Kumbe Rais Samia alisema ukweli kuhusu kesi ya Mbowe. Watanzania tutembee kifua mbele ikibidi vua hata shati tunaenda vizuri

Kumbe Rais Samia alisema ukweli kuhusu kesi ya Mbowe. Watanzania tutembee kifua mbele ikibidi vua hata shati tunaenda vizuri

Wewe unajua zaidi kuliko gaidi mbowe ambae Kila chaguzi ameshiriki period [emoji23][emoji1787]
Ugaidi ni kuwabambikia watu kesi kwa uonevu hivyo magaidi unao huko huko kwako
 
Ugaidi ni kitendo cha kuwakamata watu wasio na hatia kisha kwenda kuwafunga pingu mikono miguu saa 24 kuwalazimisha wakubali ugaidi hewa kwa kuwapiga kuwatesa huku Polisiccm wakidhalilisha jwtz zaidi pasipo kujua wakiamini mahita na kingai baadae wangepewa vyeo vikubwa sasa wanaumbuka baada ya mungu kukataa uonevu wao wote
 
Mkuu kuichafua serikali kwa propaganda mfu namna hii ni kupoteza muda wako bure. Hebu fikiria kuna watu walikuja na propaganda kabambe za ufisadi ili kuwachafua viongozi wa serikali na wa chama kilichopo madarakan kama vile kina Lowasa, Kinana nk lkn uchaguzi ulipofika 2010, 2015 na 2020 wananchi walitumia haki yao ya kupiga kura kuwaadhibu watengeneza propaganda hao bila huruma.

Hata zile propaganda za kumchafua hayati Magufuli kuwa ni dikteta, sijui anakandamiza demokrasia nk hazikusaidia upinzani kuingia ikulu 2020.. yan ilikuwa ni sawa na kujaza pipa kwa kisoda. So kama unaishi, unasomesha na hata kwenda msalani kwa malipo ya propaganda za namna hii. Nakushauri ndugu yang utafute kibarua kingine cha kukusaidka kupata riziki ingine ya halali bila kuchafua watu.
Wananchi gani waliadhibu wapinzani? Je ni wale walioiba masanduku ya kura kwenda kujaza kura za wexi wenzao!!?
Au ni ule wizi wa mchakato wa kupiga kura kwa polisi na TISS kubeba maboksi ya kura 2020? Ni lini maamuzi ya wananchi yaliheshimiwa? Saidia hapa ili tupate mwanga!!
 
Natafta thread ya kesi ya leo ila nme kosa au bado wana habari hawaja anza
 
Wewe unanifahamisha mimi kwamba "miaka yote uchaguzi huwa wa haki na huru...."? Tena unadai kabisa "najua"?
Sasa kama nikiuita huu ni upumbavu utaona kuwa nakuonea kwa kukupa sifa hiyo? Wewe ni nani hadi unipangie ninachojua?

Kiufupi ni kwamba huna uelewa, au hutaki kutumia akili yako kuelewa mambo yaliyo nje ya yale uliyokariri kuyakubali hata kama ni mambo ambayo yapo wazi kabisa kuyaelewa.
Huyu ni wale Misukule wanaopewa bando kutetea upuuzi, humjui?
 
Kwa sababu ya roho yake mbaya na uchu wa madaraka 2025 hajali kitu chochote she must be called out ni mbaya muuaji tu kama aliyemtangulia angekuwa na hofu asingesema kwabashasha kwamba mbowe ni gaidi na wenzake walifungwa
Wakati unawish hayo yatokee ,je umejaribu kuwaza ni nani atakayemrithi? Maombi mengine ni vema ukayahirisha.
 
Raisi alizungumza kuhusu kesi ya Mbowe na akasema kwamba Mbowe mwenyewe alikuwa anafahamu uwepo wa kesi hiyo mahakamani..

Pia raisi hakuzungumzia kuhusu hukumu ya kesi ya Mbowe kwani anafahamu fika kwamba kesi hiyo bado ipo mahakamani na ni mahakama pekee inayoweza kuamua kuhusu kesi hiyo.

