola - Agenda kubwa Uchaguzi ujao

Usisahau mkuu tunaishi kwenye jamii ambayo apparently lawlessness ndiyo law yenyewe. Vipi kuwa hajawajibishwa mtu hadi leo pamoja na haya kujulikana bayana?

Kutegemea haki kwenye hali kama hizi hakuna tofauti na kusubiria dodo kwenye mnazi!

Ninataka sana kesi hii itupiliwe mbali lakini haipo foolproof system yenye ku guarantee hilo.
 
Baadhi ya vitu ambavyo vinaonesha consistency ya upande wa utetezi;

- Watuhumiwa kupigwa (Lin'gwenya na mwenzake walikiri hilo) na leo mke wa Lin'gwenya kasema alipomtembelea mumewe Segerea alimkuta ana kovu mkononi.

- Watuhumiwa kukosa chakula kwa muda mrefu, wote wawili walikiri, leo mke wa Lin'gwenya kasema alipomuona mume wake Segerea alimkuta amekonda sana na macho yake yameingia ndani.

- Polisi kutofuata sheria wakati wa ukamataji na ku search nyumba ya mtu, wote wawili watuhumiwa hawakujua kama wanakamatwa na polisi, walivamiwa tu, leo mke wa Lin'gwenya kasema hakujua mume wake alipo na simu yake iliita bila kupokelewa, mwishowe haikupatikana kabisa.

- Watuhumiwa kupewa majina bandia ili ndugu zao wasijue walipo, mtuhumiwa namba mbili alikiri hili akasema aliambiwa ataitwa Johnson John, na mke wa Lin'gwenya na wa Bwire leo wamethibitisha walizunguka vituo vyote vikubwa vya polisi Dsm kuwatafuta waume zao bila mafanikio, coz walipewa majina ya uongo.

Upande wa mashtaka wao wanaegemea zaidi vitu vidogo; mfano.

- Usahihi wa tarehe ya tukio, wanasahau kinacho-matter mahakamani ni tukio likiunganishwa na sheria, sio lilifanyika tarehe gani, hapa judge keshawaambia kuhusu hili.

- Usahihi wa mtuhumiwa (mf. kwamba kama mke hakuwepo nyumbani alijuaje waliokagua walikuwa polisi) wakati mke alishasema afisa upepelezi aliacha namba yake nyumbani ili mke akirudi amtafute.
 

Ninakazia:

'"hii nchi hii kuna 'inavyotakiwa kuwa na ilivyo' Ni vitu viwili tofaut kabisa."

Tusilalie mlango wazi bado katiba mpya yenye kushinikiza na kusimamia uhuru kamili wa mihimili hatuna. Si mbaya kufahamu Hangaya asingependa tuwe nayo kabla hajakwiba chaguzi 2024/25.
 
Kimsingi, ukamatwaji wa watuhumiwa toka mwanzo ulilenga kuwakomoa kwa nini wameajiriwa na Mbowe (kiongozi wa upinzani), ndio wakawapachika kesi ya ugaidi ili wajihalalishie kuwaweka ndani muda mrefu (kuwabambika kesi kama kawaida yao).

Mbowe aliposema anaenda Mwanza kwa ajili ya lile kongamano la Katiba Mpya wakaona nae wamkamate ili asitimize lengo lake la kudai Katiba Mpya.

Baada ya hapo, ndio wakamchukua Mbowe wakamuunganisha na wale walinzi wake waliokamatwa na kwa pamoja wakapachikwa kosa la ugaidi, leo hii ndio tunaona hizi sarakasi mahakamani, ni kesi ya kutengeneza hii.
 

Leo kweli ni 2021 lakini tokea 2015 mahakama zetu zimepoteza kujisimamia kwake labda kuliko hata 1980s. Credit nyingi kwake mwendazake 😂😂😂!

Yuko wapi Lijenje. Wako wapi Ben na kina Azory? Haya hayakutokea enzi za 1980s.

Nani alitaka kumshambulia Lissu? Nini kimefanyika kuhusiana na jaribio kwenye maisha ya Lissu?

