kutokana na mdahalo wa jana nimesikia kua kuna wabunge kumi waligoma kutoka bungeni wakati wabunge wa chadema wakitoka nje ya bunge, yalielezwa na Hamad akijibu hoja ya Mbowe kuwa CUF inaonyesha kutowaunga mkono
jamani kwa nn hili hamlitaki kuliongelea
mjadala huo unaweza kuupata MZALENDO.NET « …Ni wakati wa ukweli na uwazi
Sikweli asemalo Mtu wa pwani ukweli ni kwamba wabunge 10 hawaku ingia kabisa bungeni siku hio na sio waligoma kutoka bungeni
:hungry:
Walikuwa wanaogopa kuvunja kiapo walichokula. Kumbuka walikula kiapo kuilinda katiba ya bongo ambayo ndo imemuweka madarakani rais. Na pia kuvunja ahadi ya kuwatumikia wananchi waliowachagua kuingia madarakani. Waliona bora lawama kuliko fedheha.
- The FACT ni kwamba yote Mh. Hamad aliyosema ambayo sio kweli Mh. Mbowe alijibu, lakini hili hakujibu hiyo ni FACT sihitaji zaidi in that case of the FACT, as a FACT!
William.
lakini hr nadhani sio mtu makini katika kutoa matamshi... Hadithi aliyoitoa kuhusu mazungumzo yake na ndesamburo kuwa chadema ni wakatoliki na cuf waislamu haikupaswa kuongelewa kwenye jukwaa kama lile. Yaani hapo aliharibu pande zote mbili. Ni maneno usiyotegemea kutoka kwa viongozi makini, isipokuwa tu kwa wale wasioweza kuzuia hisia zao.
kutokana na mdahalo wa jana nimesikia kua kuna wabunge kumi waligoma kutoka bungeni wakati wabunge wa chadema wakitoka nje ya bunge, yalielezwa na Hamad akijibu hoja ya Mbowe kuwa CUF inaonyesha kutowaunga mkono
jamani kwa nn hili hamlitaki kuliongelea
mjadala huo unaweza kuupata MZALENDO.NET « …Ni wakati wa ukweli na uwazi
- Hapa sasa mkuu ndio kabisaa unakubaliana na hoja yangu kwamba mambo ya haraka haraka kabla ya wakati ndio yametufikisha hapa tulipo, ukweli ni kwamba matokeo ya uchaguzi yanaonyesha exactly wananchi walichosema then kwamba bado wanataka chama kimoja, Mwalimu alitakiwa kuwasikiliza wananchi maana ndio Demokrasia yaani wananchi kuamua wanachotaka, kuwalazimisha wasichotaka ndio matokeo yake haya ndugu yangu, wananchi bado wanachagua CCM tu!
- Maana yake ni kwamba tulifkiri kwamba vyama vingi ndio jawabu, sasa sio siri kwamba hatukuwa tayari, naona imeanza ya katiba sasa utabadili vipi katiba na majority ya CCM, ndio ninasema tusidanganyane jamani, mambo badooo kidogo tusitafute njia za mkato mkato ndio zimelifikisha hili taifa tulipo sasa, yaani kwenye dead end!
William.
- Kuongezeka kwa Demokrasia hakuwezi kulazimishwa kwa nguvu na kubadili katiba under our current political situation ndio ndoto zenyewe hasa, maana utakua unabadili katiba under expense ya CCM na wananchi walioichagua kutawala, siamini kwamba hao walioandika kuhusu Demokrasia ndicho walichosema!
- Nimetoa mfano mdogo sana, eti ili NEC iwe fair itachaguliwa na nani under hiyo katiba mpya ya Chadema?
William.
Thanks kwa taarifa, mbona hata vyombo vya habari havijatamka juu ya hilo. Tupatie majina yao tuwajue "MATRAITORS".
JAMANI ujinga huu haujaanzia hapo tu, lazima tufuatilie tujue tabia zao toka utotoni na hata walipokuwa shuleni walikuwa ni watu wa aina gani.
hili ni funzo tunapochagua viongozi tusisome CV zao tu, maana CV za utotoni huwa hawaziweki.
Wengine unakuta walikuwa ni kina "TOTO TUNDU" waioambilika.
