Kumbe hili suala la mikataba ya siri sio Tanzania tu na bandari zetu, huko Kenya raisi anahusishwa na kutaka kutoa Jomo Kenyatta Airport kwa siri!

Kumbe hili suala la mikataba ya siri sio Tanzania tu na bandari zetu, huko Kenya raisi anahusishwa na kutaka kutoa Jomo Kenyatta Airport kwa siri!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Karibu viongozi wote wa Afrika wana tabia moja inayofanana - kujitajirisha binafsi kwa kuingia mikataba ya siri inayoumiza nchi zao, huku wakidanganya umma mikataba hiyo ni kwa faida ya nchi zao. Mtu yeyote mwenye akili atajua kwamba mkataba ambao kweli una nia ya kuinufaisha nchi hauwezi kufanywa uwe wa siri. Utaufanya wazi ili ukusaidie kujinadi kwa watu wako.

Viongozi wa Afrika wengi sana wanapenda kusifiwa. Sasa jiulize, kama kiongozi anafanya mambo kwa manufaa ya nchi yake, pamoja na mikataba, kwa nini afanye iwe siri badala ya kuiweka wazi ili watu wamsifie kuwa kiongozi mzuri, badala ya kutumia pesa nyingi kujifanyia kampeni? Tangu lini mtu anaependa sifa akafanya kitu kizuri kwa ajili ya watu kwa siri?

Na ndivyo ilivyo kwa mikataba mingi inayofanywa hapa Tanzania, hasa nchini ya uongozi wa sasa wa Raisi Samia. Inafanywa kuwa siri kubwa. Na watu hata hawajiulizi; Raisi wetu anapenda sana kusifiwa kuwa anapiga mwingi au apewe maua yake. Sasa kwa nini afanye mambo ambayo ni kwa faida ya Tanzania kwa siri? Kama hii mikataba ni kwa faida ya Tanzania, kwa nini asiiweke peupe ili tumsifie hata zaidi na hata baadhi ya wale wenzetu wajinga wajinga wale waanze kusema tubadilishe Katiba awe raisi kwa vipindi vya miaka kumi kumi? Utafanyaje mambo makubwa mazuri kwa siri ili utumie fedha nyingi kujinadi kwa wapiga kura? Contradiction.

Sasa leo hii, huko Kenya imegundulika kuwa uongozi wa Kenya uliamua kuingia mkataba wa siri wa kumpa mwekezaji toka India achukue airport kwa miaka 30, kwa bei chee kabisa. Mkataba huu ulikuwa wa siri sana kiasi kwamba hata makamu wa Raisi wa Ruto hakushirikishwa, na inaonekana ilikuwa ni dili ya Ruto.

Lakini tofauti na sisi Yombayomba wa Tanzania, wenzetu Wakenya wamekuja juu wanasema hii airport hachukui mtu hapa,piga ua! Natamani tungefanya hivyo kwa ajili ya badnari zetu.


1727767991596.png
 
Umesema, "Badnari zetu zilishakwenda..."?

Kwahiyo,
Chugani inakwenda...?
Vya majini vinadumu...?

Endeleeni tu kuwa wabinafsi na kukaa kwenye comfort zone.....Suluhutani akikamilisha yake, mnatiwa minyororo.
 
Umesema, "Badnari zetu zilishakwenda..."?

Kwahiyo,
Chugani inakwenda...?
Vya majini vinadumu...?

Endeleeni tu kuwa wabinafsi na kukaa kwenye comfort zone.....Suluhutani akikamilisha yake, mnatiwa minyororo.
Tuendelee? Na wewe je?
 
Tuendelee? Na wewe je?
Zama sio zangu tena...enzi zetu, tulitoa mpaka wakimbizi ahahaha.

Usitegemee kupambania maslahi mapana ya nchi na ustawi wake kwa kuwashirikisha waliozidi 35 kwa kizazi hiki, watakurudisha nyuma tu.
  • Wanajua raha ya maisha ya uhuru
  • Washakuwa chawa ili kurahisisha maisha yao
  • Wana watu nyuma yao wanaowategemea.
  • Ngono ndo inapowanogea zaidi, -me kwa vitoto vya y2k, -ke kwa vimario na watumia mkongo.
  • Wameshashika madaraka mbalimbali maeneo yao ya ridhiki.
  • Mifumo imeshawainamisha

Wenye kizazi chenu, pambanieni zama zenu, mkiishia kucheza Playstation na kujazana Kidimbwi na Guest houses kila weekend, mtazeeka kuwa washauri tu kama sisi, na circle itaendelea kujirudia milele.
 
Zama sio zangu tena...enzi zetu, tulitoa mpaka wakimbizi ahahaha.