Hii ya kusema kuwa raisi alisema Mbowe kaisha hukumiwa kwa ugaidi ni uongo mtupu ambao hauwezi kuachwa hivi hivi. Kuhusu haki ya uchaguzi bila shaka unajua kwamba miaka yote uchaguzi huwa wa haki na huru ndio maana kina Mbowe, Lisu, Lema nk waliweza kushinda chaguzi mbali mbali na kutangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi.

Ila kwa vile miaka yote walioshinda hakuna cha maana walichofanya katika majimbo yao zaidi ya kujineemesha wao na watoto wao ndio maana mwaka 2020 wananchi wakaamua kuwagalagaza kwa kuwanyima kura, na dalili za unyimwaji wa kura kutoka kwa wananchi zilianza kuonekana pale mwenyekiti wa Chadema na mbunge wa Hai ndugu Freeman Mbowe alipotupiwa chupa za maji na kuzomewa na wapiga kura wake mwenyewe kutokana na kuchoshwa na ulaghai wa mwanasiasa huyo na genge lake.
Nimesoma nikaishia kukudharau tuu kuwa maneno yako mengi lakini ujinga mtupu
 
Niwakumbushe tuu kidogo Rais akihojiwa na shirika la habari la Uingereza BBC aliitamkia Dunia na Tanzania kuwa Mbowe ni gaidi alikimbilia kujificha Kenya na wenzie alio kuwa akishilikiana nao walisha hukumiwa alibakia Mbowe tuu kuhukumiwa.

Watanzania wengi tulishitushwa na taarifa hiyo na kumshutumu Rais kuwa anasema uongo. Kwa kuwa hapakuwa na kesi yoyote ya Ugaidi Mahakamani iliyo hukumiwa Wala mtuhumiwa yeyote wa Ugaidi aliye hukumiwa zaidi ya wale Mashekhe wa Uamsho kutolewa Mahabusu.

Lakini ushahidi unao tolewa Mahakamani na Washitakiwa ambao pia ni Mashahidi upande wa Jamhuri unatuoonesha wazi kuwa Kuna Watuhumiwa wawili tayari wamesha hukumiwa. Na hukumu yao ilitekelezwa kuteswa na baadae kutupwa.

Mashadi wanasema walimuona Moses Lijenje na Denisi Urio wakiteswa na polisi na Kisha polisi wakawaeleza mwenzao Moses Lijenje wamemtupa baada ya kumtesa.Kwamba Moses Lijenje ametupwa kaburini au baharini hatujui ila uhakika ni kwamba wametupwa.

Hatuwezi kutilishaka maelezo ya Washitakiwa kuwa Kuna wenzao wamesha uawa na polisi kwa kuwa maelezo yao yanafanana na maelezo ya Rais aliyoyasema akihojiwa na BBC kuwa Kuna Watuhumiwa tayari wamesha hukumiwa alibakia Mbowe tuu.

Kuhusu CCM kuua raia hilo halina shaka ushahidi ndio huu Rais ameusema wazi wazi na Watuhumiwa pia wamekiri wenzao wameuwa. Pia aliyekuwa Katibu mkuu CCM Bashiru Ally alikiri hadharani akisema CCM tunatumia Dora kubakia Madarakani

Sio hivyo tuu hata kiongozi wa umoja wa vijana CCM ambaye Sasa amepewa cheo Cha Ukuu wa Wilaya Kheri James eti ndio mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya alisema walimkosa kosa Tundu Lissu kumuua kwa Risasi ila kwa Sasa watatumia sumu kumuua.