Mikutano ya kisiasa imepigwa marufuku kinyume cha katiba. Tunaweza kukimbilia mahakamani kupata haki zetu?

Vipi rafu za kwenye uchaguzi wa 2019/20 kulikuwa na possibility ya kupata haki kwa kukimbilia mahakamani?

Bila katiba mpya yenye kuweka mahakikisho thabiti "there can't be joy yet."

Kwa hali ilivyo kufurahia kwa lolote au kuweka matumaini kwenye lolote ni wishful thinking au kama kujilisha upepo tu.
 
Kama maamuzi yata andikiwa Ikulu/ Lumumba basi ushahidi wa kubumba wa polisi uta pokelewa. Lakini kama Jaji ana maamuzi yake binafsi, basi hakuna ushahidi utapokelewa.. Na hakuna kesi...

Nini kinamfunga jaji kuwa na maamuzi yake binafsi? Dhamira yake tu?

Kumbuka tulisikia yule mwingine aliyekataliwa akisemekana kuwa alikuwa pale kwa malengo maalumu.
 
Wewe so hauhitaji hata kuusoma kwa kuwa hautendi kwa kufuatamiongozo, hiyo hivyo hunahaja nao. 😆
 
alieanza kuharibu hii movie ni kingai ... amekamata madawa ya kulevya... haonyeshi ameyathibitisha kwa mkenya mkuu ... kituko zaidi ni watuhumiwa hawajafunguliwa charge ya madawa ... haya madawa ya kulevya kingai aeleze ameyatoa wapi
 
Pale mwishoni siku Mahita alipofanyiwa cross examination na Kibatala.
Mimi ni mbumbu wa sheria hivyo naomba nieleweshwe hili kama kuna mtu anajua sheria. Mshtakiwa anapopelekwa mahakamani na kukataa kuwa maelezo aliyotoa hakutoa kwa hiari bali aliteswa, kwa nini mahakama isikubali moja kwa moja? I mean kama mwenye maelezo anayakana mwenyewe kwa nini anatiliwa shaka? Kwa nini zisitumike njia nyingine tu za kumtia hatiani? Najua ndivyo sheria ilivyo lakini kwangu mimi naona kuna ukakasi na kunatoa loophole kwa polisi kutumia njia ya mateso ili kupata maelezo kutoka kwa mshtakiwa. All in all, watuhumiwa wa kesi kama hii naweza kusema kwa uhakika kabisa ni IMPOSSIBLE kwa polisi wa Tanzania kuwakamata na kuwafikisha mahakamani bila kuwatesa.
 
Wewe so hauhitaji hata kuusoma kwa kuwa hautendi kwa kufuatamiongozo, hiyo hivyo hunahaja nao. 😆
Kwa kutumia uzoefu wa mtaani ni wazi kabisa hii kesi ni ya kutunga. Nilipomsikia rais Samia anasema wana ushahidi nilidhani kuwa wana jambo la maana kumbe siyo. Na laiti polisi wangekuwa na hata ka-ushahidi kidogo kabisa kabisa, hii kesi ingeonyeshwa kwenye TV moja kwa moja.
 
Una utaalamu wowote wa Sheria? Kama huna basi kuwa na subira, muda ndiyo utatoa majibu, sidhani kama hapa JF utapata jibu sahihi zaidi ya mihemko ya ki CCM na CDM.
Wewe unadhan hapa JF wote ni vilaza hakuwa wanasheria, majaj na mahakim na ata wa ufaham wa sheria ambao kwa mujibu wa mtoa mada hawawez kuchangia chochote mpaka mahakam? Au wee ni Mahita nn? Au kingai?
 
Weee mbona ume elezea mikanganyo ya upande wa ushahidi wa washtakiwa, bila kueleza mapungufu ya PGO. Mahita alisemalisema hajui alipoulizwa PGO

Mpaka akasema muheshimiwa Hakim huyu ananionyesha kitu kingine. Hakim akamjibu... Unafikiri mm siijui PGO? Hukuona hayo mapungufu? Kote Kuna shida Ila Mungu atasimama tu
 

Tuendelee kuweka rekodi sahihi pia - mdada wa leo ni mke wa Adamoo.
 
Kila jambo hatua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…