Wengine "TOTO JOGA" likigomwa kidogo tu Kiliooooo hadi majirani wasikie
Wengine " TOTO DEKA" kila kitu ng'eee ng'eee mama mie nataka ileee, mmm hii sitaki mama nataka ileeee!
wengine "TOTO JIZI" mama na baba wakiondoka nyumbani kazi kupekua masanduku au kuramba sukari.
sasa tusikurupuke kuchagua viongozi kwa kuangalia CV zao za masomo tu haya ndio matokeo yake.
kumbuka hata mashuleni tulipokuwa tukisoma, ukiwekwa msimamo fulani unakuwa wengine wanasepa haoooo huwaoni, au wale wanafunzi wa kujipendekeza, yaani likimwona teacher na mkoba, utaona hilo mbio kwenda mkumpokea, "shikamoo mwalimu".
VIJITABIA ni Kadhia kubwa inayotukabili ktk viongozi wetu wengi maana hawajaviacha vijitabia hivyo hadi sasa.
- The FACT ni kwamba yote Mh. Hamad aliyosema ambayo sio kweli Mh. Mbowe alijibu, lakini hili hakujibu hiyo ni FACT sihitaji zaidi in that case of the FACT, as a FACT!
William.
Mkuu Willy,Mheshimiwa Willima, Heshima sana,
Kwanza napenda kukupongeza kuwa kila mara wewe huleta hoja zinazojadilika na kuzungumzika humu jf. Leo umenichosa na mtazamo wako hasi juu ya suala la mabadiliko ya katiba na hata mfumo mzima wa NEC. Nadhani haya ni matokeo ya kutoshiriki siasa za nyumbani moja kwa moja na kuona matatizo yanayotuzunguka kama taifa.
Wakati huu tusipoziba ufa ujuwe kwa hakika tutajenga ukuta na utakuwa huko ulipo ukitoa ushauri na maoni kwenye mtandao kama unavyofanya leo. Ziko sababu za kutosha za katiba yetu kutazamwa upya kabisa
1. Suala la Muungano: Mfumo wa sasa hauturidhishi watanzania tlio wengi, na Kataba haiko clear kuhusu jambo hili, leo Zanzibar wana Makamu wa rais wawili ambao hawapo katika katiba yetu ya Jamhuri kwa sababu tu ya mfumo wa Zimamoto, Uwiwano wa uongozi na mzigo mkubwa unaobebwa na raslimali za bara kuendesha Zanzibar ni moja ya Changamoto kubwa.
2. Upatikanaji wa tume ya uchaguzi na namna inavyofanya kazi; Uchaguzi huu tume bila aibu inawaambia watanzania matokeo ya kawe na Ubungo yamechelewa kutangazwa kwa sababu ya matatizo ya miundombinu ya usafiri huku ikiwa tayari imetangaza matokeo ya Ngorongoro, Hivi Will huko US ndivyo mnavyofanya kazi kweli? Tume inasubiri watu wapigwe mabomu Mwanza ndiyo itangaze matokeo alafu unaipigia makofi Willy? Uko wapi uwiano wa Demokrasia unaouzungumzi! Alafu hakuna sheria ya kuwawajibisha hawa watu kisha unasema katiba inatosha iko sawa!! Ahaaa mzee think twice hapo, Tumeona katika kampeni hizi wakuu wa wilaya wakisoma taarifa za kazi kwa RizI ili mtoto asiharibu unga kwa baba, nguvu nyingi za serikali zimetumika kwenye kampeni kubeba chama tawala kwa sababu ya ubovu wa katiba, Hakuna mwenye chuki na RZ1 mbona nyie hatukuwaona mkitumia nafasi za wazee wenu ku propage siasa?? Rais ana vyeo vyingi mno vya kuteua watu na hivyo wanalazima kutumika kwa namna yoyote ili walinde nafasi zao alafu unasema hatutaki katiba itakayopunguza nguvu ya Rais, Bunge liliazimia mambo mengi baada ya Saga ya richmond, kwa sababu ya katiba mbovu hayakuenda popote maan na hiari ya Mkulu kuyafanyia kazi au kuyashiti, Hii ni aibu Willy nchi inahitaji katiba kabla kina Kayumba hawajachoka, watauana vibaya watakapochoshwa na mfumo unaoongeza mzigo wa umaskini vichwani mwao na kwa kuwa hutakuwepo utafuatilia kwenye Luninga na mtandao huku ukishaa. Mzee nchi inahitaji katiba iweke mambo sawa.