Usitegemee kupambania maslahi mapana ya nchi na ustawi wake kwa kuwashirikisha waliozidi 35 kwa kizazi hiki, watakurudisha nyuma tu.
  • Wanajua raha ya maisha ya uhuru
  • Washakuwa chawa ili kurahisisha maisha yao
  • Wana watu nyuma yao wanaowategemea.
  • Ngono ndo inapowanogea zaidi, -me kwa vitoto vya y2k, -ke kwa vimario na watumia mkongo.
  • Wameshashika madaraka mbalimbali maeneo yao ya ridhiki.
  • Mifumo imeshawainamisha

Wenye kizazi chenu, pambanieni zama zenu, mkiishia kucheza Playstation na kujazana Kidimbwi na Guest houses kila weekend, mtazeeka kuwa washauri tu kama sisi, na circle itaendelea kujirudia milele.
Nimekuelewa sana. Tatizo letu ni kwamba hawa wenye kizazi kinachohusika, Generation Z, wamekuwa corrupted sana na maisha ya rafiki zao ambao wazazi wao ndio wapo hapo juu, kiasi kwamba wameshaanza kuwaona kuwa mabwana zao wa baadae. Je, unakumbuka wale waliofunga kamba za viatu za watoto wa waliojuu kwa matarajio ya kutupiwa kitu hapo baadae? Na uliona walifanikiwa sivyo?

Sasa hapa kwetu Generation Z iko tayari kuridhika na makombo wanayopata kutoka kwa watoto wa walio juu, na haijihusishi kabisa na maslahi mapana ya nchi. Wao wanachotaka ni nani leo watawa sposor ili waweze kunywa Chivas na Jack Daniels, mambo ya Bandari sijui imefanya nini hilo haliwahusu hata kidogo. Hii sio Kenya, kwa sababu ukienda Kenya, watoto wa walio juu hawa interract na watoto wa walio chini, kiasi kwamba watoto wa walio chini wanaona wazi kwamba wako deprived na benefits fulani na wako tayari kuzipigania. Sio hapa Tanzania. Watoto wetu wakiwa na urafiki na mtoto wa Abdul akamnunulia pegi ya Chivas au kumwahidi siku moja kumpeleka Ikulu mama akiwepo, basi usimwambie kitu kuhusu kuuzwa bandari!
 
Karibu viongozi wote wa Afrika wana tabia moja inayofanana - kujitajirisha binafsi kwa kuingia mikataba ya siri inayoumiza nchi zao, huku wakidanganya umma mikataba hiyo ni kwa faida ya nchi zao. Mtu yeyote mwenye akili atajua kwamba mkataba ambao kweli una nia ya kuinufaisha nchi hauwezi kufanywa uwe wa siri. Utaufanya wazi ili ukusaidie kujinadi kwa watu wako.

Viongozi wa Afrika wengi sana wanapenda kusifiwa. Sasa jiulize, kama kiongozi anafanya mambo kwa manufaa ya nchi yake, pamoja na mikataba, kwa nini afanye iwe siri badala ya kuiweka wazi ili watu wamsifie kuwa kiongozi mzuri, badala ya kutumia pesa nyingi kujifanyia kampeni? Tangu lini mtu anaependa sifa akafanya kitu kizuri kwa ajili ya watu kwa siri?

Na ndivyo ilivyo kwa mikataba mingi inayofanywa hapa Tanzania, hasa nchini ya uongozi wa sasa wa Raisi Samia. Inafanywa kuwa siri kubwa. Na watu hata hawajiulizi; Raisi wetu anapenda sana kusifiwa kuwa anapiga mwingi au apewe maua yake. Sasa kwa nini afanye mambo ambayo ni kwa faida ya Tanzania kwa siri? Kama hii mikataba ni kwa faida ya Tanzania, kwa nini asiiweke peupe ili tumsifie hata zaidi na hata baadhi ya wale wenzetu wajinga wajinga wale waanze kusema tubadilishe Katiba awe raisi kwa vipindi vya miaka kumi kumi? Utafanyaje mambo makubwa mazuri kwa siri ili utumie fedha nyingi kujinadi kwa wapiga kura? Contradiction.

Sasa leo hii, huko Kenya imegundulika kuwa uongozi wa Kenya uliamua kuingia mkataba wa siri wa kumpa mwekezaji toka India achukue airport kwa miaka 30, kwa bei chee kabisa. Mkataba huu ulikuwa wa siri sana kiasi kwamba hata makamu wa Raisi wa Ruto hakushirikishwa, na inaonekana ilikuwa ni dili ya Ruto.

Lakini tofauti na sisi Yombayomba wa Tanzania, wenzetu Wakenya wamekuja juu wanasema hii airport hachukui mtu hapa,piga ua! Natamani tungefanya hivyo kwa ajili ya badnari zetu.


View attachment 3111886
Ila kilichonivutia kwenye huo mkataba wahindi walikuwa wanaweka ela ndefu kuliko ela ambayo sisi tuliambiwa itawekezwa kwenye bandari. Yani ni ela ndefu sana waliokuwa wanaenda kuwekeza.
 
Ila kilichonivutia kwenye huo mkataba wahindi walikuwa wanaweka ela ndefu kuliko ela ambayo sisi tuliambiwa itawekezwa kwenye bandari. Yani ni ela ndefu sana waliokuwa wanaenda kuwekeza.
Lakini bado Wakenya wakaona hakuna maslahi! Wamekuja hapa kwetu na hela fupi, na mradi kama bandari ambao unaingiza hela kuliko hata airport, tunawapokea kwa mikono miwili na ngonjera tunawaimbia! Wananchi wakilalamika tunawaita wapumbavu!
 
Back
Top Bottom