Sio hivyo tuu Makamu mwenyekiti wa CCM Philpi Mangula alinusurika kuuwa akiwa ktk kikao na Wana CCM wenzake kwa kupewa sumu. Polisi walisema wanawatafuta walio husika lakini mpka Sasa hakuna mtuhumiwa hata mmoja ili hali walio hudhuria kikao hicho kilicho ongozwa na mwenyekiti wao wanajulikana

Tunawakumbusha CCM msije sema hatukuwaambia baadae. Kesi za jinai hazina muda hata ipite miaka 30 zitaibuliwa hukumu yenu ipo pale pale.
Endeleeni kutuua raia tuu Kama kuku mwenzenu Albashiri Sasa yupo mikono salama Sudani imekubali akabidhiwe I C C
akajibu mauji aliyo yafanya.
CCM oyeeeee
Rais safiiiii
Kingai oyeeee
Mahita juuu
JWTZ oyeee
Polisi safiiiiii!!
Siro ngangariiii!!

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Mkuu ,hatima ya CCM ni mbaya mno, MUNGU kaniambia CCM haitaachia madaraka kwa hiari hadi mapinduzi ya kijeshi yafanyike,na hilo jambo lipo karibuni sana kutokea.[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji16][emoji16][emoji16], CCM go to[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Kinachosikitisha zaidi ni kwa nini chombo hiki kikubwa kabisa cha ulinzi na usalama wa nchi yetu kimeachwa bila uzio? yaani JWTZ Commando's ama ma Luteni wajeshi wanatekwa na ktenswa namna hii bila JWTZ kutoa kauli.

Ingeleta faraja kama jeshi lenyewe liwe na mechanism yake ya kujichunguza badala ya kuwatoa baadhi ya wanajeshi wao ili wakateswe na kudhalilishwa, wapi heshima ya JWTZ - sasa hatujui yawezekana Komandoo Moses hayupo duniani.

Wapi Komandoo Moses?

1633345130470.jpeg
 
Wananchi gani waliadhibu wapinzani? Je ni wale walioiba masanduku ya kura kwenda kujaza kura za wexi wenzao!!?
Au ni ule wizi wa mchakato wa kupiga kura kwa polisi na TISS kubeba maboksi ya kura 2020? Ni lini maamuzi ya wananchi yaliheshimiwa? Saidia hapa ili tupate mwanga!!
Mkuu bila shaka hawa ndio walikulisha matango pori kama walivyolishwa wenzako enzi za Lowasa na baadae 2015 kukiri wenyewe katika kampeni zao kuwa yale waliyokuwa wanaongea kuhusu Lowasa yalikuwa matango pori. Hata haya matango ya sanduku za kura siku mmoja wao kati ya Lisu, Mnyika au yoyote akijitoa chamani ataongea ukweli kuwa madai ya kuiba masanduku ya kura sio ya kweli. Inahitaji mtu ukose hata elimu ya chekechea ndo uwaamini tena hawa jamaa.

images (7).jpeg


images (12).jpeg


images (10).jpeg
 
Hivi Mama snasubiri nini kuunda tume ya Majaji na Viongozi wa dini ili wazunguke Magereza yote kubaini kama kweli kuna mahabusu wa kesi za kisiasa za kubambikwa kesi tena baada ya watuhumiwa kuteswa na kuumizwa vibaya. Tume ikithibitisha hayo basi ,Siro awajibike na kuwekwa pembeni haraka sana. Lakini pia Kingai na wote waliofanya utesaji wachukuliwe hatua Kali. Kingai alikua anatafuta nini kwa kutumia cheo chake kinyume cha sheria ?
Je, aligongwa au aliahidiwa nini!!!

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
Watanzania wengi wameanza kuwalaani kingai na mahita na Albadiri zinaandaliwa kuwasomea wale wote wanaoshiriki vitendo haramu vya hovyo kuwabambikia kesi wapinzani kuwakamata watu wasio na hatia kuwafunga pingu mikono miguu kuwatesa kuwalazimisha wakubali ugaidi ambao hawana haupo na haujawahi kuwepo, endapo Serikali haitawafukuza kazi akina kingai mahita na wenzao basi wajue laana tokea kwa wananchi inawasubiria
 
Mkuu bila shaka hawa ndio walikulisha matango pori kama walivyolishwa wenzako enzi za Lowasa na baadae 2015 kukiri wenyewe katika kampeni zao kuwa yale waliyokuwa wanaongea kuhusu Lowasa yalikuwa matango pori. Hata haya matango ya sanduku za kura siku mmoja wao kati ya Lisu, Mnyika au yoyote akijitoa chamani ataongea ukweli kuwa madai ya kuiba masanduku ya kura sio ya kweli. Inahitaji mtu ukose hata elimu ya chekechea ndo uwaamini tena hawa jamaa.