Mimi sikupiga kura mwaka huu, nina sababu nyingi za hovyo hovyo tu, moja ni kuchoshwa na mfumo mbovu usio na matumaini ya kumkomboa mtanzania, huko US manesi na madaktari ni moja kati ya makundi yanayolipwa vizuri hapa kwetu malipo mazuri yako kwenye siasa (Consumer unawalipa vizuri kuliko wanasayansi producer) Alafu Willy bado hutaki katiba eti tukuwe, hatuwezi kukuwa chini ya mfumo mbovu huu tuliionao ila tutadidimia
Mzee nina mengi lakini ngoja niache tu. nCHI INAHITAJI MABADILIKO YA KATIBA KABLA AKINA KAYUMBA WA MANZESE, BUGARIKA, MABATINI, HAWAJACHOSHWA NA HUU UFUKARA WA KUPINDUKIA
- Mkuu heshima yako sana, sikatai kwamba katiba yetu ina mapungufu ni kweli sana isipokuwa tatizo langu ni how to go about kuirekebisha kwa maudhui ya wananchi wote, wengi mnaolilia kubadilishwa mnaonekana kuwa na hisia kali sana bila kujali POLITICAL FACTS on the ground, hamuwajali kabisa wananchi wengi walioichagua CCM kushika power kwenye huu uchaguzi. Mnaonekana kuamini sana kwamba ni nyinyi tu Chadema wenye wabunge 46 ndio wenye mandate ya wananchi kuhusu the political future of our nation.
- Mnakosea sana, ushauri wowote wa kubadili katiba lazima uwajali CCM kwanza kwa sababu wananchi ndio wamewachagua for the last 50 years, nimesema na ninarudia kwamba Demokrasia, inataka wananchi wazungumze kupitia kwenye kura, kama kweli unaamini in Demokrasia then utaelewa point yangu kwamba ni vigumu sana kuibadilisha katiba under political system ya CCM wabunge 270 Vs Chadema wabunge 46, it is simply impossible. Otherwise inaonekana mnashauri tuvunje katiba, yaani tutumie njia za mkato kuirekebisha kwa ku-overpass katiba inayodai 2/3 ya wabunge kuirekebisha kikatiba,
- Kwa maneno mengine tuvunje katiba kwa ajili ya kuirekebisha katiba, ili wabunge wa upinzani 46 wawe na nguvu sawa na wabunge 270 wa chama tawala, hivi mkuu huoni kwamba itakua the joke of the century! Ninawaulizeni swali dogo sana, under your new proposal ya katiba mpya ili NEC iwe fair inatakiwa kuchaguliwa na nani?
William
Point of Correction, Mimi si mwanachama wa CDM, Mimi ni mwanachama wwa ccm hai anayelipa ada na michango yote ya chama. Kwa hiyo kudhani kuwa wanaotaka mabadiliko ya Katiba ni CDM tu hili kosa kubwa sana unalofanya.
Unapoangalia mwenendo wa siasa ya nchi ni muhimu kuwa makini zaidi kwenye maslahi wa nchi kuliko maslahi ya ccm, ni kweli CDM ina wabunge 48 tu lakini unatakiwa ukumbuke kuwa CDM wana madiwani 600 tena kutoka miji mikubwa yenye population kubwa ya wapiga kura wa nchi yetu. Sasa Jiji la Mwanza, nusu ya Arusha, Mbeya, Iringa, Moshi zote ziko mikononi mwa wapinzani, hata KAWE iko mmikononi mwa wapinzani. Kama ccm itaendelea kutumia mawazo yako hayo ya kupinga kila kitu kwa kuwa tu hakikuanzishwa na ccm nchi yetu itazama katika dimbwi baya sana.
NARUDIA TENA NI VEMA TUANGALIE SUALA LA KATIBA NA KUREKEBISHA MAPUNGUFU MENGI YALIYOMO KABLA KINA KAYUMBA HAWAJACHOKA, NCHI HII HAITAKALIKA. Majaji wawili Kisanga Nyarari wote kwenye tume zao zilizowafikia wananchi zilipendekeza mabadiliko ya katiba sasa sijui unazungumzia wananchi gani tena Willy,
Nawasilisha
Lakini HR nadhani sio mtu makini katika kutoa matamshi... Hadithi aliyoitoa kuhusu mazungumzo yake na Ndesamburo kuwa Chadema ni wakatoliki na CUF waislamu haikupaswa kuongelewa kwenye jukwaa kama lile. Yaani hapo aliharibu pande zote mbili. Ni maneno usiyotegemea kutoka kwa viongozi makini, isipokuwa tu kwa wale wasioweza kuzuia hisia zao.