Kumbe Askofu Gwajima anaweza kuanzisha chama cha siasa na kikawa na nguvu kuliko CHADEMA

Huyu ikitokea akahama ccm harafu akahamia chama kingine na kupewa nafasi Kama kiongozi atakuwa na nguvu ya AJABU Sana maana nchi nzima Kila Kona uungwaji mkono ni mkubwa kuliko kawaida,, Japo awe makini wata msumuraizi au kumlowasaraizi au kumwangemberaizi au kumgufuraizi otherwise anatakiwa asome kwa umakini wa hali ya juu Sana alama za nyakati.
 
Hivi unafikili kuanzisha chama na kufika level ya watawala kukiogopa ni kazi nyepesi
 
Ni mweli hata Mimi nimeshangaa sana Siro alivyomtetea Kibwetere wa Tanzania.
Nakumbuka Kule Moshi kuna gaidi wa kidini alimwaga mafuta na kuwashawishi watu kwenda kuyakanyaga kwa spidi kali huku akijua kuwa mafuta yanateleza. Matokeo yake aliua watu zaidi ya 20 na ushee.

Alitoroka na baadae akajipeleka kwenda kujidhamini na kurudi nyumbani kwake . Yani MTU ameua watu 20 kwa mgongo wa dini kama Kibwetere halafu hata mahakamani hakufikishwa ili ushahidi uletwe kuthibitisha kuwa hakuua kwa kukusudia lakini anachukuliwa poa tu kwa sababu in shabiki wa CCM.

Sasa Rais chanjo ni salama ,waziri anasema Chanjo ni salama ,wataalamu na wansayance wanasema chanjo ni salama lakini Gwajima anapinga kwa nguvu zote bila ushahidi wa kitaalam.
Anachanganya watu na kuoyumbisha serikali.

Siro ameonyesha upendeleo wa wazi kwa kada huyu wa CCM alitetumia dini kupinga pinga serikali na nia ya serikali ya kuwakinga watu wake na korona.
Mbowe alikua ana nia tu ya kwenda kwenye kongamano la Kuunga mkono Katiba Mpya iliyoanzishwa kihalali na serikali ya CCM. Lakini akaambiwa kuwa ni Gaidi.

Sasa Gwajima aliyeipinga serikali na Msimamo wa Rais mpaka sasa Siro anamkingia kifua na kusema kuwa hakuna Jinai. Tujiulize wale waliokua wanasali kule Mbeya na Mwanza walifanya Jinai gani kwenye Ibada ?
Je, kumwombea Kiongozi wa Upinzani ni Jinai kubwa kuliko kumpinga Rais kwa sababu ya imani za kidini?

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
😂😂😂😂 Chadema yenye wanachama mil 10 na 7m wanalipa kila mwaka anakazi sana
 
Kikanisa chake kimemshinda ndio chama cha siasa?!
 
Kwa vyama vya upinzani vimeonekana kupigania maslahi ya vyama vyao zaidi kuliko ya wananchi na kwa kuwa vyama vingi vya upizani vimepoteza vibali kwa wananchi kutokana na kupinga maendeleo ya wananchi na kwenda kinyume na misimamo yao na sera zao zilizowapa umaarufu, ikiwa Gwajima atafanya hivyo kuna uwezekano mkubwa akawa ndio mpinzani mkuu.
 
Naunga mkono hoja na wananchi wote tuliokuwa tunamkubali Jpm tutahamia hicho chama, maana Ccm tumeichoka ila hatuoni mbadala wa chama cha kuhamia mpaka sasa
 
Labda atawapata misukule,
 
Askofu Gwajima anaizidi kwa mbali sana Chadema. Hakuna kitu Chadema kwa sasa, Chadema ilikuwa enzi hizo siyo hawa vibaraka wa mabeberu wa sasa na wafanya ugaidi
Hta Hamad Rashid ama Zitto mliwajaza hivi hivi. Leo hii wako wapi!! CHADEMA iangalie tu hivi tayari kna hard core supporters kabla ya kampeni walau wana kura 2m mfukoni!! Hakuna chama kingine cha upinzani kina capital hiyo.

Gwajima maybe ataenda ACT awe mgombea Urais hapo ata mount serious challenge ila linapokuja suala la wabunge na madiwani ataambuliaa viti maybe 5 maximum!! Chama kinahitahi network ya grassroots inachukua miaka 15 kufikia ilipo CHADEMA so umaarufu wa wiki hizi 4 usimpe kichwa. Kumbuka Membe alivyotrend humu mitandaoni ila alipohamia tu ACT kwisha habari.
 
Alichofanikiwa pekee ni KUJIUA NA KUJIFUFUA mwenyewe .......!!
 
Aanzishe chama? Utaratibu wa kuanzisha Chama unafikiri unamalizika kwenye makaratasi?
Haipo na haitawezekana
Akomae muesisi huko huko ampokonye mother uenyekiti! Watanzania wanatafuta mtu jasiri kama yeye!!
 
Niliwaza jana angetema cheche, Kawa mdogo kama piritoni tangu ahojiwe na tume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…