View attachment 1962539

View attachment 1962540

View attachment 1962541
Hakuna cha matango pori wewe kwa ujinga wako ulijilisha mwenyewe ukaona kama wengine wanalishwa kama ulijidanganya, wananchi wanawachagua wapinzani vizuri lakini Polisiccm Tumeccm wakurugenziccm Msajiliccm mnaunajisi uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani
 
Kinachosikitisha zaidi ni kwa nini chombo hiki kikubwa kabisa cha ulinzi na usalama wa nchi yetu kimeachwa bila uzio? yaani JWTZ Commando's ama ma Luteni wajeshi wanatekwa na ktenswa namna hii bila JWTZ kutoa kauli.

Ingeleta faraja kama jeshi lenyewe liwe na mechanism yake ya kujichunguza badala ya kuwatoa baadhi ya wanajeshi wao ili wakateswe na kudhalilishwa, wapi heshima ya JWTZ - sasa hatujui yawezekana Komandoo Moses hayupo duniani.

Wapi Komandoo Moses?

View attachment 1962494
Jwtz wameogopa kupaza sauti kwa sababu ni fedheha kwao kudhalilishwa na Polisiccm na endapo itatokea malumbano itahatarisha usalama wa Nchi, kinachowasikitisha jwtz kwa sasa ni Tabia ya hovyo ya utawala wa CCM kuwabambikia kesi wapinzani pasipo kutafakari kabla matokeo yake imekwenda kuleta Aibu na fedheha kwa jwtz na Taifa kwa ujumla
 
Natafta thread ya kesi ya leo ila nme kosa au bado wana habari hawaja anza
Baada ya siri za jwtz kudhalilishwa na Polisiccm kuvuja wamebuni mfumo wa kuzui watu kujua yanayojili mahakamani sasa , lakini wajue tayari mahita kingai na wenzao laana zinawangojea mda wote kwa kuwatesa watu kuwapiga kuwalazimisha wakubali ugaidi ambao hawana haupo na haukuwahi kuwepo
 
hahaaa mkuu umemtaja mpaka kingai, hahahaaaaa inchaji manyota mzee mkubwa afande anauliza eti hiyo PGO sijui GPO ndionini, na mtu ni kiongozi kheeeeeeeeeeeee hatari sana , vijana someni mjiajiri hii ni fedheha
 
Wananchi gani waliadhibu wapinzani? Je ni wale walioiba masanduku ya kura kwenda kujaza kura za wexi wenzao!!?
Au ni ule wizi wa mchakato wa kupiga kura kwa polisi na TISS kubeba maboksi ya kura 2020? Ni lini maamuzi ya wananchi yaliheshimiwa? Saidia hapa ili tupate mwanga!!
Wananchi walichagua wapinzani waliwapa kura nyingi sana lakini Polisiccm Tumeccm wakurugenziccm wakaunajisi uchaguzi mkuu kwa kuwapora haki ya kuchagua wakawasimika CCM kwa njia haramu za kishetani
 
hahaaa mkuu umemtaja mpaka kingai, hahahaaaaa inchaji manyota mzee mkubwa afande anauliza eti hiyo PGO sijui GPO ndionini, na mtu ni kiongozi kheeeeeeeeeeeee hatari sana , vijana someni mjiajiri hii ni fedheha
Albadiri zinaandaliwa lazima wajutie unyama wao
 
Huko mitaani mkimuona mahita kingai muulizeni walipo hao wanajeshi wawili ambao wamepotea
 
Back
Top Bottom