Kumbe mafuta nayotumia kwenye gari ni sawa na ningekua napanda bodaboda!!

Kumbe mafuta nayotumia kwenye gari ni sawa na ningekua napanda bodaboda!!



Huyu naye hayajui magari, Naona anatafuta Ngo'ombe wa kumkamata amuuzie gari yake.

Hakuna 1kr ya piston 4

Hakuna 1kr ya Cc1290

Hiyo aliyopost hapo ni Passo ya piston 3

Na engine yake ni 1kr na ina Cc990

Passo ya Piston 4 muonekano wa engine hauko hivo.

Passo ya piston 4 ambayo ina engine K3-VE muonekano wake ni huu...👇🏾👇🏾

images (47).jpeg




Na inakuwa na Cc1290.
 
Usafiri wa bidaboda kwa dar umekuwa usafiri ghali sana especially peak hours , kweli ukipiga hesabu vizuri gari binafsi inakuwa ni salama na rahisi .
Jana kuna boda kadhaa wameni ' quote ' shs 7000 one way kutoka tabata hadi uhasibu mataa,hii ni route ambayo hata nusu lita haiishi kwa babywalker
 
Nchi za wenzetu gari ni part and parcel ya basic needs, yani kununua gari hakumpi mtu stress kama sisi huku.

Wabongo tunanunua gari sababu ya ufahari tuu.

Na kwa umbumbumbu wetu wabongo tukiona mtu kanunua gari basi ndo tunafanya kama kipimo cha maendeleo kumbe sio kweli.
 
Kwahiyo gharama za gari ni mafuta tu? Mwaka mzima wa kumiliki passo nilijua ushamba ushakutoka kumbe bado [emoji1][emoji1]
Gharama kubwa kwenye gari ni maintanace! Service za kawaida haziumizi sana pesa
Unaweza kupunguza matengenezo mengi kwa kuwa makini na uendeshaji wako , kuna wanaotumia magari kwa miaka mingi na hisikii kama kabadilisha ball joints au bush yoyote ,
 
Gharama kubwa kwenye gari ni maintanace! Service za kawaida haziumizi sana pesa
Unaweza kupunguza matengenezo mengi kwa kuwa makini na uendeshaji wako , kuna wanaotumia magari kwa miaka mingi na hisikii kama kabadilisha ball joints au bush yoyote ,
Ni kweli kabisa mkuu
 
Nchi za wenzetu gari ni part and parcel ya basic needs, yani kununua gari hakumpi mtu stress kama sisi huku.

Wabongo tunanunua gari sababu ya ufahari tuu.

Na kwa umbumbumbu wetu wabongo tukiona mtu kanunua gari basi ndo tunafanya kama kipimo cha maendeleo kumbe sio kweli.
Kipimo cha maendeleo ni kulala nyumba za nyasi Mkuu ...Maendeleo ya watu au Nchi ni wananchi wake kutumia vitu bora ambavyo vinawarahisishia utendaji kazi na wanakula lishe bora na pia hawaumizi kichwa saana kupata mahitaji muhimu...gari ni kama simu tuu ni vile tumechelewa ndio maana tumeweka kwenye kundi la starehe..
 
Umetimia mwaka sasa tangu ninunue gari yangu hii ya kwanza. Babywoka safi inanitosha, 1290cc engine 1KR.

Tangu ninunue hii babywoka nilikua sijawahi kukaa na kufanya 'cost-analysis' upande wa mafuta nayotumia.

Zaidi nilikua nahisi kama gari 'inanifilisi' vile navokua natoa 20,000 au 30,000 kwa mkupuo napoingia "sheli".

October 2, 2021 Jmosi saa mbili usiku niliweka mafuta ya 50,000.

Sio kawaida yangu maana hata jamaa wa pale Petrol Station (GUDAL) napo-endaga kuweka alinitania "naona leo umeamua kaka..."

Kabla ya kuweka nilisoma ODOMETER nikaweka record kwenye 'sticky note' ya simu.

Basi nikaendelea na mizunguko yangu weeee... Mwenge, Sinza, Kariakoo mara chache, Mbagala Chamazi, Bunju kidogo, Bahari beach kule nakadhalika.

By the way, kwa sasa nakaa pande za Makongo. Office location ipo pale Shekilango Ubungo Business Park (kule ndan kwenye ma-godown yale). So you can imagine my daily routes.

October 25 2021, Jtatu saa mbili usiku 'gauge' ya mafuta ikarudi ilipokua tarehe 2. Nikachukua kalamu na karatasi.

Katikati hapo nilishaongeza mafuta ya 15,000 halafu 20,000. Sio kwamba yalikua yameisha. Nilipata safari ambazo hazikuwa kwenye 'monitoring process'.

Kwahiyo basi;

Mafuta nilinunua jumla 85,000/=
Bei kwa lita: 2,427/=
Jumla lita: 35 ltrs
No. of days: 23 days
Total distance covered: 344 km

Average Consumption:
Distance covered per litre: 344 km ÷ 35 litres = 9.8km/ltr.

Cost per day: 85,000 ÷ 23 days = 3,700/= per day.

Tuseme roughly kwa siku natumia shilingi 4,000 kama gharama za mafuta (asante babywoka yangu).

Hii ni almost sawa na ningekua natumia bodaboda (kwenda 2,000 kurudi 2,000). Na hapo nime-assume ni strictly route ya maskani-ofisini-maskani.

Kumbe hamna tofauti kiviiile.
Tena naona afadhali kwangu, maana naweza kwenda popote, muda wowote.
Naweza kumpa mtu/watu lift. Sinyeshewi mvua. Sipigwi jua.

Hata demu wangu nahisi nilimpata sababu ya hii babywoka. Japokua amenipiga kibuti.

View attachment 1987573
Hii toy itakuwa ni 4wd maana inakula sana wese.
 
Back
Top Bottom