Kumbe kuna watu wana PhD halafu wanalipwa laki 5?

Kumbe kuna watu wana PhD halafu wanalipwa laki 5?

kiufupi jamaa hajui kwanini alisoma ni ajira tu ndo ilimkaa kichwani na hayo ndo madhara ya kusoma ili uajiriwe....unapoteza muda pesa alafu eventually unalipwa laki tano kisha unakufa....ipi faida ya kuwa na PhD sasa....
Ni laana
 
kiufupi jamaa hajui kwanini alisoma ni ajira tu ndo ilimkaa kichwani na hayo ndo madhara ya kusoma ili uajiriwe....unapoteza muda pesa alafu eventually unalipwa laki tano kisha unakufa....ipi faida ya kuwa na PhD sasa....
[emoji2][emoji2][emoji2]Kuna ambaye anasoma ili akalime mkuu? Si kila mtu anasoma aajiriwe
 
[emoji2][emoji2][emoji2]Kuna ambaye anasoma ili akalime mkuu? Si kila mtu anasoma aajiriwe
Nisamehe mkuu kwa nnachoandika. Comment yako hapo juu inaendana sana na hali ilivyo sasa au kuanzia 2008 mpaka sasa, elimu imekua njia ya kuchangamsha akili ili upate maarifa ya kuzalisha kulingana na ulichofundishwa shule. Sasa wale wa 2007 mpaka huko chini wengi wetu tumekuzwa na wazazi ambao either walikua wanaamini katika elimu ndo njia ya kupata kazi na kufanikiwa ki maisha or walikua huru kwa watoto wao na kuwasapoti. Wengi tumekuzwa na hizi wa wazazi wanaoamini ktk Elimu mpaka unafanikiwa na mifano ilikuwepo kipindi hiko na hili likatufanya sie watoto tuamini ktk nikipata tu diploma, degree nabkundelea basi nimemaliza, kumbe ni tofauti na mazingira yanavyotaka. Sio wote Elimu inawasaidia, kuna msemo huku mtaan kwetu kwamba huyu nae alienda shule kujua kuandika na kusoma tu, alaf huyo jamaa au dada ana master yake. Ndo pakujiuliza hivi Elimu inatakiwa ianzie wapi hasa ili tuweze kwenda sawa na kasi ya maendeleo???
 
Vyeo kama hivyo vina marupurupu mangi.. pia huko ccm ilikua geresha mara nyingi watu kama hao wanakua ni wa TISS.
 
Huyu mtu kama ni kweli yupo basi kichwa chake hakipo sawa au ni uzushi au atakuwa amepata hiyo Ph.D nchi kama India au China, vile vyuo vidogo vidogo. Itakuwa alikuwa akiomba kazi maeneo mbali mbali wanatilia mashaka elimu yake vyuo alivyosoma.

Dhumuni kuu la kusoma Ph.D nini? Either uwe mtafiti au mwalimu wa chuo kikuu. Sasa kazi zote hizi hulipa mishahara zaidi ya $1,000 Afrika mashariki hata Tanzania ikiwemo. Labda kama alikuwa anasoma bora liende bila kujua akimaliza kusoma atafanya nn, mwisho wa siku anakuja kufanya kazi hahitaji hata kuwa msomi kitaaluma.

Mshahara wa Lecturer (Mhadhiri) vyuo vya umma kama chuo kikuu cha Dar es Salaam mwenye elimu ya uzamivu (Doctor of Philosophy, Ph.D) - Tshs. 3.2 M ~ 3.5 M, na kila siku vyuo vya umma vinahitaji waalimu wenye Ph.D na vigezo vyao sio vigumu. Mf. Udsm wanataka undergraduate & Masters uwe na GPA ya 4.0+ na kwa Ph.D, Pass.
 
Gharama ya Masters tu bila 7M hutoboi, sasa PHD kwa vyuo vya bongo si chini ya 13M. Sasa mshahara upewe 500k dah inatia huzuni ukiona hivyo ujue ndo bomu sasa.
 
Wakuu, recently nilisikia Mkulu akijisifu kuwa Baharia ambaye ni PhD holder akila 500,000 kwa mwezi na kwamba huyu Daktari alikua "vere komfotabo"!

Kwa sasa kwa Tz gharama za Masters si chini ya million tatu na PhD si chini ya 10m, sasa kama unafanya investment ya more than 15m pamoja na miaka uliyosoma yote kisha unalipwa laki tano na uko poa tu Basi either wewe ni tatizo au hio PhD yako ni ya kubumba.

Soma ili uweze kujitegemea na uweze kuwasaidia na wengine, kwa laki tano kamwe narudia kamwe utakua umeharibu muda wako na kuwapotezea wengine hizo bahati za kusoma na kuw productive, huwezi kuwa productive kwa salary ya laki tano.

Watu kama hawa unakuta hawawezi kuandika hata two pages Concept Note, narudia either yeye au hio degree yake ina matatizo.

Shukrani
Kusifiwa kwa kufanya jambo la kijinga ni dharau
 
Back
Top Bottom